Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata mimi nilihisi hivyo hivyo[emoji23][emoji23]...Mara ya kwanza nilikuwa nahisi hisi tu huyu Mgeni Mwema ndio Jason kumbe kweli bana.
Duh![emoji849]...ngoja sasa akute rehema wake kafa kiherehere kitamuisha
Haha![emoji23][emoji23]...Kipigo oyeee!
Kweli haya ni zaidi ya makubwa, hata mimi nashangaa tu, maskini Zainabu nakuonea huruma maskiniView attachment 2275058
184
“Mmh, makubwa!” yule muuguzi aliguna na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Kwa vyovyote utakuwa umenichanganya na mtu mwingine, dada!” nilimwambia baada ya kumwona akiwa ameduwaa akinitazama kwa mshangao kama aliyeona kitu fulani cha kustaajabisha. Kisha nikaongeza, “Kwani hapa nipo wapi?”
“Upo hospitali, na mimi ni muuguzi wa wadi hii!” yule muuguzi aliniambia huku uso wake ukionesha wasiwasi kidogo.
“Najua kuwa nipo hospitali, wodini… ila nataka kujua nipo hospitali gani?” nilimuuliza tena huku nikiilamba midomo yangu iliyokuwa imekauka.
“Hospitali ya Wilaya ya Kilosa,” yule muuguzi alinijibu kwa sauti tulivu. Macho yake yalitulia kwenye uso wangu.
“Kilosa? Tangu lini nimelazwa hapa?” nilizidi kumsaili yule muuguzi huku mshangao wangu ukizidi.
“Leo ni siku ya tatu tangu uletwe hapa na jamaa zako ukiwa huna fahamu,” yule muuguzi alinijibu kwa utulivu huku akiendelea kunitazama kwa tuo.
“Kwa nini niletwe hapa Kilosa?” nilimuuliza tena kwa mshangao.
“Kumbe ulitaka upelekwe wapi! Kwani unajua nini kilikutokea hadi ukaletwa hapa?” yule muuguzi aliniuliza.
“Najua…!” nilimjibu kisha nikaongeza, “Tulikuwa tunatoka Arusha kwenye fungate na tunakwenda Dodoma, tukapata ajali eneo la Makutupora. Ninachoshangaa imekuwaje kutoka Makutupora niletwe huku Kilosa badala ya Dodoma au hata hospitali iliyo karibu na hapo?”
Na hapo nilimwona yule muuguzi akinitazama kwa mashaka mno, kwa namna ambayo sikuweza kupata tafsiri kabisa! Macho yake yaliongezeka ukubwa na kuwa ya duara na uso wake ulionesha kupambwa na mashaka makubwa. Sikujua alidhani labda nilikuwa nimerukwa na akili zangu!
“Samahani… kwani mke wangu yuko wapi?” nilimuuliza tena yule muuguzi na kumwona akishtuka kidogo, huenda nilikuwa nimemzindua toka kwenye mawazo yake.
“Alikuwepo hapa mchana alipoletea chakula akidhani labda umezinduka,” yule muuguzi alinijibu na kuitazama saa yake ya mkononi. “Hata hivyo bado dakika chache tu ufike muda wa kuona wagonjwa. Vuta subira huenda yeye akakufahamisha vizuri.”
Niliposikia hivyo nikapata matumaini nikiamini kuwa kumbe Rehema alikuwa mzima, nikaamua kujipa subira nikiamini kwamba angenifafanulia kila kitu.
“Kwa hiyo yeye ni mzima wa afya?” nilimuuliza yule muuguzi nikitaka kuhakikisha Rehema hakuwa na majeraha.
“Yeye hana shida ila mtoto ndiyo anaumwa,” yule muuguzi aliniambia jambo ambalo lilinifanya nijikute nikishangaa mno.
“Mtoto gani?” niliuliza kwa mshangao.
“Mtoto wenu, Mariam… kwani huna mtoto?” yule muuguzi alisema.
“Hatuna mtoto, ndiyo kwanza tumetoka kuoana,” nilimjibu huku nikianza kupata mashaka kuwa huenda alikuwa amenichanganya na mtu mwingine.
Kwa kusema hivyo nilimwona yule muuguzi akifungua mdomo wake kutaka kusema neno kisha akasita na kunitazama kwa mshangao mkubwa. Katikati ya mshangao wake alibetua midomo yake huku akinitazama kwa mashaka, “Daah! Basi kuna shida kubwa sana! Itabidi niongee na daktari wako.”
Sikusema neno, nilibaki na mshangao. Yule muuguzi akapiga kofi dogo la mshangao na kuongeza, “Mara sijui jina lako ni Jason nani, mara ooh nimepata ajali Makutupora, mara tumetoka kuoana! Dah… haya sasa makubwa!”
Nami nilimshangaa sana yule muuguzi, nilihisi kuwa kama ni kuchanganyikiwa basi ni yeye aliyekuwa amechanganyikiwa na si mimi. Nilimwona akishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akiendelea kunitazama kwa namma ambayo ilinidhihirishia kuwa alikuwa kama anaona kitu cha kustaajabisha sana.
Huenda alidhani jeraha nililopata kichwani lilikuwa limeichanganya akili yangu. Kisha alitingisha kichwa chake na kuanza kuondoka.
“Nesi, samahani…” nilimwita yule muuguzi kabla hajatokomea na kumfanya ageuke kunitazama kwa wasiwasi, uso wake ulikuwa umejaa mashaka.
Alinitazama kwa kitambo akionekana kama aliyekuwa akijishauri iwapo arudi au aendelee na safari yake, kisha nikamwona akishusha pumzi na kusema, “Unasemaje, nisubiri nakuja sasa hivi.” Kisha aliondoka haraka na kuniacha nikiwa nimeshangaa sana. Nilimsindikiza kwa macho wakati akiondoka.
“Bila shaka watakuwa wamechanganya majina! Mgeni Mwema ndiyo nani?” nilijiuliza mwenyewe huku nikigeuza shingo yangu kuwatazama wagonjwa wengine mle wodini.
Hata hivyo, niliamua kuupisha utulivu kichwani mwangu huku nikiyazungusha macho kutazama mle wodini kisha nikayarudisha tena kule alikoelekea yule muuguzi. Na hapo fikra zangu zikahamia kutafakari juu ya Rehema na jamaa zangu.
Nilijiuliza kama kulikuwa na dosari yoyote juu yangu au pengine ni kweli nilikwisha anza kuchanganyikiwa! Na kwa nini yule muuguzi asisitize kuwa jina langu ni Mgeni wakati nilijua fika kuwa si langu? Hadi wakati huo nilikuwa na uhakika wa asilimia mia moja kwamba nilikuwa sahihi.
Swali jingine likawa; ni kweli Rehema alikuja pale hospitali akiwa na mtoto anayeitwa Mariam? Huyo Mariam alikuwa mtoto wa nani? Kila nilipojaribu kuwaza zaidi nilihisi kuchanganyikiwa mno. Sasa nilimwomba Mungu anipe unafuu haraka ili nitoke pale hospitali na kurudi nyumbani.
“Mgeni!” nilishtushwa na sauti ya mwanamume aliyeita kwa furaha huku akiharakisha kuja pale kitandani kwangu. “Mungu mkubwa, hatimaye umeamka?”
Nilishangaa sana na kumtazama yule mwanamume aliyeyasema hayo, kwa umakini, alikuwa mrefu na mwembamba akiwa amevaa suruali ya bluu ya dengrizi na shati la mikono mirefu la rangi ya samawati. Mkononi alikuwa amebeba mfuko mwekundu.
Mwanamume huyo alikuwa ameongozana na wasichana wawili, warembo ingawa walionekana wamechoka, mmoja wao alikuwa na mtoto wa miaka takriban mitatu. Wote walikuwa wakinitazama kwa furaha wakiwa hawaamini macho yao. Yule msichana aliyekuwa na mtoto alinyoosha mikono yake juu kumshukuru Mungu kisha akaharakisha kuja pale kitandani na kunikumbatia kwa furaha huku akitokwa na machozi ya furaha machoni.
Mwanzoni nilidhani labda walikuwa wamenifananisha na pindi wakigundua wangeniomba radhi na kuondoka lakini nilipomwona yule msichana mwenye mtoto akizidi kunikumbatia kwa nguvu na kuning’ang’ania huku akisema, “Jamani mume wangu…” nikamtazama kwa mshangao kisha nikayahamisha macho yangu kutoka kwa msichana huyo na kuwatazama wale wengine wawili. Nao walinitazama kwa furaha wakiwa hawana wasiwasi wowote.
“Nyinyi ni akina nani?” niliwauliza wale watu kwa mshangao huku hasira zikianza kuchipua ndani yangu, niliwakazia macho kwani nilihisi kitendo kile cha kuchangamkiwa na watu nisiowajua kilikuwa ni cha kutaka kucheza na akili yangu.
Wale watu wakaonekana kushtuka kidogo baada ya swali lile na kunitazama kwa mshangao mkubwa, kisha wakatazamana.
“Mume wangu, inamaana umenisahau kama ni mimi Zainabu mkeo?” yule msichana mwenye mtoto ambaye sasa nilimtambua kwa jina la Zainabu aliniuliza kwa mshangao huku akijaribu kunishika begani lakini niliusukuma mkono wake.
Endelea...
Kweli mkasa unasisimua, ahsante BishopView attachment 2280500
194
Nilizidi kumsogelea taratibu hadi karibu yake, nikasimama huku nikimtazama kwa tabasamu. Yeye aliendelea kusimama kama sanamu pasipo kupepesa macho jambo lililoanza kumshtua kila mtu aliyekuwemo pale sebuleni. Tulitazamana. Nilikuwa namtazama kwa umakini nikiwa siamini kama niliyekuwa namwona kasimama mbele yangu alikuwa mke wangu mpenzi, Rehema. Nilisimama pale nikiyashuhudia machozi yakiendelea kumtiririka mashavuni utadhani milizamu iliyopasuka.
Kwa sekunde kadhaa watu wote pale sebuleni walibaki katika taharuki wakitutazamana bila kusema neno, kisha kama aliyegutuka, Rehema alikweza khanga yake na kufuta machozi kwa kutumia pembe ya khanga na kisha akapenga kamasi zilizoanza kumtoka. Halafu akashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.
Na hapo nikapata nguvu na kuinua mikono yangu, nikamkumbatia. Yeye pia alinyanyua mikono yake akanikumbatia. Tulikumbatiana kwa furaha kwa muda tusioweza kuukumbuka, mioyo yetu ilikuwa inadunda kwa kasi na jasho jepesi lilikuwa linatutoka.
Wakati tukiwa bado tumekumbatiana nilimsikia Rehema akivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu huku akiwa amekilaza kichwa chake kwenye kifua changu. Hadi muda huo hakuweza kuongea neno lolote. Nilijikuta nikizama katika kuuajabia mwili wa Rehema, nikauhusudu urembo wake usiochujuka japo alikuwa ametoka kujifungua lakini bado aliweza kuonekana mrembo.
Kisha Rehema aliinua uso wake kunitazama na hapo akalihisi joto la pumzi zangu jambo nililoamini kuwa lilimfanya kuamini kuwa nilikuwa mtu hai na si mzimu.
Kwa muda wote huo hali ilikuwa ya taharuki kidogo ndani ya ile sebule, watu wote walikuwa kimya wakishuhudia kilichokuwa kikiendelea kati ya wanandoa tuliokuwa tumepotezana kwa takriban miezi kumi, huku mimi nikidhaniwa kuwa nimekufa.
“Rehema!” hatimaye nilimwita Rehema kwa sauti ndogo.
“Abee!” Rehema aliitika kwa sauti ya chini huku akinitazama usoni, uso wake ulikuwa na michirizi ya machozi yaliyolilowesha shati langu eneo la kifuani.
“Ni mimi Jason mumeo, niko hai… usilie mimi ni mzima kama unionavyo,” nilisema huku nikimpapasa nywele zake.
Maneno hayo yalionesha kumwingia sana Rehema, alinitazama kwa haya, alinitazama tangu unyayoni hadi utosini, kisha macho yetu yaligongana na kumfanya aachie tabasamu laini. Mashavu yake yakaonesha vishimo vidogo, pembe za midomo yake zikafinya na macho yake yakafanya kuelea. Midomo yake yenye maki ikafunguka na sauti iliyotoka humo ilitosha kabisa kumtoa nyoka pangoni mwake.
“Hata sijui niseme nini, mume wangu! Ila namshukuru sana Mungu kwa kukurejesha nyumbani ukiwa mwenye afya, karibu tena maisha kwangu,” Rehema alisema na kushusha pumzi ndefu kama aliyetoka kumaliza mbio ndefu za marathoni.
Kwa maneno hayo, mkondo wa umeme ulikuwa umepitishwa katika mwili wangu. Nilishusha pumzi na kumwachia Rehema kisha nikamsogelea Grace na kusimama nikimtazama Jason Junior aliyepakatwa mikononi. Kuona hivyo Grace akanyoosha mikono yake kunipa mtoto.
Nilimchukua mtoto na kumtazama kwa umakini, nikashusha pumzi za ndani kwa ndani na kumbusu kwenye paji la uso wake, kisha nikamkumbatia kifuani kwangu huku nikijitahidi kuyazuia machozi yaliyokuwa yakinilengalenga machoni.
Grace alinyanyuka toka pale alipokuwa ameketi na kunipisha, akaketi kwenye kochi jingine lililokuwa kando kabisa ya sebule. Niliketi huku nikiendelea kumtazama Jason Junior kwa umakini. Kitambo kirefu cha ukimya kikapita huku kila mmoja akiwaza lake na ukimya ule ulipokuwa mbioni kushika hatamu nikanyanyua uso wangu kuwatazama watu walioketi pale sebuleni.
“Habari za hapa?” niliwasalimia mle ndani huku nikivunja ukimya ulioanza kutawala pale sebuleni.
“Za hapa nzuri,” wote walijibu. Mama Mchungaji akaongeza, “Sisi hatujambo kama unavyotuona. Pole sana.”
“Nimekwisha poa,” nilijibu kisha nikamtazama Rehema, “Pole sana kwa maisha ya upweke na yote yaliyotokea wakati mimi sipo.”
“Hivi sasa sina tena upweke,” Rehema alisema huku akiangua kicheko hafifu cha kimahaba.
“Hata hivyo akili yangu inashindwa kukubali, ni kama vile mambo haya yametendeka ndani ya wiki moja tu tangu ile ajali itokee,” nilisema huku nikiutazama mkono wangu wa kushoto uliofungwa plasta ngumu.
Rehema aliyapeleka macho yake kuutazama mkono wangu wenye plasta ngumu kwa umakini huku akijitahidi kuyazuia machozi yake, kisha alinisogelea na kuketi sakafuni huku akiishika miguu yangu kwa upendo. Akamwagiza Grace alete maji kwenye kikombe kikubwa na beseni dogo.
Grace aliinuka na kuleta maji kwenye kikombe na beseni dogo na kumpa Rehema ambaye alivipokea na kunivua viatu na soksi, kisha akaniosha miguu yangu kwa upendo huku akiyakinga yale maji kwenye beseni, halafu akayanywa yale maji aliyonioshea. Kila mtu alimtazama kwa mshangao lakini yeye hakujali.
“Kwa miezi tisa nimeishi kwa ukiwa, sikujua kama ingetokea siku kama ya leo tukiwa pamoja na mtoto wetu Junior,” Rehema alisema huku akifuta machozi yaliyokuwa yanamlengalenga machoni.
Muda mfupi uliofuata Grace alielekea jikoni na kurudi akiwa amebeba sinia kubwa la mbao safi ambalo lilikuwa na majagi mawili makubwa ya kioo, moja likiwa na sharubati ya mchanganyiko wa embe na passion na jingine lilikuwa na sharubati ya parachichi. Akayaweka juu ya meza na kuondoka tena, akarejea na bilauri kadhaa. Kisha alimimina sharubati kwenye zile bilauri na kutukaribisha.
Kila mmoja alichukua bilauri ya sharubati kulingana na alivyopenda halafu tukagongesha bilauri zetu kutakiana afya njema na maisha marefu. Tukanywa taratibu huku tukiongea na kufurahi kwa pamoja.
“Haya ni maajabu kabisa! Hiki kilichotokea ni kama ile hadithi ya mwana mpotevu wa kwenye Biblia,” Eddy alisema huku akiachia kicheko hafifu. Watu wote walicheka kwa furaha huku wakionekana kuafikiana na maneno yake.
“Wala hujakosea, mimi pia ni mwana mpotevu, nilipotea na sasa nimepatikana. Nilikufa na sasa nimefufuka,” nilisema kwa furaha huku nikinyanyua bilauri yangu juu kisha nikapiga funda kubwa la sharubati.
“Ni kweli, wewe ni mwana mpotevu ila tofauti yako na yule wa kwenye Biblia ni kwamba, mwenzio aliondoka akiwa na fahamu zake na wewe uliondoka ukiwa huna kumbukumbu zako na ukaishi maisha ya kufikirika,” Grace alisema huku akiangua kicheko. Kisha aliinuka na kunifuata huku akinyoosha mkono wake wenye bilauri, tukagongesha bilauri zetu.
“Cheers!” tulisema kwa pamoja na kuinua bilauri, tukapiga mafunda mfululizo kana kwamba tulikuwa kwenye mashindano.
“Long live, my dear brother!” Grace alisema kwa sauti kubwa akiwa na furaha.
“Long live, my dearest sister!” nilijibu mapigo huku nikiikita ile bilauri tupu juu ya meza kwa furaha.
“Na ninyi mkishakutana basi tabu tupu,” Eddy alisema huku akitabasamu.
“Wacha tufurahi, kaka… mwana mpotevu amefufuka na kurudi nyumbani,” Grace alisema huku akicheka kisha akaongeza huku akinitazama usoni, “Kwanza juice haipandi kabisa, hapa tungepata Castle baridi ingependeza zaidi, au vipi brother?”
“Hiyo pombe yenu mkainywee huko huko si ndani ya nyumba ya Mchungaji,” Eddy alisema kwa utani na hapo tukageuza shingo zetu kumtazama Mchungaji Ngelela aliyeketi kwa utulivu kwenye kochi.
* * *
Saa 11:30 jioni…
Jioni ya siku hiyo ilinikuta nikiwa nimesimama mbele ya kaburi ambalo ulizikwa mwili uliodhaniwa kuwa wangu, nililitazama kaburi hilo kwa huzuni kubwa huku mawazo yangu yakirudi nyuma miezi tisa iliyokuwa imepita siku tuliyopata ajali. Kisha nilijaribu kuwaza kuhusu maisha mapya niliyoishi kama Mgeni lakini sikuwa na kumbukumbu zozote.
Wakati nikilitazama lile kaburi nilishindwa kuyazuia machozi yangu hasa nilipoyaona maandishi makubwa yaliyokuwa yameandikwa juu ya msalaba wa zege, maandishi ambayo yalikuwa yanawakilisha jina langu, tarehe ya kuzaliwa na ya kufa.
Nilikuwa nimeambatana na Mchungaji Ngelela, Eddy na Grace waliosimama kando yangu huku wakinifariji. Nilisimama pale kwa dakika kadhaa nikilitazama lile kaburi kisha nikashusha pumzi ndefu na kufuta machozi yaliyokuwa yakinitoka. Halafu kwa kusaidiana na watu niliofuatana nao tuliuondoa ule msalaba kutoka kwenye lile kaburi.
Baada ya kuhakikisha kuwa sijaacha alama yoyote yenye kuonesha utambulisho wangu kwenye lile kaburi, niliinamisha kichwa changu kwa huzuni mbele ya kaburi lile na kufumba macho. Kisha nilimshukuru Mungu kwa kuniepusha na mauti na nikamwomba anipe nguvu na maisha marefu yenye heri, halafu nilimwombea marehemu aliyezikwa kwenye kaburi hilo ili Mungu ampumzishe mahala pema.
Nilipomaliza nikaondoka taratibu kwa huzuni huku nikifuatwa na jamaa zangu niliokuja nao.
* * *
Endelea kuufuatilia mkasa huu wa kusisimua...
[emoji120][emoji120]...Daaah hii simulizi ni balaa, kongole kwako mkuu Bishop Hiluka
Karibu sana...Kila siku inazidi kuwa nzuri! Hongera Mtunzi kwa kunipa ushawishi wa kuendelea kufuatilia
I wish i was u ila subra ndo nimenyimwa everytime nakuja kuchungulia hola. Kuna namna mtu ukifaulu kusubiri iishe una faida sana maana wengine kususa tunatamani ila ndo hivo tena.....watunzi wazuri wanajua kutuweka roho juu honestly...Nasubiri iishe niisome
Haha! Endelea kusubiri...Nasubiri iishe niisome