Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #461
SEHEMU YA 361
Jioni ya siku hiyo, mama Erica alitoka kidogo na kumuacha mwanae nyumbani, muda kidogo alikuja mgeni na kugonga mlango, Erica alipoenda kufungua alikuwa ni Tumaini hata akamshangaa kuwa siku hiyo kafata nini kwao, Tumaini bila salamu alimuuliza Erica,
“Mama yupo?”
“Mama yangu wa nini?”
“Nimekuuliza tu yupo? Nijibu”
“Hayupo katoka”
Erica akashtukia kapigwa kibao, cha kwanza na cha pili kwakweli Erica hakumuelewa kabisa Tumaini kumbe aliulizia kuhusu uwepo wa mama yake Erica ili aweze kumpiga Erica, aliamua kumuuliza,
“Haya umenipiga, umenipigia nini sasa?”
“Unaona ulichomtendea kaka yangu ni sahihi? Umefanya kajifungia ndani na kusema Erica Erica, umekuwa nani wewe katika jamii?”
“Tumaini naomba uondoke maana nisije kuongea maneno mengine ya karaha ukashindwa kuvumilia hapa, naomba uondoke”
“Hebu ongea hayo maneno yako ya karaha nikusikie”
“Hivi wewe Tumaini una nini na mimi lakini? Kama unamtaka kaka yako si ukatembee nae”
“Unasemaje wewe”
Tumaini akataka kumvaa Erica ila akatokea Bahati na kuingia katikati yao, alishangaa sana kuona ule ugomvi na akamuuliza Erica kuwa kuna nini, ila Erica alijibu kwa kujiamini,
“Namshangaa huyu dada, toka nipo na kaka yake kutwa kufatilia maisha yangu, sijui haridhishwi huko kwingine! Kama unamtaka kaka yako kamchukue uone laana itakavyokufatilia”
Kwakweli Tumaini alifura hasira kitendo ambacho Bahati aliamua kumuingiza Erica ndani na kumwambia Tumaini aondoke kisha yeye kuingia ndani, akaanza kuongea na Erica,
“Kwanini uwe na mwanaume ambaye ndugu zake wanakunyanyasa hivi wakati mimi nipo!”
“Usinichekeshe na wewe, ndugu zako si ndio ukoo mzima hawanitaki sasa hiyo wewe upo ndio nini?”
“Erica, mimi nipo tayari kwa chochote hata ukitaka leo hii naenda kumuacha Yule mwanamke wala simpendi wala nini, nakupenda wewe Erica, naomba ukubali nikuoe”
“Bahati ushachelewa, Yule mwenyewe nilikuwa namjibu tu ila kwasasa sitaki mahusiano ya aina yoyote bora niwe mwenyewe tu, sitaki mwanaume yeyote, nitalea mwanangu tu”
“Erica usiseme hivyo wakati mimi nipo na ninakupenda sana, Erica nilishasema hata dunia nzima iseme kuwa wewe malaya na unajiuza ila mimi nitaendelea kukupenda tu. Maana nimefundishwa kupenda na si kitu kingine, nitakupenda maisha yangu yote”
“Asante Bahati ila kwasasa hapana, mimi na wewe tubaki tu marafiki au ndugu”
Basi Bahati alikuwa akijitahidi pale kusema ya moyoni mwake ila ilikuwa ngumu sana kueleweka kwa Erica.
Muda huu mke wa Bahati alikuwa na mawazo sana ya jambo la kufanya aliamua kumpigia simu Salma ili ajaribu kumshirikisha anachowaza,
“Salma ndugu yangu mwenzio nimefikiria nimeona tukingoja mpaka arobaini iishe tutakuwa tumeumia sana, huyu Erica ni ana nitesa vilivyo”
“Eeeeh kafanyaje tena?”
“Hebu fikiria nimetoka kujifungua ila mume hanijali wala nini yani, hataki ndugu zangu waje kuniuguza hapa wala ndugu zake anasema nikitaka kuuguzwa niende ila sio ndugu kuja hapa, na mimi siwezi kuiach nyumba yangu nimeamua kuvumilia tu, jamani jana tumerudi nyumbani hata sikuwa na raha muda kidogo simu, sijui Erica anapiga, mwanaume anahaha huku na kule, muda kidogo simu sijui Erica anataka nini, nikaamua kuficha simu bafuni, ndugu yangu alivyogundua nimeficha simu, nimepigwaje? Yani nimepigwa hatari na tangu aondoke hiyo alfajiri hajarudi hadi muda huu, hebu fikiria mume wa mtu kweli anafanya hivi jamani!”
“Sikia Nasma, mimi niliongea na Yule mmama akasema kuna dawa sijui ya kumfunga mume ila kwa upande wangu huyu mume wangu sijui kama atafungika jamani, na ndugu zake wakijua nimemfunga yani wataniharibu maana hapa naishi kwao tena sababu ya mama mkwe ana roho nzuri, sasa sijui tufanyeje?”
“Mimi nina wazo Salma”
“Wazo gani?”
“Tumfanye Erica kuwa chizi, yani wote watamkimbia, huyo mumeo atamkimbia na Bahati wangu atamkimbia, yani awe chizi kabisa abaki kuhangaika na familia yake”
“Mmmh hilo swala zuri, ila inawezekanaje?”
“Kuna mtaalamu namfahamu yani kinachotakiwa ni kupata majina matatu ya Erica basi kazi imeisha, sasa sijui hayo majina tuitayapata wapi maana mimi hata kumuuliza mume wangu siwezi, nitapigwa hadi nishangae”
“Hiyo sio kazi kwangu, nina shemeji yangu ana undugu na Erica yani yeye ndio atanitajia majina matatu ya Erica hata usiwe na shaka. Nakwambia huyo Erica habari yake imekwisha maana akiwa kichaa nani tena atamtaka?”
“Hakuna, yani tutamkomesha. Basi nakutegemea, tufanye haraka maji ya shingo yamenifika dhoga yangu”
“Aaaah usijali, ndani ya siku mbili hizi atakuja tu Yule shemeji kuniona nitakupa majina ya Erica sio kazi kuyapata”
Basi walifurahia na kupongezana kwa ajenda yao.
Jioni ya siku hiyo, mama Erica alitoka kidogo na kumuacha mwanae nyumbani, muda kidogo alikuja mgeni na kugonga mlango, Erica alipoenda kufungua alikuwa ni Tumaini hata akamshangaa kuwa siku hiyo kafata nini kwao, Tumaini bila salamu alimuuliza Erica,
“Mama yupo?”
“Mama yangu wa nini?”
“Nimekuuliza tu yupo? Nijibu”
“Hayupo katoka”
Erica akashtukia kapigwa kibao, cha kwanza na cha pili kwakweli Erica hakumuelewa kabisa Tumaini kumbe aliulizia kuhusu uwepo wa mama yake Erica ili aweze kumpiga Erica, aliamua kumuuliza,
“Haya umenipiga, umenipigia nini sasa?”
“Unaona ulichomtendea kaka yangu ni sahihi? Umefanya kajifungia ndani na kusema Erica Erica, umekuwa nani wewe katika jamii?”
“Tumaini naomba uondoke maana nisije kuongea maneno mengine ya karaha ukashindwa kuvumilia hapa, naomba uondoke”
“Hebu ongea hayo maneno yako ya karaha nikusikie”
“Hivi wewe Tumaini una nini na mimi lakini? Kama unamtaka kaka yako si ukatembee nae”
“Unasemaje wewe”
Tumaini akataka kumvaa Erica ila akatokea Bahati na kuingia katikati yao, alishangaa sana kuona ule ugomvi na akamuuliza Erica kuwa kuna nini, ila Erica alijibu kwa kujiamini,
“Namshangaa huyu dada, toka nipo na kaka yake kutwa kufatilia maisha yangu, sijui haridhishwi huko kwingine! Kama unamtaka kaka yako kamchukue uone laana itakavyokufatilia”
Kwakweli Tumaini alifura hasira kitendo ambacho Bahati aliamua kumuingiza Erica ndani na kumwambia Tumaini aondoke kisha yeye kuingia ndani, akaanza kuongea na Erica,
“Kwanini uwe na mwanaume ambaye ndugu zake wanakunyanyasa hivi wakati mimi nipo!”
“Usinichekeshe na wewe, ndugu zako si ndio ukoo mzima hawanitaki sasa hiyo wewe upo ndio nini?”
“Erica, mimi nipo tayari kwa chochote hata ukitaka leo hii naenda kumuacha Yule mwanamke wala simpendi wala nini, nakupenda wewe Erica, naomba ukubali nikuoe”
“Bahati ushachelewa, Yule mwenyewe nilikuwa namjibu tu ila kwasasa sitaki mahusiano ya aina yoyote bora niwe mwenyewe tu, sitaki mwanaume yeyote, nitalea mwanangu tu”
“Erica usiseme hivyo wakati mimi nipo na ninakupenda sana, Erica nilishasema hata dunia nzima iseme kuwa wewe malaya na unajiuza ila mimi nitaendelea kukupenda tu. Maana nimefundishwa kupenda na si kitu kingine, nitakupenda maisha yangu yote”
“Asante Bahati ila kwasasa hapana, mimi na wewe tubaki tu marafiki au ndugu”
Basi Bahati alikuwa akijitahidi pale kusema ya moyoni mwake ila ilikuwa ngumu sana kueleweka kwa Erica.
Muda huu mke wa Bahati alikuwa na mawazo sana ya jambo la kufanya aliamua kumpigia simu Salma ili ajaribu kumshirikisha anachowaza,
“Salma ndugu yangu mwenzio nimefikiria nimeona tukingoja mpaka arobaini iishe tutakuwa tumeumia sana, huyu Erica ni ana nitesa vilivyo”
“Eeeeh kafanyaje tena?”
“Hebu fikiria nimetoka kujifungua ila mume hanijali wala nini yani, hataki ndugu zangu waje kuniuguza hapa wala ndugu zake anasema nikitaka kuuguzwa niende ila sio ndugu kuja hapa, na mimi siwezi kuiach nyumba yangu nimeamua kuvumilia tu, jamani jana tumerudi nyumbani hata sikuwa na raha muda kidogo simu, sijui Erica anapiga, mwanaume anahaha huku na kule, muda kidogo simu sijui Erica anataka nini, nikaamua kuficha simu bafuni, ndugu yangu alivyogundua nimeficha simu, nimepigwaje? Yani nimepigwa hatari na tangu aondoke hiyo alfajiri hajarudi hadi muda huu, hebu fikiria mume wa mtu kweli anafanya hivi jamani!”
“Sikia Nasma, mimi niliongea na Yule mmama akasema kuna dawa sijui ya kumfunga mume ila kwa upande wangu huyu mume wangu sijui kama atafungika jamani, na ndugu zake wakijua nimemfunga yani wataniharibu maana hapa naishi kwao tena sababu ya mama mkwe ana roho nzuri, sasa sijui tufanyeje?”
“Mimi nina wazo Salma”
“Wazo gani?”
“Tumfanye Erica kuwa chizi, yani wote watamkimbia, huyo mumeo atamkimbia na Bahati wangu atamkimbia, yani awe chizi kabisa abaki kuhangaika na familia yake”
“Mmmh hilo swala zuri, ila inawezekanaje?”
“Kuna mtaalamu namfahamu yani kinachotakiwa ni kupata majina matatu ya Erica basi kazi imeisha, sasa sijui hayo majina tuitayapata wapi maana mimi hata kumuuliza mume wangu siwezi, nitapigwa hadi nishangae”
“Hiyo sio kazi kwangu, nina shemeji yangu ana undugu na Erica yani yeye ndio atanitajia majina matatu ya Erica hata usiwe na shaka. Nakwambia huyo Erica habari yake imekwisha maana akiwa kichaa nani tena atamtaka?”
“Hakuna, yani tutamkomesha. Basi nakutegemea, tufanye haraka maji ya shingo yamenifika dhoga yangu”
“Aaaah usijali, ndani ya siku mbili hizi atakuja tu Yule shemeji kuniona nitakupa majina ya Erica sio kazi kuyapata”
Basi walifurahia na kupongezana kwa ajenda yao.