kindikwili
JF-Expert Member
- Oct 5, 2016
- 1,862
- 2,875
Amani iwe kwenu wapendwa!
Siku ya mwaka mpya nilikutana na Baba yangu mdogo ambaye alisomea upadre hadi level ya ushemasi na kwakweli alibakiza muda mfupi sana kupewa daraja la upadre, isivyo bahati aliacha kuendelea na wito wa upadre na hivyo aliamua kuwa mlei (mwanandoa).
Sasa juzi hiyo tukiwa tunapiga stori kuhusu mambo ya kanisa na kuhusu maandiko ya biblia pamoja na mafundisho aliniambia kitu ambacho sikukitegemea kutoka kwake. Aliniambia watumishi wa Mungu wako wa aina mbili, kwanza wako wale waliosoma BIBLE KNOWLEDGE halafu wako wale waliosoma SCRIPTURES. Nikamuuliza nini utofauti wa watu hawa?. Aliniambia kama umesoma scriptures kama yeye yaani kama mapadre wanavyosoma basi hutakuwa na complications juu ya biblia. Anasema mtu aliyesoma scriptures anafundishwa biblia kwa kina , chimbuko la andiko hilo , sababu za kuandikwa kwake na mazingira yaliyopelekea kuandikwa kwa kitabu hicho. Kwahiyo kuna vitabu viliandikwa kwa ajili ya watu wa jamii moja ya wana wa Israel mfano Walawi kitabu hicho kiliandikwa kwa watu hao, kwasababu maalum na kwa mazingira ya wakati huo. Anasema kuchukulia kitabu hicho na kukikumbatia kwa waamini wa Tanzania wa karne ya 21 si kosa lakini pia si sahihi sana. Anasema si kosa kwasababu huenda liliandikwa kuonya jamii na kuwapa muongozo ambao huenda mpaka leo unahitajika, lakini siyo sahihi kwasababu kwanza hakikulenga jamii au kanisa la sasa.
Alisema yapo mafundisho mengi ambayo wakristo wanafundishwa kutoka kwenye biblia ila hayakuandikwa kwa ajili yao. Anatolea mfano sera ya ujamaa ambao kwa wakati huo ulikuwa sahihi lakini kwasasa au kwa miaka zijazo hazitakuwa sahihi kutokana na kubadilika kwa mazingira na kutokana na kutoweka kwa walengwa. Anasema VITABU KWENYE BIBLIA VINAFAA KWA MAFUNDISHO ILA VITABU VYA AGANO JIPYA NDIVYO VYA LAZIMA KWA MKRISTO YEYOTE YULE KUVISHIKA, KUVIFUATA KWA USAHIHI WAKE NA KUVIISHI. ANASEMA UKISTO NI UFUASI WA YESU KRISTO NA HAKUNA UFUASI WA KRISTO WAKATI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI. Akaendelea kusema agano jipya ndilo msingi wa imani ya kikristo na ukristo umejengwa juu ya imani ya mitume wa Yesu na manabii.
Mwisho akanimbia wale wachungaji waliosoma bible knowledge wao wamesoma biblia na namna ya kuitafsiri lakini kuna vitu vingi vya msingi hawajasoma wala kufundishwa , yaani kwa kifupi anasema wana uelewa wa kati kwenye maandiko.
Nini maoni yako.
Siku ya mwaka mpya nilikutana na Baba yangu mdogo ambaye alisomea upadre hadi level ya ushemasi na kwakweli alibakiza muda mfupi sana kupewa daraja la upadre, isivyo bahati aliacha kuendelea na wito wa upadre na hivyo aliamua kuwa mlei (mwanandoa).
Sasa juzi hiyo tukiwa tunapiga stori kuhusu mambo ya kanisa na kuhusu maandiko ya biblia pamoja na mafundisho aliniambia kitu ambacho sikukitegemea kutoka kwake. Aliniambia watumishi wa Mungu wako wa aina mbili, kwanza wako wale waliosoma BIBLE KNOWLEDGE halafu wako wale waliosoma SCRIPTURES. Nikamuuliza nini utofauti wa watu hawa?. Aliniambia kama umesoma scriptures kama yeye yaani kama mapadre wanavyosoma basi hutakuwa na complications juu ya biblia. Anasema mtu aliyesoma scriptures anafundishwa biblia kwa kina , chimbuko la andiko hilo , sababu za kuandikwa kwake na mazingira yaliyopelekea kuandikwa kwa kitabu hicho. Kwahiyo kuna vitabu viliandikwa kwa ajili ya watu wa jamii moja ya wana wa Israel mfano Walawi kitabu hicho kiliandikwa kwa watu hao, kwasababu maalum na kwa mazingira ya wakati huo. Anasema kuchukulia kitabu hicho na kukikumbatia kwa waamini wa Tanzania wa karne ya 21 si kosa lakini pia si sahihi sana. Anasema si kosa kwasababu huenda liliandikwa kuonya jamii na kuwapa muongozo ambao huenda mpaka leo unahitajika, lakini siyo sahihi kwasababu kwanza hakikulenga jamii au kanisa la sasa.
Alisema yapo mafundisho mengi ambayo wakristo wanafundishwa kutoka kwenye biblia ila hayakuandikwa kwa ajili yao. Anatolea mfano sera ya ujamaa ambao kwa wakati huo ulikuwa sahihi lakini kwasasa au kwa miaka zijazo hazitakuwa sahihi kutokana na kubadilika kwa mazingira na kutokana na kutoweka kwa walengwa. Anasema VITABU KWENYE BIBLIA VINAFAA KWA MAFUNDISHO ILA VITABU VYA AGANO JIPYA NDIVYO VYA LAZIMA KWA MKRISTO YEYOTE YULE KUVISHIKA, KUVIFUATA KWA USAHIHI WAKE NA KUVIISHI. ANASEMA UKISTO NI UFUASI WA YESU KRISTO NA HAKUNA UFUASI WA KRISTO WAKATI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI. Akaendelea kusema agano jipya ndilo msingi wa imani ya kikristo na ukristo umejengwa juu ya imani ya mitume wa Yesu na manabii.
Mwisho akanimbia wale wachungaji waliosoma bible knowledge wao wamesoma biblia na namna ya kuitafsiri lakini kuna vitu vingi vya msingi hawajasoma wala kufundishwa , yaani kwa kifupi anasema wana uelewa wa kati kwenye maandiko.
Nini maoni yako.