UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,753
- 12,932
Mpumbavu ushaanza upumbavu!Ushamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Badilika
#Usipobadilikatutakubadilisha
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mpumbavu ushaanza upumbavu!Ushamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Ya Zambia mtu anaweza kununua kitu cha kwacha elfu 10 akakupa 5, afu akakwambia 5 atakumalizia week ijayo. Na kweli ukienda week ijayo mnamalizana. Bongo nilikuwa naleta lap top, sim, plasma tv nk, tena katika ofisi zinazoaminika kuwa ni za watu wenye pesa. Lkn akikupa hela nusu na kukwambia uje week ijayo, basi week ijayo ukifika humkuti au huwakuti unaowadai wote. Bora mtu ajifiche chooni masaa matatu, lkn ahakikishe nimeondoka bila kunilipa 😂😂😂Uchumi wa Zambia ni mdogo sana kulinganisha NA Tanzania ila wazambia wengi wao ni waaminifu sana.
Ya kweli mkuu huko nako uaminifu usalama upo wa kutosha.Ongezea na Namibia, Botswana, Ushelisheli
Shukran mkuu, bora umenisaidia kumuelimisha jamaa. Watu wa aina hii huwa wanafurahi pale mtu anapoleta uzi unaozungumzia kina Zali, Wema Sepetu, Diamond, Kiba nk. Ila hizi thread zenye uhalisia wa maisha hawazipendi kwa sababu hazina mipasho ile waliyoizoea kule kwa kina Diamond na Kiba.Mpumbavu ushaanza upumbavu!
Badilika
#Usipobadilikatutakubadilisha
Aiseeee brother Hivi umekielewa ulichokiandika au umeamua tu kuandika acha hizo bwana.Mambo ya kishamba kabisa umeandikaUshamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Jaribu kuwapora au uwafanyie ujanjaujanja.Aisee,utalogwa uwe chizi au kifo kibaya kitafuata.Cha mtu kiheshimu kama ambavyo jasho la mtu haliliwi bila ruhusa.Ya mkuu, inawezekana hii ikawa sababu moja wapo, ya watu wengi kutokuwa na tamaa ya kuwaibia wengine.
Agiza udondo was pemba na limao ntakuja kulipa ee bibieUshamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Umeongea ukweli mtupu mkuu,sisi wazee wa road trips ndani ya barabara za Zambia 🇿🇲 unaweka kambi popote na kama unawasiwasi zaidi unalala kwenye check points za police au jeshi!Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.
Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.
Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.
Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.
Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.
Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.
Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Mila Zao zinachangiaYa mkuu, inawezekana hii ikawa sababu moja wapo, ya watu wengi kutokuwa na tamaa ya kuwaibia wengine.
Uko sahihi Somalia ndio kibokoUsalama unaanzia udogoni kwani watoto wanashuhudia wazazi na jamaa wanavyofanya biashara na kuaminiana nao wanakua na kuiga
Sisi ni tofauti kabisa mtoto anakuwa kwa kushuhudia utapeli au nyumbani mtu anagonga kuja kudai utasikia mtoto anaambiwa mwambie baba hayupo
Wizi ni janga la Taifa letu na hakuna wa kumuamini na utakaesema huyu kalia sana Acha nimkope ndio kabisa hiyo imekula kwako
Lingine ni kuwa kuna wengi wanatetea wizi yaani mfanyakazi au kiongozi serikalini au sekta binafsi anaiba na akibainika utasikia- Safi sana wacha waibe hata mimi nisingeacha
Hapo tegemea hakuna mwenye unafuu na wizi hautaisha hata serikalini
Hili la kuweka hela za kubadilisha hadharani zipo sehemu kadhaa hata kuna mji Somaliland panaitwa Hargeisa ipo kwenye YouTube
Yaani kina mama wanauza Dhahabu hadharani huku vijana wakibadilisha hela zikiwa juu ya meza kibao na hakuna wa kuiba
Tena anaenda kusali anafunika na shuka [emoji3064]
Utashangaa ya Zambia ila kuna wengine waaminifu pia
Dah,bado napapenda sana chingolaWewe ndio mshamba sasa kakosea nini kueleza alichokiona
Ni kweli kabsa yan uko sheria zao kali na wanazifatilia sana ndio maana wananchi wao wanatii sheria bila shuruti!! Lakin waho wazambia braza wako na roho mbaya sana kuna visa wanatufanyia sana sisi wapita njia mi nimeishi hapo MPIKAHabari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.
Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.
Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.
Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.
Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.
Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.
Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Uko sahihi Somalia ndio kiboko
Mtu anaenda msikitini kaacha maburungutu ya hela wazi njiani anapobadilishia na haibi mtu
Nchi Haina amani vurugu tupu lakini uaminifu wa pesa uko juu mno kuliko Sisi watanzania tuliojaa amani
Acha kutetea ujinga.Kwahiyo unajiona mjaaanja kumnanga mtu wakati hujui kajibana kiasi gani kutujumuisha katika uzoefu wake!?Hakuna niliposema kakosea. Pole dada!
Mtoa mada hajamaanisha kuwa katoboa kamaanisha Zambia Usalama mkubwa kutembea na hela kuliko TanzaniaUshamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Nimekumbuka kitu kutokana na mchango huu!!Uko sahihi Somalia ndio kiboko
Mtu anaenda msikitini kaacha maburungutu ya hela wazi njiani anapobadilishia na haibi mtu
Nchi Haina amani vurugu tupu lakini uaminifu wa pesa uko juu mno kuliko Sisi watanzania tuliojaa amani