Siku ya Wanawake Duniani isitumike kutengua maandiko ya vitabu vitakatifu

Waefeso 5:22-24 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo na wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Kolosai 3:18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.

1 Petro 3:1-2 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno
 
Safi sana mkuu!

Shida ipo kwa hawa kina Mwamposa badala ya wahubiri mistari konki kama hii wao wako busy kulisha watu keki
 

Umemaliza..kila.mtu asimame kwenye nafasi yake hapo upendo wa kweli utatamalaki...
Bdw sio wanawake wote wanawish kuolewa...na sio kila mwanamke kaandikiwa kuolewa...
Wanawake wote 100% wanataman kuwa na watoto
 
Maarifa na Akili unayapimaje kwa wote wawili!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Inaonekana tu..hata watoto wanakua wanaona..mfano mm leo hii hata niwe na shida kubwa ipi ya hela namwambia kwanza mama amwambie baba...upo? Kwasabab toka nakua namuona baba ndo anaprovide kila kitu...na ni hvyohvyo kwa familia nyingine mama ndo kila kitu.. mie mpak leo hom hata chumvi iishe baba anatoa hela...ndo utagundua hapo nan ana power
 
Kwani wewe Baba yako ni Mzanzibari!? Maana hao ndiyo Wanaume wanaoenda hadi sokoni !!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Katika kutafuta tafuta uku na kule nilipata baadhi ya wanawake waliozalisha siku ya Wanawake Duniani kule Beijing nilitaka kujua historia yao kuanzia makuzi nk.nikagundua %90 ya wanawake wale walikuwa wapagani hawakujiusisha na mambo ya Mungu kabisa.
Jambo jingine walikuwa hawana wanaume waliishatengwa walikuwa wanatafuta mali na vyeo.
Mwisho kabisa walikuwa wanatafuta nafasi ili walipe visasi kwa wale waliowatenda.
Sasa leo mtu amejazwa Roho anamsaport mpagani kwa kutafuta 50/50 ukifatilia mitandaoni wale wafurukutwa niwale waliolelewa na wazazi upande mmoja (mama)
Sasa ukiuliza aya mambo mnayatoa kwenye Biblia gani wote hawana majibu.
Ukitafuta wanaume wanaosaport mpango huu nao ni wale waliokimbiwa na baba zao wanasahau jambo moja tu thamani yao ipo muda wanaotegemewa kulipa karo na mahitaji muhimu ao watoto wakikua wataimba nani kama mama mtoto wa kiume akioa anataka akae na mama uko mbali aliko baba anabaki nyumbani anaangaika kama hawana mfanyakazi mzee yumo anapika anafua na mambo mengine kibao mama itamchukua kama mwezi kurudi akifika mala binti kajifungua akienda uko mwezi au miwili mzee yumo tu baada ya muda mzee kwisha msongo wa mawazo nk.kinachofata mnakijua wenyewe.

Adamu alipoteza nafasi ndio maana Hawa alitatuta hekima za nyoka.
Hii 50/50 Nikukiuka maelekezo ya Mungu aliyemfanya Mwanamume kuwa matawala.
Swali kwa wanawake wa Kilokole mnadai haki zipi?
Naona umu wengine ni wachungaji wengine manabii nk.
Ukiwauliza wanaume Walokole wanaosaport wake zao kudai 50/50 ni haki ipi humpatii mke wako mpaka aandamane?
Namaliza kwa kuwataadhalisha wanaume asa wanaomjua Mungu kuacha kufata mkumbo yatawakuta yaliyomkuta Samson.
 
Maandiko yamesema baba ni kichwa cha familia, ila hayajasema mama ni mkia! Acha upotofu na kashfa kwa wanawake! Kama baba ni kichwa, na Mama wa familia ni msaidizi, kwa nini usimfananishe na shingo? Mkia una kazi gani katika mwili wa binadamu? Maana sidhani maandiko yanaongelea kichwa cha yeyote zaidi ya binadamu.
 
Mfano mzuri muangalie yule dada mwanasheria wa kule twiter mwana fatuma
Kuna mwingine anaitwa Joyce Kiria...hao wana kasoro gani wanashindwa kukaa na waume? Yan wapo wengi mno
 
Kama Hawa wanawake wanaosifiwa leo ndo Hawa Hawa wa siku zote Bhasi hii Dunia Bila Unafiki Haiendi
 
Vitabu vimemfanya mwanamke kuwa chini ya mwanaume, sasa kuna ulazima mwanamke nae apambanie haki yake, kuna wanawake wengi wenye akili na maarifa kuliko wanaume wengi, wanayo haki ya kuwa juu ya wanaume kama wamewazidi akili na maarifa.
Akili na maarifa pekee hayatoshi kumfanya mwanamke akawa juu ya mwanaume, sababu Historia imeandika juu ya wanawake walio kuwa na sifa za wanaume ila walikuwa chini ya wanaume. Ujuu wetu sisi Wanaume dhidi ya Wanawake ni silika na hii ndiyo inaainisha majukumu.

Mwanamke apambanie haki yake ipi na umejuaje kama hiyo ni haki yake ?

Maarifa na akili ya Mwanamke anatakiwa aitumie nyumbani katika kulea na kusimamia mali za mume na kumshauri, ila Mwanamke kutska kuwa jui ya Mwanaume ni kwenda kinyume na asili na ni kujitafutia matatizo kama wanayokutana nayo leo hii, japo wanajidai ni hamnazo.
 
[emoji83] [emoji83] [emoji83] [emoji83]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…