Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Zambia hii hii madereva wetu wanavyoibiwa coper na mafuta au zambia ya kwenye mitandao?

Hapo lusaka ni kama boda tuu na hizo pesa wanazobadikisha ata bida zetu karibia zote zipo hivyo labda kipindi cha awanu ya 5 ndio wakalazimisha iwe kubadili pesa ni benki pekee.

Ukitaka kujua udhaifu wa Zambia miliki lorry au tafuta wanaisafirisha mizigo huko.
 
Hujakosea kabisa kuhusu Zambia
Hata askari polisi wao si washenzi kama wa kwetu. Askari ni waadilifu, wanatumia akili.
Hali ya hewa pia ni nzuri. Ni nchi fulani naipenda sana, ukiongeza na Namibia, Seychelles, Botswana na Cape Verde.
Hivi ni hawa hawa askari wa kutoka Nakonde to kasumbalesa ndio mnaowasifia humu?
Nina clip nyigi tu za madereva wetu juu ya manyanyaso wanayoyapata huko zambia.

Kama unapita na basi hayo hauwezi kuyajua wala kuyaona.
 
Sijawahi kufika Chingola, ila Kitwe, Kapilimposhi, Lusaka na Ndola. Chingola kina kipi?
Chingola kumetulia,mji uko kama vimji vya waingereza bado...kamji hkana kokoro
Hata kitwe pia nimepapenda,nmekaa sana nkana East hapo na Riverside
Ukitokea chilalabombwe kama unaelekea chingola kuna sehemu inaitwa musenga ndani kule kuna mashamba ya wazungu na wanafuga pia,nilikaa pia....huko sasa ndy tuliwasanua wazambia biashara ya skrepa miaka hiyo
Vitabiatabia fulani wanavyo,sema kdg wazambia wana ustarabu,ila ni watu wa kuhoji mambo na kuwaburuza wagumu

Ova
 
Kuna siku pale magomeni kanisani palikuwa na foleni. Kuna abiria mwenzetu aliagiza maji kwa wale wanaopitisha madirishani, kabla hajamkabidhi hela daladala likaondoka.

Yule abiria akamwomba dereva apunguze mwendo ili ampe yule muuzaji hela yake, licha ya kuwa dereva alichomoa kwamba pale sio kituo tena, lakini abiria wa karibu waligeuka wote kumwangalia yule ni abiria wa namna gani.
Kufika mapipa akashuka tukaona anarudi (tulihisi anaenda kumpatia hela muuzaji), mle kwenye basi ukawa mjadala kwamba inawezekana yule sio mtanzania maana sisi watz kwa tunavyojuana uaminifu ni sifuri kabisa asilimia kubwa.
 
Jail system. za zambia zipo very active , na punishment for misconducts are hefty too.

Ukiwa mtu wa matukio lazima utadakwa na utaadhibiwa ipasavyo, sio kama huku kwetu , mtoto anajulikana kabisa mtaani kuwa ni kibaka na hafanywi kitu kwa sababu baba ake ni mganga maarufu au mjumbe wa mtaa.
Kama baliega kule gomz pamoja na kujua tabia zake walikuwa wanamlea tu mpka pale alipouwawa wanajifanya wanalia wana huzuni
 
Hivi ni hawa hawa askari wa kutoka Nakonde to kasumbalesa ndio mnaowasifia humu?
Nina clip nyigi tu za madereva wetu juu ya manyanyaso wanayoyapata huko zambia.

Kama unapita na basi hayo hauwezi kuyajua wala kuyaona.
Kwa upande wa askari ni kweli wanaushz fulani,Rushwa wanayo
Jela zao lockup zenyewe siyooo

Ova
 
Kwa haraka haraka kuwa pale siku 5 niligundua hivi:, chakula anachukula mvuta Guta wa Zambia mwalimu wa Tanzania hawezi kukila mfulilizo kwa wiki nzima unless akubaliane kusave laki ama elfu 80 kwa mwezi.
2) wanawake wa Zambia uwatenganishi na vazi la kanga/kitenge.
Wanapenda sana kujifunga kanga na vitenge no matter kavaaje utamkuta kajifunga kitenge/kanga.
Huyo mvuta guta licha ya kula hicho chakula bado anafanya mambo mengine ya Maendeleo vizuri tu kushinda Mwalimu wa Kibongo.
 
Back
Top Bottom