Si kila kitabu kwenye Biblia ni kwa ajili ya wakristo wote

Si kila kitabu kwenye Biblia ni kwa ajili ya wakristo wote

Na mpaka sasa hajanijibu.

Anaamini Mungu yupo.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote, ujuzi wote, utukufu wote. Aliyeumba ulimwengu huu unaoruhusu mabaya mengi. Matetemeko ya ardhi. Magonjwa. Vita etc.

Kwa nini hakuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya?

Mungu huyu alishindwa kufanya watu waandike kitabu ambacho kitaeleweka bila utata kwa watu wote, muda wote?

Hajajibu maswali.
Labda hana majibu sahihi.
 
Mi muislam hainihusu ngoja nikae pembeni mchambane wenyewe
 
agano la kale kimsingi lilileta sheria na yakupasa kujua bila sheria hakuna dhambi. agano jipya limeleta uwokovu kwa njia ya NEEMA KATIKA YESU KRISTO. TORATI YOTE NA MANABII UKAMILISHO WAKE NI YESU KRISTO. AGANO LA KALE LILILETA SHERIA, LAKINI TUNAONA HAKUNA ALIYEWEZA KUOKOLEWA KWA MATENDO YA SHERIA MAANA WOTE WALITENDA DHAMBI NA KUVUNJA SHERIA. NAMNA PEKEE YA KUMKOMBOA MWANADAMU ILIBAKI KUWA NEEMA KATIKA YESU KRISTO. YESU ALIKUWEPO KABLA YA KUWEKWA MISINGI YA DUNIA SO KILA UNACHOKIONA KATIKA BIBILIA NI KWA WATU WOTE KATIKA ULIMWENGU WA ROHO. ACHA KUSOMA BIBILIA KAMA KITABU CHA HISTORIA
Amen.... Huyo ni ROHOMTAKATIFU amekufunulia siri hii
 
Amani iwe kwenu wapendwa!
Siku ya mwaka mpya nilikutana na Baba yangu mdogo ambaye alisomea upadre hadi level ya ushemasi na kwakweli alibakiza muda mfupi sana kupewa daraja la upadre, isivyo bahati aliacha kuendelea na wito wa upadre na hivyo aliamua kuwa mlei (mwanandoa).

Sasa juzi hiyo tukiwa tunapiga stori kuhusu mambo ya kanisa na kuhusu maandiko ya biblia pamoja na mafundisho aliniambia kitu ambacho sikukitegemea kutoka kwake. Aliniambia watumishi wa Mungu wako wa aina mbili, kwanza wako wale waliosoma BIBLE KNOWLEDGE halafu wako wale waliosoma SCRIPTURES. Nikamuuliza nini utofauti wa watu hawa?. Aliniambia kama umesoma scriptures kama yeye yaani kama mapadre wanavyosoma basi hutakuwa na complications juu ya biblia. Anasema mtu aliyesoma scriptures anafundishwa biblia kwa kina , chimbuko la andiko hilo , sababu za kuandikwa kwake na mazingira yaliyopelekea kuandikwa kwa kitabu hicho. Kwahiyo kuna vitabu viliandikwa kwa ajili ya watu wa jamii moja ya wana wa Israel mfano Walawi kitabu hicho kiliandikwa kwa watu hao, kwasababu maalum na kwa mazingira ya wakati huo. Anasema kuchukulia kitabu hicho na kukikumbatia kwa waamini wa Tanzania wa karne ya 21 si kosa lakini pia si sahihi sana. Anasema si kosa kwasababu huenda liliandikwa kuonya jamii na kuwapa muongozo ambao huenda mpaka leo unahitajika, lakini siyo sahihi kwasababu kwanza hakikulenga jamii au kanisa la sasa.

Alisema yapo mafundisho mengi ambayo wakristo wanafundishwa kutoka kwenye biblia ila hayakuandikwa kwa ajili yao. Anatolea mfano sera ya ujamaa ambao kwa wakati huo ulikuwa sahihi lakini kwasasa au kwa miaka zijazo hazitakuwa sahihi kutokana na kubadilika kwa mazingira na kutokana na kutoweka kwa walengwa. Anasema VITABU KWENYE BIBLIA VINAFAA KWA MAFUNDISHO ILA VITABU VYA AGANO JIPYA NDIVYO VYA LAZIMA KWA MKRISTO YEYOTE YULE KUVISHIKA, KUVIFUATA KWA USAHIHI WAKE NA KUVIISHI. ANASEMA UKISTO NI UFUASI WA YESU KRISTO NA HAKUNA UFUASI WA KRISTO WAKATI WA KITABU CHA MAMBO YA WALAWI. Akaendelea kusema agano jipya ndilo msingi wa imani ya kikristo na ukristo umejengwa juu ya imani ya mitume wa Yesu na manabii.

Mwisho akanimbia wale wachungaji waliosoma bible knowledge wao wamesoma biblia na namna ya kuitafsiri lakini kuna vitu vingi vya msingi hawajasoma wala kufundishwa , yaani kwa kifupi anasema wana uelewa wa kati kwenye maandiko.

Nini maoni yako.
Kwa mtazamo wake huo lazima angeacha wito.
 
Hata mimi naona hivyo.

Ila hata huko kwenye agano jipya kuna vitabu bado havifai kwa wakristo wote. Mfano nyaraka za Paulo....nyingi aliandika kulingana na makabila na tamaduni na mazingira ya wakati huo.
Mnapotoshwa
 
Hata mimi naona hivyo.

Ila hata huko kwenye agano jipya kuna vitabu bado havifai kwa wakristo wote. Mfano nyaraka za Paulo....nyingi aliandika kulingana na makabila na tamaduni na mazingira ya wakati huo.
Kikubwa ni kuacha dhambi , ukiacha dhati utachagua kitabu cha kusoma
 
Aisee mbona ambapo tuna IQ ndogo na akili average hatutakaa tukanyage mbinguni..

Mbinguni wataenda watu wenye akili,wenye uweze wa kusoma biblia kwa akili fulani mahususi na uelewa fulani hivi special..Sisi wengine tusiokua na akili hizo imekula kwetu..

Na kama hatuna hela ya kununua na kusoma biblia tutaenda motoni milele

Na kama tumezaliwa Siberia huko au Uchina huko wasiojua nini kitu Yesu Kristo,tutaenda motoni milele,wakati hata sikua na uwezo wa kuchagua kuzaliwa huko,nilijikuta tu nimezaliwa huko bila uamuzi wangu binafsi

Etc

Etc

Etc

Huyu mungu wa wakristo ni baguzi la kutupwa,na wakristu wote ni watu wa ajabu hawafai kukaa hapa duniani kabisa...
 
Si kweli hata kidogo, mazingira yalimfanya Mungu atoe sheria na taratibu kwa wana wa Israel kwa wakati huo tu na hakulenga jamii nzima ya dunia wala karne nyingi zilizokuwa zinakuja. Hapa ndipo kuna umuhimu wa kusoma scriptures. Mfano habari ya talaka, habari za kufunga, habari za kutoa sadaka za kuteketeza, habari za vyakula etc. Haya ni mafundisho na maandiko kamili ya biblia lakini zilihusu jamii ya wana wa Israeli kwa wakati na mazingira yale ndiyo maana baadaye Yesu Kristo anakuja kuyarekebisha.
Yesu alikuja kutimiza torati na sio kuiondoa usipotoshe ndugu nakukaribisha tujifunze kwa unyeyekevu huku tukiomba Roho mtakatifu atufundishe neno lake
 
Yaaap anaye tafsiri biblia kwa kigezo cha roho mt. Huwa wanatafsiri kwa mizuka.....hisia....kiasi kwamba hadi muumini anaingiwa na Yale maneno Na anasema ni roho wa Mungu.....kumbe mchungaji ameweza kugusa roho yako kwa sauti za hisia na ameweza Kuhusanisha biblia na matqtizo yako.
.

.

.ndoa....

Vyuma kukaza....


Uchawi..
.


Kukosa kazi.....

Madeni.......


Elimu.

Hapa ndo utaona watu wanavyo anguka.


Lakn mapadre wapo tofauti sana.
Anafanya uelewe sio Kuku umiza kihisi
 
Kwa uhalisia nadhani huyo jamaa hana upadre wowote.
Kwanini nasema Hivyo?
Bible Knowledge ni Ufahamu Wa Biblia
Scripture ni Maandiko.
Biblia ni mkusanyiko wa maandiko fulani..............
Sasa itakuwa ajabu leo Bible knowledge na Scripture vikawa masomo mawili tofauti.

Pia Hiyo Bible Knowledge sio Somo la Wachungaji Ni somo kama masomo mengine tu kama History/Mathematics Biology/Islamic Studies etc
Mimi Nimesoma Shule za Kidini(Za Wakristo)
Bible Knowledge kwa Kidato cha kwanza na Pili NI Lazima Kusoma Sio Option (Kwa Shule za Kikristo)
NIlipofika Advance nikasoma Divinity
Na Wachungaji hawana somo hilo zaidi zaidi unakutana nalo katika madarasa ya Wainjilisti nalo haliwi zito kama vile shule za Sekondari.
Mtoa Uzi Next Time Uwe makini acha kuleta Mikanganyiko Hapa.
Unajua Mada kama hizi inakupasa uwe hata wewe unaifahamu kwa upana zaidi mbali na masimulizi tu unayopatiwa huko lakini uweze kupata namna ya kuileza na kutetea ili usilete maswali zaidi kwa wasomaji.
Si vema kuleta hoja ambayo huna ujuzi nayo na kisha ikaleta ukakasi na mambo tofauti kwa wasomaji

Naambatanisha Ni Uzi Huu hapa ukibonyeza ukaone masomo yanayotambuliwa Na Serikali Ambayo Ni Ya Dini pamoja na ambayo Sio Ya Dini BONYEZA HAPA
 
Sasa kile cha makabila yetu kiko wapi? Kile cha utamaduni wetu kiko wapi? Mtoa mada anadhani mtu wake ndiye peke aliyesoma maandiko kwa kina. Anapotofautisha scriptures yaani maandiko na Bible Knowledge yaani elimu ya Biblia ana maana gani? Wanaosoma Bible Knowledge ama Theology au Teolojia (Elimu ya Mungu) na fani zingine husika hurejea maandiko ya Biblia. Maandiko ndiyo rejea kuu (Primary Source). Bible Knowlege ni hatua ya mwanzo katika sayansi ya kutafsiri Maandiko (Hermeneutics). Ili kupata kiini ama kina cha habari na tafsiri bora unafanya biblical exegesis yaani uchanganuzi wa kina wenye kuhusisha mambo mengi yakiwemo historia ya kifungu, walengwa, maana ya asili ya mwandishi na mazingira ya wakati huo; ndipo unafanya matumizi ya ujumbe uliomo katika zama za sasa, walengwa wa sasa katika lugha ya wahusika na desturi zao za sasa. Biblia ni kwa ajili ya vizazi vyote ina tafsiri moja bali matumizi (application) nyingi. Mfano kut 18:19 Yethro ampa Musa sifa za kuweka wakuu wa watu wamsaidie kazi. Sifa hizo zinafanana na sifa za Mzee wa Kanisa katika Tito 1:5-9 na sifa za Askofu katika 1 Tim 3:1-5. Leo Januari 2018 twaweza pia kutumia baadhi ya sifa kama inavyotuhusu. Mfano mzuri ni kuwa kiongozi asiwe mwenye kupenda pesa ama mwenye kutafuta mapato ya aibu. Tutaitumia sifa hiyo leo pia maana inahusika.Taz Kut 18:21, 1Tim 3:7 na Tit 1:3
 
Pengine huyu ndugu yako aliyekuwa anasomea upadri angemalizia masomo yake ndio angeweza kukupa picha kamili.. Biblia iko wazi kuwa kila neno lenye pumzi ya Mungu la faa kwa mafundisho, kuonya na kuelekeza..Hakuna namna unayoweza kuisoma na kuielewa biblia bila msaada wa Roho Mtakatifu ambaye ndiye mwalimu wa kweli akuongoze, vimginevyo pamoja na hoja yake bado hakuna jambo lolote linalomshinda Mungu kutumia kitabu chochote katika Biblia kutimiza makusudi yake kwetu.
 
kila andiko lenye pumzi ya MUNGU lafaa kwa mafundisho na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kuwaongoza,na kwa kuwaadibisha katika haki; ili kila mtu wa MUNGU awe kamili,amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema;
haya mambo yanahitaji sana maombi na ufunuo wa akili sio darasa,ikiwa hayo aliyosema yako sahihi basi Biblia yote haiko sawa,LA HASHA hakika yeye ndio hayuko sahihi kabisa;
Biblia haikuandikwa kwetu ila imeandikwa kwa ajili yetu;
Mbona hutoi sadaka za kuteketezwa kama walawi(makuhani? walivyofanya?
 
Back
Top Bottom