Simiyu: Wananchi wavamia Kituo cha Polisi wakidai kuna matukio mengi ya Watoto kupotea

Simiyu: Wananchi wavamia Kituo cha Polisi wakidai kuna matukio mengi ya Watoto kupotea

Baadhi ya Wananchi wameandamana na kuvamia Kituo cha Polisi cha Lamadi wakidai askari Polisi wa eneo hilo wameshindwa kuwajibika wakidai kuna muendelezo wa matukio ya Watoto kupotea Mkoani hapo.

Baadhi ya Wananchi wengine pia walifunga Barabara ya Kuu ya Mwanza-Simiyu-Mara, baada ya tukio hilo inadaiwa Jeshi la Polisi limetumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya

Taarifa zaidi zitafuata

MAANDAMANO SIMIYU, RPC ASEMA “HALI SIYO NZURI NITAWAPA TAARIFA BAADAYE
Chanzo cha Maandamano inadaiwa baadhi ya Wananchi wanashutumu Polisi kutowajibika wakidai kuna ongezeko la matukio ya Watoto kupotea

Kamanda wa Polisi Mkoa, Edith Swebe amesema “Nipo kwenye eneo la tukio 'situation' sio nzuri, naomba mnipe muda niwape taarifa baadaye.”

Inadaiwa kuna uharibifu wa mali, Watu kadhaa wamejeruhiwa na Waandamanaji wameweka Magogo Barabara ya Mwanza-Simiyu-Mara.

==============

Wananchi wa mji mdogo wa Lamadi Wilaya Busega Mkoani Simiyu, wamelazimika kuandamana na kufunga Barabara kuu ya Mwanza - Lamadi - Mara kwa magogo huku wakiyarushia mawe magari kuzuia yasipite, kwa kile wanachodai kuchoshwa na matukio ya watoto kupotea ambayo wamesema kwamba yamekuwa yanatokea katika Mji huo.

Sintofahamu hiyo imedumu kwa takribani Saa Tano kuanzia Saa Tatu Asubuhi hadi Saa Nane Mchana ambapo Jeshi la Polisi na Askari, wamefika katika eneo hilo na kuanza kuwatuliza kwa kupiga mabomu ya machozi, wakiwatawanya wananchi wanaoandamana, huku magari ya abiria yakilazimika kusindikizwa na Askari ili kusaidia yaweze kupita katika eneo hilo kwa usalama pasipokupigwa mawe.

Kwa sasa hali ya utulivu imerejea katika eneo hilo huku jeshi la polisi likisalia maeneo hayo kwa ajili ya kuendelea kuimarisha ulinzi.


=============

Ngoja nimtag jamaa yangu mmoja hapa Lucas Mwashambwa
 
Ndugu zangu wasukuma na matumizi sahihi ya akili ni vitu tofauti,hapo wakiambiwa waorodheshe watoto waliopotea, hawana
We shoga, Wakoloni Waingereza walipotaka kuondoka watu waliowaona wenye akili wanaofaa kukabidhiwa nchi ni wawili tu, Msukuma Chifu David Makwaia na Mchaga Chifu Thomas Marealle.

Umewahi kujiuliza ni kwanini hawakumfikiria Chifu wako na Kikabila chako? Kilaza mkubwa we.
 
We shoga, Wakoloni Waingereza walipotaka kuondoka watu waliowaona wenye akili wanaofaa kukabidhiwa nchi ni wawili tu, Msukuma Chifu David Makwaia na Mchaga Chifu Thomas Marealle.

Umewahi kujiuliza ni kwanini hawakumfikiria Chifu wako na Kikabila chako? Kilaza mkubwa we.
Walimwandaa nyerere muda tu na wakampa nchi, usukumani watoto bado hunya kuzunguka nyumba
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema sitokuja kutoa miguu yangu kuingia barabarani kuandamana tanzania hii Ili ufe wengine waishi Jana Kuna jamaa KAPIGWA risasi kafa lamadi raia wanawakimbia polisi ndio ujue Tanzania usijifanye kielele aliyechomwa picha ya raisi mbeya Nate wameshazika Kuna mizee ambayo ilichezea maisha ujanani kwao Sasa hivi inawaambia vijana waandamane hicho kitu hakipo Kila nikiangalia Salio langu bank Hala unakuta mjinga mmoja humu mtandaoni anasema vijana tuingie barabarani kisa yeye ana njaa hua namuangalia nasemahivi kweli anaakili timamu Tanzania ni ya kuandamana
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema sitokuja kutoa miguu yangu kuingia barabarani kuandamana tanzania hii Ili ufe wengine waishi Jana Kuna jamaa KAPIGWA risasi kafa lamadi raia wanawakimbia polisi ndio ujue Tanzania usijifanye kielele aliyechomwa picha ya raisi mbeya Nate wameshazika Kuna mizee ambayo ilichezea maisha ujanani kwao Sasa hivi inawaambia vijana waandamane hicho kitu hakipo Kila nikiangalia Salio langu bank Hala unakuta mjinga mmoja humu mtandaoni anasema vijana tuingie barabarani kisa yeye ana njaa hua namuangalia nasemahivi kweli anaakili timamu Tanzania ni ya kuandamana
Kwanini uandamana wakati kila kitu kiko sawa........
 
Kama kichwa Cha habari kinavyosema sitokuja kutoa miguu yangu kuingia barabarani kuandamana tanzania hii Ili ufe wengine waishi Jana Kuna jamaa KAPIGWA risasi kafa lamadi raia wanawakimbia polisi ndio ujue Tanzania usijifanye kielele aliyechomwa picha ya raisi mbeya Nate wameshazika Kuna mizee ambayo ilichezea maisha ujanani kwao Sasa hivi inawaambia vijana waandamane hicho kitu hakipo Kila nikiangalia Salio langu bank Hala unakuta mjinga mmoja humu mtandaoni anasema vijana tuingie barabarani kisa yeye ana njaa hua namuangalia nasemahivi kweli anaakili timamu Tanzania ni ya kuandamana
Ndio umaiti aliousema Kenyatta! Wewe ni maiti. WEWE NI MAITI, MAITI , MAITI
 

Attachments

  • KENYATTA.mp4
    3 MB
Back
Top Bottom