Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #261
SEHEMU YA 208
Alivyofika kwao alishangaa kuna ugeni, alishangaa kumuona kaka yake ambaye kwa siku nyingi sana alikuwa akiishi kwa mjomba wao, alimsogelea na kukumbatiana kwa nguvu na kaka yake,
“Kheee Erica mdogo wangu umekuwa mkubwa jamani hadi una mtoto! Wakati kaka yako wala sina”
Erica alikuwa akitabasamu tu, kisha kumkaribisha vizuri kaka yake nyumbani,
“Kaka Tony, karibu sana ndio ulizamia Arusha jamani utafikiri ulikuwa nchi nyingine ambavyo hukutaka kurudi nyumbani. Karibu sana”
Walifurahiana nae na kuongea mambo mbalimbali kwa furaha kisha Erica aliinuka na kwenda chumbani kwake, alifunga mlango wa chumba chake kwani alikuwa na mawazo sana na alihitaji apate hata muda kidogo wa kulia.
Alivyojifungia mlango alianza kulia huku akijilaumu jinsi alivyoyafanya maisha yake, maneno ya mama yake kuwa yeye ndiye aliyekuwa na uwezo wa kuchagua maisha yake yalimrudia akilini na kuanza kujisemea,
“Kama mimi ndio nilikuwa na uwezo wa kuchagua maisha yangu, mbona maisha yangu nimechaguliwa? Nilikuwa nawasiliana vizuri sana na John hadi tukaahidiana mambo mbalimbali ila kitendo cha mimi kusahau simu mezani ikawa ndio mwisho wa mawasiliano yangu na John kwani hata niliporudi bado majanga, mama alisema simu kaitumbukiza kwenye maji na laini imevunjika. Sikuweza kuwasiliana tena na John. Kumbe alinitafuta sana, huenda ndio angekuwa mume wangu na wala yote haya ya kukutana na watu wa ajabu ajabu yasingetokea, mama yangu kachangia pakubwa sana kuharibu maisha yangu ila hataki tu kukubali ukweli. Asingeleta vurugu shuleni wala usikute hadi leo ningekuwa na Erick na wala nisingetangatanga na wanaume, akaniharibia kwa Erick, akaniharibia kwa John na pia akaniharibia kwa Bahati halafu bado anajitoa kuwa hakuna alichoharibu kwangu eti nimejiharibia mwenyewe”
Akainama tena na kulia sana, ila muda huu alikuwa hajamchukua bado mtoto wake, kwahiyo mama yake alienda kumgongea ili amchukue mtoto wake, Erica alifuta machozi na kwenda kufungua mlango,
“Kheee nimekusikia saa nyingi sana kuwa umerudi na ulikuwa ukiongea na kaka yako, kumbe hujaoga hata kuoga! Hebu nenda kaoge huko umnyonyeshe mjukuu wangu, sio umnyonyeshe na majashojasho yako ya huko njiani”
Erica alienda kuoga ila bado alikuwa na mawazo sana, kwani kimsingi maisha yake mengi yameharibika na chanzo kikubwa ni mapenzi, na sasa alikuwa akihitaji mtoto wake apate malezi ya baba na mama, ila atajielezeaje kwenye familia ya John kuwa alikuwa na mahusiano na Rahim yani hapo ndio palimshinda na kumfanya hata siku hiyo ashindwe kujieleza maana kilishatokea kitu cha kumuwekea pingamizi.
Alivyofika kwao alishangaa kuna ugeni, alishangaa kumuona kaka yake ambaye kwa siku nyingi sana alikuwa akiishi kwa mjomba wao, alimsogelea na kukumbatiana kwa nguvu na kaka yake,
“Kheee Erica mdogo wangu umekuwa mkubwa jamani hadi una mtoto! Wakati kaka yako wala sina”
Erica alikuwa akitabasamu tu, kisha kumkaribisha vizuri kaka yake nyumbani,
“Kaka Tony, karibu sana ndio ulizamia Arusha jamani utafikiri ulikuwa nchi nyingine ambavyo hukutaka kurudi nyumbani. Karibu sana”
Walifurahiana nae na kuongea mambo mbalimbali kwa furaha kisha Erica aliinuka na kwenda chumbani kwake, alifunga mlango wa chumba chake kwani alikuwa na mawazo sana na alihitaji apate hata muda kidogo wa kulia.
Alivyojifungia mlango alianza kulia huku akijilaumu jinsi alivyoyafanya maisha yake, maneno ya mama yake kuwa yeye ndiye aliyekuwa na uwezo wa kuchagua maisha yake yalimrudia akilini na kuanza kujisemea,
“Kama mimi ndio nilikuwa na uwezo wa kuchagua maisha yangu, mbona maisha yangu nimechaguliwa? Nilikuwa nawasiliana vizuri sana na John hadi tukaahidiana mambo mbalimbali ila kitendo cha mimi kusahau simu mezani ikawa ndio mwisho wa mawasiliano yangu na John kwani hata niliporudi bado majanga, mama alisema simu kaitumbukiza kwenye maji na laini imevunjika. Sikuweza kuwasiliana tena na John. Kumbe alinitafuta sana, huenda ndio angekuwa mume wangu na wala yote haya ya kukutana na watu wa ajabu ajabu yasingetokea, mama yangu kachangia pakubwa sana kuharibu maisha yangu ila hataki tu kukubali ukweli. Asingeleta vurugu shuleni wala usikute hadi leo ningekuwa na Erick na wala nisingetangatanga na wanaume, akaniharibia kwa Erick, akaniharibia kwa John na pia akaniharibia kwa Bahati halafu bado anajitoa kuwa hakuna alichoharibu kwangu eti nimejiharibia mwenyewe”
Akainama tena na kulia sana, ila muda huu alikuwa hajamchukua bado mtoto wake, kwahiyo mama yake alienda kumgongea ili amchukue mtoto wake, Erica alifuta machozi na kwenda kufungua mlango,
“Kheee nimekusikia saa nyingi sana kuwa umerudi na ulikuwa ukiongea na kaka yako, kumbe hujaoga hata kuoga! Hebu nenda kaoge huko umnyonyeshe mjukuu wangu, sio umnyonyeshe na majashojasho yako ya huko njiani”
Erica alienda kuoga ila bado alikuwa na mawazo sana, kwani kimsingi maisha yake mengi yameharibika na chanzo kikubwa ni mapenzi, na sasa alikuwa akihitaji mtoto wake apate malezi ya baba na mama, ila atajielezeaje kwenye familia ya John kuwa alikuwa na mahusiano na Rahim yani hapo ndio palimshinda na kumfanya hata siku hiyo ashindwe kujieleza maana kilishatokea kitu cha kumuwekea pingamizi.