Simpendi Rais Samia ila yawezekana Akitokea mtu akaniambia alichofanya cha maana Tangu aingie Madarakani naweza kubadili mawazo nikampenda

Amerudisha demokrasia ikiwemo ya mtu kama wewe kuelezea hisia zako bila hofu yoyote, ameboresha mahusiano na mataifa ya nje hali iliyofungua milango ya uwekezaji na biashara za ndani, n.k.

Tatizo wengi mnatekwa kisiasa kwa maslahi ya wanasiasa
Biashara kama zipi?,Hizi za kuuza bandari zetu?
 
Una macho au vidonda huoni maendeleo ya ngorongoro au unataka kumchafua tu rais
 
Mkuu ukimpenda mama yako aliyekuzaa inatosha
 
Mojawapo cha maana alichokifanya ni watu kama wewe kuwa huru kuropoka mkiwa mmeshiba ugali hapo kwa shemeji zenu. Au unaona huu uhuru wa kuropoka umejileta tu? Enzi za JPM mliweza kuropoka?
 
Angalia utaona
 
Kupanda kwa gharama za bundle, kupanda kwa Bei za mafuta kila jumatano ya kwanza ya mwezi, kukosekana kwa mafuta, kukosekana kwa dollar, kukatika kwa umeme kila Mara Hadi zaidi ya masaa 12 kwa siku, kuteua na kutengua kila Mara huku utendaji ukibaki uleule, etc etc etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…