Si kila kitabu kwenye Biblia ni kwa ajili ya wakristo wote

Si kila kitabu kwenye Biblia ni kwa ajili ya wakristo wote

Amani iwe kwenu wapendwa!
Siku ya mwaka mpya nilikutana na Baba yangu mdogo ambaye alisomea upadre hadi level ya ushemasi na kwakweli alibakiza muda mfupi sana kupewa daraja la upadre, isivyo bahati aliacha kuendelea na wito wa upadre na hivyo aliamua kuwa mlei (mwanandoa).

Sasa juzi hiyo tukiwa tunapiga stori kuhusu mambo ya kanisa na kuhusu maandiko ya biblia pamoja na mafundisho aliniambia kitu ambacho sikukitegemea kutoka kwake. Aliniambia watumishi wa Mungu wako wa aina mbili, kwanza wako wale waliosoma BIBLE KNOWLEDGE halafu wako wale waliosoma SCRIPTURES. Nikamuuliza nini utofauti wa watu hawa?. Aliniambia kama umesoma scriptures kama yeye yaani kama mapadre wanavyosoma basi hutakuwa na complications juu ya biblia. Anasema mtu aliyesoma scriptures anafundishwa biblia kwa kina , chimbuko la andiko hilo , sababu za kuandikwa kwake na mazingira yaliyopelekea kuandikwa kwa kitabu hicho. Kwahiyo kuna vitabu viliandikwa kwa ajili ya watu wa jamii moja ya wana wa Israel mfano Walawi kitabu hicho kiliandikwa kwa watu hao, kwasababu maalum na kwa mazingira ya wakati huo. Anasema kuchukulia kitabu hicho na kukikumbatia kwa waamini wa Tanzania wa karne ya 21 si kosa lakini pia si sahihi sana. Anasema si kosa kwasababu huenda liliandikwa kuonya jamii na kuwapa muongozo ambao huenda mpaka leo unahitajika, lakini siyo sahihi kwasababu kwanza hakikulenga jamii au kanisa la sasa.

Alisema yapo mafundisho mengi ambayo wakristo wanafundishwa kutoka kwenye biblia ila hayakuandikwa kwa ajili yao. Anatolea mfano sera ya ujamaa ambao kwa wakati huo ulikuwa sahihi lakini kwasasa au kwa miaka zijazo hazitakuwa sahihi kutokana na kubadilika kwa mazingira na kutokana na kutoweka kwa walengwa. Anasema VITABU KWENYE BIBLIA VINAFAA KWA MAFUNDISHO ILA VITABU VYA AGANO JIPYA NDIVYO VYA LAZIMA KWA MKRISTO YEYOTE YULE KUVISHIKA, KUVIFUATA KWA USAHIHI WAKE NA KUVIISHI. ANASEMA UKISTO NI UFUASI WA YESU KRISTO NA HAKUNA UFUASI WA KRISTO WAKATI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI. Akaendelea kusema agano jipya ndilo msingi wa imani ya kikristo na ukristo umejengwa juu ya imani ya mitume wa Yesu na manabii.

Mwisho akanimbia wale wachungaji waliosoma bible knowledge wao wamesoma biblia na namna ya kuitafsiri lakini kuna vitu vingi vya msingi hawajasoma wala kufundishwa , yaani kwa kifupi anasema wana uelewa wa kati kwenye maandiko.

Nini maoni yako.
Unaleta Udini na uchochezi. Utafutwaaaaaaaa.
 
wewe si hauamini katika uwepo wa Mungu?haya mambo na utata wake tuachie sisi tunaoamini katika uwepo wake!!
Kwa nini?

Wewe una mamlaka gani ya kuniambia mimi cha kufuatilia na cha kuacha?

Kama Mungu hayupo na habari za kuwepo kwake ni uongo unaoumiza watu kuanzia kuogopa moto ambao haupo, kupoteza muda mpaka kutoa sadaka ambazo zinaliwa na watu waroho tu huku watoa sadaka masikini wakiaminishwa zinafanya kazi ya Mungu, habari ya kuumulika na kuuondoa uongo huu ili watu wengi waujue na kuepukana nao kwa nini iachwe kwa wanaoamini Mungu yupo tu?

Wanaoamini Mungu yupo watamulikaje uongo wanaouamini?

Hujajibu swali langu.

Mungu wako alishindwa kufanya watu wandike kitabu kimoja kitakachokuwa na maana ile ile kwa watu wote wa miaka yote bila utata?
 
Huyo padre ana kila sababu kutoendelea kuwa kama Mtumishi maana ufaham wake ni mdogo sana,
Biblia nzima inamsema Yesu kikubwa ni ufahamu wako
 
Huyo padre ana kila sababu kutoendelea kuwa kama Mtumishi maana ufaham wake ni mdogo sana,
Biblia nzima inamsema Yesu kikubwa ni ufahamu wako
 
kila andiko lenye pumzi ya MUNGU lafaa kwa mafundisho na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kuwaongoza,na kwa kuwaadibisha katika haki; ili kila mtu wa MUNGU awe kamili,amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema;
haya mambo yanahitaji sana maombi na ufunuo wa akili sio darasa,ikiwa hayo aliyosema yako sahihi basi Biblia yote haiko sawa,LA HASHA hakika yeye ndio hayuko sahihi kabisa;
Biblia haikuandikwa kwetu ila imeandikwa kwa ajili yetu;
saafi sana big point
 
Hata huyo Baba yangu mdogo Shemasi Mlei hakatai agano la kale kutumika , yeye anasema si vitabu vyote kwenye biblia ni relevant kwa wakristo wa leo japo yanaweza kutumika kufundishia. Anasema kuna vitabu viliandikwa kwa jamii fulani ya wana wa Israeli kwa wakati na mazingira hayo. Mfano kwenye biblia hasa agano la kale Mungu aliwaruhusu watu kuoa wanawake wengi wala haikuwa shida, habari za vyakula, habari za talaka, habari za kulipiza kisasi, habari za adhabu za moja kwa moja kutoka kwa Mungu etc. Hizi zilisadifu mazingira ya wakati huo na kwasasa msingi kamili wa Ukristo ni YESU na Mitume. Anasema agano jipya ni standard kwa wakristo wote duniani
yakupasa kujua YESU alikuja kuukomboa ulimwengu wote na siku ya mwisho atahukumu ulimwengu wote. ndani ya YESU kuna UTEULE NA UTAKATIFU na ndio maana wanaomfuata YESU jina sahihi kwao ni wateule, watakatifu au wana wa MUNGU. kusema YESU ni alikuja kwa wanaojiita wakristo tu si sawa.
 
Kwa nini?

Wewe una mamlaka gani ya kuniambia mimi cha kufuatilia na cha kuacha?

Kama Mungu hayupo na habari za kuwepo kwake ni uongo unaoumiza watu kuanzia kuogopa moto ambao haupo, kupoteza muda mpaka kutoa sadaka ambazo zinaliwa na watu waroho tu huku watoa sadaka masikini wakiaminishwa zinafanya kazi ya Mungu, habari ya kuumulika na kuuondoa uongo huu ili watu wengi waujue na kuepukana nao kwa nini iachwe kwa wanaoamini Mungu yupo tu?

Wanaoamini Mungu yupo watamulikaje uongo wanaouamini?

Hujajibu swali langu.

Mungu wako alishindwa kufanya watu wandike kitabu kimoja kitakachokuwa na maana ile ile kwa watu wote wa miaka yote bila utata?

unawezaje kujikita katika mjadala wa kitu ambacho unaamini hakipo???kama unaamini yupo karibu tujadiliane!!wewe unafaa katika mada za wanaoamini Mungu yupo vs Wasioamini katika uwepo wake!!sasa hii mada ni ya wanaoamini ktk uwepo wake
 
unawezaje kujikita katika mjadala wa kitu ambacho unaamini hakipo???kama unaamini yupo karibu tujadiliane!!wewe unafaa katika mada za wanaoamini Mungu yupo vs Wasioamini katika uwepo wake!!sasa hii mada ni ya wanaoamini ktk uwepo wake
Naweza kujikita katika mjadala wa kitu ambacho hakipo kama daktari anayejua kwamba ugonjwa A hauna dawa, halafu akasikia matapeli wanasema wanauza dawa inayoponya ugonjwa huo.

Ingawa dawa haipo, daktari huyu anayejua dawa haipo anaingia katika mjadala kuionesha jamii kwamba kuamini kitu ambacho hakipo kwamba kipo kunaweza kuwa hatari.

Kwa sababu watu ambao wangeweza kujikinga wasipate ugonjwa A wanaweza kupunguza kujikinga wakijua kuna dawa.

Pia watu wanaweza kuibiwa hela na matapeli kwa kuuziwa kitu kinachoitwa dawa ya ugonjwa A wakati si dawa.

Zaidi, uongo ni uongo tu. Mtu anayejua huu ni uongo hahitaji sababu zaidi kuupinga.

Mungu wenu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote, utukufu wote na uoendo wote, mnayesema kaumba dunia hii inayowezekana kuwa na mabaya mengi, hayupo.

Dhana ya kuwepo kwake ina contradiction.

Kusema yupo ninsawa na kusema pembetatu yenye pembe nne katika Euclidean geometry.

Au kusema katika base ten math square root ya 2 ni 10.

Contradictions.
 
Mkuu wewe umesoma bible knowledge au scriptures? hapo penye rangi nyekundu mbona jamaa alielezea vzr kama nilivyosema hapo juu? Jamaa anasema si kosa kufundisha watu kuhusu habari za mambo ya walawi lakini vitabu vingi vya agano la kale viliandikwa si kwa wakristo wala watu wote bali yaliandikwa kwa watu maalumu kwenye mazingira na nyakati maalumu. Jamaa anasema HAKUNA UKRISTO BILA YESU, HAKUNA KITU KWENYE UKRISTO ZAIDI YA KUFUATA MAFUNDISHO YA YESU NA MISINGI ILIYOWEKWA NA YESU PAMOJA NA MITUME WAKE. Hakatai watu kusoma biblia nzima ila kuna vitabu siyo relevant kwa wakristo.
Unaposoma Biblia, unatakiwa kujua ujumbe huo uliandikwa kwa nani na kwa nini uliandikwa pia ulikusudiwa kutoa somo gani kwa wakati huo na mwisho unatakiwa ujihoji kwetu sisi tunapata fundisho gani. Kwa kweli hata agano jipya liliandikwa kwa jamii ya wakati huo kutokana na hali iliyo kuwepo mfano nyaraka za Paulo ambapo analiandikia kanisaalmu ama mtu mmoja kulingana na hali iliyo kuwepo cha msingi kwetu ni kuchukua jumbe hizo zote za Biblia bila kujali ni agano gani na lujiuliza kwetu sisi tunajifunza nn. Maana kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho
Mkuu wewe umesoma bible knowledge au scriptures? hapo penye rangi nyekundu mbona jamaa alielezea vzr kama nilivyosema hapo juu? Jamaa anasema si kosa kufundisha watu kuhusu habari za mambo ya walawi lakini vitabu vingi vya agano la kale viliandikwa si kwa wakristo wala watu wote bali yaliandikwa kwa watu maalumu kwenye mazingira na nyakati maalumu. Jamaa anasema HAKUNA UKRISTO BILA YESU, HAKUNA KITU KWENYE UKRISTO ZAIDI YA KUFUATA MAFUNDISHO YA YESU NA MISINGI ILIYOWEKWA NA YESU PAMOJA NA MITUME WAKE. Hakatai watu kusoma biblia nzima ila kuna vitabu siyo relevant kwa wakristo.
 
wewe si hauamini katika uwepo wa Mungu?haya mambo na utata wake tuachie sisi tunaoamini katika uwepo wake!!
Hata kama haamini katika uwepo wa mungu,bado ana haki ya kuhoji kuhusu huyo mungu.

Unachotakiwa wewe ni kumpa majibu kwa swali alilouliza.

Uenda kupitia majibu yako yasiyo na mashaka wala kujipinga akaamua kubadili msimamo na kumuamini mungu.
 
Hata kama haamini katika uwepo wa mungu,bado ana haki ya kuhoji kuhusu huyo mungu.

Unachotakiwa wewe ni kumpa majibu kwa swali alilouliza.

Uenda kupitia majibu yako yasiyo na mashaka wala kujipinga akaamua kubadili msimamo na kumuamini mungu.
Na mpaka sasa hajanijibu.

Anaamini Mungu yupo.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote, ujuzi wote, utukufu wote. Aliyeumba ulimwengu huu unaoruhusu mabaya mengi. Matetemeko ya ardhi. Magonjwa. Vita etc.

Kwa nini hakuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya?

Mungu huyu alishindwa kufanya watu waandike kitabu ambacho kitaeleweka bila utata kwa watu wote, muda wote?

Hajajibu maswali.
 
Huyo baba yako mdogo ndo maana walimtimua hawakumpa upadre.

Wapi nimesema walimtimua? nimesema aliacha mwenyewe. Halafu ungetuambia kosa lake kwenye hayo mazungumuzo yetu siyo kumhukumu tu bila sababu
 
Huyo padre ana kila sababu kutoendelea kuwa kama Mtumishi maana ufaham wake ni mdogo sana,
Biblia nzima inamsema Yesu kikubwa ni ufahamu wako

Mkuu huyo kasoma SCRIPTURES katika ukweli na uhalisi wake, kasoma historia ya biblia na mazingira ya uandishi wake. Anajua anachokisema, tena anatushangaa sana tunavyohangaika na habari nyingine
 
yakupasa kujua YESU alikuja kuukomboa ulimwengu wote na siku ya mwisho atahukumu ulimwengu wote. ndani ya YESU kuna UTEULE NA UTAKATIFU na ndio maana wanaomfuata YESU jina sahihi kwao ni wateule, watakatifu au wana wa MUNGU. kusema YESU ni alikuja kwa wanaojiita wakristo tu si sawa.

Mkuu hiyo habari za Yesu kuja kwa ajili wa wakrito nani kasema?
 
Hata kama haamini katika uwepo wa mungu,bado ana haki ya kuhoji kuhusu huyo mungu.

Unachotakiwa wewe ni kumpa majibu kwa swali alilouliza.

Uenda kupitia majibu yako yasiyo na mashaka wala kujipinga akaamua kubadili msimamo na kumuamini mungu.

mkuu,jamaa ana tatizo akikuta mada za kiroho zenye muelekeo flani anazipindisha na kuzisukumia katika muelekeo wake,ndio maana simjibu atakavyo!Ni mvurugaji mada kama wavurugaji wengine wanaotumia mbinu ya kuingizia mada juu ya mada.Ni hilo tu!Unadhani sipo sahihi mpaka hapa??
 
kama ndivyo basi Yesu Kristo angekuja na amri mpya za Mungu kwa sababu zile za agano la kale ziliwahusu waisrael tu tena wakiwa safarini na ningetegemea baada ya kuwa wamefika basi wangepewa amri mpya kwa sababu safaria ilikuwa imeisha. Huyo shemasi mlei hapo hayuko sahihi hata kidogo, haya mambo hayahitaji shule pekee bali zaidi Roho wa Mungu kukuongoza
 
mkuu,jamaa ana tatizo akikuta mada za kiroho zenye muelekeo flani anazipindisha na kuzisukumia katika muelekeo wake
Uelekeo wake ni upi?

Kwanini kuzipindisha na kuzisukumia mada kwenye uelekeo wake kuwe na tatizo?

ndio maana simjibu atakavyo
Na kamwe usimjibu atakavyo.

Mjibu kwa kadri ya ukweli wa mambo ulivyo.
Ni mvurugaji mada kama wavurugaji wengine
Kwanini kuuliza kwake iwe ni kuvuruga mada na si kutaka kujua tu?
 
Back
Top Bottom