Siku ambayo askari MP alipojitayarisha kumpiga risasi askari Sajenti kwa amri ya Mkuu wa Kambi ya Mgambo JKT

Yupo sahihi ila ana complicate sana.
Asante.
 
Mimi sio askari lakini ninachofahamu mimi kuruta ni askari ambaye ndio ameanza mafunzo ya awali kutoka kuwa raia na kuwa askari.
Private anakuwa amemaliza mafunzo lakini begani hana kitu,hajapewa V
Kuruta ni recruit. Kiswahili sahihi ni msajiliwa. Ukishajua hilo basi mengine yanatiririka tu.

Unajua jeshini bwana ni babu zetu walikuwa wanatamka maneno ya kizungu kwa Kiswahili.

Hivi unajua kuwa "Ajua" maana yake ni "as you were"

Utakuta afande amekazana nyuma geuka, ajua! Mnanitania, mnageuka kama babuni anataka kuona matako yake kama yamebadilika rangi, kurutaa!! Afandeee!
 
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
Basi kuna Mmasai mmoja mrefu sana tulikuwa nae jeshini. Sasas yeye mkiambiwa mbele tembea, alikuwa anajichanganya sana kuanza. Unakuta mara kaanza na mguu wa kushoto mara wa kulia. Sasa akitaka kurekebisha anajikuta anapeleka mkono na mguu wa upande mmoja mbele!

Sasa siku moja afande kamwambia, na wewe ndio kutembea gani huko unatuletea jeshini? Jamaa akasema afande, mie nasaliwa hivihivi siwezi!

Ennhe, greenkwanja wakarukia, afande, huyu anamtukana mama yake huyu, anasema mama yake nae anatembea hivi!!!

Yaani jeshini mara nyingine ilikuwa burudani sana🤣🤣🤣🤣
 
ndio akili ya askari inatakiwa iwe hivyo
 
Hapa analengwa luteni na sajenti ambaye ni MP, au MP analenga sajenti na Luteni? Yaani Luteni anaambiwa na CO ondoka, halafu CO tena anamwambia MP amlenge Sajenti - sijaelewa!
 
mkuu jeshini ni amri tu na nidham mbele bila hivyo kusingekalika kule
Na vitendo pia.
Kuna kambi moja nasikia CO alirudi kalewa alipofika lango kuu aliaamrishwa ajitambulishe, akakataa, then akapelekewa moto na kuelekea kuzimu!
 
Hapa analengwa luteni na sajenti ambaye ni MP, au MP analenga sajenti na Luteni? Yaani Luteni anaambiwa na CO ondoka, halafu CO tena anamwambia MP amlenge Sajenti - sijaelewa!
Hujaelewa kwa kuwa hujasoma thread vizuri.

Nimesema kwamba, mara ya kwanza niliandika ni Sajenti aliyetaka kupigwa risasi. Kuna jamaa alikuwapo Mgambo akaweka post kwamba hapana, yule jamaa aliyetaka kupigwa risasi alikuwa Luteni mmoja Msukuma bongebonge hivi, sio sajenti. Kwa hiyo nikarekebisha, ila sasa siwezi kurekebisha kichwa cha thread. Ndio maana kuna huo mkanganyikano
 
Sawa.
 
🤣🤣🤣 Nadhani ndio maana waliamua kuwawekea bia zao za bei chee ili wasije kunywa uraiani
Dah hivi pale kawe msasani bado ipo ile bar ya jeshi.
Tulikua tunalewa huku tunakula mbata na makonzi utatulia mwenyewe ukichoka utaondoka taratibu.demu ukimuona usitongoze wao huyo🤣🤣🤣
Ila sikukoma,kila w end niko mpk wakanizoea pale.
Aah hapo sasa wachumba walikoma na mi nikajifanya mjeshi basi kiulaini.
Ile sehemu ilikua na mandhari nzuri sana beach kule i mean view ya masaki na msasani ile mijumba,pale bar palikua takataka na upepo mzurii
 
Pale Mgambo miaka hiyo mazinguzi ya silaha yalikwepo saanaa , kuna afande mmoja alikwenda kwa nick name Kablasi, alipigwa marafuku kushika silaha baada ya kumtishia kumshuti ofisa mmoja kwa madai yakuonewa, aliamriwa kutogusa bunduki tena na akafanywa dereva wa punda kutoa mboga garden na kuleta kikosini, tembea yenyewe ya kablasi ilikuwa burudani, wazee wa miaka ile mupo na story za afande kiwembe kata madem
 
Nilipangiwa kwenda hiyo kambi, wakati tunajiandaa kwenda utaratibu wa kwenda JKT kwa lazima ukafutwa.

Nyongeza nyingine:
Sasa hivi unakula kuku kwa mrija pande zipi kamanda?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…