Siku hizi kila mgahawa una banda la chipsi, na 90% ya wateja utawakuta wanakula chipsi

Siku hizi kila mgahawa una banda la chipsi, na 90% ya wateja utawakuta wanakula chipsi

Aramun

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2023
Posts
461
Reaction score
2,213
Hii trend sasa ni rasmi katika miji yote. 99% ya migahawa au cafe au vyovyote vile utakavyoiita, kwa nje lazima waweke na banda la chipsi.

Na 90% ya wateja utawakuta wanakula chipsi. Na wakila chipsi lazima wanunue na kinywaji kama soda cha kusukumia hizo chipsi, kama ujuavyo chipsi ni viazi na vina tendecy ya kukwama kooni.

Mimi sina neno na ulaji wenu, ila ndani ya miaka 10 ijayo tujiandae kuteseka na magonjwa yasiyoambukiza ambayo ni mabaya kushinda yanayoambukiza.

Sababu kuu ni kwamba mijini wengi wetu hatufanyi manual works, tunafanya tu light duties ambazo hazifanyi kuyatumia hayo mafuta tunayoyala kwa wingi. Mwisho wa siku yanakundikana mwilini na kuziba mishipa ya damu, hii inapelekea moyo kupata shida ya kusukuma damu na kuishia kwenye magonjwa kama Presha ya Kupanda na Kisukari.

Kwa sasa ukienda hospitali ya taifa Muhimbili, kwa siku hukosi wagonjwa wapya wa Kiharusi (Stroke) kuanzia 5 na kuendelea. Jiji la Dar miaka 10 kila nyumba itakuwa na atleast mwanafamilia mwenye magonjwa yasiyoambukiza hasa Pressure na Kisukari.

Chukua hatua, uamuzi ni wako kusuka au kunyoa.

IMG_20240529_134542.jpg


IMG_20240529_134517.jpg
 
Chips tu mbona hukemei bar na vi grocery zinazo uza bia, vinywaji vikali ambavyo vingi vinahatarisha maisha yetu na vipo vilivyochakachuliwa ingredients ambazo ni hatari sana kwa mwanadamu, tupunguze vitu ambavyo vinahatarisha afya yetu
 
Kwq vyakula vya kununua ukiwa mbalinna nyumbani naona angalu chips kwenye mazingira yasioeleweka basi chips ni chaguo kwanza kinapatikana chapu na pia unakiona kwa macho yako kinatoka jikoni na ni vya moto kabisa tofauti na vyakula vingine hujuwi kimepikwaje maji gani yametumika.
 
Hii trend sasa ni rasmi katika miji yote. 99% ya migahawa au cafe au vyovyote vile utakavyoiita, kwa nje lazima waweke na banda la chipsi.

Na 90% ya wateja utawakuta wanakula chipsi. Na wakila chipsi lazima wanunue na kinywaji kama soda cha kusukumia hizo chipsi, kama ujuavyo chipsi ni viazi na vina tendecy ya kukwama kooni.

Mimi sina neno na ulaji wenu, ila ndani ya miaka 10 ijayo tujiandae kuteseka na magonjwa yasiyoambukiza ambayo ni mabaya kushinda yanayoambukiza.

Sababu kuu ni kwamba mijini wengi wetu hatufanyi manual works, tunafanya tu light duties ambazo hazifanyi kuyatumia hayo mafuta tunayoyala kwa wingi. Mwisho wa siku yanakundikana mwilini na kuziba mishipa ya damu, hii inapelekea moyo kupata shida ya kusukuma damu na kuishia kwenye magonjwa kama Presha ya Kupanda na Kisukari.

Kwa sasa ukienda hospitali ya taifa Muhimbili, kwa siku hukosi wagonjwa wapya wa Kiharusi (Stroke) kuanzia 5 na kuendelea. Jiji la Dar miaka 10 kila nyumba itakuwa na atleast mwanafamilia mwenye magonjwa yasiyoambukiza hasa Pressure na Kisukari.

Chukua hatua, uamuzi ni wako kusuka au kunyoa.

View attachment 3002692

View attachment 3002694
Ungejua vile sipendi chips. Ila kuna jamaa yangu kila akitoka kazini anabeba na chips sijui haoni vyakula vingine
 
2022-2024 nimekula chipsi mayai ya kienyeji mara 5, nyama ya ng'ombe ya kubanika mara 12.
2010-2024 soda fanta orange mara 2 tu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Back
Top Bottom