Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #61
Kolola,Umuhimu wa hii khabari upo hapo
Afrika ya Kusini au Tanganyika?Kolola,
Kleist Sykes...
Kleist Sykes ni mmoja katika wazalendo ambae historia yake imo ndani ya Dictionary of African Biography (DAB).
Yeye ni muasisi wa African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933.
DAB ni volumes 6 na ulikuwa mradi wa Oxford University Press, New York na Harvard.
Kolola,Afrika ya Kusini au Tanganyika?
Sisi wafia dini ya islamia brain zetu haiziweki kwenye kumbukumbu jina lolote la mkristo.Muulize huyo Mzee, kule St Joseph shule ya Kanisa, katikati ya jiji, alikokuwa anasoma miaka mingi, hakufahamiana au kujenga urafiki na mtu yeyote asiye Muislamu? Hata Baniani?
KumbeKolola,
Kleist kazaliwa Pangani
1897.
Mama yake Mnyaturu jina lake Kwemah.
Mtoto wa miaka 3 hadi 4 hawezi kukumbuka kupelekwa clinic halafu akaona kitu ambacho SIYO visually appealing au special kimaumbo au kivyovyote kama simu ya mezani, halafu aliweke tukio hili kwenye long term memory yake.Njabu...
Mimi nitaeleza niyajuayo na kuyakumbuka wako wengi wananiamini.
Lakini ikiwa wewe utaniona mimi muongo hiyo ni bahati mbaya.
Hivyo mzee wewe ni mnyamwezi au mmanyema kwa asili?N...
Lakini ili historia ipendeze inahitaji pawepo matukio ya kuhadithiwa.
Nina makala nimepata kuandika miaka ya nyuma kuhusu mitaa.
Nikiipata In Shaa Allah nitaiweka hapa.
Ngabu...Mtoto wa miaka 3 hadi 4 hawezi kukumbuka kupelekwa clinic halafu akaona kitu ambacho SIYO visually appealing au special kimaumbo au kivyovyote kama simu ya mezani, halafu aliweke tukio hili kwenye long term memory yake.
Ruta....Hivyo mzee wewe ni mnyamwezi au mmanyema kwa asili?
Itabido jamii forum ijivunie sana wewe kuwa member active kabisa tena na umri huo..SIKU NILIYOIONA SIMU KWA MARA YA KWANZA ODEON CINEMA 1955 AU 56 AU NYUMA YA HAPO KIDOGO SIJAVUKA UMRI WA MIAKA MINNE
Nakumbuka kama jana vile.
Nilikuwa mgonjwa na baba yangu mdogo Mzee Issa akanichukua kunipeleka hospitali.
Ilikuwa usiku lakini si usiku mkubwa kiasi cha saa moja hivi.
Nina hakika na hili kwa kuwa Mzee Issa kanibeba tunatoka nyumbani Mtaa wa Kipata (Sasa Kleist Sykes Street) kwa miguu na nawaona watu mtaani njia nzima hadi tunafika New Street tunavuka Mnazi Mmoja tunapita kushoto tunaelekea Sultan Street (Libya Street).
Hapa Mnazi Mmoja palikuja kujengwa Mnara wa Uhuru.
Siku zile Mnazi MMoja ile ilikuwa uwanja mtupu hauina chochote ni mchanga mtupu.
Tunaingia Ring Street (Sasa Jamhuri Street) tunapita pembeni ya Odeon Cinema tunaingia mitaa ya Uhindini jirani na Msikiti wa Sunni kulikuwa na hospitali maarufu sana ya daktari wa Kihindi nakumbuka ingawa sina hakika jina lake lilikuwa kama Dr. Koya.
Mama zetu wakimsifia sana kwa kutibu watoto.
Hii hospital imedumu hapo kwa miaka mingi hadi mimi nimekuwa mtu mzima nikipita pale nikiiona.
Baada ya kutibiwa baba yangu mdogo Mzee Issa miaka ile alikuwa kijana akawa ananirudisha nyumbani.
Ndipo tulipopita tena Odeon Cinema tukaingia ndani kwenye call box (kibanda cha simu) kilichokuwa pale ndani.
Baba yangu alikuwa kazini akifanyakazi Telephone Exchange.
Jumba hili hadi leo lipo.
Mzee Issa akatia pesa kisha akapiga simu kuzungumza na baba yangu kumfahamisha kuwa kanipeleka hospitali na nimetibiwa.
Mzee Issa akanipa simu nimwamkie baba yangu.
Sikuweza kuzungumza.
Miaka mingi ikapita.
Siku moja nikamhadithia Mzee Issa habari hii.
Alishtuka.
Akawa kashangaa kisha akaniuliza, ''Mohamed unakumbuka habari hii?''
Ulikatazwa kwenu kuwa na ukaribu na watu wasiyo wa imani yako katika makuzi, au hukumbuki kuwahi kuwa na urafiki na mtu yoyote asiye wa imani yako? Inakuwaje kwa mtu ambaye umesoma shule za kanisa siyo chini ya mbili? Hiyo ya msafara wa Dada ws Malkia mtoto anaweza kuweka kwenye long term memory sababu ni tukio la kipekee kwa maana ya umati kukusanyika pembezoni mwa barabara, magari mengi na Mhusika Mkuu kuwa Mzungu wa kike. Naamini hata ingekuwa Ulaya enzi hizo watoto wa umri huo wengi wana kumbukimbu ya kumtupia macho kwa mara yao watu wenye ngozi nyeusi.Ngabu...
Nilikuwa napitia na mhariri mswada wa kitabu nilichoandika na kuna mahali nimeeleza kisa nilichokiona nikiwa mtoto wa miaka 4.
Yule mhariri akawa haamini kama ulivyokuwa huamini wewe.
Nikamhadithia mambo mengine niliyoshuhudia.
Akazidi kushangaa.
Princes Magret alipokuja Tanganyika 1956 nimeuona msafara wake ukipita Kitchwele Street.
Nakumbuka mpaka leo na wapi tulisimama.
Tulisimama Mtaa wa Sikukuu na Kitchwele nje ya duka la Toti.
Natafuta picha nitaiweka hapa In Shaa Allah.
Nilikuwa na miaka minne.
Sure hata mm kuna matukio nakumbuka nikiwa na miaka 3 au 4.Ngabu...
Nilikuwa napitia na mhariri mswada wa kitabu nilichoandika na kuna mahali nimeeleza kisa nilichokiona nikiwa mtoto wa miaka 4.
Yule mhariri akawa haamini kama ulivyokuwa huamini wewe.
Nikamhadithia mambo mengine niliyoshuhudia.
Akazidi kushangaa.
Princes Magret alipokuja Tanganyika 1956 nimeuona msafara wake ukipita Kitchwele Street.
Nakumbuka mpaka leo na wapi tulisimama.
Tulisimama Mtaa wa Sikukuu na Kitchwele nje ya duka la Toti.
Natafuta picha nitaiweka hapa In Shaa Allah.
Nilikuwa na miaka minne.
Covid...Sure hata mm kuna matukio nakumbuka nikiwa na miaka 3 au 4.
Tena ni matukio ambayo sisahau kabisa.
Ngabu...Ulikatazwa kwenu kuwa na ukaribu na watu wasiyo wa imani yako katika makuzi, au hukumbuki kuwahi kuwa na urafiki na mtu yoyote asiye wa imani yako? Inakuwaje kwa mtu ambaye umesoma shule za kanisa siyo chini ya mbili? Hiyo ya msafara wa Dada ws Malkia mtoto anaweza kuweka kwenye long term memory sababu ni tukio la kipekee kwa maana ya umati kukusanyika pembezoni mwa barabara, magari mengi na Mhusika Mkuu kuwa Mzungu wa kike. Naamini hata ingekuwa Ulaya enzi hizo watoto wa umri huo wengi wana kumbukimbu ya kumtupia macho kwa mara yao watu wenye ngozi nyeusi.
Covid...Itabido jamii forum ijivunie sana wewe kuwa member active kabisa tena na umri huo..
Hongera sana.
Waanzilishi wa Saigon walikuwa Waarabu au waingereza?Niache....
Saigoon ilikuja 1967 baada ya mgawinyoko wa club yetu ya kwanza Everton.
Sote tulikuwa shule ya msingi.
Mimi nilikuwa na umri wa miaka 15 wastani wa umri wetu sote ulikuwa katika hapo yaani miaka 15, 16, 17.
Wala hatukujua kama hii club itakuwa maarufu kiasi hiki.
Picha hiyo hapo chini ni Saigon Club 1980s Mtaa wa Sikukuu na Narung'ombe.
View attachment 2497529
Kulia: Marehemu Yunus, Mussa Shagow, Mohamed Said, Mkongo na Marehemu Ghalib Hamza(Guy).
Saigon katika 2020s:
View attachment 2497531
Kulia: Marehemu Nusura Faraj, Manzi, Marehemu Abdulkarim Shah (BuljiI) chini kulia Shariff Pazi na Mshike.
Proved,Waanzilishi wa Saigon walikuwa Waarabu au waingereza?
Covid...Itabido jamii forum ijivunie sana wewe kuwa member active kabisa tena na umri huo..
Hongera sana.
Njabu...Alipokuwa na miaka 4 kakumbuka hadi alipokatiza mtaa wa Kleist Sykes SIKU MOJA?!! Mitaa yote ya Kariakoo hadi kufika Odeon Cinema ya wakati huo kaicha.
kumbe mzee wangu mtu wa bara weweCvez,
Aaah bwana kwani ni jambo kubwa hilo?
Tusingeweza sote tuzaliwe Dar es Salaam.
Nikushangaze.
Mama yangu kazaliwa Musoma.
Baba yake Sheikh Mohamed Mvamila kazaliwa Mkamba akaenda Musoma katika ujana wake kusomesha dini.
Amekufa Musoma na kazikwa Musoma.
Alitoka Mkamba na mkewe bibi yangu Mwatum bint Rajabu Mgeni kabila Mluguru hawajapata mtoto huko Musoma ndiyo wakamzaa mama yangu na ndugu zake wanne.
Baba yangu kazaliwa Tabora lakini kakulia Dar es Salaam.
Baba yake kazaliwa Shirati Musoma.
Babu yake kazaliwa Bukavu Belgian Congo kaingia Germany Ostafrika mwishoni 1800 kama askari katika jeshi la Wajerumani na akafikia Shirati na hapo ndipo babu yangu Salum Abdallah alipozaliwa.