Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #421
SEHEMU YA 330
Muda huu sasa alimfata mama yake kwani alihitaji kujua mapenzi ni nini ikiwa kila anachofanya kinamuumiza tu katika mapenzi,
“Mama, nimemaliza sasa nahitaji kujua mapenzi ni nini?”
“Kwanza kwanini unataka kujua mapenzi ni nini? Tuanzie hapo ndio nitaweza kukuelewesha kidogo”
“Mama, mwanao nimekuwa nikipata changamoto mbalimbali za mapenzi, nimekuwa nikikutana na watu mbalimbali wakidai wananipenda ila kumbe si kweli walikuwa na lengo lao tu, yani mpaka nachanganyikiwa hapa kuwa mapenzi haya ni kitu gani na kwanini mimi yananiumiza hivi”
“Mwanangu pole sana, ila mara nyingine ni kosa langu kutokukaa na wewe na kukuelimisha kuhusu swala zima la mapenzi kwani sikufikiria kuwa mwanangu umekuwa sasa, ila mwanangu mapenzi yamejaa unafki sana, kwanini nasema hivi sababu mtu anaweza kukuonyesha anakupenda hadi unaweza hisi nikimuacha huyu atakufa, kumbe kuna kitu anahitaji toka kwako ndiomana anaonyesha anakupenda, haya yuko wapi baba Angel? Si ulisema alikuwa hadi anakutumia pesa? Ziko wapi hizo pesa sasa? Angekuwa mwingine si ndio angekujali sana hivi una mtoto wake? Yani mapenzi kila mtu anayatafsiri kwa namna yake ila yakikupitia ndio unajua haswaa mapenzi ni nini, ndiomana nimekuuliza hujawahi kuumizwa na mapenzi? Kama umewahi, unawezaje kumuamini mtu asiye mume wako? Ingawa hata kwenye swala la ndoa kuna watu wanaingia kwenye ndoa sio sababu ya mapenzi ila kuna kitu anahitaji, yani mapenzi ni swala pana kidogo”
“Mama, jana nimetukanwa sana mwanao na huyo unayemsema baba Angel, ndiomana nashindwa hata kuelewa mapenzi ni nini. Huyu mwanaume aliniambia kuwa ananipenda kuliko msichana yeyote humu ulimwenguni, ila jana alivyonitukana kama si yeye aliyesema maneno yale kipindi kile”
Mama yake alicheka kama anamcheka mwanae vile, kisha akamwambia amuonyeshe alivyomwambia, kwavile Erica alishaamua kuwa mkweli kwa mama yake hakuona kama ni tatizo kumuonyesha alichoandikiwa na Rahim, alienda kuchukua ile simu yake na kufungua mtandao wa kijamii kisha kumuonyesha mama yake zile jumbe ambazo Rahim alikuwa akimtumia jana,
“Yani kaniita malaya kweli!”
“Hajakosea, wewe ni malaya ndio ndiomana ukamkubali shetani kama yeye bila hata kujiuliza, kumbe ulikuwa ukiniongopea nasafiri halafu unaenda kukutana na shetani kama hili! Watu wanagombana ila sio kufikia hatua ya kutukanana na kuhisi mmoja hafai, Erica mwanangu nilikufundisha kama naimba nyimbo, mwanangu jitunze hadi ndoa ila wapi ukaona natwanga maji kwenye kinu, umeona asante ya mwanaume eeeh! Yani mwanaume anakupa na mbinu ya kutoroka kwenu ila mwisho wa siku anakuona malaya kwa starehe yake mwenyewe, ila mwanangu usijali wala usiumizwe na maneno ya huyu Rahim, mi ninachokuombea ni uolewe tu mwanangu na huyu Rahim na familia yake yote tutawaalika kwenye harusi yako, wala maneno yake yasikukatishe tamaa, yani kuna mijitu haina akili hata kidogo, mwanamke kajitoa kubeba mimba kwaajili yako, kazaa kwa uchungu na analea mtoto wako kwenye mazingira ya kusemwa kila siku kuwa kazaa nje ya ndoa halafu unashindwa hata kufikiria mazingira anayopitia Yule mwanamke unafurahi tu kumuita malaya! Nimechukia sana, simpendi huyo Rahim yani simpendi kabisa, nimechukia sana. Acha tu mwanangu uendelee kujifariji kwa huyo Erick, natumaini atakuwa wako kweli”
Kwahiyo alijikuta na mama yake mada yako ya kuelezana mapenzi ni nini imeishia hapo kusikitishwa na majibu ya Rahim tu, maana hata mama yake Erica hakufikiria kama Erica angepata tabia za kuweza kuitwa kwa jina baya vile, alimuangalia mwanae na kusema tena,
“Unajua nakuangalia Erica sikumalizi, hivi ni kweli ni wewe niliyekulea katika maadili yote? Mtu anafikia kusema hakuna mwanaume atakayekuoa mwanamke kama wewe, kwaini aseme hivyo? Najiuliza sana, hivi ulianzaje kutembea na familia nzima? Najiuliza bado, ulianzaje kutembea na shetani kama Derick? Unajua ninavyokuangalia na haya mambo yanayokuhusu hakika huendani nayo, hivi ilikuwaje Erica! Aaah kama sikukulea mimi vile dah! Najaribu kukufikiria nakosa jibu, si utakuwa umemaliza kijiji mwanangu wewe, na sijui kama huyo Mzee Jimmy hukutembea nae kweli! Wewe uliweza hata kutembea na Yule Bahati kipindi kile anavua samaki hukuona hata kinyaa mmmh! Ila mwanangu ni mchafu wewe loh! Bora nikalale mie, nisije kuongea na mengine”
Erica nae alijisikia vibaya sana, ilikuwa ni usiku tayari alienda chumbani kwake.
Muda huu sasa alimfata mama yake kwani alihitaji kujua mapenzi ni nini ikiwa kila anachofanya kinamuumiza tu katika mapenzi,
“Mama, nimemaliza sasa nahitaji kujua mapenzi ni nini?”
“Kwanza kwanini unataka kujua mapenzi ni nini? Tuanzie hapo ndio nitaweza kukuelewesha kidogo”
“Mama, mwanao nimekuwa nikipata changamoto mbalimbali za mapenzi, nimekuwa nikikutana na watu mbalimbali wakidai wananipenda ila kumbe si kweli walikuwa na lengo lao tu, yani mpaka nachanganyikiwa hapa kuwa mapenzi haya ni kitu gani na kwanini mimi yananiumiza hivi”
“Mwanangu pole sana, ila mara nyingine ni kosa langu kutokukaa na wewe na kukuelimisha kuhusu swala zima la mapenzi kwani sikufikiria kuwa mwanangu umekuwa sasa, ila mwanangu mapenzi yamejaa unafki sana, kwanini nasema hivi sababu mtu anaweza kukuonyesha anakupenda hadi unaweza hisi nikimuacha huyu atakufa, kumbe kuna kitu anahitaji toka kwako ndiomana anaonyesha anakupenda, haya yuko wapi baba Angel? Si ulisema alikuwa hadi anakutumia pesa? Ziko wapi hizo pesa sasa? Angekuwa mwingine si ndio angekujali sana hivi una mtoto wake? Yani mapenzi kila mtu anayatafsiri kwa namna yake ila yakikupitia ndio unajua haswaa mapenzi ni nini, ndiomana nimekuuliza hujawahi kuumizwa na mapenzi? Kama umewahi, unawezaje kumuamini mtu asiye mume wako? Ingawa hata kwenye swala la ndoa kuna watu wanaingia kwenye ndoa sio sababu ya mapenzi ila kuna kitu anahitaji, yani mapenzi ni swala pana kidogo”
“Mama, jana nimetukanwa sana mwanao na huyo unayemsema baba Angel, ndiomana nashindwa hata kuelewa mapenzi ni nini. Huyu mwanaume aliniambia kuwa ananipenda kuliko msichana yeyote humu ulimwenguni, ila jana alivyonitukana kama si yeye aliyesema maneno yale kipindi kile”
Mama yake alicheka kama anamcheka mwanae vile, kisha akamwambia amuonyeshe alivyomwambia, kwavile Erica alishaamua kuwa mkweli kwa mama yake hakuona kama ni tatizo kumuonyesha alichoandikiwa na Rahim, alienda kuchukua ile simu yake na kufungua mtandao wa kijamii kisha kumuonyesha mama yake zile jumbe ambazo Rahim alikuwa akimtumia jana,
“Yani kaniita malaya kweli!”
“Hajakosea, wewe ni malaya ndio ndiomana ukamkubali shetani kama yeye bila hata kujiuliza, kumbe ulikuwa ukiniongopea nasafiri halafu unaenda kukutana na shetani kama hili! Watu wanagombana ila sio kufikia hatua ya kutukanana na kuhisi mmoja hafai, Erica mwanangu nilikufundisha kama naimba nyimbo, mwanangu jitunze hadi ndoa ila wapi ukaona natwanga maji kwenye kinu, umeona asante ya mwanaume eeeh! Yani mwanaume anakupa na mbinu ya kutoroka kwenu ila mwisho wa siku anakuona malaya kwa starehe yake mwenyewe, ila mwanangu usijali wala usiumizwe na maneno ya huyu Rahim, mi ninachokuombea ni uolewe tu mwanangu na huyu Rahim na familia yake yote tutawaalika kwenye harusi yako, wala maneno yake yasikukatishe tamaa, yani kuna mijitu haina akili hata kidogo, mwanamke kajitoa kubeba mimba kwaajili yako, kazaa kwa uchungu na analea mtoto wako kwenye mazingira ya kusemwa kila siku kuwa kazaa nje ya ndoa halafu unashindwa hata kufikiria mazingira anayopitia Yule mwanamke unafurahi tu kumuita malaya! Nimechukia sana, simpendi huyo Rahim yani simpendi kabisa, nimechukia sana. Acha tu mwanangu uendelee kujifariji kwa huyo Erick, natumaini atakuwa wako kweli”
Kwahiyo alijikuta na mama yake mada yako ya kuelezana mapenzi ni nini imeishia hapo kusikitishwa na majibu ya Rahim tu, maana hata mama yake Erica hakufikiria kama Erica angepata tabia za kuweza kuitwa kwa jina baya vile, alimuangalia mwanae na kusema tena,
“Unajua nakuangalia Erica sikumalizi, hivi ni kweli ni wewe niliyekulea katika maadili yote? Mtu anafikia kusema hakuna mwanaume atakayekuoa mwanamke kama wewe, kwaini aseme hivyo? Najiuliza sana, hivi ulianzaje kutembea na familia nzima? Najiuliza bado, ulianzaje kutembea na shetani kama Derick? Unajua ninavyokuangalia na haya mambo yanayokuhusu hakika huendani nayo, hivi ilikuwaje Erica! Aaah kama sikukulea mimi vile dah! Najaribu kukufikiria nakosa jibu, si utakuwa umemaliza kijiji mwanangu wewe, na sijui kama huyo Mzee Jimmy hukutembea nae kweli! Wewe uliweza hata kutembea na Yule Bahati kipindi kile anavua samaki hukuona hata kinyaa mmmh! Ila mwanangu ni mchafu wewe loh! Bora nikalale mie, nisije kuongea na mengine”
Erica nae alijisikia vibaya sana, ilikuwa ni usiku tayari alienda chumbani kwake.