Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza

Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza

Watu wenye madaraka wakishindwa kutumia akili wanamlaumu shetani.
Ingetumika akili kidogo tu ya mwendo wa kiasi wafiwa wasingekua na maumivu kiasi hiki.
Lkn mkuu anawahi, speed hiyo v eite spiti Mia arobaini, Sheria za barabarani tupa kule as if wazungu waliozitunga hawana akili
 
Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari ya waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

--
Rais Samia atoa salamu za Rambirambi

''View attachment 2076839

====


Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari la waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu akiwa eneo la tukio, Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

Amesema kati ya vifo hivyo kuna vifo vya waandishi wa habari wanne na dereva wa waandishi na watu wengine sita walifariki papo hapo

“Ni kweli ajali hiyo imetokea, watu 11 wamefariki kwenye eneo la tukio wakiwemo waandishi wa habari 4 na dereva na wengine sita waliokuwa kweneye gari lingine” amesema Zakaria na kuongeza

“Dakika chache majeruhi waliopelekwa kwenye kituo cha afya cha Nasa watatu walifariki, wakiwemo wale waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyo, Blasius Chatanda yupo katika hospitali ambako majeruhi walikopelekwa akiahidi kuwa atatoa taarifa baadaye.

Chanzo: Mwananchi

======

UPDATES;

=====

Waandishi waliofariki kwenye ajali ya gari ni

1. Husna Mlanzi wa ITV

2. Vanny Charles wa Icon. TV

3. Johari Shani wa Uhuru Digital

4. Antony Chuwa wa Habari leo Digital

5. Abel Ngapemba Afisa habari Mwanza

6. Steven Msengi Afisa Habari Ukerewe

7. Paul Silanga Dereva wao

Miili yao imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Nassa wilayani Busega mkoani Simiyu.

Poleni wafiwa na majeruhi
 
Watu wenye madaraka wakishindwa kutumia akili wanamlaumu shetani.
Ingetumika akili kidogo tu ya mwendo wa kiasi wafiwa wasingekua na maumivu kiasi hiki.
Lkn mkuu anawahi, speed hiyo v eite spiti Mia arobaini, Sheria za barabarani tupa kule as if wazungu waliozitunga hawana akili
140km/hr kwenye barabara zetu ni kutafuta yaliyotokea
 
Wakulaumiwa Ni huyo kiongozi.
Speed ya magari unaiona lkn uko kimya tu hukemei.
Mkuu wa mkoa angemuambia dereva wake apunguze spidi hakuna mtu ambaye Ange overtake gari la mkuu. Lkn mkuu mwenyewe yupoyupo tu anataka kuwahi. Sijui alichelewa wapi.
Nawashangaaga hawa watu sijuwi wanawaigi wapi,maana wanakwenda na maspidi
Ya ajabu
Jamaa wakiwa kwenye magari wanakuwa na mzuka +wenge+misifa
Waendega tu mwendo wa kawaida,ona sasa watu wanapoteza uhai,wengine hawana vino wanabakia vilema

Ova
 
Kutokana na uwongona unafiki wa serikali hii ya kusema walioachwa ni kwasbsb ya kuwania urais ,, mwenyezi mungu kwa kukataa unafiki, leo ajali ya msafara wa mkuu wa mkoa umesababisha maafa ya watu 18 na majruhi wengi na waliathirika zaidi wakiwa ni waadishi wa habari. Bila kutubu dhambi zetu basi mwaka huu ukame utakuwa mkali na amamfa yatatuandama, kazi kwen
Unapaswa kuwa umeshakufa had sasa,sijui kifo kinafeli wapi kukuondoa!
 
Nina rafiki zangu kibao kwenye tasnia hiyo waliopo Mwanza. Natamani nifahamu majina ya waathirika, lakini nimeshindwa kuwapigia simu mmoja mmoja! Natamani niwatambue kwa njia nyingine!
Aliyepata majina, naomba atupatie!
Soma hapo umeandikiwa mbona
 
Waandishi wa habari kubebwa kwenye magari ya serekali hii ni rushwa kabisaa unadhani watakwenda kuripoti kitu tofauti na anavchokipenda kiongozi huyooo?? Maana kabla hawaja panda Hilo gari najua lazima mkononi walishikishwa bahasha nono ili wakaandike ya kumpendezesha kiongozi
 
Ni vizuri mkuu wa mkoa akajiuzulu
Ukiangalia kosa lililomfanya Mzee mwinyi nyakati hizo kujiuzulu ni kama tone kwenye bahari ukilinganisha na hili.

Siku hizi kujiuzulu imekuwa kinyume na ndio maana mtu asiyeelewa mahesabu akiomba msaada wa jinsi gani deni linavyokua na kutishia nchi isinadiwe ufafanuzi wake ni kumtaka ajiuzulu lakini hapa hili kosa halina athari na 2025
 
Mimi ninashauri hawa madereva wa serikali wanunuliwe gari za kawaida kama za kwetu watu wa chini. Hizi gari zenye uwezo mkubwa zinawapa viburi na kujiamnini kukimbia mwendokasi wenye matokeo kama haya. Inatakiwa wapewe gari kama kirikuu (suzuki carry) ili tuone kama wataendelea na mwendokasi, wameonywa lakini hawasikii.
Mkuu hizo Landcruiser 1HZ hazina ukubwa wowote pia hazina safety features yoyote ile ndo maana ikila mzinga kwenye speed kali maafa hua ni makubwa sana...
 
Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari ya waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

--
Rais Samia atoa salamu za Rambirambi

''View attachment 2076839

====


Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari la waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu akiwa eneo la tukio, Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

Amesema kati ya vifo hivyo kuna vifo vya waandishi wa habari wanne na dereva wa waandishi na watu wengine sita walifariki papo hapo

“Ni kweli ajali hiyo imetokea, watu 11 wamefariki kwenye eneo la tukio wakiwemo waandishi wa habari 4 na dereva na wengine sita waliokuwa kweneye gari lingine” amesema Zakaria na kuongeza

“Dakika chache majeruhi waliopelekwa kwenye kituo cha afya cha Nasa watatu walifariki, wakiwemo wale waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyo, Blasius Chatanda yupo katika hospitali ambako majeruhi walikopelekwa akiahidi kuwa atatoa taarifa baadaye.

Chanzo: Mwananchi

======

UPDATES;

=====

Waandishi waliofariki kwenye ajali ya gari ni

1. Husna Mlanzi wa ITV

2. Vanny Charles wa Icon. TV

3. Johari Shani wa Uhuru Digital

4. Antony Chuwa wa Habari leo Digital

5. Abel Ngapemba Afisa habari Mwanza

6. Steven Msengi Afisa Habari Ukerewe

7. Paul Silanga Dereva wao

Miili yao imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Nassa wilayani Busega mkoani Simiyu.

Kuna UPUMBAVU, NASEMA UPUMBAVU wa hali ya juu sana ktk nchi hii. Kila anayeendesha gari ya serikali anaamini sheria za barabarani hazimuhusu! Folish! Roho za watu zinateketea bila sababu.

Ni aibu kwamba polisi hawafuati sheria, majaji hawafuati sheria, wabunge hawafuati sheria, wanajeshi hawafuati sheria, mawaziri hawafuati sheria, nk. wapuuzi ni wengi! Sijui kwa nini hali hii imedekezwa bila sababu.
 
Kutokana na uwongona unafiki wa serikali hii ya kusema walioachwa ni kwasbsb ya kuwania urais ,, mwenyezi mungu kwa kukataa unafiki, leo ajali ya msafara wa mkuu wa mkoa umesababisha maafa ya watu 18 na majruhi wengi na waliathirika zaidi wakiwa ni waadishi wa habari. Bila kutubu dhambi zetu basi mwaka huu ukame utakuwa mkali na amamfa yatatuandama, kazi kwenu
Ni coincidence tu..
 
Kwa kweli umeongea jambo la muhimu sana.

Nimewahi kuwa mikoani kwa shughuli kadhaa zinazohusiana na ofisi ya mkuu wa mkoa, wilaya ama mkurugenzi.

Kwa kweli kama ni kwenda kukagua miradi, misafara ya magari kwenye ziara huwa inakiuka kwa wazi kabisa sheria za usalama barabarani katika maeneo yafuatayo:
1. Mwendo kasi - ni kama vile kwa kuwa tu mpo kwenye msafara basi hakuna anayejali tena kuhusu mwendo kasi uliopitiliza.( Hata maaskari wa usalama wa barabarani huwa hawafanyi chochote kwa kuwa tu ni msafara wa mkuu wa mkoa, wilaya ama mkurugenzi.

2. Matumizi ya ''Hazard'' - yaani kwenye hii misafara kitu madereva wanajua ni kuwasha taa za hazard kisha wanakuwa huru kufanya chochote barabarani.

Ni muhimu sasa kwa madereva na wale wanaokuwa kwenye hii misafara kuzingatia sheria za barabarani.
Boss! Akili za viongozi wetu ni MBOVU! Wanaotakiwa kuonesha ufahamu wa sheria za nchi ndo wasiotaka kufuata sheria za barabarani. Polisi, wanajeshi, uhamiaji, majaji, wabunge, mawaziri, n.k. wote wanaona sifa kutofuata sheria za barabara. Yaani kukiuka sheria nayo ni privilege! PUMBAVU Kabisa watu hawa! Siku hizi hata magari ya kampuni ya reli pia hayafuati, SU zote hazifuati!
 
Dah.... RC wa Mwanza ndani ya Simiyu...ziara ya kikazi..... Kama bi Mkubwa anashinda ndani ya ndege....Basi wengine Ni kina Nani hasa hata wasipende padiemu? 🤣🤣🤣🤣🤭
Alikuwa anenda Ukerewe iliyoko ndani ya mkoa wake lakini ili afike huko analazimika kupitia mikoa miwili ya Simiyu na Mara kwa njia ya kivuko cha Kisorya badala ya kivuko cha Mwanza Nansio/Ukara.

Mtakumbuka humu niliwahi kuleta mada ya kwamba Ukerewe ipewe mkoa wa Mara badala ya Mwanza, ajali ni ajali tu lakini labda isingekuwa hivi kama Ukerewe ingekuwa wilaya ya mkoa wa Mara.

Mika takriban 20 iliyopita, kada mkongwe wa chama Dr. Anthony Diallo aliwahi kukaa majini kwa masaa manane akishikilia boya hadi msaada ulipomfikia na wenzake baada ya meli/kivuko kuzama kati ya Mwanza na Ukerewe.

JK aliwahi kuzimikiwa kivuko kati ya Kisorya na Ukerewe.

Rais, napaza sauti kwamba:
1. Ipeleke Ukerewe Mara,
2. Jenga daraja la ziwani kuunganisha Bunda na Ukerewe.
Kutokana na uwongona unafiki wa serikali hii ya kusema walioachwa ni kwasbsb ya kuwania urais ,, mwenyezi mungu kwa kukataa unafiki, leo ajali ya msafara wa mkuu wa mkoa umesababisha maafa ya watu 18 na majruhi wengi na waliathirika zaidi wakiwa ni waadishi wa habari. Bila kutubu dhambi zetu basi mwaka huu ukame utakuwa mkali na amamfa yatatuandama, kazi kwenu
Mbona naona kama waliojitokeza hadharani kugombea urais (Januari na Mwigulu) 2015 ndiyo wamebaki kwenye baraza, na hawa ambao hawajawahi kujitokeza hadharani kutangaza nia hiyo ndiyo wametupwa nje akiwemo mzee wa K-VANT. Hii inakaaje?

Walikuwa wanaelekea Ukerewe, kufika Ukerewe kuna njia mbili, moja ya Meli pale Mwanza, na nyingine kupitia Bunda ambako wangepanda kivuko.
Hao walipita hiyo ya Bunda ambayo unapitia Wilaya ya mkoa wa Simiyu.
Mama anahusikaje hapo?
Umefafanua vizuri.
 
Steven Msengi alikuwa hata hajamfaidi Vizuri Mke wake. Dogo kashakuwa mjane gafla
FB_IMG_1641914668754.jpg
 
Back
Top Bottom