Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu, mpaka siku niliyokutana na yule Mzee

1st Portion:

Kama ilivyo kwa wazazi wengine, wazazi wangu pia walikuwa wanatamani sana kijana wao nisome shule. Kile kitendo cha kuishia njiani, kwa upande wao hakikuleta taswira nzuri. Pamoja na mengi yaliyokuwa yamejitokeza, Bado tamanio lao la kuona naenda shule liliendelea kuwepo. Kitendo cha kukaa nje ya mfumo wa elimu, nilijiona kama vile regular education ishanitupa mkono, sana sana nilikuwa nafikiria kama nitaenda kusoma, basi walau iwe mafunzo ya ufundi, sikutaka kukaa darasani tena.

Ila kwa upande wa wazazi, hasa Mshua, yeye alikuwa anatamani niendelee na advance, maana sikuwa nimefeli O level, na yeye hakushindwa kuniendeleza, ni ile kiburi cha kitoto ndio kilitibua mambo. Ilifikia hatua nikiwasiliana na mshua, pakitokea quarrel ya aina yoyote, lazima swala la elimu liingiziwe, hata kama mada aihusiani. At last niliamua ngoja nirudi shule tu. Nilivyowafikishia ile taarifa Mshua aliipokea neutral, haoneshi kama kafurahi au la. Ila alikubaliana nayo.

Tokea nimalize form 4, ulikuwa umepita muda kiasi, Mshua alipata tabu kunipatia usajili katika shule ya serikali. Nakumbuka Mshua alikuwa muda wote ni kuongea na simu tu, mara kapiga huku, mara kule, mara kaenda kukutana na mtu huyu au yule. Maana mfumo wa government ulikuwa unanikataa. Option ya kwenda shule za private ilikuwepo, ila sikuelewa kwanini Mshua alikuwa analazimisha nisome shule ya serikali. Alifosi sana anavyojua yeye, hatimae nikafanikiwa kupenyezwa kwenye shule ya serikali, japo nilianza kwa kuchelewa takriban miezi mitatu.

Binafsi nilikuwa sitaki kusoma nje ya Dar, wakati mshua yeye alikuwa anaamini, nikipata shule Dar sitosoma. Kwahiyo aliniwahi na kauli moja, kama sitokubali kwenda kwenye shule itakayopatikana, basi nitarudi kwenda kusomea kule kijijini walipo. Sikuwa na namna. Hatimae nikabahatika kusajiliwa katika shule iliyokuwa pale mkoani Tanga.

Changamoto na Mzee wangu Bado ikarudi pale pale, kwenye swala la combination. Mzee yeye anasema nisome zile za Arts, binafsi sikuwa na mpango nazo. Tena kuonesha Yuko serious, kabla ya kwenda rasmi shule, alininunulia vitabu kadhaa vya language na Kiswahili. Mshua yeye alikuwa anaamini kwavile napenda kusoma vitabu, basi njia sahihi kwangu ni Arts. Ila kwa upande wangu, kusoma vitabu ni hobby tu. Sikutaka kubisha, nikavipokea, nikaenda shule rasmi shule.

Kitu cha kwanza nilichofanya baada ya kupokelewa pale shuleni, ilikuwa ni kutaka kujua combi zinazotolewa pale. Palikuwa na PCB, PCM, CBG na HKL tu. Nikaanza mchakato wa kuomba kubadilishiwa combination . Baada ya kuzungushwa sana, mwishowe nikauvagaa mziki wa PCM. Nilivyompa taarifa mshua, kwa mara ya kwanza Mshua akanitukana, kisha akaniambia "Hivi unajua nimepoteza hela kiasi gani mpaka wewe umepata hiyo nafasi, au unadhani nina hela za kuchezea?". Kila nikijaribu kujitetea, ananicrash, mwisho wa siku akaniambia "Unatumia nguvu sana kutaka kuniletea aibu kwenye familia, sasa Sikia ukipata zero nisikuone tena hapa kwangu"

Tukaishiana hivyo.

***** ****** ** ***

Nilipata tabu sana pale shuleni, sana yani. Ile miezi 3 ya mwanzo ilikuwa kama miaka mitatu. Kila walim wakitangaza kuna test, nakosa amani kabisa, maana kama sijawa wa mwisho, basi ni wapili kutokea mwisho. Kuna jamaa alikuwa anaitwa Athuman au Ochu, huyo ndiye tuliyekuwa tunapokezana nafasi mbili za mwisho, akidoji test ya namba, basi ujue mkiani nitakuwa Mimi. Hapo kipindi Mimi shule naiona kama gereza, kuna wadau wanafanya solving kwenye nekta ya form 6, na maswali yanawatii. Kuna jamaa mmoja nikamganda sana awe ananikatia mapindi, maana kidogo alikuwa njema. Alivyojua Sina topic yoyote ambayo nimeshasoma, alinishangaa sana, akaniambia "Dogo hii ni PCM, hatuji shule kichwa kichwa". Huyu jamaa ndio alikuja kunionesha mchikichini, na hapo ndio nilikutana na watu (walimu) ambao walinibadilisha kabisa, walioniondolea aibu na fedhea darasani (mmoja kwasasa ni marehemu, Mungu amlaze pema).

Nilipoingia form 6, nishakuwa mwenyeji sasa pale Tanga, hakuna ratiba ya baikoko ambayo nilikuwa siijui. Hakuna malaya wa Chichi na La Cassa ambae nilikuwa simjui. Wamama hao ndio usiseme, Ijumaa mpaka Jumapili nilikuwa sionekani kabisa maeno ya hostel. Na baadhi ya Jumatatu, nilikuwa naenda shule kutokea nyumbani kwa Mama Mariam.

Nilijikuta nahitaji sana hela, ili kuweza kukeep up na movements zangu. Nilikuwa na jamaa yangu mmoja wa karibu sana, yeye alikuwa ni mzawa wa kule kule, aliitwa Ochu. Jamaa alichoresha mchoro, tuibe mahindi kwenye store ya shule, walau yatupatie vihela kadhaa tukiyauza.

Lile deal lilienda vizuri, maana tulikuwa tunahamisha mahindi kidogo kidogo, then tunaenda kuyahifadhi kwa bi mkubwa ambae mumewe ndio tulipatana tumletee gunia moja. Bahati mbaya, yule Mama akajikuta raia mwema, akavujisha ile issue kwa Mwalim. Siku hiyo kama kawaida tumejaza mahindi kwenye mabegi tunapeleka kwa jamaa, tunakuta Mwalim anatusubiria. Akatulaza kituoni, then kesho yake kesi ikasomwa assembly.

Tukala stick mbele ya umati. Kisha tukapewa suspension ya miezi 3, tukirudi tuje na wazazi pamoja na hela ya fine.

Issue inaanza, ni mzazi gani nitamuita? Mama hawezi kuja, Mshua yuko mbali sana na pale, lakini hata ingekuwa karibu nisingeweza kumwambia ule ujinga. Kwa upande wa mwanangu Ochu, wiki kama 2 zilizopita alikuwa na msala home kwao, kwahiyo alikuwa kwenye kipindi cha tahadhari, so hakuweza kuwaambia home kwao, japo yeye ni mzawa wa pale. Mwisho wa siku tukaadhimia tuite wazazi wa kukodi, japo mwana yeye lile wazo hakuliafiki hata kidogo. Hostel za ile shule niliyokuwa nasoma, zilizopo nje ya shule, zilikuwa opposite na vijumba fulani vya mbao, vimechoka sana, walikuwa wanaviita Kijiji Cha 21 (kama sijakosea), sasa mwanangu Ochu ndio akaenda kuchukua Mzee mmoja pale, aende akaigize kama baba ake mdogo. Siku ambayo Ochu alienda na baba ake mdogo feki, na Mimi nilienda kwa dhumuni la kuomba niendelee na masomo, mzazi wangu yupo njiani anakuja. So wakati tumesima pale, Mwalim wa nidham akamuuliza yule baba mdogo feki wa Ochu amekuja pale kwa dhumuni la nani? Yule dingi akasema yeye amekuja kusikiliza kesi ya Ochu, Mimi hanifahamu.

Mwalim: "Mzee umekuja kwa ajili ya nani hapa? Au wote?"
Mzee : "Nimekuja kwa ajili ya huyu (akimnyooshea kidole Ochu"
Mwalim: "Mwanao anaitwa nani?
Mzee: "Ochu.... , Athuman"
Mwalim: "Athuman nani?"
Mzee : Akawa Kimya. Mwalim akarudia tena swali, ila Mzee kimya.
Mwalim: "Una uhusiano nae gani?"
Mzee: "Mtoto wa kaka angu"
Mwalim: "Huyo kaka ako anaitwa nani?"
Mzee: (kimya)
Mwalim (akamnyooshea Ochu kidole) : "Haya, wewe na baba ako, ondokeni mkaje na baba enu"

Kisha akanigeukia na Mimi, wewe pia ondoka, bila mzazi nisikuone hapa.
Nikatangulia Mimi kutoka, wakanifata kina Ochua, hao tukaenda nje ya shule. Hapo tayari nishaingia ubaridi, maana sioni namna naweza kumwambia mshua aje.

Baada ya kama wiki hivi ya kuzurura zurura pale mjini, nikaenda sehemu moja inaitwa Nguvu Mali, kule kulikuwa na jamaa yangu anasoma Galanosi. Nilivyomuelezea msala wangu, akasema atanikutanisha na jamaa mmoja hivi, mchaga, ambae alikuwa na biashara yake karibia na maeneo ya shuleni kwao. Huyo mchaga, alikuwa anatumiwa sana na wanafunzi wa Tanga Tech kwenye misala kama hiyo. Kwa ufupi alikuwa mbobezi (kwa maelezo aliyonipa jamaa yangu)

Basi alivyonikutanisha nae, ikabidi nimpange issue ilivyo, kwamba kuna kesi ya uongo na kweli nimepewa huko shuleni, akaniuliza maswali mawili matatu, pia nikamuelezea jinsi Ochu alivyoumbuka ofisini, yule jamaa akacheka tu. Akasema hayo mambo madogo, kesho kutwa ntakuja. Wakati nataka kuondoka, akaomba advance 10k, maana tulipatana 25k.
Nimejilazimisha kusoma na nimetokea kuielewa,sasa isiwe ndefu saaaaaaaaanaaa.
 
2nd Portion:

... Ilivyofika siku aliyosema ataenda pale shule, niliwasiliana nae mapema tu asubuhi, akaniambia nitangulie shule, anikute ofisini.

Nikasubiria wanafunzi wengine wametoka assembly na kuingia madarasani, Kisha mdogo mdogo nikaingia eneo la shule. Kufika ofisini, Mwalim ananiuliza umefata nini bila ya mzazi?. Nikamjibu kuwa baba Yuko njiani, amesema anikute ofisini. Hapo namjibu, ila nina hofu ya kutosha, kwanza sielewi yule mchaga akija atasema Nini, tusije umbuka kama Ochu. Sasa ile hofu niliyokuwa nayo, ikamhadaa Mwalim, akaona kijana nipo serious, nimeshikika. Nikaambiwa nikae kwenye benchi nje ofisi pale.

Kama dakika 45 hivi, mchaga hatokei. Head Master akanimind, walim nao wakaanza kunisema (siunajuaga walim wakiwa wengi ofisini). Ghafla naona yule mchaga kaja, begi lake mgongoni kama vile katoka safari. Kufika karibu, akapokewa na head Master. Wakati wanasalimiana, nikageuza shingo ili nimsalimie, maana alinipita wakawa kama wamesimama nyuma yangu. Kumbe wakati nageuka, nae alikuwa ameplan kunipiga kofi, kwahiyo kile kitendo cha kugeuka, nilikutana na kofi Kali la uso, hadi nikachanika kidogo mdomo wa chini.

Hata Head Master hakuwa ametarajia lile swala, akawa ameshtuka, akamuuliza "We Mzee unafanya nn? Hebu tulia, usije kusabisha majanga hapa"

Yule mchaga akamkunjia sura Head Master "Huyu ni mwanangu, Nina haki ya kufanya lolote". Head Master akavunga. Mchaga akaomba taarifa kamili ya kilichotokea, akakaribishwa ofisini kwa Mkuu. Kikao kikaanza, Mchaga, Mkuu, Mwalim wa nidham, pamoja na Mwalim aliyetushika siku ile. Muda huo nimepigishwa magoti. Mchaga akaelezwa issue nzima ilivyokuwa. Alikuwa amekaa, akasimama kwanza, akawa kama anataka kutoka nje ya ofisi, alafu akarudi. Walim wanamtuliza "Mzee hebu tulia kwanza" alaf mkuu akamuagizia maji walau yamsaidia kupunguza presha. Yule dingi baada ya kunywa maji, aliinama kama dakika 5 yupo kimya tu. Baada ya hapo akaomba fimbo. Alininyuka hadi fimbo ikaisha, akaanza kunipiga makofi. Walim wanafanya kumzuia.

Sijawahi kupatwa hasira kama niliyopata siku ile, maana alinibutua sana, alaf sikuwa na lolote ninaloweza kufanya. Maana ningemdindia, maana yake msala wa kuleta mzazi ungeendelea kuwepo. Mwisho wa siku wakayaongea pale, nikapungiziwa adhabu, badala ya miezi mitatu, nikaambiwa nirudi baada ya mwezi mmoja na nusu alaf siku ya kuripoti nije na 150k kama faini.

Tukatoka nje ya shule, mdogo mdogo tukaizunguka shule, tukachukua uelekeo zilipo hostel za nje. Kwenye zile hostel ng'ambo ya barabara kulikuwa na bustan, tukaenda kukaa pale. Hapo njia nzima tupo kimya, hakuna anayeongea, maana nilitaka kuongea akaniambia nitulie, tutaongea tukifika. Sasa tumefika pale, cha kwanza kuniambia "Pole sana kijana, wale ni watu wazima, kugain trust yao sio kazi ndogo"

Nikawaka, "hata kama, sio unipige vile". Mchaga nae akawaka "Kwanza uliniongopea, ulisema kesi ya uzushi, kumbe umeiba mahindi ya shule? Sasa unataka wenzako wafe njaa?" Nikaanza kujiuliza huyu jamaa vipi, mzima kweli? Mchaga akaendelea "Watoto kama wewe ndio wanasababisha watoto wetu wanafeli, mnaenda shule kusumbua wengine, kama hutaki shule acha, ila usiwape wakati mgumu watoto wa wengine, kwanza naomba hela yangu iliyobaki".

Yani kunipiga kote kule, Bado unataka hela nyingine? Akaniambia "Dogo sijaja Tanga kusoma kama wewe, nimekuja kutafuta hela, usijitoe akili, ntarudi shule nikakuharibie". Nikaona isiwe kesi, nikatoa 20 nikampa akate 15k, mchaga akasema hapa hairudi chenji, ile 25k ilikuwa ni makubaliano kwavile ulisema wamekusingizia kesi, ila ungeniambia ukweli, dau lingepanda.

Nikataka kubisha, ila sikuona dalili za kuipata hiyo elfu 5, so ikabidi nipigie kimya tu. Akaniambia "Usihudhunike sana, nimekusaidia sana, tena next time nitakupunguzia, sitokufanyia Bei kubwa, tushakuwa wana". Nikaona huyu Mzee mbona kama ananichulia? Next time ipi?. Akaniuliza shule unamaliza lini kwani? Nikamjibu mwakani. Akatabasam kidogo, Kisha akaniambia "Kwa jinsi ninavyokuona, ni mbali sana, tunza namba yangu utanihitaji tena kabla hujamaliza shule". Akaamsha.

Alivyoondoka, nikaanza kujiuliza huo mwezi mmoja na nusu naumaliza vipi bila sehem rasmi ya kuishi? Maana sikutakiwa kuonekana hostel. Na kwavile Mzee ameshakuja, hivyo walim wanaamini nitaondoka nae, hakuna mzazi anayeweza kumuacha mwanae arande rande tu. Nakusema kukaa kwa mwanamke mwezi na nusu, bila kuwa na hela, isingekuwa rahisi.

Nikafikiria kwenda kwa ule mshangazi wangu wa buguruni sokoni, ila nikaona nitapoteza. Nikajikuta out of options, ikabidi niamue kurudi Dar kwa muda. Dar sikuwa na sehemu ya kufikia zaidi ya kwake. Hata hivyo sikuwa na mpango wa kukaa sana pale, baada ya kama siku 4 nikapanda bus kwenda Mbeya, kuna jamaa yangu nilikuwa nafahamiana nae mtu wa migodini, sema sio mchimbaji, yeye anafanya biashara ndogo ndogo kama kuuza sigara, bangi, mirungi, boxer n.k

Kitu ambacho najilaumu mpaka sasa, ule muda niliokuwa nimepewa suspension, walau ningeutumia kupiga pindi mchikichini, au hata kujisomea, ndio kwanza nazurura. Nikafika mpaka Mbeya, then nikachukua gari za kunifikisha Songwe, kule nilienda sehemu moja inaitwa Ngwala, jamaa ndio alikuwa kule. Nilivyofika, sikukaa siku nyingi, jamaa akasema kwa kipindi kile, pale hakuna hela, akasema twende kwenye migodi mingine tucheki harakati. Tulikuwa tunazunguka na kukaa sehemu kutegemeana na movements za wachimbaji. Ukiachana na uuzaji wa zile bidhaa, lakini pia sometime nasi tulikuwa tunajumuika na wadau wengine waliokuwa wanachambua chambua mabaki ya mchanga wa madini, au pia kufanya kazi zingine zinazojitokeza. Makapi makapi tuliyokuwa tunaokota na kuuza, yalikuwa yanatupa vihela viwili vitatu vya kusogeza siku.

Ubaya wa migodini, kuna watu tangia wameenda kule, hawajawahi kurudi makwao, kibaya zaidi wengine hata hawajulikani kwa majina yao halisi, ni mwendo wa nicknames tu. Nakumbuka kuna mwamba mmoja aliugua hadi akafa, ila hakuna aliyekuwa anamjua ndugu yake hata mmoja. Jamaa ilibidi azikwe kule kule tu, unaweza kuta ndugu zake mpaka leo wanaimani ndugu yao kaenda kutafuta, atarudi, kumbe jamaa hadi kuoza ameshaoza tayari. Lile tukio lilinifikirisha sana, itakuwaje likinitokea Mimi? Ndo yale mambo, unaangalia zako taarifa ya habari, unasikia kifusi kimefunika watu machimboni, mzazi unachukulia kawaida, unawapa pole wafiwa, ukiamini mwanao yeye yupo shule, kumbe ni miongoni mwa majeruhi au waliofukiwa.

Katika uokotaji kwenye yale mabaki, kuna siku jamaa yangu alibahatisha kajiwe fulani hivi kadogo. Kwavile Giza lilikuwa lishaanza kuingia, tukaamua kwenda kumcheki yule anaeyanunua, tupate hela ya kula then tulale. Jamaa kale kajiwe alikachukua kwa milioni mbili na nusu. Nikamwambia jamaa silali huku leo, naamsha usiku huu huu. Tukachukua pikipiki zikatupeleka mpaka center, lengo ni tulale pale, alaf asubuhi tuchukue gari za kutupeleka mjini. Mpaka muda huo, ile hela tulishagawana pasu kwa pasu, kila mtu anayake.

Kufika center, tukachukua room moja kwenye bar tuliyofikia. Jamaa yangu ni mtu wa tungi, so after kuoga, akashauri tuchukue bia kadhaa tunywee room. Binafsi sikuwa mnywaji pombe, ila nikaona sio kesi, jamaa kaagiza Serengeti, Mimi nikachukua safari 5 tu maana sikuwa mzoefu, tukarudi gheto. Ila binafsi sikuwa na amani kabisa, maana yule jamaa ni mzoefu, nikahisi naweza nikalewa, alaf akapita na hela zote nisijue nampatia wapi. Maana tumefahamiana kwenye harakati tu, tena niliunganishwa na jamaa mwingine ambae ndio alikuwa rafiki yetu wote. Nikawa namtegea jamaa anywe, ila nae akauchuna. Ananiuliza "Mbona hunywi?", Namjibu nitakunywa. Kiufupi mpaka kunakucha, hakuna aliyegusa bia hata moja, kulala yenyewe ilikuwa unasinzia kidogo, then unashtuka. Kulivyokucha, Mimi ndio nilianza kuondoka, maana safari yangu ilikuwa ndefu, nilitaka niunge Dar moja kwa moja, bia zote nilimuachia yeye.

Mbeya mjini, nikaweka kiasi cha zile hela kwenye account, then nikachukua chuma ya kwenda Dar. Hapo ni mwezi mzima unaenda kuisha tokea nitoke Tanga. Baada ya kufika Dar, plans zangu ilikuwa nikanunue materials alaf hizo siku chache nikazimalizie Galanosi kwa jamaa yangu. Nikiwa ndio bado nazunguka kwenye centers tofauti tofauti kununua past papers, Mshua akanipigia simu. Tukaongea fresh, akaniuliza maendeleo, nikamjibu kila kitu kinaenda vizuri, baada ya story mbili tatu tukaagana.

Usiku huo huo, akanipigia simu head prefect kwamba kuna usajili unaendelea pale shuleni kwa wanafunzi wa kidato cha 6, hivyo nifanye mpango niende haraka. Akaniambia pia kuhusu suspension, kwavile siku zimebaki chache, niende na mzazi wangu tena pale shuleni na hela ya fine, atafanya mpango nitapokelewa tu.

Nikaona wazo zuri, kumpigia simu yule Mchaga, akasema aina noma, kesho yake nirudi Tanga, then siku inayofatia twende wote shule akamalizie msala.

Ambacho Mimi na yeye hatukukijua, kumbe Mshua wangu akiwa kwenye kufatilia biashara zake, aliamua aje pale shule kuniangalia kabla hajarudi kijijini. So, muda wote tulioongea na simu Jana yake, tayari alikuwa na taarifa zangu full.

Mimi na yule Mchaga tulikuwa tumeandaliwa mtego. Kilichoenda kutokea, Mchaga alisema hatonisahau........
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣!
Mchagga alinikosha hio reaction vyake dogo acha kujizimadata hahahaha!!!

Naendelea kusoma 🙇
 
3rd Portion:

... Maelezo ambayo nilikuja kupewa baadae na head prefect, ni kuwa inaonekana mshua alinitafuta sana kwenye simu kabla hajaenda pale shule, ila hakufanikiwa kunipata. Kwavile hatujawasiliana muda mrefu, na akisema arudi kijijini, maana yake utapita muda mrefu mwingine bila kuonana, ndio akaona afunge safari mpaka shule. Kufika pale akajitambulisha kama mzazi wangu, na akaomba kuonana na mimi. Walim wakashangaa, mzazi wake Analyse?, Wewe ni baba yake mkubwa au mlezi? Dingi akawa hajaelewa. Akawaambia yeye ni Mzee wangu kabisa, Mwalim wa nidham akaona mshua anamletea masihara, ili swala la wanafunzi kuleta wazazi feki inabidi likomeshwe, akamwambia Mzee akae kwenye benchi. Baada ya kushauriana na mkuu wa shule, wakataka kumpeleka Mzee Polisi. Mshua akawakazia, walivyoona yupo serious sana, wakamuomba ID yoyote.

Akawapa voters ID, walivyoona mfanano wa majina, walim wakachoka. Ikabidi waanze kuulizana, kama wewe ndio baba yake, yule aliyekuja nae ni nani? Hapo ndio wakampa picha nzima. Mzee akacheka (Mzee wangu akiwa na hasira sana, kuna kicheko fulani kinakujaga automatically). Mwisho wa siku wakaazimia head prefect awe ananipigia simu mara kwa mara, akinipata, anipe zile taarifa za kuhitajika shule kwa ajili ya usajili. Na ahakikishe ananishawishi niende na mzazi niliyempeleka last time.

Walimu walikuwa na shauku ya kuniona Mimi maana nimecheza na akili zao, ila Mshua target zake ilikuwa ni kumuona yule mzazi niliyempeleka badala yake. Mwamba Sina ili wala lile, kesho yake nikapanda Simba Mtoto, safari ya shule ikaanza. Nilivyofika, nikaunga moja kwa moja mpaka nguvu mali, nikapoa kwa mshikaji wangu pale Galanosi, kesho yake asubuhi, tukabebana Mimi na yule Mchaga hao mpaka shule.

Ile shule ilivyo, ukishaingia kupitia main entrance, unakata upande wa kulia, ndio kuna ofisi za walim pamoja na head master. Upande wa kushoto, kulikuwa na korido inayoelekea madarasani, lakini pia mwanzoni kuna njia ya kwenda vyooni, na ngazi za kuelekea madarasa ya juu. Sasa kwenye hizi ngazi ndio alikuwa kakaa Mshua ananisubiria Mimi na baba yangu tufike. Na sisi tulivyofika, direct tukakata kona kulia, hatukuangalia nyuma. Mzee akatuungia tela mdogo mdogo. Machale ni kama yalinicheza hivi, nikapata hisia zinaniambia geuka nyuma, kugeuka nakutana na Mshua kakaza sura kimtindo, mikono yote miwili kaikutanisha nyuma ya makalio, kama wanavyopendaga kutembea wazee. Alipoona nimegeuka, akasimama kwa muda Nikapatwa na mshtuko, maana sikutarajia kumuona pale, nikajikuta nimeita "Baba?". Yule Mchaga alikuwa bado hajausoma mchezo, akaitikia "Naam jembe langu". Ila alivyogeuka, na kukuta nimeelekeza attention kwa mtu mwingine, akili yake ikaload faster, akajikuta anatukana kichini chini "Ku***na walai".

Mshua akawa anamuangalia tu, huku kaweka tabasam la mamba. Mchaga akapiga hesabu za haraka, akaona hapa akiingia ofisini, basi hatoweza kutoka, anaweza akaishia polisi. Akapitisha wazo la kutoweka eneo lile, ila njia peke rahisi ni kupitia upande aliosimama Mshua, pia japo shule haikuwa na fensi, ila kukimbilia upande waliopo wanafunzi inaweza ikawa msala zaidi, maana wanafunzi hawana dogo. Akaamua kurudi na njia tuliyojia, upande aliosimama Mshua. Kosa alilofanya Mchaga, alim-underestimate Mshua, labda alijiona yeye kijana zaidi akijilinganisha nae, so angemzidi nguvu. Mchaga alitoka speed ghafla, mshua akawahi kumrukia, wakavaana mpaka chini. Kitendo cha kuanguka chini tu, Mshua kama kawaida yake, akamuwahi Mchaga na kabali moja matata. Mchaga kila akirusha ngumi, Mshua hana habari, ndio kwanza anazidi kukaza mikono. Wanafunzi wakajaa madirishani, kelele zikazagaa eneo lile, wengine wakaanza kutoka madarasani kuja kushuhudia kwa ukaribu.

Walim ikabidi waanze zoezi la kuwaachanisha, walipofanikiwa, Mchaga macho yalikuwa mekunduu kama katoka kulala au kulia. Walim wakawa wanafukuza wanafunzi warudi madarasani, Kisha wakawaomba Baba na yule Mchaga waende ofisini kwa mazungumzo, maana kwa umri wao haifai kushikana mashati namna ile. Wakiwa wanakaribia mlango wa ofisi ya walim, yule Mchaga aligeuka, akatoka speed, akaelekea upande zilipo hostels za wanafunzi wa advance, akapita kwenye senyenge, alivyotokea upande wa pili, akaongeza speed, akapotelea kwenye makazi ya watu. Hakuna hata mwalim aliyejisumbua kumkimbiza, wakabaki wanamwangalia tu. Ila wanafunzi ndio wakawa wanamzomea. Jamaa akasepa, msala nikabaki nao peke yangu. Kikao kikafanyikia ofisi ya walimu wote, mwanenu nikapigishwa magoti huku nasemwa..

Ubaya wa ofisi ya walimu, hata yule mwalim ambae hakujui, lazima apate cha kukuongelea. Nilitembezewa fimbo za kufa mtu siku ile, japo mshua hakunipiga, ila alichangia pakubwa sana kuikuza adhabu yangu, maana aliongea mengi sana, kiasi kwamba nikaonekana kituko. Mshua alilipa ile hela ya faini, nikaruhusiwa kwenda darasani. Aliamua kuondoka siku hiyo hiyo, hakujisumbua kuongea na Mimi baada ya kutoka mle ofisini, na hakunipa hata shiling 10 Kwa ajili ya matumizi pale shuleni. Kiufupi aliniacha kikauzu sana. Nimeingia class sina mzuka hata kidogo, mda wote nimelala kwenye dawati. Mida ya mchana baada ya msosi, nikaamsha zangu kuelekea hostel. Nikalala mpaka mida ya jioni.

Wakati natoka kula msosi wa usiku shuleni, yule jamaa yangu wa Galanosi akanipigia simu, anauliza nimemfanya nini Mchaga? Maana kakutana nae ana nundu kwenye kona ya uso, alaf kamuahidi kwamba siku akikutana na Mimi, sitokaa nimsahau maishani mwangu kwa atakachonifanya. Ikabidi nimuelezee kwa ufupi yaliyojili. Jamaa alicheka sana, mwishowe akaniambia nikienda shuleni kwao niende kwa tahadhari, maana Mchaga alimaanisha alichokisema. Tukaishiana hapo, then nikaenda chamber kupiga msuli. Tokea siku ile nikaanza kupiga sana msuli, sikuwa na msala mwingine wowote, japo walimu waliendelea kuwa wananizingua hapa na pale, ila niliamua kuwa mpole.

Mshua hakuwahi kunitafuta tena, sio kwa simu wala msg. Ni kama alinizila. Kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa mwisho, nikaanza kumfukuzia demu mmoja wa O level pale pale shuleni, alikuwa mweupe, sauti nyembamba na kishundu fulani cha kuvunjia shingo, maana akikupita lazima ugeuke. Siku moja nimekaa nae maeneo ya garden mida ya jioni, naendelea kuingizia mistari, maana alikuwa bado hajaeleweka. Katika maongezi akaniambia "Wewe hapa Tanga sio kwenu, unasema unanipenda, wakati siku sio nyingi utamaliza shule, utaacha umenitumia alafu utaondoka".

Nikamjibu kuwa mgeni Tanga hainizuii Mimi kumpenda yeye, umbali sio kikwazo kwangu. Akaniuliza "Unamaanisha unachosema? Kuwa utarudi kwa ajili yangu?, Niambie ukweli, sitaki uongo". Nikasita kidogo kutoa jibu, yeye akaendelea "Mimi ninachohitaji kujua ni Nia yako tu, kama kweli utataka kurudi, mimi nitakurudisha". Ile kauli ikanimakinisha kidogo, nikamuuliza "Utanirudisha kivipi? " Akajibu "Wewe ilo niachie Mimi, je ni kweli unanipenda na ungependa kurudi kwa ajili yangu, nikurudishe??

Nikabaki nimeduwaa kwa muda, najiuliza "Huyu anaongelea nini?".....

"Naam jembe langu"🤣🤣🤣🤣🤣🤣!
Hii story khakhakhaaaa!!!
Mchagga nukseee sana!
 
Aise nimecheka kinoma story nzuri
ila na mimi nikikumbuka nilimpeleka mzazi feki kutoka kwenye bar ya mbege duh jamaa alikuwa ananukia pombe hatari, ofisini naulizwa ndio baba yako nikasema ndio mwalimu alisizi kama 5 min hivi akituangalia tu ndio maongezi yakaendelea tukamaliza nikampa 10k yake moto.
Ila ujana bn tena wa shule, nimemiss zile hustle sana
 
Back
Top Bottom