Maisha safari ndefu Mkuu.Duh! Kumbe mama alipanic kwa sababu ya kudhani kwamba ulikuwa umeenda kumtalisha huyo mwanamke kwake Kama mkeo[emoji23]
Maxence Melo mkuu naomba JF ID yangu kuanzia sasa hivi isome "MZEE KESHO YETU au KISAUTI " 😁😁😁13th Portion:
... Sikuwa na kitu nilichoweza kufanya kwa wakati ule. Hata kama ningesema nimbembeleze, still isingefanya kazi, maana sijui dhamira yake halisi ni ipi.
Sikutaka hata kulala pale. Nikaamua kurudi gheto kwangu, PS4 yake nikamuacha nayo.
Njia nzima kichwa kimezongwa na mawazo hasa juu ya yale mazungumzo na yule Mzee. Kuna muda unaweza ukawa umezungukwa na watu wengi, alaf wasiwe na faida, na wale wachache wenye faida pia usiweze kuwatambua. Kutwa nalalamika maisha magumu, michongo hakuna, alaf watu wenye uwezo wa kunipa michongo ndio nawapotezea, Kisha nakumbatia wasio na umuhimu.
Usingizi ulinipaa kabisa. Niliwaza mengi sana, kiasi kwamba nikajikuta namtumia msg yule Mzee kuomba kuonana nae tena siku inayofuata. Sikutegemea anijibu muda ule ule, maana ilikuwa ni karibia saa nane kasoro. Niliendelea kuwaza mambo tofauti tofauti mpaka nilipopitiwa na usingizi.
***** ****** ****** ******
Asubuhi niliamshwa na mlio wa simu yangu, iliyokuwa ikiita. Kuiangalia nakuta Mshua ndio anapiga. Sijui kwanini, ila nilishtuka sana. Nikajikuta naogopa kuipokea ile simu, maana najiuliza anataka kuniambia nini?. Yule Mzee amemwambia kama tumeonana? Au nikipokea nitaweza kuongea na comfortable?. Ushawahi kufanya jambo fulani la aibu sana, alafu ukutane na mtu au watu wanaolifahamu, huwa unapoteza ule uchangamfu mbele yao. Hata katika story utakazopiga nao, wakicheka utahisi wanakucheka ile aibu yako. Hiyo hali ndio nilikuwa najihisi muda huo wakati Mshua anapiga. Kwa mara ya kwanza nikashindwa kupokea simu ya Mshua. Ikaita hadi ikakata.
Nikiwa bado nipo pale pale kitandani, simu ikaanza kuita tena. Nilishtuka kana kwamba nimepigwa shoti ya umeme. Nilishusha pumzi za amani baada ya kuona jina la mpigaji. Ni yule Mzee ndio alikuwa ananipigia. Niliipokea, tukaongea mambo kadhaa, ila akaniambia Kwa hiyo siku hatokuwa na nafasi, lakini pia hata siku zinazofata, bado angekuwa busy. Hivyo akashauri kama alivyoniambia jana, kuwa wik end ndio ratiba yake inakuwa wazi. Tukakubaliana niende tena kule kule shambani kwake, siku ya jumamosi.
Baada ya kukata simu, mawazo yakanirudia tena. Picha ikanijia, ni Kwa namna gani masaa 24 yanaweza kubadili kila kitu. Maana ni ndani ya masaa 24, kutoka kuwa mtu anayeongea na Baba yake kwa vicheko na bashasha, hadi kuanza kumuogopa.
Baada ya masaa kadhaa ya kujivuta vuta pale kitandani, nikaanza kutafakari siku yangu niipeleke vipi. Unajua tatizo la kuwa jobless, ni kwamba unakuwa na muda mwingi sana, ila vitu vya maana vya kufanya ndio hakuna.
Baada ya kuwaza sana, nikaona ngoja niende kule maeneo ya katikati ya jiji, nikamtafute Mzee Dingi. Jamaa alitembea na karibia million 15, huku pakiwa na karibia million 6 ya kina Kisauti, ambayo hakuitolea jasho kabisa. Mawazo yakaniambia nimtafute walau nipate mgao wangu, maana tayari nishatumikia adhabu.
Nikasogea hadi maeneo ya Samora, ila hakuwepo. Nikatembelea vijiwe vyake vyote ila nikaambulia patupu, sielewi nampatia wapi. Kwenye simu bado kaniblock. Nikafikiria kwenda kwa Shani, ila nikaona tutaenda kulumbana, alaf ugomvi uzidi kuwa mkubwa. Nikajaribu kumpigia yule mpenzi wangu, nikakuta bado kaniblock. Nikaamua kurudi zangu home.
** * ***
Zilipita kama siku mbili hivi, Mzee Dingi akanipigia simu.
Mzee Dingi: "Uko wapi Apostle?"
Analyse: "Nipo gheto, vipi?"
Mzee Dingi: "Najua bado una hasira, ila wanaume hatuwekagi vinyongo, njoo tufanye kazi"
Analyse: "Nyie fanyeni tu mtajirike, Mimi Sina mpango na hizo kazi zenu"
Mzee Dingi: "Dogo mambo hayaendi hivyo, hakuna tuzo kwa ajili ya watu wanaopata hela kwa shida. Kazi zipo nyingi, utapata hela, na utasahau habari ya ilo deni unalonidai"
Analyse: "Siwezi fanya kazi alaf nimfaidishe mtu mwingine, nyie fanyeni tu ambao mnawezana"
Mzee Dingi: "Ile ilitokea tu, kwasababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. Safari hii tutakuwa mguu kwa mguu apostle"
Nikajifikiria kwa muda kidogo, nafsi ikawa mguu nje mguu ndani, Sina mchongo town, bills nitazilipa vipi?
Nikamuuliza, "Kuna dili gani sasa hivi?"
Mzee Dingi: "Hayo sio mambo yakuongelea kwenye simu, kesho njoo ofisini tujadiliane kwa kina"
Analyse: "Sina nauli, kama hatuwezi kuongea kwenye simu, Mimi siji"
Hakunijibu kitu, akakata simu. Alafu baada ya kama dakika tatu, ikaingia elfu sabini kwenye tigopesa toka kwa Mzee Dingi, Kisha akaniandikia msg.
"Kesho fanya juu chini uje Apostle. Usiende makao makuu, njoo tawi la kinondoni"
Nikamjibu "Poa"
Unajua kupambana kunaumiza, ila kukata tamaa kunaumiza zaidi. Maana aliyekata tamaa hana dira, anaweza kujikuta anafanya mambo ambayo hakuwahi kutarajia. Story na yule Mzee zilinifanya nikajiona hopeless sana. Nikajikuta nimeridhia kwa moyo mmoja kujiunga na kina Mzee Dingi.
. ***** ***** ***** ******
Kesho yake nikatimba pande za Kino, nikakuta timu ya watu watatu, Mzee Dingi akafanya utambulisho. Nikajiunga nao rasmi.
Tulijadili mipango kadhaa, na tokea siku ile tukaanza kupiga dili kulingana na zinavyokuja. Siwezi elezea in details ni kwanma gani tulikuwa tunafanikisha hizo deals, ni watu gani tuliwapiga au hata kuyataja hayo madili, maana sio lengo la story lakini pia huwezi jua nani anasoma, nisijekuamsha hasira zilizolala.
Tulikuwa tunahama vijiwe kadiri tunavyopiga dili, ili kuepuka kukutana na wale tunaowapiga. Wengi tuliokuwa tunawapiga, michongo yote ilikuwa based on coincidences, ndio maana baada ya kuspend time sana na kina Mzee Dingi, I will never ever believe in coincidence, NEVER.
Baada ya kama miezi miwili au mitatu, Mzee Dingi akaniomba tukutane wawili tu, Mimi na yeye. Tulikutana baa maeneo ya buguruni.
Mzee Dingi: "Apostle kuna mtu anataka kukutana na wewe. Kuna dili limejitokeza"
Analyse: "Ni nani huyo? Na kwanini atake kukutana na Mimi?"atake
Mzee Dingi: "Huyu mtu shoo zake sio ndogo ndogo Apostle. Dili zake zote ni mikia ya kondoo"
Analyse: "Mikia ya kondoo kivipi?"
Mzee Dingi: "Huyu kwa mwaka akipiga dili nyingi ni nne, ila mkwanja unaopatikana hapo, unaweza kwenda likizo muda mrefu, tena kwa mtoto kama wewe, unaweza Kaa hata mwaka bila stress ya kipato, ni matumizi tu"
Analyse: "Duh anaitwa nani huyo Mzee?"
Mzee Dingi: "Jina lake la kazi tunamuita Kesho Yetu"
Analyse: "Kwanini sasa anataka kuonana na Mimi?"
Mzee Dingi: "Wewe fanya mpango kesho tuonane nae pale Kinondoni, kuna dili analeta, linahitaji watu kadhaa, na wewe ametaka uwepo"
Analyse: "Ananijua kwani?"
Mzee Dingi: " Ndio anakujua, ameona kazi kadhaa ulizoshiriki, uchangamfu na usharp wako ndio anautaka"
Nikaguna pale, ila mwisho wa siku tukakubaliana, kesho yake tukutane pale Kino...
***** ****** ****** *****
Kesho yake asubuhi na mapema nikatimba Kinondoni Manyanya. Nikamcheki Mzee Dingi, akanielekeza walipokuwa wamekaa. Yupo yeye, mwanasheria feki, na Mzee mwingine ambae ndio ilikuwa mara ya kwanza namuona, kwa jina la kazi alikuwa anafahamika kama Kidevu.
Kitu kingine nilichonote, hawa jamaa wote hakuna aliyekuwa anafahamika kwa jina lake halisi. Na hiyo ndio sababu ilifanya Mimi niwaache waendelee kuniita apostle. Na kingine hakuna aliyekuwa anajulikana anapokaa. Kiufupi, ingetokea mmoja akakamatwa, angeishia kutaja majina ya apostle, Mzee Dingi, Kidevu au Kesho Yetu. Akiambiwa akaoneshe wanapokaa hao watu, wangezunguka Dar nzima.
Baada ya utambulisho. Mchongo mzima ukawekwa mezani. Kulikuwa na mwalim mstaafu ametoka kuchukua mafao yake. Yule mwalim alikuwa anahitaji eneo kubwa kwa ajili ya mradi wake wa green house aliotaka kuuanzisha. Lakini pia, alikuwa anahitaji vifaa kwa ajili ya umwagiliaji, na kuchimbiwa kisima kwenye ilo eneo atakalo nunua. Sasa mpango ilikuwa apigwe kwenye eneo, alafu dili likisha kamilika, apigwe kwenye vifaa na uchimbaji.
Mzee Dingi yeye alitakiwa kucheza kama dalali wa eneo linalouzwa, mwanasheria feki na yule Mzee Kidevu, wao wawe majirani, Mimi nikaambiwa niwe kama afisa mtendaji au mwenyekiti wa kile Kijiji. Mzee Dingi ananiambia:
"Wewe apostle inabidi uwe mtendaji wa kile Kijiji. Unajua watendaji wengi ni vijana na wasomi. Ni rahisi yule Mama kuamini"
Nikabaki na mwangalia tu. Akaendelea
"Yule Mama tukishamaliza kuuziana nae kiwanja, itabidi hapo hapo wewe (Mimi) kama mtendaji umwambie unaweza kumsaidia kutafuta kampuni ya uchimbaji visima, na kuweka set up nzima ya kila kitu kwa ajili ya project yake".
"Yani inabidi tukimaliza tu kulipana hela za kiwanja, malipo ya hizo process zingine yafatie. Kuna watu tutakuunganisha nao ambao ndio utaendelea nao kwenye hiyo nngwe ya pili"
Wakati tunaendelea kuongea pale. Kuna Mzee mwingine akaja, yuko smart, kabeba begi muundo wa briefcase au zile za kubebea laptop. Yule Mzee sidhani kama kuna mhuri ambao hana. Kibriefcase chake Kiko full, mihuri, Karatasi, Calculator nk. Akatoa mihuri kadhaa akaiweka mezani. Eneo ambalo alitakiwa akauziwe yule mstaafu, lilikuwa vigwaza. Huyu Mzee smart aliyeongezeka, ndio Mzee Dingi akanitambulisha kwake kama 'Kesho Yetu'. Huyu ndio alikuwa mastermind wa huu mchongo wote, na ndiye aliyetakiwa kuact kama muuzaji wa eneo. Na Kwa mujibu wao, tulitarajia kati ya million 50 mpaka 70, kutegemeana na namna tutakavyofatisha maelekezo ya Mzee Kesho Yetu.
Kila kitu kikawekwa sawa, then yule mstaafu akapigiwa simu, na makubaliano yakafikiwa kuwa kesho akalione lile eneo.
Unajua sometime unaweza Sikia story mtu katapeliwa,alafu ukaanza kumcheka na kumuona mjinga, ila huyu Mzee Kesho Yetu alinibadilisha mtazamo wangu. Mtu akitapeliwa, usimlaumu sana, peleka sifa kwa yule aliyemtapeli. Watu wana mahesabu makali sana, jinsi huyu Mzee Kesho Yetu alivyokuwa anapanga mambo, accuracy yake ni almost 100%. Kinachotakiwa ni kufatisha maelekezo yake tu.
Na hata dili nyingi ndogo ndogo tulizokuwa tunafanya na kina Mzee Dingi, zilikuwa zinatoka kwake zikiwa na full deatils ya kuzipush. Yeye alikuwa anapewa percent fulani ya mgao, alikuwa hashiriki. Ukiona kashiriki, basi ilo dili liko very serious, na target sio chini ya million 50. Na hata hii deal nilidhani usharp na usmart wangu ndio ulifanya anielewe na kuniunganisha kama jinsi Mzee Dingi alivyoniambia, lakin kumbe alikuwa na sababu ya tofauti kabisa. Kitu ambacho sikuwahi kukifikiria kabisa, ila yeye kwa upande wake alishakifikiria miezi mingi iliyopita. Na jibu alilipata ni "Apostle". Nilikuwa funguo yake bila hata ya Mimi mwenyewe kujua.
Tulivyoagana, wakati wengine washaanza kuondoka, nikamsimamisha Mzee Dingi.
Analyse: "Mzee hii deal inahusisha sura ngeni nyingi, na pia hela yake ni ndefu, kuna kila dalili ya kudhurumiwa hapa"
Mzee Dingi: "Apostle unaongea nini wewe?. Hakuna wa kukudhurumu hapa"
Nikamsikiliza tu, lakini sikuwa na amani kabisa.
Tukaagana nikaamsha. Mida ya jioni jioni, Mzee Dingi akaniwekea laki mbili kwenye simu. Kisha akanipigia
Mzee Dingi: "Apostle najua utakuwa na uhitaji wa hela, chukua hiyo, piga ua kesho inabidi utokee"
Analyse: "Tunakutania wapi?"
Mzee Dingi: "Wewe na wale wengine mtatangulia asubuhi sana. Mimi nitakuja na yule mlengwa baadae."
Analyse: "Poa poa"
Mzee Dingi: "Maelezo ya ziada utayapata kule kule, hakikisha unakuwa smart sana, usisahau begi lako"
Analyse: "Sawa nimeelewa "
Alivyokata simu tu, Shani akanipigia
Shani: "Uko wapi we Mtu?"
Analyse: "Nipo gheto tu"
Shani: "Naona umenisusa tokea siku ile. Mimi nishakumiss"
Analyse: "Me nipo"
Shani: "Unaweza kuja kwangu muda huu? "
Analyse: "Poa nakuja"
Shani: "Ndio maana nakupenda, huwekagi vitu rohoni. Haya njoo nakusubiri"
Nikaenda kuoga, ili niende.. ..
[Mimi pia nimejisikia vibaya
Shani Ni shangazi anayetaka kuzaa😂😂😂Mstaafu mwenyewe Shani🤣🤣
Blood ilikuwa wapi hapo? Labda tu hiyo sweet, sweat and tearsBadilisha title isome "blood, sweat and tears"
fupi au umefakamia kwenye usomaji,, ungesoma taratiiibu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Khaaa!!!!! Mbon'fupi sana? [emoji17]
Hii part ya mchagga imenichekesha kama mwehu[emoji23]3rd Portion:
... Maelezo ambayo nilikuja kupewa baadae na head prefect, ni kuwa inaonekana mshua alinitafuta sana kwenye simu kabla hajaenda pale shule, ila hakufanikiwa kunipata. Kwavile hatujawasiliana muda mrefu, na akisema arudi kijijini, maana yake utapita muda mrefu mwingine bila kuonana, ndio akaona afunge safari mpaka shule. Kufika pale akajitambulisha kama mzazi wangu, na akaomba kuonana na mimi. Walim wakashangaa, mzazi wake Analyse?, Wewe ni baba yake mkubwa au mlezi? Dingi akawa hajaelewa. Akawaambia yeye ni Mzee wangu kabisa, Mwalim wa nidham akaona mshua anamletea masihara, ili swala la wanafunzi kuleta wazazi feki inabidi likomeshwe, akamwambia Mzee akae kwenye benchi. Baada ya kushauriana na mkuu wa shule, wakataka kumpeleka Mzee Polisi. Mshua akawakazia, walivyoona yupo serious sana, wakamuomba ID yoyote.
Akawapa voters ID, walivyoona mfanano wa majina, walim wakachoka. Ikabidi waanze kuulizana, kama wewe ndio baba yake, yule aliyekuja nae ni nani? Hapo ndio wakampa picha nzima. Mzee akacheka (Mzee wangu akiwa na hasira sana, kuna kicheko fulani kinakujaga automatically). Mwisho wa siku wakaazimia head prefect awe ananipigia simu mara kwa mara, akinipata, anipe zile taarifa za kuhitajika shule kwa ajili ya usajili. Na ahakikishe ananishawishi niende na mzazi niliyempeleka last time.
Walimu walikuwa na shauku ya kuniona Mimi maana nimecheza na akili zao, ila Mshua target zake ilikuwa ni kumuona yule mzazi niliyempeleka badala yake. Mwamba Sina ili wala lile, kesho yake nikapanda Simba Mtoto, safari ya shule ikaanza. Nilivyofika, nikaunga moja kwa moja mpaka nguvu mali, nikapoa kwa mshikaji wangu pale Galanosi, kesho yake asubuhi, tukabebana Mimi na yule Mchaga hao mpaka shule.
Ile shule ilivyo, ukishaingia kupitia main entrance, unakata upande wa kulia, ndio kuna ofisi za walim pamoja na head master. Upande wa kushoto, kulikuwa na korido inayoelekea madarasani, lakini pia mwanzoni kuna njia ya kwenda vyooni, na ngazi za kuelekea madarasa ya juu. Sasa kwenye hizi ngazi ndio alikuwa kakaa Mshua ananisubiria Mimi na baba yangu tufike. Na sisi tulivyofika, direct tukakata kona kulia, hatukuangalia nyuma. Mzee akatuungia tela mdogo mdogo. Machale ni kama yalinicheza hivi, nikapata hisia zinaniambia geuka nyuma, kugeuka nakutana na Mshua kakaza sura kimtindo, mikono yote miwili kaikutanisha nyuma ya makalio, kama wanavyopendaga kutembea wazee. Alipoona nimegeuka, akasimama kwa muda Nikapatwa na mshtuko, maana sikutarajia kumuona pale, nikajikuta nimeita "Baba?". Yule Mchaga alikuwa bado hajausoma mchezo, akaitikia "Naam jembe langu". Ila alivyogeuka, na kukuta nimeelekeza attention kwa mtu mwingine, akili yake ikaload faster, akajikuta anatukana kichini chini "Ku***na walai".
Mshua akawa anamuangalia tu, huku kaweka tabasam la mamba. Mchaga akapiga hesabu za haraka, akaona hapa akiingia ofisini, basi hatoweza kutoka, anaweza akaishia polisi. Akapitisha wazo la kutoweka eneo lile, ila njia peke rahisi ni kupitia upande aliosimama Mshua, pia japo shule haikuwa na fensi, ila kukimbilia upande waliopo wanafunzi inaweza ikawa msala zaidi, maana wanafunzi hawana dogo. Akaamua kurudi na njia tuliyojia, upande aliosimama Mshua. Kosa alilofanya Mchaga, alim-underestimate Mshua, labda alijiona yeye kijana zaidi akijilinganisha nae, so angemzidi nguvu. Mchaga alitoka speed ghafla, mshua akawahi kumrukia, wakavaana mpaka chini. Kitendo cha kuanguka chini tu, Mshua kama kawaida yake, akamuwahi Mchaga na kabali moja matata. Mchaga kila akirusha ngumi, Mshua hana habari, ndio kwanza anazidi kukaza mikono. Wanafunzi wakajaa madirishani, kelele zikazagaa eneo lile, wengine wakaanza kutoka madarasani kuja kushuhudia kwa ukaribu.
Walim ikabidi waanze zoezi la kuwaachanisha, walipofanikiwa, Mchaga macho yalikuwa mekunduu kama katoka kulala au kulia. Walim wakawa wanafukuza wanafunzi warudi madarasani, Kisha wakawaomba Baba na yule Mchaga waende ofisini kwa mazungumzo, maana kwa umri wao haifai kushikana mashati namna ile. Wakiwa wanakaribia mlango wa ofisi ya walim, yule Mchaga aligeuka, akatoka speed, akaelekea upande zilipo hostels za wanafunzi wa advance, akapita kwenye senyenge, alivyotokea upande wa pili, akaongeza speed, akapotelea kwenye makazi ya watu. Hakuna hata mwalim aliyejisumbua kumkimbiza, wakabaki wanamwangalia tu. Ila wanafunzi ndio wakawa wanamzomea. Jamaa akasepa, msala nikabaki nao peke yangu. Kikao kikafanyikia ofisi ya walimu wote, mwanenu nikapigishwa magoti huku nasemwa..
Ubaya wa ofisi ya walimu, hata yule mwalim ambae hakujui, lazima apate cha kukuongelea. Nilitembezewa fimbo za kufa mtu siku ile, japo mshua hakunipiga, ila alichangia pakubwa sana kuikuza adhabu yangu, maana aliongea mengi sana, kiasi kwamba nikaonekana kituko. Mshua alilipa ile hela ya faini, nikaruhusiwa kwenda darasani. Aliamua kuondoka siku hiyo hiyo, hakujisumbua kuongea na Mimi baada ya kutoka mle ofisini, na hakunipa hata shiling 10 Kwa ajili ya matumizi pale shuleni. Kiufupi aliniacha kikauzu sana. Nimeingia class sina mzuka hata kidogo, mda wote nimelala kwenye dawati. Mida ya mchana baada ya msosi, nikaamsha zangu kuelekea hostel. Nikalala mpaka mida ya jioni.
Wakati natoka kula msosi wa usiku shuleni, yule jamaa yangu wa Galanosi akanipigia simu, anauliza nimemfanya nini Mchaga? Maana kakutana nae ana nundu kwenye kona ya uso, alaf kamuahidi kwamba siku akikutana na Mimi, sitokaa nimsahau maishani mwangu kwa atakachonifanya. Ikabidi nimuelezee kwa ufupi yaliyojili. Jamaa alicheka sana, mwishowe akaniambia nikienda shuleni kwao niende kwa tahadhari, maana Mchaga alimaanisha alichokisema. Tukaishiana hapo, then nikaenda chamber kupiga msuli. Tokea siku ile nikaanza kupiga sana msuli, sikuwa na msala mwingine wowote, japo walimu waliendelea kuwa wananizingua hapa na pale, ila niliamua kuwa mpole.
Mshua hakuwahi kunitafuta tena, sio kwa simu wala msg. Ni kama alinizila. Kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa mwisho, nikaanza kumfukuzia demu mmoja wa O level pale pale shuleni, alikuwa mweupe, sauti nyembamba na kishundu fulani cha kuvunjia shingo, maana akikupita lazima ugeuke. Siku moja nimekaa nae maeneo ya garden mida ya jioni, naendelea kuingizia mistari, maana alikuwa bado hajaeleweka. Katika maongezi akaniambia "Wewe hapa Tanga sio kwenu, unasema unanipenda, wakati siku sio nyingi utamaliza shule, utaacha umenitumia alafu utaondoka".
Nikamjibu kuwa mgeni Tanga hainizuii Mimi kumpenda yeye, umbali sio kikwazo kwangu. Akaniuliza "Unamaanisha unachosema? Kuwa utarudi kwa ajili yangu?, Niambie ukweli, sitaki uongo". Nikasita kidogo kutoa jibu, yeye akaendelea "Mimi ninachohitaji kujua ni Nia yako tu, kama kweli utataka kurudi, mimi nitakurudisha". Ile kauli ikanimakinisha kidogo, nikamuuliza "Utanirudisha kivipi? " Akajibu "Wewe ilo niachie Mimi, je ni kweli unanipenda na ungependa kurudi kwa ajili yangu, nikurudishe??
Nikabaki nimeduwaa kwa muda, najiuliza "Huyu anaongelea nini?".....
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Shukrani Apostle
Mtaafu asije kuea yule rafiki ake babaake. VitaumanaYaani nimemwonea mstaafu huruma,jamani pata picha Ni wewe au mama yako,naomba kimoyomoyo deal lisifanikiwe
Shukrani Apostle
Hii strory yako ina mengi sana ya kujifunza!!
Wacha niendelee kuchukua notes!
Huchelewi kulewq na sifa ukaanza kutusumbua unaleta baada ya wiki kujifanya unasafiri kikazi😀 kazi yenyew ni kumridhisha ShaniHapana bhana. Mimi nitaweka kila siku mpaka ifike mwisho. Wala usiwe na shaka 😅😅😅
@Analyse anapenda mishangaz [emoji23]Huchelewi kulewq na sifa ukaanza kutusumbua unaleta baada ya wiki kujifanya unasafiri kikazi[emoji3] kazi yenyew ni kumridhisha Shani