Siku hayati Magufuli aliposimama imara kutetea wamachinga, mbele ya Samia

Siku hayati Magufuli aliposimama imara kutetea wamachinga, mbele ya Samia

Bado sijaona sababu ya msingi kabisa ya kuwaondoa wamachinga barabarani.

Kama wanaziba njia na wanakaa kwenye mifereji ilo linazungumzika na inawezekana kuwasogeza sio kuwafukuza kama mbwa. Hii nchi ni ya kila mmoja.

Kuna watu nimeona wanasema nchi za weupe hakuna wamachinga....nawaambia watembee waone kuna nchi wamachinga mpaka kwenye reli.

Kuna watu wanajiona wameyaweza maisha..
Ana cheo, ana gari ana nyumba familia inakula vizuri n.k unategemea afanye nini juu ya wamachinga?
Atakwambia wamachinga wanaziba barabara, wanaharibu taswira ya mji n.k

hakuna nchi ambayo haina wamachinga duniani hapa...
Ila hapa kwetu kunaviongozi wapumbavu hivi kwao machinga ni kero!
 
Nchi. Hii bwana,ajira hakuna,watu wameajiajiri kwenye umachinga,badala ya Serikali kuwatafutia utaratibu mzuri wa kufanya biashara,serikali inawafukuza kama inatoa kinyesi,sasa mnawafukuza waende wapi?waishi vipi?
Si wajiunge hata wa5 na wakodi fremu jmn?.
Mjini pale watawekwa wapi?.
 
Magufuli alikuwa anavunja sheria alizozikuta.
Kwamba hakuna kipengele cha uhuru wa kutafuta kipato 😣😣😣 wale ni watanzania halali wanaotafuta kula yao bila kukaba na kunyang'anya. JPM aliandaa utaratibu mzuri tu wa kuwatafutia vitambulisho
 
Serikali isikwepe wajibu wake, kama haiwezi kutafuta permanent solution basi itafute temporary solution. Hawa watu wanafukuzwa wanaenda wapi?
 
Kwamba hakuna kipengele cha uhuru wa kutafuta kipato 😣😣😣 wale ni watanzania halali wanaotafuta kula yao bila kukaba na kunyang'anya. JPM aliandaa utaratibu mzuri tu wa kuwatafutia vitambulisho
Huo ndo ujinga tunaouona sasa.
Kila mwenye duka Kariakoo anafunga duka lake, halipi kodi, na anapanga bidhaa zake nje ya duka kwa malipo ya shs 20,000!
 
Kumbe hata Mwendazake aliona kwamba wamachinga wanahitaji kuwekewa utaratibu mzuri ndio wahamishwe. Ndio agizo la Mama Samia pia. Hawatofautiani.
 
Kwenye hiyo video JPM anataka wapewe utaratibu mzuri wa kufanya biashara kabla ya kuwaondoa.

Wapewe na nani ? sheria tayari zipo tatizo letu ni utamaduni wa kulalamika. Hawa wamepewa sehemu lakini wanataka kufanya kila kitu wanavyotaka bila kufuata utaratibu. Tumshukuru Raisi Samia kwa kuweka sheria mbele
 
W
Baadaye huo utaratibu ulipoanza kuwekwa akafoka sana, akasema waachwe wauze popote wanapojisikia na wasisumbuliwe
Hapo unadanganya!! Alichokataa ni kuwaondoa bila kuwaonesha na kuwaandalia sehemu sahihi! Akatolea mfano wa kigamboni ambako wamacninga walipewa sehemu maalumu ya kufanyia biashara zao
 
Kwenye hiyo video JPM anataka wapewe utaratibu mzuri wa kufanya biashara kabla ya kuwaondoa.
Mbona hata yeye hakuwawekea utaratibu zaidi yakuwasaidia kuvunja sheria hivi ni kweli barabara ziwe ndio frem zamaduka tatizo wotendio haohao na ce kwa mizaha hatujambo
 
Huo ndo ujinga tunaouona sasa.
Kila mwenye duka Kariakoo anafunga duka lake, halipi kodi, na anapanga bidhaa zake nje ya duka kwa malipo ya shs 20,000!
Huoni kwamba tumeokoa maelfu ya vijana ambao hawana ajira kwa kujiajiri hao wenye Maduka ni wachache tena wengi ni wakwepa kodi.

Kinachokutatanisha wewe kwamba hao wenye Maduka kutokana na kufunga Maduka yao hawaiingizii nchi mapato 😄😄😄 mapato yao ya naingia kwa njia ya kulipia mizigo Bandarini
 
Bado sijaona sababu ya msingi kabisa ya kuwaondoa wamachinga barabarani.

Kama wanaziba njia na wanakaa kwenye mifereji ilo linazungumzika na inawezekana kuwasogeza sio kuwafukuza kama mbwa. Hii nchi ni ya kila mmoja.

Kuna watu nimeona wanasema nchi za weupe hakuna wamachinga....nawaambia watembee waone kuna nchi wamachinga mpaka kwenye reli.
Na kwa nini tuwe na wamachinga kwenye reli, barabarani (sehemu za watembea kwa miguu, baiskeli) juu ya mifereji ya maji machafu, mbele ya vibaraza vya wenye fremu etc etc?? Huu ujinga umefumbiwa macho kwa muda mrefu, kijana badala ya kubaki kijijini atafute ekari mbili alime mbogamboga na kuja kuuza mjini ili apate fedha za maana unakuta jitu na nguvu zake limepanga Karanga na vitunguu barabarani halafu eti watu wanafurahia. Hili jambo lingekuwa controlled from the beginning wala hii shida isingekuwepo kwa sababu wamachinga wachache, tena wenye leseni wangepangiwa maeneo maalumu kama magulio (mfano Saba Saba kule Morogoro, au Maimoria kule Moshi). Pia baadhi ya barabara kwenye mitaa ingeweza kufungwa kila Jumapili ili wamachinga wenye leseni wakauze bidhaa zao pale kuanzia saa 12 asubuhi mpaka saa 4 usiku. Ni lazima mini yetu iwe katika mpangilio maalumu ili iweze kusafishwa kwa urahisi, kuimarisha ulinzi na pia kuwa na mandhari nzuri. Haiwezekani kila kijana eti awe mmachinga, kwanza hili neno mmachinga linapotoshwa kwa sababu asili yake ilikuwa wale vijana wanaotembeza bidhaa mitaani kwa miguu huku wakiwasaka wateja huko huko walipo (ofisini, sehemu za biashara au majumbani). Na enzi hizo walikuwa hawaleti usumbufu wowote kwani walikuwa hawana sehemu maalumu, sasa wanasiasa wakaanza kuleta mambo yao mara kaeni pale hamtosumbuliwa, mara tokeni hapo nendeni hapa na ndiyo wakazidi kujaa mijini wakikimbia huko vijijini kwao.
 
Na wewe unaunga mkono wakapange biashara hata kwenye mlango wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya? Hilo litakuwa ni Taifa la namna gani? JPM anafahamika alikuwa mtu wa kupenda sifa za hovyo hovyo especially kutoka kwenye makundi ya watu wenye uelewa mdogo katika jamii
Ungetulia kusikiliza ungemwelewa
 
Aliwatetea vipi ?

Ni sawa sawa wewe unazama kwenye maji alafu nahodha ambaye inabidi akuokoe anakutupia boya uendelee kukaa kwenye maji kwenye baridi badala ya kukutoa kwenye maji na kukupa taulo ujikaushe na kikombe cha kahawa uburudike...

 
Wavuvi wanalipa kodi?
Wakulima wanalipa kodi?
Wafugaji wanalipa kodi?

Mnachekesha na vijisababu vyenu [emoji23][emoji23]
Labda utakuwa unaishi Afghanistan wewe... Huwezi kuvua bila leseni, mkulima kuna ushuru wa mazao kwa gunia ukipeleka sokoni, mfugaji ukipeleka mifugo mnadani kuuza unalipa ushuru pale mnadani...
 
Kila miundombinu iliwekwa kwa kazi yake maalum, so wewe unafurahi wamachinga kuziba barabara, njia za watembea kwa miguu, mitaro ya maji, kupanga biashara zao mbele ya maduka ya watu, kutumiwa na wenye maduka kuwauzia bidhaa zao ili kukwepa kodi?? Huo ni ujinga!! Utaratibu wanaowekewa hawautaki, wanataka wabembelezwe, wao ni akina nani hasa hadi wabembelezwe kwenye hii nchi? Kuna makundi mengi tu nchi hii na hayabembelezwi, wao ni akina nani haswa?? Serikali makini haiwezi kuogopa kufanya jambo sahihi kisa eti watu watafanya vurugu, ni serikali dhaifu na iliyofeli tu ndiyo itaogopa kufanya maamuzi sahihi!! Waambie wafanye hizo vurugu zao then watajua nini maana ya mamlaka!! And sidhani kama kiongozi anayejiamini ataogopa kuwa unpopular kwa ajili ya kufanya maamuzi sahihi, viongozi wasiojiamini pekee ndiyo huwa wanapenda kuwatumia watu kama machinga kusaka sifa za kijinga...
Hujui kitu wewe...nao pia ni wananchi...wanna haki katika nchi yao...artikali ndiyo inayopaswa kuja na mkakati wa kujenga maeneo ya watu wa Aina hiyo kufanya biashara...uongozi ni pamoja na kuwa na majibu na ufumbuzi wa matatizo yaliyopo...wale eneo ambalo ambalo ni strategic ili wafanye biashara na walipe Kodi...
Ningekuwa ni Mimi kiongozi ningeifanya mnazi mmoja kwa Dar es Salaam kuwa sehemu ya wamachinga ningehamisha hospitali ya mnazi mmoja na majengo yote pale na kujenga miundo mbinu kwa wamachinga...ni gharama lakini maendeleo ni gharama...wekeza shilingi trillion mbili pale...vunja Kila kitu na wekeza kwa wamachinga pale..kwa Temeke, kinondoni ni hivyo hivyo unachagua eneo strategic na kuwekeza kwa wamachinga...kwa hiyo Kila mji, Kijiji ni hivyo hivyo...lakini viongozi wetu hawafikiri Bali ni kujaza matumbo tu...mijitu utaiona inatembea kwenye magari ya serikali na taasisi za serikali hayana fikra chanya vichwani...makao makuu ni Dodoma lakini mijitu kutwa kucha bado inasafiri na magari kuja Dar es Salaam..na magari yao wale hayafuatii sheria za barabarani spidi Kama zote na kuovertake ovyo barabarani na kusababisha ajali na vifo...
Tuna baachi ya viongozi wa ajabu kabisa...Bodi nyingi za wakurugenzi kwenye taasisi za umma zimejaa watu wa hovyo kabisa...hawana fikra mpya...kwenye halmashauri nyingi ni hivyo....mtu anatoa amri ya kuvunja vibanda vya wamachinga na anaona sawa...kiongozi wa namna hiyo ni mnyama na Hana akili na anayeshabikia ni hivyo hivyo...taifa kwa Sasa limekuwa la wamachinga kwa kuwa hakuna ajira na hi ilipaswa kuwa ajenda ya kitaifa...vijana wamemaliza chuo kikuu wanauza vocha, wanaendesha bodaboda na bajaji na wanna vibanda vya biashara lakini mijitu inaona hii ni sawa...wanajadili kujenga barabarani za lami mjini lakini wanasjindwa kujadili kujenga maeneo ya biashara ndogo ndogo...hovyo Sana baadhi ya watu nchi hii...nchi ina raslimali za kutosha lakini hakuna viongozi wenye positive thinking kwa watu wao...Leo wanasema hivi kesho vile...hopeless kabisa...
 
Hujui kitu wewe...nao pia ni wananchi...wanna haki katika nchi yao...artikali ndiyo inayopaswa kuja na mkakati wa kujenga maeneo ya watu wa Aina hiyo kufanya biashara...uongozi ni pamoja na kuwa na majibu na ufumbuzi wa matatizo yaliyopo...wale eneo ambalo ambalo ni strategic ili wafanye biashara na walipe Kodi...
Ningekuwa ni Mimi kiongozi ningeifanya mnazi mmoja kwa Dar es Salaam kuwa sehemu ya wamachinga ningehamisha hospitali ya mnazi mmoja na majengo yote pale na kujenga miundo mbinu kwa wamachinga...ni gharama lakini maendeleo ni gharama...wekeza shilingi trillion mbili pale...vunja Kila kitu na wekeza kwa wamachinga pale..kwa Temeke, kinondoni ni hivyo hivyo unachagua eneo strategic na kuwekeza kwa wamachinga...kwa hiyo Kila mji, Kijiji ni hivyo hivyo...lakini viongozi wetu hawafikiri Bali ni kujaza matumbo tu...mijitu utaiona inatembea kwenye magari ya serikali na taasisi za serikali hayana fikra chanya vichwani...makao makuu ni Dodoma lakini mijitu kutwa kucha bado inasafiri na magari kuja Dar es Salaam..na magari yao wale hayafuatii sheria za barabarani spidi Kama zote na kuovertake ovyo barabarani na kusababisha ajali na vifo...
Tuna baachi ya viongozi wa ajabu kabisa...Bodi nyingi za wakurugenzi kwenye taasisi za umma zimejaa watu wa hovyo kabisa...hawana fikra mpya...kwenye halmashauri nyingi ni hivyo....mtu anatoa amri ya kuvunja vibanda vya wamachinga na anaona sawa...kiongozi wa namna hiyo ni mnyama na Hana akili na anayeshabikia ni hivyo hivyo...taifa kwa Sasa limekuwa la wamachinga kwa kuwa hakuna ajira na hi ilipaswa kuwa ajenda ya kitaifa...vijana wamemaliza chuo kikuu wanauza vocha, wanaendesha bodaboda na bajaji na wanna vibanda vya biashara lakini mijitu inaona hii ni sawa...wanajadili kujenga barabarani za lami mjini lakini wanasjindwa kujadili kujenga maeneo ya biashara ndogo ndogo...hovyo Sana baadhi ya watu nchi hii...nchi ina raslimali za kutosha lakini hakuna viongozi wenye positive thinking kwa watu wao...Leo wanasema hivi kesho vile...hopeless kabisa...

Heshma yako 1954

John Pombe Joseph Magufuli atabaki kwenye historia ya nchi kama Mwamba, Shujaa na rais wa karne kwa mengi makubwa na mazuri aliyofanya.

Dunia itamkumbuka kama Rais bora kuwahi kutokea, rais aliyekua kwaajili ya nchi na wananchi wake, rais aliyeweza kuweka maslahi ya watu wake mbele bila kujali dunia ingemuonaje, rais aliyeweza kusema hapana kwa waliodhani maskini anatakiwa kusema ndio kwa kila tajiri

Aendelee kulala salama kipenzi chetu🕊😍🇹🇿🙏
 
Wote tuna haki na nchi yetu Ila nyie mnaujinga mwingi hamtaki kuwa wastaarabu.
 
Heshma yako 1954

John Pombe Joseph Magufuli atabaki kwenye historia ya nchi kama Mwamba, Shujaa na rais wa karne kwa mengi makubwa na mazuri aliyofanya.

Dunia itamkumbuka kama Rais bora kuwahi kutokea, rais aliyekua kwaajili ya nchi na wananchi wake, rais aliyeweza kuweka maslahi ya watu wake mbele bila kujali dunia ingemuonaje, rais aliyeweza kusema hapana kwa waliodhani maskini anatakiwa kusema ndio kwa kila tajiri

Aendelee kulala salama kipenzi chetu🕊😍🇹🇿🙏
Thanks Mama D....uko sahihi Sana kwa. andiko lako hili....sisi wengine tumebahatika kuona awamu zote zauongozi wa nchi hii..kwangu Mimi baada ya Nyerere kiongozi anayefuatia kwa mikakati ya dhati kwa nchi yake na hasa maendeleo ya watu wake ni JPM...this man was a true son of Tanzania and Afrika....Binafsi huwa namfananisha na Thomas Sankara aliyeuawa kwa mbinu za kijasusi za ufaransa...JPM alikuwa anaipenda nchi hii kwa dhati...ila yeye mwenyewe alijua asingedumu kwa muda mrefu na ndiyo maana alikuwa anasema amejitoa mhanga...mabeberu siku zote hawako tayari kumuona kiongozi wa nchi ya dunia ya tatu na mwenye msimamo Kama wa JPM...ndiyo maana viongozi Kama Chavez, Sankara, Ghadafi, Lumumba na wengine waliuawa...
Tanzania tulibahatika kuwa na JPM na itachukua miaka mingi TZ na Afrika kumpata Kama yeye....
 
Kwani Magufuli ndio nani? Alikuwa Rais ambaye alikuwa hajali kuhusu sheria za nchi, alijali kufurahisha genge tu kwa sifa za kisiasa
Machinga lazima wapangwe
 
Back
Top Bottom