Siasa, unafiki na usanii: Ufaulu wa kidato cha nne mwaka 2023 umejificha ndani ya divisheni 4

Siasa, unafiki na usanii: Ufaulu wa kidato cha nne mwaka 2023 umejificha ndani ya divisheni 4

Walimu ndo kwanza wanajichanga kumchukulia bi hadija fomu, uchawa linaenda kuwa janga kubwa kwa taifa zaidi ya ugonjwa wa tauni.
 
Hawo wote ni zero tu na ukijumlisha wote wenye zero na foo, wanafika 96% ya wanafunzi wote. Waliopata 1 mpaka 3 ni asilimia 4% tu. Hii nchi ina mambo ya kipumbavu sana aisee!
Bila kuthibiti tabia za uchawa zilizoanza kukita mizizi hatutafika popote, Mwalimu Nyerere alichukia sana tabia za uchawa na kujipendekeza.......kilichozingatiwa ni sifa stahiki zikiwemo weledi, utu, umahiri nk. Kwa sasa uchawa umetamalaki kila eneo, wenyewe wanaita connection hadi wahamiaji haramu wanapata connection kwenye teuzi.....​
 
Wewe Mzazi mtoto wako amefeli.. unailaumu Serikali...
Weww ulichukua hatua gani kumsaidia huyo mtoto tokea akiwa Form one.. mfdno Kukaa nae na kummsisitiza kuhusu elimu; kumnunulia Vitabu vya ziada; Kumtafutia remedial class
Unabaki kulia lia tu Serikali impe mtoto wako Ufaulu
Papaya lilooza
 
Ukiachilia mbali Mapungufu ya Serikali yetu katika Sekta ya Elimu.WAZAZI PIA WANAMAKOSA MAKUBWA SANA,KI VP?
Wazazi wengi wanaamini mtoto kwenda shule na kurudi ndiyo kusoma.Mtoto kutoka asubuhi na kurudi mchana ndiyo kusoma uku wakiamini mwishoni atafaulu (HAPANA NA SIO KWELI).Ili mtoto afaulu ni lazima apate muda wake binafsi wakujisomea yeye kama yeye.
KUFAULU KUNA STAGES TATU
1:Kutafuta materials(Vitabu,Past papers,Quiz papers)kuhakikisha notes zote za masomo unazo.
Mzazi unatakiwa kuhakikisha mwanao ana vitabu vyote vya masomo anayosoma shuleni.Nenda shuleni kwao uliza mtoto wangu ansoma masomo gani, Je shule ina vitabu vya kutosha mtoto wako anaweza akapata kama hamna nenda kanunue au omba kitabu ukatoe copy,kule karume wanauza vitabu vya copy bei rahisi.Mtafutie tuition ya ziada mwanao,Mtafutie Reviews za mitihani iliyopita ya miaka ya nyuma kwa maana maswali ni yale yale yanajirudia.
2:Kuhamisha materials hayo kutoka kwenye vitabu kwenda kichawani.
Hapa ndipo kwenye mtihani na ugumu na wazazi wengi wanafeli hapa,mzazi ni lazima uhakikishe mtoto wako anasoma kila siku,kila atakaporudi shule ni lazima ajisomee alichofundishwa shule ni lazima uhakikishe mtoto wako ana ratiba ya kujisomea na anaifata ratiba (sio ratiba imfate yeye).Ni ratiba uhakikishe mtoto wako halali bila ya kujisomea isipite siku bila ya kujisomea, Mtoto kwenda shule na kurudi sio kusoma
3:Kuhamisha materials kutoka kichwani kwenda kwenye mtihani.
Mzazi kaa na mwanao chukua kitabu muulize maswali kwa utani tu kujua kama anakumbuka,au unaweza ukamwambia nifundishe ulichosoma bila kuangalia kwa kitabu kwa utani tu uku mnafurahi.Hapa mtoto hawezi kusahu

Siku zote anza kujipigania wewe mwenyewe usisubiri mtu mwengine akufikirie na akupiganie.
 
Ukiachilia mbali Mapungufu ya Serikali yetu katika Sekta ya Elimu.WAZAZI PIA WANAMAKOSA MAKUBWA SANA,KI VP?
Wazazi wengi wanaamini mtoto kwenda shule na kurudi ndiyo kusoma.Mtoto kutoka asubuhi na kurudi mchana ndiyo kusoma uku wakiamini mwishoni atafaulu (HAPANA NA SIO KWELI).Ili mtoto afaulu ni lazima apate muda wake binafsi wakujisomea yeye kama yeye.
KUFAULU KUNA STAGES TATU
1:Kutafuta materials(Vitabu,Past papers,Quiz papers)kuhakikisha notes zote za masomo unazo.
Mzazi unatakiwa kuhakikisha mwanao ana vitabu vyote vya masomo anayosoma shuleni.Nenda shuleni kwao uliza mtoto wangu ansoma masomo gani, Je shule ina vitabu vya kutosha mtoto wako anaweza akapata kama hamna nenda kanunue au omba kitabu ukatoe copy,kule karume wanauza vitabu vya copy bei rahisi.Mtafutie tuition ya ziada mwanao,Mtafutie Reviews za mitihani iliyopita ya miaka ya nyuma kwa maana maswali ni yale yale yanajirudia.
2:Kuhamisha materials hayo kutoka kwenye vitabu kwenda kichawani.
Hapa ndipo kwenye mtihani na ugumu na wazazi wengi wanafeli hapa,mzazi ni lazima uhakikishe mtoto wako anasoma kila siku,kila atakaporudi shule ni lazima ajisomee alichofundishwa shule ni lazima uhakikishe mtoto wako ana ratiba ya kujisomea na anaifata ratiba (sio ratiba imfate yeye).Ni ratiba uhakikishe mtoto wako halali bila ya kujisomea isipite siku bila ya kujisomea, Mtoto kwenda shule na kurudi sio kusoma
3:Kuhamisha materials kutoka kichwani kwenda kwenye mtihani.
Mzazi kaa na mwanao chukua kitabu muulize maswali kwa utani tu kujua kama anakumbuka,au unaweza ukamwambia nifundishe ulichosoma bila kuangalia kwa kitabu kwa utani tu uku mnafurahi.Hapa mtoto hawezi kusahu

Siku zote anza kujipigania wewe mwenyewe usisubiri mtu mwengine akufikirie na akupiganie.
Hili nalo neno mkuu. Upewe maua yako.
 
Hivi serikali ya Samia (sio ya CCM) inamdanganya nani kwa haya matokeo ya kupika? Matokeo ya mitihani ya mwaka huu ni mabaya kuliko tunavyoelezwa na hawa wasanii wa CCM.
 
Back
Top Bottom