Tyrone Kaijage
JF-Expert Member
- Jul 19, 2021
- 1,617
- 3,405
Pesa zambia ipo, bidhaa ziko chini, fursa ni nyingi iwe lusaka, iwe kitwe, iwe copperbelt ni wewe tu, sema jamaa wanakula sana bata wabongo wanasubiri,
Walevi sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pesa zambia ipo, bidhaa ziko chini, fursa ni nyingi iwe lusaka, iwe kitwe, iwe copperbelt ni wewe tu, sema jamaa wanakula sana bata wabongo wanasubiri,
Zambia hii hii madereva wetu wanavyoibiwa coper na mafuta au zambia ya kwenye mitandao?Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.
Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.
Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.
Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.
Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.
Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.
Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Hivi ni hawa hawa askari wa kutoka Nakonde to kasumbalesa ndio mnaowasifia humu?Hujakosea kabisa kuhusu Zambia
Hata askari polisi wao si washenzi kama wa kwetu. Askari ni waadilifu, wanatumia akili.
Hali ya hewa pia ni nzuri. Ni nchi fulani naipenda sana, ukiongeza na Namibia, Seychelles, Botswana na Cape Verde.
Hivi ungekaa kimya Dada angu ungepungukiwa nini?Punguza shobo basi ukikuta wanaume wanaongeaUshamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Huyo Dada ana shida zake tu MkuuMtoa mada hajamaanisha kuwa katoboa kamaanisha Zambia Usalama mkubwa kutembea na hela kuliko Tanzania
Chingola kumetulia,mji uko kama vimji vya waingereza bado...kamji hkana kokoroSijawahi kufika Chingola, ila Kitwe, Kapilimposhi, Lusaka na Ndola. Chingola kina kipi?
Ile huduma yao ya kupokea kutuma pesa na kupokea,we tuma pokea hata mln 200 utapewa..Asante kwa Hilo
Tamaa hakuna na biashara inafanyika hata kama hakuna maandishi
Kama baliega kule gomz pamoja na kujua tabia zake walikuwa wanamlea tu mpka pale alipouwawa wanajifanya wanalia wana huzuniJail system. za zambia zipo very active , na punishment for misconducts are hefty too.
Ukiwa mtu wa matukio lazima utadakwa na utaadhibiwa ipasavyo, sio kama huku kwetu , mtoto anajulikana kabisa mtaani kuwa ni kibaka na hafanywi kitu kwa sababu baba ake ni mganga maarufu au mjumbe wa mtaa.
Mademu uko vipiPesa zambia ipo, bidhaa ziko chini, fursa ni nyingi iwe lusaka, iwe kitwe, iwe copperbelt ni wewe tu, sema jamaa wanakula sana bata wabongo wanasubiri,
Kwa upande wa askari ni kweli wanaushz fulani,Rushwa wanayoHivi ni hawa hawa askari wa kutoka Nakonde to kasumbalesa ndio mnaowasifia humu?
Nina clip nyigi tu za madereva wetu juu ya manyanyaso wanayoyapata huko zambia.
Kama unapita na basi hayo hauwezi kuyajua wala kuyaona.
Kula nyapu saudia mpka uoe tofauti na hapo kama hutochinjwa utapigwa mawe mpaka ufeBata Ni dunia nzima labda Saudia (japo nao wanaendaga nchi jirani Bahrain kula vyombo na nyapu) na kurudi Saudia wepesi.
Kaa mbali na wabongo wanaokaa hukoSijawahi kufika Zambia ila ninakiu ya kupeleka bidhaa zangu kufanya biashara huko, one day YES
Huwa wanawafanyajeN hata sasa Kuna mgogoro Kati ya Tz vs Zambia khs Namna Zambia wanavyowa-treat waTz wanaondesha malorry.Bungeni Waziri akisema wanaangalia Namna ya kuweza kuikwepa Zambia wkt wa kupeleka mizigo Congo.
Picha halisi ya mbongo ndio kama hii!Ushamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Huyo mvuta guta licha ya kula hicho chakula bado anafanya mambo mengine ya Maendeleo vizuri tu kushinda Mwalimu wa Kibongo.Kwa haraka haraka kuwa pale siku 5 niligundua hivi:, chakula anachukula mvuta Guta wa Zambia mwalimu wa Tanzania hawezi kukila mfulilizo kwa wiki nzima unless akubaliane kusave laki ama elfu 80 kwa mwezi.
2) wanawake wa Zambia uwatenganishi na vazi la kanga/kitenge.
Wanapenda sana kujifunga kanga na vitenge no matter kavaaje utamkuta kajifunga kitenge/kanga.