Siasa za kutishana hazitoimarisha Amani- Rais Samia

Siasa za kutishana hazitoimarisha Amani- Rais Samia

Mama anajisahau kuwa serikali yake ndyo serikali ya vitisho na ubabe!

Hao CHADEMA wasio na jeshi lolote wakitegemea wananchi waoga kuwaunga mkono wana vitisho na ubabe gani??

Je, CHADEMA walishawah kupora uchaguzi Kama CCM alivyofanya 2019 serikali za mitaa??
Vipi kuhusu uchafuzi mkuu 2020, mbabe na mporaji na mtishaji alikua Nani??

Mama ananyoosha kidole kwa CHADEMA huku vidole vyote vitano vikimrudia yeye!!
Lengo ukiporwa ushindi utulie, sio kama wafanyavyo chadema kudai haki yao, mie nashangaa wale mashehe na wachungaji wanajukumu gani kwenye shughuli za kitaifa? Dua sana halafu waliopo hapo hapo wanatenda dhambi hadharani ya kuonea wengine, kuto fuata katiba, au dua zile zina kasoro? Hivyo Mungu hazipokei?
 
Lengo ukiporwa ushindi utulie, sio kama wafanyavyo chadema kudai haki yao, mie nashangaa wale mashehe na wachungaji wanajukumu gani kwenye shughuli za kitaifa? Dua sana halafu waliopo hapo hapo wanatenda dhambi hadharani ya kuonea wengine, kuto fuata katiba, au dua zile zina kasoro? Hivyo Mungu hazipokei?
Siku hizi hamna masheihk Wala wachungaji, njaa inatusumbua sana, lita 10 ya mafuta ya kula ipo around elfu sitin na kitu huko, watakumbuka kusimamia kweli ya Mungu!!?
 
CHADEMA kususia huu mkutano kumemuudhi sana SSH.. hata Msajili wa vyama amekuwa 'helpless' kwenye hili..
 
Kama ana akili na anajiamini aruhusu uchaguzi huru! Atashika adabu huyu mlevi wa madaraka
 
Amesema Mbowe amevunja sheria ama wewe umeongezea?

Kama amesema hivyo, basi tayari ameshamuhukumu na kuingilia muhimili wa mahakama ili ufuate anayoyataka yeye. Kama ni kweli kuongea hayo, huyu ataingia kwenye historia ya kuwa rais wa hovyo kuliko wote hapa Tanzania.

Pia kama ametumia hicho kikao chao kuleta mipasho, badala ya kujikita kwenye agenda walizo nazo kama zilikuwepo, kumeonyesha ni kwa jinsi gani utawala huu tumeingia choo cha kike.

Eti CHADEMA waache vitisho na ubabe? Anajuwa maana ya hayo maneno?

Vitisho na ubabe vinatoka kwenye serikali yake kwa mihimili yote mitatu kushiriki kwenye ukandamizaji wa demokrasia na uvunjaji wa katiba ya nchi.
Ndiyo maana Ulimwengu alisema Maza haijui Tanzania ....!!
 
Mheshimiwa Rais awaasa kina chadema kuhusu kutumia vitisho ubabe, kejeli na dharau kwa kushinikiza wayatakayo.

Mbowe amevunja sheria anapaswa wajibike kwa mujibu wa sheria

mama anashusha nondo
Siasa za kubembelezana zimepitwa na wakati , tz siyo nyumba binafsi ya mtu yoyote , KILA mtu amuheshim mwenzake hasa linapokuja swala la kisiasa, sio kisa una mamlaka Basi watu wakubali KILA Jambo unalotaka, yale yenye maslahi mapana ya Taifa lazima kupiganiwa KWa nguvu kubwa Sana bila kujali vikwazo
 
hiyo hiyo katiba ndio inatuambia Mahakama ni mhimili unaojitegemea na hauingiliwi na mtu..

Jaji kuwa mteuliwa hakumfanyi kushindwa kuamua, kwani jaji anaweza kutenguliwa ujaji?.. hapa ni utashi binafsi wa jaji mhusika kuamua kufuata sheria au kusikiliza mamlaka...
Hata hiyo katiba mpya ikiwepo bado jaji anaweza tu kuamua kuweka weledi pembeni na akaamua kwa utashi wake na tusimfanye kitu... KENYA WANA KATIBA MPYA LAKINI KILA SIKU TUNASHUHUDIA HIYO MIGOGORO YA KISHERIA NA WATU KUISIGINA KATIBA...

Hakuna Mahala Katiba hii tunayotumia imesema Rais yuko juu ya sheria....mihimili iko mitatu na yote inajitegemea.....Katiba inasimamiwa na watu, watu wasipostaarabika wataivunja tu hata iweje..
Katiba haiusemi udhaifu wake. Ila matokeo ya udhaifu wake yanaonekana wazi kabisa.

Kwani rais si alimpandisha cheo kabisa yule jaji kuwa jaji mkuu kiongozi baada ya kazi yake nzuri dhidi ya Mbowe kuonekana.

Mtu anayekuteuwa unawezaje kwenda kinyume naye? Hata hiyo tume ya uchaguzi ni yale yale tu.

Ukiwa mnufaika wa ujinga unaoendelea huwezi kuona hizo kasoro.
 
That is a Political maturity..... hongera Rais Mama Samia kwa kufahamu na kuzingatia kanuni mojawapo muhimu ya kidemokrasia ambayo viongozi wengi wa Kiafrika wameshindw kuizingatia.
Political maturity my foot!! Kuzungumzia kesi iliyoko mahakamani tena kwa kumsema vibaya mtuhumiwa unafikir hao majaji wa michongo wanapata ujumbe gani?
 
Leo anasema huwezi kufata democracy ya watu wanazaidi ya miaka 200 wakati wewe una 60. Akimaanisha katiba kwake na democracy sio vitu muhimu
 
"Mbowe amevunja sheria anapaswa wajibike kwa mujibu wa sheria"

Amesema hivyo kweli?

Nadhani hii sio sawa, ni dhahiri Rais anajua impact ya maneno yake.

Kesi ipo mahakamani, Mbowe bado hajatiwa hatiani.

Kauli kama hizi ndo zinazidi kuaminisha watu kwamba hukumu ilishafanyika.

Rais wetu mama Samia ana busara, naamini hajasema haya.
 
Naapa ndiyo mwanzo kaisha liamsha dude tulijuwa Mbowe ni gaidi kumbe hamna,,
 
Mheshimiwa Rais awaasa kina chadema kuhusu kutumia vitisho ubabe, kejeli na dharau kwa kushinikiza wayatakayo.

Mbowe amevunja sheria anapaswa wajibike kwa mujibu wa sheria

mama anashusha nondo
Huu ni ujinga kama ujinga mwingine wowote. Anayeshika watu na kuwafunguliza kesi za kubambikiza ndiye mwenye vitisho. Anayeteka watu kwa kutumia watu wasiojulikana ndiye mwenye vitisho.
 
kwani si zitto ndio aloanza kuizungumzia na kumuomba mwenzao aachiwe, yy kamjibu kua sheria ifatwe

..hata kumuachia ni kufuata sheria.

..lakini Raisi kutamka " Mbowe amevunja sheria " anakuwa amekwenda mbali na sio sahihi.

..mahakama [ Jaji jamhuri utetez] bado wako ktk mchakato wa kufafahamu kama Mbowe amevunja sheria. au la.
 
Back
Top Bottom