Simba kuhudhiria wengi Simba day ni njia nyingine ya kuishinda Yanga nje ya uwanja

Simba kuhudhiria wengi Simba day ni njia nyingine ya kuishinda Yanga nje ya uwanja

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ni jambo zuri sana sisi wapenzi wa Simba kwenda wengi kwenye tamasha letu la Simba day. Ukweli kuujaza uwanja kuliko Yanga walivyofanya ni njia nyingine sahihi ya kutibu sonona iliyotokana na timu yetu kufanya vibaya ndani ya uwanja dhidi ya Yanga kwa misimu 2 mfululizo.

Kujaza huku kwa uwanja mapema kunachagizwa na Yanga kushindwa kuujaza uwanja kutokana na kulewa furaha za mafanikio msimu uliopita, viingilio vikubwa na tamasha kupangwa katikati ya mwezi watu hawana hela, na matumaini mapya ya usajili mzuri uliofanywa na uongozi wa simba. Wachezaji wa simba walishindwa kutupa furaha ndani ya uwanja na Sasa tunakwenda kuwakopesha imani zetu tena kwa msimu ujao.

Angalizo hapa ni moja tu kwa uongozi, bench la ufundi na wachezaji wa simba kuwa wasifurahie sana mashabiki kuujaza uwanja, taabu kwao itakuwa kubwa sana kama timu isipofanya vizuri tena kiwanjani.

Vinginevyo hongera sana Simba kwa kujitokeza kwa wingi kukata tiketi mapema.
 
Ni jambo zuri sana sisi wapenzi wa Simba kwenda wengi kwenye tamasha letu la Simba day. Ukweli kuujaza uwanja kuliko Yanga walivyofanya ni njia nyingine sahihi ya kutibu sonona iliyotokana na timu yetu kufanya vibaya ndani ya uwanja dhidi ya Yanga kwa misimu 2 mfululizo. Kujaza huku kwa uwanja mapema kunachagizwa na Yanga kushindwa kuujaza uwanja kutokana na kulewa furaha za mafanikio msimu uliopita, viingilio vikubwa na tamasha kupangwa katikati ya mwezi watu hawana hela, na matumaini mapya ya usajili mzuri uliofanywa na uongozi wa simba. Wachezaji wa simba walishindwa kutupa furaha ndani ya uwanja na Sasa tunakwenda kuwakopesha imani zetu tena kwa msimu ujao.

Angalizo hapa ni moja tu kwa uongozi, bench la ufundi na wachezaji wa simba kuwa wasifurahie sana mashabiki kuujaza uwanja, taabu kwao itakuwa kubwa sana kama timu isipofanya vizuri tena kiwanjani.

Vinginevyo hongera sana Simba kwa kujitokeza kwa wingi kukata tiketi mapema.
Hongera mtani, naona mmeongeza kombe jingine kabatini. Kombe la kujaza uwanja
 
Mwisho wa siku maumivu bado yako pale pale. Kwa simba hii bado naiona ni dhaifu sana kushindana kugombania vikombe na timu iliyokamilika kwenye kila idara, kama Yanga.
 
PR ya Simba imekaa poa ukweli PR ya Yanga bado iko chini na imejaa ujivuni
Tulitoa maoni kuwa kiingilio ni kikubwa na hamasa ni ndogo wakati mda ni mfupi lakini tukaishia kufokewa na kupewa mifano ya Manchester united au Liverpool tena walienda mbali na kutoa mfano wa real Madrid
Wasipojifunza kwa zama hizi za ushindani utashinda Kila kitu ila utaishia kupata mashabiki wachache
 
inaonekana Simba kujaza uwanja inakuuma sana, umesahau post yako ya kutaka serikali na TFF wapange viingilio.
Aliosema huko wenye akili wapo wawili hakukosea.
 
Weak area Kivipi mkuu? Wakati unalinganisha na Yanga, ilifaa pia ulinganishe na kima Cha chini Cha kiingilio kwenye events zote mbili.
Hakuna ubishi kuwa lengomama la matamasha haya ya vilabu ni kukusanya fedha kwaajili ya klabu, hata ukimhoji Mzee Dalali aliyeanzisha Simba day atakwambia lengo lilikuwa kukusanya pesa. Simba kima cha chini ni Sh. 5,000 na Yanga kilikuwa Sh 10,000, hii ni kusema kama kuwa yanga walihitaji watu 20,000 ili kukusanya sh. 200,000,000 lakini Simba watahitaji watu 40,000 ili kukusanya kiasi hichohicho cha sh. 200,000,000, ni hesabu tu. Hii ni kusema inawezekana Simba wakawa wengi lakini wakazidiwa mapato ya mlangoni na Yanga wachache. Kitu kikubwa kwa Simba ni idadi kubwa ya wanasimba watakaokwenda kujitibu sonona kwakutumia furaha ya tamasha la simba day.
 
Yanga timu kubwa yenye malengo ya kitoto na ya woga!! Timu iliyofika fainali kwenye kombe la losers haina ubavu wa kuweka malengo makubwa CAF champions league!! Malengo yake rasmi ni kufika hatua ya makundi basiii!! Je hapo wataweza kujilinganisha na Simba yenye malengo ya kufika nusu fainali? Mwenye macho haambiwi tazama!! Timu kubwa Tz ni wekundu wa msimbazi, ndio maana hawaanzii mchangani kama yanga kwenye CAF champions league 2023/2024!! Nawasilisha!!
 
SIKU KUBWA NA SIKU YA WAKUBWA INAHUDHURIWA NA WAKUBWA TU. KARIBU MAMA WA NCHI. WANAPOCHEZA WENYE NCHI MGENI RASMI NI MWENYE NCHI. BROTHER ACHA KUNUNA BROTHER MAMA SAMIA NI WA WOTE ATA WEWE BROTHER.
FB_IMG_1691141903938.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
PR ya Simba imekaa poa ukweli PR ya Yanga bado iko chini na imejaa ujivuni
Tulitoa maoni kuwa kiingilio ni kikubwa na hamasa ni ndogo wakati mda ni mfupi lakini tukaishia kufokewa na kupewa mifano ya Manchester united au Liverpool tena walienda mbali na kutoa mfano wa real Madrid
Wasipojifunza kwa zama hizi za ushindani utashinda Kila kitu ila utaishia kupata mashabiki wachache
Lengo la tamasha ni wadau kukusanya pesa za kuisaidia timu yao kutoka kwa mashabiki wa timu husika, na sio watu kwenda kushangaa na kuinyonya timu yao. Yaani huu ndio muda pekee ambao hata mashabiki wanaichangia timu yao kile walichonacho. Haiwezekani mule ndani nywe bia 5 za sh. 10,000, uangalie live show za wanamuziki wakubwa wengi na kuangalia live mechi kubwa ya timu kubwa kwa kiingilio cha sh. 5000 (2 USD) tu. Na ukumbuke kuwa hizi ni timu za wananchi ambazo wanachama wanamiliki 51% na mwekezaji 49%. Mchango wa wanachama hauwezi kuwa mdogo kiasi hiki,
 
Yanga timu kubwa yenye malengo ya kitoto na ya woga!! Timu iliyofika fainali kwenye kombe la losers haina ubavu wa kuweka malengo makubwa CAF champions league!! Malengo yake rasmi ni kufika hatua ya makundi basiii!! Je hapo wataweza kujilinganisha na Simba yenye malengo ya kufika nusu fainali? Mwenye macho haambiwi tazama!! Timu kubwa Tz ni wekundu wa msimbazi, ndio maana hawaanzii mchangani kama yanga kwenye CAF champions league 2023/2024!! Nawasilisha!!
Mipango si matumizi
 
Back
Top Bottom