Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Uchumi wa Zambia ni mdogo sana kulinganisha NA Tanzania ila wazambia wengi wao ni waaminifu sana.
Ya Zambia mtu anaweza kununua kitu cha kwacha elfu 10 akakupa 5, afu akakwambia 5 atakumalizia week ijayo. Na kweli ukienda week ijayo mnamalizana. Bongo nilikuwa naleta lap top, sim, plasma tv nk, tena katika ofisi zinazoaminika kuwa ni za watu wenye pesa. Lkn akikupa hela nusu na kukwambia uje week ijayo, basi week ijayo ukifika humkuti au huwakuti unaowadai wote. Bora mtu ajifiche chooni masaa matatu, lkn ahakikishe nimeondoka bila kunilipa 😂😂😂
 
Mpumbavu ushaanza upumbavu!

Badilika

#Usipobadilikatutakubadilisha
Shukran mkuu, bora umenisaidia kumuelimisha jamaa. Watu wa aina hii huwa wanafurahi pale mtu anapoleta uzi unaozungumzia kina Zali, Wema Sepetu, Diamond, Kiba nk. Ila hizi thread zenye uhalisia wa maisha hawazipendi kwa sababu hazina mipasho ile waliyoizoea kule kwa kina Diamond na Kiba.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Umeongea ukweli mtupu mkuu,sisi wazee wa road trips ndani ya barabara za Zambia 🇿🇲 unaweka kambi popote na kama unawasiwasi zaidi unalala kwenye check points za police au jeshi!
 
Usalama unaanzia udogoni kwani watoto wanashuhudia wazazi na jamaa wanavyofanya biashara na kuaminiana nao wanakua na kuiga

Sisi ni tofauti kabisa mtoto anakuwa kwa kushuhudia utapeli au nyumbani mtu anagonga kuja kudai utasikia mtoto anaambiwa mwambie baba hayupo

Wizi ni janga la Taifa letu na hakuna wa kumuamini na utakaesema huyu kalia sana Acha nimkope ndio kabisa hiyo imekula kwako

Lingine ni kuwa kuna wengi wanatetea wizi yaani mfanyakazi au kiongozi serikalini au sekta binafsi anaiba na akibainika utasikia- Safi sana wacha waibe hata mimi nisingeacha

Hapo tegemea hakuna mwenye unafuu na wizi hautaisha hata serikalini


Hili la kuweka hela za kubadilisha hadharani zipo sehemu kadhaa hata kuna mji Somaliland panaitwa Hargeisa ipo kwenye YouTube
Yaani kina mama wanauza Dhahabu hadharani huku vijana wakibadilisha hela zikiwa juu ya meza kibao na hakuna wa kuiba
Tena anaenda kusali anafunika na shuka [emoji3064]
Utashangaa ya Zambia ila kuna wengine waaminifu pia
 
Usalama unaanzia udogoni kwani watoto wanashuhudia wazazi na jamaa wanavyofanya biashara na kuaminiana nao wanakua na kuiga

Sisi ni tofauti kabisa mtoto anakuwa kwa kushuhudia utapeli au nyumbani mtu anagonga kuja kudai utasikia mtoto anaambiwa mwambie baba hayupo

Wizi ni janga la Taifa letu na hakuna wa kumuamini na utakaesema huyu kalia sana Acha nimkope ndio kabisa hiyo imekula kwako

Lingine ni kuwa kuna wengi wanatetea wizi yaani mfanyakazi au kiongozi serikalini au sekta binafsi anaiba na akibainika utasikia- Safi sana wacha waibe hata mimi nisingeacha

Hapo tegemea hakuna mwenye unafuu na wizi hautaisha hata serikalini


Hili la kuweka hela za kubadilisha hadharani zipo sehemu kadhaa hata kuna mji Somaliland panaitwa Hargeisa ipo kwenye YouTube
Yaani kina mama wanauza Dhahabu hadharani huku vijana wakibadilisha hela zikiwa juu ya meza kibao na hakuna wa kuiba
Tena anaenda kusali anafunika na shuka [emoji3064]
Utashangaa ya Zambia ila kuna wengine waaminifu pia
Uko sahihi Somalia ndio kiboko

Mtu anaenda msikitini kaacha maburungutu ya hela wazi njiani anapobadilishia na haibi mtu

Nchi Haina amani vurugu tupu lakini uaminifu wa pesa uko juu mno kuliko Sisi watanzania tuliojaa amani
 
Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Ni kweli kabsa yan uko sheria zao kali na wanazifatilia sana ndio maana wananchi wao wanatii sheria bila shuruti!! Lakin waho wazambia braza wako na roho mbaya sana kuna visa wanatufanyia sana sisi wapita njia mi nimeishi hapo MPIKA
 
Uko sahihi Somalia ndio kiboko

Mtu anaenda msikitini kaacha maburungutu ya hela wazi njiani anapobadilishia na haibi mtu

Nchi Haina amani vurugu tupu lakini uaminifu wa pesa uko juu mno kuliko Sisi watanzania tuliojaa amani

Yaani unaweza kuacha mzigo kwa msomali hata baada ya mwaka ukaukuta
Wizi hakuna utakula shaba hadharani
 
Uko sahihi Somalia ndio kiboko

Mtu anaenda msikitini kaacha maburungutu ya hela wazi njiani anapobadilishia na haibi mtu

Nchi Haina amani vurugu tupu lakini uaminifu wa pesa uko juu mno kuliko Sisi watanzania tuliojaa amani
Nimekumbuka kitu kutokana na mchango huu!!

Ndugu zetu Waislam asilimia kubwa hujitahidi kuyaishi wanayofundishwa tofauti ki % na upande mwingine.(naomba nisishambuliwe ni mtazamo wangu)
 
Back
Top Bottom