Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza

Simiyu: Watu 14 wafariki dunia kwenye ajali katika msafara wa Mkuu wa Mkoa Mwanza

Walikuwa wanaelekea Ukerewe, kufika Ukerewe kuna njia mbili, moja ya Meli pale Mwanza, na nyingine kupitia Bunda ambako wangepanda kivuko.
Hao walipita hiyo ya Bunda ambayo unapitia Wilaya ya mkoa wa Simiyu.
Mama anahusikaje hapo?
Ndiyo elimu ya power point- majibu kabla ya kusikiliza
 
Dah.... RC wa Mwanza ndani ya Simiyu...ziara ya kikazi..... Kama bi Mkubwa anashinda ndani ya ndege....Basi wengine Ni kina Nani hasa hata wasipende padiemu? [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2960]
Mkuu kijiografia mwanza na simiyu hasa wilaya ya Busega ni jirani,na kabla ya mkoa wa simiyu, Busega ilikuwa Mwanza,hapo mkuu wa mkoa wa Mwanza alikuwa anaenda ukerewe kwa ziara ya kikazi,so ili ufike ukerewe ni eidha upite Mwanza kwa kupanda meli ambapo ni almost masaa 3 Hadi 4 kufika ukerewe,au upite njia ya nchi kavu kwa kupitia Busega ,Bunda badae kibara dheni ukerewe,hapa utavuka kwa kivuko toka chisorya Hadi ng'ambo ambapo Ni dakika 30 kufika ukerewe.

Nadhani mkuu wa mkoa kwa uharaka aliokuwa nao aliopt njia ya nchi kavu ili awahi kufika ,so usishangae kusikiwa mkuu wa mkoa wa Mwanza kukutwa na ajari simiyu.
 
Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari ya waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

--
Rais Samia atoa salamu za Rambirambi

''View attachment 2076839

====


Watu 14 wamefariki dunia baada ya gari la waandishi wa habari iliyokuwa kwenye msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RC), Robert Gabriel kugongana na gari ya abiria Hiace katika eneo la Nyamikoma wilaya ya Busega Mkoani Simiyu.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu akiwa eneo la tukio, Mkuu wa Wilaya ya Busega (DC), Gabriel Zakaria amethibitisha kutokea vifo hivyo.

Amesema kati ya vifo hivyo kuna vifo vya waandishi wa habari wanne na dereva wa waandishi na watu wengine sita walifariki papo hapo

“Ni kweli ajali hiyo imetokea, watu 11 wamefariki kwenye eneo la tukio wakiwemo waandishi wa habari 4 na dereva na wengine sita waliokuwa kweneye gari lingine” amesema Zakaria na kuongeza

“Dakika chache majeruhi waliopelekwa kwenye kituo cha afya cha Nasa watatu walifariki, wakiwemo wale waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyo, Blasius Chatanda yupo katika hospitali ambako majeruhi walikopelekwa akiahidi kuwa atatoa taarifa baadaye.

Chanzo: Mwananchi

======

UPDATES;

=====

Waandishi waliofariki kwenye ajali ya gari ni

1. Husna Mlanzi wa ITV

2. Vanny Charles wa Icon. TV

3. Johari Shani wa Uhuru Digital

4. Antony Chuwa wa Habari leo Digital

5. Abel Ngapemba Afisa habari Mwanza

6. Steven Msengi Afisa Habari Ukerewe

7. Paul Silanga Dereva wao

Miili yao imehifadhiwa katika Kituo cha Afya Nassa wilayani Busega mkoani Simiyu.

Huyu Husna Milanzi ni yule aliyekuwaga StarTv?
 
Walikuwa wanaelekea Ukerewe, kufika Ukerewe kuna njia mbili, moja ya Meli pale Mwanza, na nyingine kupitia Bunda ambako wangepanda kivuko.
Hao walipita hiyo ya Bunda ambayo unapitia Wilaya ya mkoa wa Simiyu.
Mama anahusikaje hapo?
Nadhani watu wanapenda tu kulaumu bila kuhoji/kufikiria kwa undani. Ni sawa na RC wa pwani atoke kibaha kwenda katika ziara kisarawe apate ajali DSM halafu mtu unaanza kuhoji
 
Kuna taratibu zake unapokuwa kwenye misafara ya viongozi kisheria, tunaongelea upande mmoja lakini vipi dereva wa basi dogo inawezekana aliingia barabarani wakati msafara haujaisha hivyo kusababisha ajali.
Tatizo la misafara yetu huwa tunajuwa mwanzo wa msafara lakini mwisho hakuna alama au gari itakayotujuza watumia barabara kuwa msafara umeishia hapa hivyo unaweza ingia barabarani kumbe bado gari za msafara hazijaisha.
Kingine ni uzoefu wa dereva pia maana unaweza kuwa na dereva lakini hatumiki kwenye safari ndefu leo umuweka kwenye msafara na mwendo ni mkubwa sana anaweza kushindwa imudu gari ikiwa mwendo kasi.
 
Huu utaratibu wa magari yaliyoko kwenye msafara wa viongozi kuendeshwa kama yanaendeshwa na vichaa ufikia mahali ufe.

Hakuna wanapowahi zaidi ya kaburini tu halafu utasikia "ni mpango wa Mungu".

Stupid fools.
Yaani unakuta barabara imejaa magari na wapita njia lakini hawajali. superiority complex imewaathiri sana. Sasa Ona wanavyopoteza maisha ya wapendwa wetu.
 
Huu utaratibu wa magari yaliyoko kwenye msafara wa viongozi kuendeshwa kama yanaendeshwa na vichaa ufikia mahali ufe.

Hakuna wanapowahi zaidi ya kaburini tu halafu utasikia "ni mpango wa Mungu".

Stupid fools.
Tatizo ni madereva vilaza,wanajiona wemefika wanapokuwa kwenye hayo ma V8 yao,ajari nyingi za magari ya Serikali husababishwa na uzembe Wa madereva,spidi kali
 
Kwa nini mnawazia ajali tu? Kuna vitu vingine ni kafara mjue!! Viongozi wengi wakuu ni Aliens wenye miili yetu..hivyo wakitaka kunywa damu wanachinja tu kwa style hiyo...chunguzeni mtaona
Ni kweli kabisa, hapo Kuna watu wamegeuzwa sadaka hyo mendokasi ni kisingizio tu nakumbuka Kuna mtu alianzisha Uzi jinsi walivokuwaga wanasababisha ajali huku watu tukisingizia mwendokasi
 
Wanaambiwa na Nani wakati katibu mkuu kashasaini kibali mtu ahame, na wakati huo halmashauri nyingine watu wanapewa vibali....ni kutoheshimu mamlaka na roho mbaya tu ya huyo mkurugenzi, haya mwenzie kafariki sasa, hiko kibali akafungie vitumbua, au akibandike ukutani iwe ukumbusho.
Mamii polee mkuu lakini usimlaumu sana huyo boss inawezekana kibali kilikuwa tayari lakini bado hakukuwa na mfanyakazi mbadala wake hivyo alikuwa anangoja apate mtu mbadala aachie kibali ni taratibu tu za kazi .
Na kama alikuwa hampendi kwa nini ampe safari maana ina marupurupu hiyo safari kwa dereva. Bosi angeendelea kumbana na hata safari asingepata. Pole sana Mamy.
 
Back
Top Bottom