Siku aliyozaliwa Yesu bado Kitendawili

Siku aliyozaliwa Yesu bado Kitendawili

Hebu tueleze japo kidogo, kuna dhambi gani kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu?
Pia kusherehekea birthday kuna ubaya gani?
Eleza hayo inawezekana tukakuelewa.
Ndugu, sijasema ni DHAMBI au Si DHAMBI kusherehekea!!

Nilichowauliza wakristo, Kanisa, maelekezo ya kusherehekea Christmas tarehe 25 December wameyatoa wapi?

Je ni maelekezo ya Roho mtakatifu kusherehekea Christmas tarehe 25 December na BIRTHDAYS?

Karibu🙏
 
Una ushahidi wa kimaandiko kuhusu Ruhusa hiyo?

Roho mtakatifu ndani Yako anakushuhudia kuwa unachofanya ni sahihi mwana wa Mungu Donatila ?
Kwako wewe ushahidi ni maandiko tu?

Utakuwa ni mlokole au msabato
 
Kwani ina athari gani kiroho? Hoja kwamba tarehe haijasemwa na biblia kuna kuna ubaya gani kukumbuka kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo kila desemba 25? Haina haja ya kuanza kukokotoa mahesabu ya siku ili kuipata tarehe hiyo, itoshe tu kuadhimisha siku hiyo
Unaamini Yesu kupitia Roho MTAKATIFU angetaka tusherehekee Christmas, angeshindwa kutupa exact date ya kusherehekea Kuzaliwa kwake?

KWANINI siku hiyo ametuficha?
 
Ndugu, sijasema ni DHAMBI au Si DHAMBI kusherehekea!!

Nilichowauliza wakristo, Kanisa, maelekezo ya kusherehekea Christmas tarehe 25 December wameyatoa wapi?

Je ni maelekezo ya Roho mtakatifu kusherehekea Christmas tarehe 25 December na BIRTHDAYS?

Karibu🙏
Ingekuwa ni Jambo baya ndo tungeanza kuhoji ni maelekezo ya nani yameleta 25december iwe siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu. Kama sio dhambi hakuna mantiki ya kujadili jambo hili.
Kwenye birthday naona napo kama unapinga au sijakuelewa vizuri?
 
Ingekuwa ni Jambo baya ndo tungeanza kuhoji ni maelekezo ya nani yameleta 25december iwe siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu. Kama sio dhambi hakuna mantiki ya kujadili jambo hili.
Kwenye birthday naona napo kama unapinga au sijakuelewa vizuri?
Nimewauliza wakristo swali Hilo,


Wakristo wanaoongozwa na Roho mtakatifu, Je ni Yeye ndiye aliyewaelekeza kusherehekea Christmas tarehe 25 December?

Ni Yeye amewaelekeza juu ya umuhimu wa kusherehekea siku ya Kuzaliwa, BIRTHDAYS?
 
Unaamini Yesu kupitia Roho MTAKATIFU angetaka tusherehekee Christmas, angeshindwa kutupa exact date ya kusherehekea Kuzaliwa kwake?

KWANINI siku hiyo ametuficha?
ili upate tarehe hiya anzia kuitafuta kwa yohana mbatizaji mama yake alipata ujauzito kipindi gani, njoo kwa mariamu ndio utajua ni kipindi gani Yesu alizaliwa
 
Nimewauliza wakristo swali Hilo,


Wakristo wanaoongozwa na Roho mtakatifu, Je ni Yeye ndiye aliyewaelekeza kusherehekea Christmas tarehe 25 December?

Ni Yeye amewaelekeza juu ya umuhimu wa kusherehekea siku ya Kuzaliwa, BIRTHDAYS?
We roho mtakatifu amekuelekezaje kwani hadi unauliza wengine?
 
jesus-teaching.jpg

Yesu wa Nazareth

WANAZUONI wengi duniani, bado wanaumiza vichwa kuhusu tarehe sahihi aliyozaliwa Yesu Kristo, ambaye ni Nabii wa Wakristo.

Miaka nenda rudi, vitabu vingi vimeandikwa na makundi ya wanazuoni wa dini na historia kuanzia Mashariki ya Kati, Amerika, Ulaya, Afrika na bado hadi leo, maandishi mapya yanaendelea kuchapishwa juu ya kuzaliwa kwa Yetu Mnazareti.

Mjadala huo upo na hakika hautakoma kwani wanaoandika wanapingana kwa hesabu na historia. Wameshindwa kupata tarehe hasa aliyozaliwa Yesu ambaye pia huitwa Masihi.

Miaka 2000 iliyopita, mtawala wa tano wa Wayahudi, Pontio Pilato alimuuliza Yesu wa Nazareti swali lifuatalo: “Ukweli ni kitu gani?”

Aliuizwa swali hili wakati anakaribia kupewa hukumu ya kuwambwa msalabani baada ya kukamatwa akituhumiwa kujiita “Mfalme wa Wayahudi.”

Yesu hakujibu swali hili. Na hadi leo, kambi kadhaa za wanazuoni zinazidi kuvutana kuhusu jawabu sahihi kwa swali hili. Mfano mzuri wa mvutano huo unajitokeza katika mjadala kuhusu “siku ya kuzaliwa kwa Yesu wa Nazareti.”

Mpaka leo, kuna siku tatu tofauti zinazotajwa kama siku za kuzaliwa kwa Yesu. Kuna Desemba 25, Januari 6 na Januari 7. Ufafanuzi wa utata huu unafuata.

Tuanze na Desemba 25. Haya ni mawazo ya Mtakatifu Hippolytus wa Roma. Kwa mujibu wa utafiti wa Profesa Andrew McGowan wa Chuo Kiukuu cha Melbourne, mwaka 204BK, Hippolytus aliandika kwamba, “Tarehe ya kuzaliwa Yesu, Bethlehem, ni Desemba 25.”

Hippolytus alianzia kwenye tukio la Malaika Gabriel kumtokea Zakaria hekaluni na kumwambia kwamba mkewe Elizabeth angepata mimba na kumzaa Yohane.

Zakaria alikuwa kwenye ibada ya malipizi ya dhambi. Kwa mujibu wa kalenda ya Kiebrania ibada hiyo ilifanyika tarehe Julai 10 kila mwaka wa Kiyahudi.

Ulinganisho wa kalenda ya kale ya Wayahudi na kalenda ya kisasa unaonyesha kuwa siku hiyo ni sawa na Septemba 24 ya siku hizi. Hii maana yake ni kwamba Elizabeth alianza ujauzito wa Yohane Septemba 24.

Kwa mujibu wa uchambuzi wa Hippolytus, miezi sita baadaye malaika Gabriel alimtokea Bikira Maria na kumwambia atapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Hivyo, ujauzito wa Yohane ulioanza Septemba 24 uliutangulia ujauzito wa Yesu kwa miezi sita.

Hii maana yake ni kwamba, mimba ya Yesu ilianza Machi 25 na akazaliwa miezi tisa baadaye, yaani Desemba 25, anahitimisha Hippolytus.

Lakini, bado wapo Wakristo waliopinga tafsiri ya Hippolytus. Walihoji uhalali wa hesabu zake, wakitaka awaonyeshe hiyo miezi tisa ilikuwa na jumla ya siku ngapi.

Hawa wenye kupinga Krismas ya Desemba 25, huadhimisha Krismas ya Januari 7. Ni wafuasi wa Mfamle Julius Kaizari wa dola ya Kirumi. Sababu za upinzani wao zinafuata.

Katika mwaka 46KK Julius Kaizari aliunda kalenda iliyotokana na imani kwamba mzunguko wa dunia unachukua siku siku 365 tu. Lakini, baadaye wanasayansi waligundua kuwa mzunguko wa dunia huchukua siku 365 na robo.

Robo nne zinaunda mwaka mmoja. Hii maana yake ni kwamba, kila baada ya miaka mitatu, yaani katika mwaka wa nne, mzunguko wa dunia huchukua siku 366.

Miaka mitatu huitwa miaka mifupi, na mwaka wa nne kuitwa mwaka mrefu. Mwaka mrefu hugawanyika kwa namba “nne.”

Kwa mujibu wa “Kalenda ya Julius” mwaka wenye siku 365 una miezi 12; ambapo miezi minne ina siku 30, kila mmoja; miezi saba ina siku 31, kila mmoja; na mwezi Februari una siku 28.

Hesabu hizi hazihusishi siku 365 pekee kati ya siku 365 na “robo” za mzunguko wa dunia. Hivyo, kila baada ya miaka minne, “Kalenda ya Julius” ikawa inapoteza siku moja kamili.

Kwa ajili ya kuondoa dosari hii, katika kila mwaka mrefu, Julius aliamua kuongeza siku moja kwenye mwezi wa Februari, ili uwe na siku 29, na hivyo kukamilisha siku 366 za mwaka mrefu.

Kalenda hii ina miezi minne ya siku 30, miezi saba ya siku 31, mwezi Februari wa siku 28 katika mwaka mfupi, na mwezi Februari wenye siku 29 katika mwaka mrefu. Huitwa “Kalenda ya Julius”.

Baadaye wanasayansi waligundua tena kuwa mzunguko wa dunia hauchukui siku “365.25” pekee, bali huchukua siku “365.24218967.” Hapa kuna tofauti ya siku “0.00781033,” sawa na dakika “11.2468752.” Yaani, kimakosa, “Kalenda ya Julius” ilikuwa imeongeza dakika “11.2468752” katika mwaka mzima.

Kanisa Katoliki lilianza kutumia kalenda ya Liturijia inayofuata mantiki ya “Kalenda ya Julius” mwaka 325. Lakini, mwaka 1582 Papa Gregory wa 13 aligundua makosa hayo yaliyo kwenye “Kalenda ya Julius.”

Hivyo, Papa akakosoa dosari husika kwa kuunda kalenda mpya, ikaitwa “Kalenda ya Gregory”. Baadhi ya Wakristo waliikataa mantiki iliyoongoza utengenezwaji wa “Kalenda ya Gregory” na kuendelea kutumia “Kalenda ya Julius.”

Hivyo, tangu mwaka 325 hadi leo imepita miaka 1697. Kwa kuzingatia tofauti ya siku “0.00781033” tulizoona hapo awali, hesabu ya kuzidisha inaonyesha kwamba “Kalenda ya Gregory” inaitangulia “Kalenda ya Julius” kwa siku “13.25413001.” Huu ni wastani wa siku 13 na robo.

Hivyo, wakati Wakristo wanaofuata “Kalenda ya Gregory” wanaposherehekea Krismas ya Desemba 25, wale wanaofuata “Kalenda ya Julius” watasubiri hadi Januari 7, yaani siku 13 baadaye.

Lakini pia, kuna Wakristo wanapinga Krismas ya Desemba 25 na kukataa Krismas ya Januari 7, wao wanaadhimisha Krismas ya Januari 6.

Kitabu cha “New Advent Encyclopedia,” kinasema hawa wanaoamini Yesu alizaliwa Januari 6 ni wafuasi wa Clement wa Alexandria, nchini Misri.

Clement alionyesha kwenye kitabu chake kiitwacho “Stromata,” kwamba Yesu alizaliwa “Januari 6.” Baadhi ya Wakristo walikubaliana na Clement hadi leo.

Kutokana na mkanganyiko huo wa siku aliyozaliwa Yesu Mnazareti, ndiyo maana yapo maeneo duniani yanaadhimisha kuzaliwa kwake Desemba 25, wengine Januari 6 na wapo wanaofanya kumbukizi Januari 7.

Mchungaji wa Kanisa la Mfalme Yesu lililoko Mwanjelwa, Mbeya, Ibarhim Kalembo akizungumza na Pambazuko kuhusu tarehe hasa ya kuzaliwa Yesu Kristo, alisema ni kweli kuna tofauti kulingana na maeneo husika, lakini uhakika kabisa hauelezwi kinagaubaga na Biblia yenyewe.

Amesema katika vitabu vingi vya vya Injili, ambavyo vikisomwa kwa pamoja, kuna utata wa siku ya kuzaliwa Yesu Kristo, kwani haitamkwi wala kuelezwa kwa uwazi.

“Hata wewe ni Mkristo, umewahi kusoma ama kuelezwa mahali kwamba Desemba 25 ndiyo hasa alizaliwa Mwana wa Mungu (Yesu), hakuna, lakini watu waliamua iwe hiyo Desemba 25 kwa wengi, pamoja na kwamba wapo wanaopinga tarehe hiyo,” ameongeza mchungaji huyo ambaye amesema ana shahada ya uzamili katika teolojia.

Anaeleza kuwa mvutano wa siku ya kuzaliwa Yesu huenda usifike mwisho na labda unaweza kutatuliwa na Yeye mwenyewe siku atakaporejea na endapo atatoa nafasi ya kuulizwa maswali.

“Hili swali limetushinda, limewashinda hata wakongwe wa historia ya maisha ya Yesu, wakiwamo Wayahudi wenyewe, huenda siku nzuri ya kupata jibu na tutakapomuona Mwenyewe,” ameongeza.

Chanzo: Gazeti laPambazuko, Toleo la Jumatatu, Desemba 26, 2022-Januari 1, 2023, ukurasa wa 10-12.
Tatizo mnalazimisha Ukiristo iwe ni Dini, wakati ata Yesu mwwnyewe haijui hiyo dini
 
Yesu huyo hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Ndio maana hata kuzaliwa kwake hakujulikani kwa vile Yesu ni Fictional character invented by religion to scam people.
 
Kwenye hiyo picha ya huyo jamaa aliyenyoosha vidole viwili kuna wahuni walim edit wakamshikisha fegi kati kati ya hivyo vidole
REJEA AMRI 10 ZA MUNGU usijifanyie kitu chochote chochote kilichopo juu mbinguni wala kukitumikia,kukiabudu sasa mapicha ya yesu katika torati ya musa haitakiw au katika taifa la Israel mpaka Leo hakuna hiko kitu
 
Ndugu, sijasema ni DHAMBI au Si DHAMBI kusherehekea!!

Nilichowauliza wakristo, Kanisa, maelekezo ya kusherehekea Christmas tarehe 25 December wameyatoa wapi?

Je ni maelekezo ya Roho mtakatifu kusherehekea Christmas tarehe 25 December na BIRTHDAYS?

Karibu[emoji120]
Hili swali lako halijibiki kwasababu wafia dini wamelevywa na mvinyo wa dini
 
Kwako wewe ushahidi ni maandiko tu?

Utakuwa ni mlokole au msabato
Bila maandiko unathibitishaje ?
Au wewe ndio wale wafuasi wa Geodav anadai anaongea na Yesu kila siku huenda akina Gwajima, Mwamposya na Manabii wa digital wana majibu ya tarehe kwa kutumia njia ya mkato
 
KWANINI TUNASHEREHEKEA CHRISTMAS MWEZI 12?

Na@Frt.Shirima

Watu wamekuwa wakijiuliza, Ikiwa Bikira Maria alichukiwa Mimba Kwa uwezo wa Roho Mtakatifu katika Mwezi wa 6, je! Inakuwaje Yesu azaliwe Mwezi wa 12? Kwahiyo alizaliwa akiwa tu na miezi 6? (Rej. Luk. 1:26-45)

Ipo hivi; pamoja na maelezo Mengine sahihi juu ya kipindi ambacho Bikira Maria alichukuwa Mimba ( The Years Before the Common Era), maana Yesu alizaliwa mwaka wa 1, yapo maelezo Mengine ambayo huitwa FUNDISHO JUU YA CHRISTMAS kama tutakavyoona.
Kwanza wakati Bikira Maria anachukuwa Mimba, Ikumbukwe hapakuwa na Utaratibu wa kuhesabu miaka Kwa kwenda Mbele kama ilivyo Sasa (A.D), LAKINI PIA IKUMBUKWE CHRISTMAS HAIKUWEKWA MARA TU BAADA YA YESU KUZALIWA, Bali iliwekwa baadaye.

Tuanze hivi; Mwanzo wa Krismasi umechipukia kutoka tamaduni za kipagani na za kirumi. Warumi walisherekea sikukuu mbili katika mwezi Desemba (12).

Sikukuu ya kwanza iliitwa Saturnalia, ambapo waliisherekea kwa wiki mbili wakimheshimu mungu wao wa kipagani aliyeitwa Saturn (jina la moja kati ya sayari). Huyu kwao alikuwa mungu wa kilimo.

Sikukuu nyingine ni ya kuzaliwa kwa Mithra au mungu Jua (kwa sababu waliliabudu jua) ambayo ilifanyika tarehe 25 Desemba.

Sherehe zote mbili walizisherekea kwa kufuru ya hali ya juu ya kufanya zinaa na kunywa pombe nyingi.
Code:
Na kwa sababu mwezi Desemba ulikuwa na giza nene kuliko miezi mingine waliwasha mishumaa na kusherekea
usiku mzima.

Ukristo ulipokuwa ukienea bara la Ulaya, maklero wamisionari hawakuweza kutokomeza kirahisi tamaduni hizi zilizozoeleka kwa miaka mingi sana ( ilikuwa ni kazi ngumu Mno).

Na kwa sababu hakuna aliyefahamu kwa uhakika wote wa tarehe haswa ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo waliamua kutumia busara ya Roho Mtakatifu kuweka hapo hiyo tarehe ya kipagani ya kufanya ufuska wa kusherekea miungu yao (mungu Jua) na badala yake kusherekea kuzaliwa kwa Yesu tarehe hiyo hiyo ya 25 Desemba (ambapo wapagani walisherekea mungu Jua).

Na tafsiri iliyokuwepo miongoni mwa wapagani, ilibadilika, ikawa kwamba Yesu ndiye Jua la kweli na la haki na takatifu, pambazuko la uumbaji mpya liletalo ukombozi dhidi ya ushetani wa kipagani na kuleta uzima wa utakatifu wa Mungu kwa watu wote wa ulimwengu kama ilivyoelezwa katika Maandiko Matakatifu na ndiyo Chimbuko la kusherehekea Christmas December 25.

Hii ilisaidia pia kuwaongoa wapagani wengi ambao Walikuwa wakiabudu wasichokifahamu, hivyo Maklero waliwafundisha habari za jua wa haki huyo, ambaye ni Kristo Yesu.

Tushirikishane Tone la Upendo.
Na.Frt. Shirima
 
Hatujui Yesu alizaliwa tarehe gani wala mwezi gani, ila tumechagua kusheherekea siku yake ya kuzaliwa Dec.25.
 
Duuhh nyie vipi.

Jamaan KANISA LA RUMI, Liliamua kuitumia siku tarehe 25/12 siku alozaliwa mungu wao wa Jua wakati ule wa RUMI YA KIPAGANI , Wakaihalalisha kua siku ya Kukumbuka Kuzaliwa Kwa YESU.


YESU HAKUZALIWA TAREHE 25/12.

Nchini URUSI Kwa wa Orthodox wao wanaazimisha Tarehe 7/1 .



JAMANI YESU HAKUZALIWA TAREHE 25/12 .


nikama tunavyokumbuka siku ya 17/3 .... Lkn sio siku alolalala.
it is true but we can do it in glory of our God JESUS ....
ile sikukuu ya kuzaliwa kwa mungu wa Jua Tammuz sisi tunaivunja na kufanya Kuwa Siku ya Kuzaliwa kwa Mkombozi Yesu.....

biblia imesema lolote unalo lifanya basi lifanye kwa ajili ya UTUKUFU wa Mungu.....

the most important thing for any christian is NOT A DAY but Accepting JESUS Christ as a survivor ....ndio maana hata Mungu hajaaona umuhimu wa kukuandikia siku ya Kuzaliwa Yesu katika biblia
 
Back
Top Bottom