Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Mimi nimeishia hapo kwa mjomba Mbagala kibonde maji.

Tuweke mzani sawa, umetembea nchi ngapi kaka kiasi useme zambia ndio nchi yenye amani na usalama zaidi? (uliyoandika humo nimesadiki ila ningependa kujua nchi ulizotembelea ila niweze kufanya tathmini)
 
Nimekumbuka kitu kutokana na mchango huu!!

Ndugu zetu Waislam asilimia kubwa hujitahidi kuyaishi wanayofundishwa tofauti ki % na upande mwingine.(naomba nisishambuliwe ni mtazamo wangu)

Japo mi mkristo ila unachosema nu kweli

Jamii za kiislamu zina ustaarabu sana kwenye biashara na mambo ya wizi wizi sio mkubwa kuliko jamii za kikristo.

Huo ni ukweli kabisa
 
Ni kweli kabsa yan uko sheria zao kali na wanazifatilia sana ndio maana wananchi wao wanatii sheria bila shuruti!! Lakin waho wazambia braza wako na roho mbaya sana kuna visa wanatufanyia sana sisi wapita njia mi nimeishi hapo MPIKA
N hata sasa Kuna mgogoro Kati ya Tz vs Zambia khs Namna Zambia wanavyowa-treat waTz wanaondesha malorry.Bungeni Waziri akisema wanaangalia Namna ya kuweza kuikwepa Zambia wkt wa kupeleka mizigo Congo.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania....
Kwa nnachoamini kila nchi ina kitu chakr ambacho imebalikiwa, wao yawezekan wamebarikiwa ilo lakin in other hand yawezekan huo ushuhuda wako hauna uhakika 100% kwasababu hujaweka wazi ni kwa muda gani umekaa uko kwajil ya utafiti huo na malengo ya utafiti wako yalikuwa ni yapi na je majibu uliyoyapata tunaweza kuyathibitisha vipi katika muktadha wa tafiti. Lakin kwa Tanzania niseme tu wazi hali ya usalama imeimarika sana kwa siku za hivi karibuni matukio kam uliyoyatolea mfano hapo kariakoo kuna baadhi ya maeneo matukio hayo hayapo kabisa.

Kwaiyo huwezi kutumia eneo mmoja kujustify kwamba Tanzania hakuna usalama ndugu yangu. Labda ungesema hali ya usalama nchini bado inakumbwa na changamoto ivyo mamlaka ziongeze nguvu ili kuhakikisha usalama unakuwepo kwa 100%.
 
Kingine kinacho fanya waheshimu hela ya mtu ni hofu ya kulogwa. Kama ujuavyo Zambia ni road kuu ya kupitisha mizigo na biashara kwenda KONGO.
Huko nyuma wakongo wengi walikuwa wanatapeliwa sana pesa na mizigo yao wakaamua kutoa fundisho kwa kuloga.
 
Na Kubadili fedha za kigeni enzi hizo mambo ya bureau Ni mizinguo tumebadilisha Sana kwa wasomali,Huku uaminifu ukiwa ni 100%

Tatizo la uswahili ni imani potovu kama ushirikina
Yaani wakiona mtu kaendelea watasema tapeli au kaenda kwa mganga ila hata siku moja huwezi kumsikia mswahili anasema kuwa jamaa kafika hapo kwa uaminifu wake

Bado tuna safari ndefu sana
 
Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Ugumu wa maisha na kutokuweko mzunguko wa fedha kwa wote ndicho hufanya kuweko na ongezeko la uharifu! Kama kila mtu añapata riziki zake hayuko wakusumbukia cha mwingine.Selikali za nchi zingine zimeweka mazingira rafiki ya sio binya mzunguko wa fedha kwa wananchi wa nvhi husika.
 
Kwa haraka haraka kuwa pale siku 5 niligundua hivi:, chakula anachukula mvuta Guta wa Zambia mwalimu wa Tanzania hawezi kukila mfulilizo kwa wiki nzima unless akubaliane kusave laki ama elfu 80 kwa mwezi.
2) wanawake wa Zambia uwatenganishi na vazi la kanga/kitenge.
Wanapenda sana kujifunga kanga na vitenge no matter kavaaje utamkuta kajifunga kitenge/kanga.
 
Tatizo la uswahili ni imani potovu kama ushirikina
Yaani wakiona mtu kaendelea watasema tapeli au kaenda kwa mganga ila hata siku moja huwezi kumsikia mswahili anasema kuwa jamaa kafika hapo kwa uaminifu wake

Bado tuna safari ndefu sana
Tukiambiwa uaminifu Ni mtaji hua tunaona Kama Ni story tu.Tunaamini hauwezi kutoboa kwny Maisha bila kuiba/kudhulumu.
 
Ya Zambia mtu anaweza kununua kitu cha kwacha elfu 10 akakupa 5, afu akakwambia 5 atakumalizia week ijayo. Na kweli ukienda week ijayo mnamalizana. Bongo nilikuwa naleta lap top, sim, plasma tv nk, tena katika ofisi zinazoaminika kuwa ni za watu wenye pesa. Lkn akikupa hela nusu na kukwambia uje week ijayo, basi week ijayo ukifika humkuti au huwakuti unaowadai wote.
Bongo majizi wengi
 
Tukiambiwa uaminifu Ni mtaji hua tunaona Kama Ni story tu.Tunaamini hauwezi kutoboa kwny Maisha bila kuiba/kudhulumu.

Hilo wengi hawalijui kwa sababu ya kukua kwenye mazingira magumu ya dhulma na uongo

Ukiwa muongo lazima utakuwa tapeli tu huwa vinaendana sana

Ila ukiwa muaminifu utaendelea haraka kwani utapata madili hata kama sio moja ya biashara zako

Unauza duka mtu anakuletea Dili la kumuuzia kiwanja kisa uaminifu tu
 
Back
Top Bottom