Sikubaliani na watu wanaoamini Fid Q ni genius

Sikubaliani na watu wanaoamini Fid Q ni genius

kwa mtazamo wangu , si genius, ila "usinitreat kama 2nd class person utakua umefanya 1st class mistake" by fareed - Am proffesional.
 
Fid ni jeshi la mtu mmoja

Sikopeshi kwa nguvu ya hoja

Niko mbio zaidi ya race na huu ujio sio wa verse moja
 
Hauna uelewa wa mambo mengi, Galileo alibishana na watu wengi sana kuhusu idea zake na kuonekana ni ovyo mpinga kanisa lakini after some years wakaja kugundua walimhkum mtu kwa kosa lao. Hiii ni kuonyesha genius anaweza ona kitu ambacho wew IQ ndogo unaona si kweli

Kama hilo jibu alilotoa FID Q, lipo kabisa katika zile UNIVERSAL LAW OF ATTRACTION,,,,,Ongeza maarifa mkuuuu.

Usikurupuke, tuendeleee kujifunza.
 
hana ubunifu wowote.
kama wewe sio msomaji wa vitabu vya kiswahili basi utaamini kuwa Huyo jamaa ni mbunifu, lakini kila anachokiandika kilishaandikwa na akina Andanenga.

jiulize ni msemo wake upi au methari au nahau iliowahi kuwekwa kwenye kumbukumbu kuwa hii ni Brand ya Fareed?
Huo ndio ubunifu ninao usemea mimi.
Kumbuka, sio watu wote wenye uwezo wa kuunga maneno na mithamiati kadhaa na kufanya msistari ya hip-hop ikasikilizika.
Ubunifu ni kufanya kitu kizuri kwakutumia kitu au vitu vingine ambavyo vilikuepo.
 
Fid Q mkaliiiiii anaandika mpaka ujue kamaanisha nini lazima akili yako ifanye kazi
 
[emoji14] [emoji14] Sawa, ila mimi sio shabiki kabisa wa fid q na nimezungukwa na raia za kutoka Arusha kibao wasiomkubali maana wale ndio awampendi sana jamaa maneno yao ni yale yale jamaa anacopy anacopy , ila mimi sijawahikubali ilo kusema jamaa sio mzuri kisa anacopy..Heshima kwake [emoji122] [emoji122]
Huwezi ku copy bila kutafuta sana.
Pia mashairi yenyewe lazima ujue kiingereza kwanza.
Kisha kuyapeleka kwenye kiswahili ili yalete maana. Viva Fid viva
 
kajibu vizuri sana swali aliloulizwa na nikki,fid genious coz on the sport kaweza kutoa jibu linalosound right na reasonable...thus what we call genious mkuu
 
Tuanzie kwenye elimu yake kwanza, laiti angesoma angefika mbali sana ni kichwa design
 
fiid q yuko sahihiwewe mleta uzi. its all about psychology.wat u think impact you.hyo inaitwa belief system.nenda kasome kwenye kitabu cha AWAKEN THE GIANT WITHIN cha TONY BOBBINS
 
Humu leo sijui kama patatosha!

Nimekuwa nikijaribu kudigest sifa ambazo wadau wengi wamekuwa wakimpatia msanii Fid Q, kwamba ni mtu makini, mwenye upeo wa hali ya juu.. Kiukweli nimejitahidi sana kuamini lakini leo acha tu nizitendee haki instincts zangu za muda mrefu..

Si kweli. Fid hana hiyo gene!

Mwaka jana mwanzoni, huko Marekani alitokea mtoto wa miaka 14 aliyebuni saa ambayo ilikuja kudhaniwa ni bomu hivyo kumkamata na kumtia kizuizini kwa masaa kadhaa kabla ya kubainika kuwa ni saa tu isiyo na madhara na baadae kuitwa Ikulu na Rais Obama kupongezwa kuwa ni genius.

Nilichopenda kwenye mkasa huo, ni jibu la mwalimu wake pale alipoulizwa kuhusu 'ukipanga' wa huyo mtoto na anajisikiaje kufundisha mwanafunzi genius darasani kwake.

Alisema hivi, "Namjua vizuri Ahmed, sio mwanafunzi genius kama inavyodaiwa, ila ana jitihada sana ya kusoma na kujifunza. Jitihada zake ni zaidi ya wanafunzi wote ninaowafundisha".

Sasa hii ni kama ambavyo Fid anatajwa kuwa genius kutokana na uandishi wa tungo zake. Kwamba anafikiria sana na ni kichwa kuliko wasanii wote. Niseme ukweli, binafsi sikuwahi kuona hivyo, bali nimekuwa nikimwona kama msanii anayejitahidi sana kujifunza kuliko wasanii wengine. Hapa tusichanganye.

For someone to be genius, ni lazima awe innovative! Lazima aache impact. Ni bora nikamfagilia MwanaFA angalau yeye ameacha misemo mingi kwenye lugha ya Kiswahili.

Kituko hiki hapa sasa..

Nikki wa Pili alipouliza swali kuhusu kwanini vichaa hawaongozi kuugua kipindupindu licha ya kula vyakula vichafu, Fid anajibu ni suala la Kisaikolojia. Eti, akili yako ukiiambia kwamba nikila hiki chakula kichafu nitaugua, utaugua kweli. Na ukisema sitougua, hutougua. Hivyo vichaa hawana hiyo time ya kujua kama ni kichafu ndio maana hawaugui. Nilichoka.


Huo ni mfano mmoja tu. Mwingine nitajazia kadri mada hii itakavyoendelea.

Poleni kwa kusoma mkeka!
 
Hakuna kitu ni baadhi ya wasukuma wenzake wanampa sifa
 
Media zina support bifu wanadai zinakuza muziki,wadau wana wasanii wabovu nyie wakali mtatoka vipi.
 
Hayakuhusu kama Rah P ,nakuja zaidi ya sister P ,Sijachuja sijavuja niiteeee MWANZA MWANZA.
 
Back
Top Bottom