Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #481
SEHEMU YA 376
Leo ndio ilikuwa siku ambayo Dora na Sia walipanga kwenda kwa babu wa Bagamoyo, kwahiyo walikutana na kuanza safari ya kwenda kwa huyo Babu ambapo alianza kuingia Dora na kueleza azma yake kisha akaonyeshwa wabaya wa Erica walioshiriki kumletea ule ugonjwa alishangaa kuona Derick nae aliungana na wale wanawake, Yule mganga akamueleza,
“Yani ni hivi, huyu mwanamke wa kwanza alienda kwa huyu mwanaume kuchukua majina ya huyo binti na kisha alipotajiwa akamtumia huyu mwanamke wa pili kisha huyu mwanamke wa pili ndio alimuendea kwa huyu mzee na kumfanya walivyomfanya, lengo lao walitaka awe chizi na mwisho wa siku rafiki yako angegongwa na gari na kufa, sema haijawezekana kuwa chizi maana rafiki yako ana imani kubwa sana na Mungu. Ila mimi nitakusaidia kukupa dawa ya kumponya kabisa na tunaweza kuwarudishia wale makombora”
“Ila ndugu zake wamekazana na maombi”
“Hii dawa waambie waache hayo maombi yao maana miungu ndio itamsaidia huyo mgonjwa wao”
“Sasa sitaweza maana hata wakiniona wananitimua, hivi nitawezaje kuwaambia waache maombi na waamini hizi dawa?”
“Najua unanijua dawa zangu huwa haziongopi na hakuna kinachoshindikana kwangu, vyote vinawezekana kuna dawa ya kunywa nitakupa ambapo muda nitakayokupa utainywa, na leo ukirudi kwako unainywa halafu kesho jiandae nenda kwa huyo rafiki yako, ukiwa unakaribia kwao inywe baada ya hapo hakikisha unaingia kwao saa saba mchana, ukiingia tu kwanza watakuwa na mshangao wa ulivyopendeza, kitendo cha wewe kuwapa salamu kitafanya wasikilize kila utakacho waambia ndio utaanza kufanya dawa kama nilivyokuelekeza na keshokutwa mtamleta huyo mgonjwa hapa kwangu ili apone kabisa maana akija hapa ndio funga kazi, yani usijali hao wenyewe watambeba mgonjwa wao na kumleta hapa, yani kwangu hakuna kinachoshindikana yani wasiokusikiliza watakusikiliza, mimi ndio kila kitu, ukisikia wananisifia babu wa Bagamoyo ujue kuna kitu kwangu ambacho wengine hawana”
Kwakweli Dora alifurahi sana kwani alitamani siku zote kupata dawa ya kusikilizwa kila anachosema, alimshukuru Yule mganga ambapo alimpa kwanza dawa hiyo ya kusikilizwa na kuinywa kama alivyoelekezwa kisha nyingine aliambiwa anywe akifika na nyingine akifika kwakina Erica, kisha akampa dawa za kumfanyia Erica na maelekezo kuwa nyingine amnyweshe na nyingine amuogeshe. Dora alishukuru sana na kuulizia ile dawa ya kusikilizwa vizuri,
“Kwahiyo nitasikilizwa na kila mtu?”
“Yani hii dawa inaenda kulainisha matamshi yako, hakuna utakachosema kisisikilizwe, hii ndio hutumiwa na wanasiasa wengi sana. Sababu wewe umekuwa mteja wangu mzuri ndiomana nimekupa, unaweza shangaa mtu kaja kakwambia jambo la ajabu tu ila umemfuta kumbe sababu yah ii dawa, matapeli wengi huitumia ndiomana anamlainisha mtu kwa maneno na mtu anatoa kila kitu baada ya hapo anajuta maana maneno yale hayana ukweli hata kidogo”
“Kwahiyo hata hawa wanaojifanya wanapenda maombi”
“Achana na habari za maombi kwangu, wewe ukifika anza na salamu ili sauti yako yenye kivutio iwaingie masikioni na hapo unajikuta umewalainisha na gafla wanaanza kukusikiliza wewe”
“Oooh asante sana babu, nashukuru sana”
Kisha akatoa laki tatu kwenye chungu cha babu kama hela ya shukrani halafu akatoka na Sia kuingia, aliambiwa aweke kifungua kilinge akatakiwa kuweka elfu hamsini sababu ya swala lake, basi Sia aliweka ile pesa, Yule babau akamwambia,
“Usishangae pesa ndefu ni sababu kazi yangu ni ya uhakika yani ukitoka hapa, leo ukimfanyia huyo mtu hiyo dawa basi nakwambia hafurukuti kwako”
Kisha akampa dawa kama alizopewa Dora za kumvuta James, ila yeye alitaka na dawa nyingine ya kumuita Erick ili aweze kumpa hiyo dawa,
“Sawa sawa, hapa hakuna kinachoshindikana ila kukuongeza dawa nyingine inabidi uandae elfu hamsini nyingine ya shukrani”
“Sawa hakuna tatizo”
Basi Yule mganga akampa dawa nyingine Sia ya kuchoma ili kumvuta Erick na akifika ampe tunda atakalokuwa ameweka dawa kisha ampe Erick na baada ya hapo ndio ampe chakula chenye dawa ili awe wake kabisa,
“Kwahiyo hii ya kuchoma uwe unachoma huku unasema Erick njoo yani unasema hivyo mpaka utakapomaliza, utaona mwenyewe yani atakuja bila kumuita sasa ndio umpe hilo tunda ale yani jitahidi kumlaghai ale hilo tunda. Ila ni vizuri uchome mchana ili jioni afike maana anaweza akalala huko huko na inakuwa rahisi kumpa chakula chenye dawa”
“Sawa, nashukuru sana”
Basi akatoa na ile hela ya shukrani na kutoka nje kisha kuongozana na Dora huku wakiondoka, yani njia nzima alikuwa akimshukuru Dora kwa kumpeleka kwa Yule mtaalamu,
“Yani sina la kukwambia nashukuru sana”
“Wewe usijali, mambo yakishakamilika niite nije nimuone shemeji”
“Sawa, hata usijali”
Muda huo Dora hakuelewa kuwa anayefanyiwa hizo dawa ni Erick Yule Yule mchumba wa Erica.
Bite alitulia na mdogo wake akiendelea kumfanyisha mazoezi mazoezi ya baadhi ya vitu, akapiga simu Yule mwanamaombi na kuwaambia kuwa amesharudi kwahiyo ataenda kesho yake kwaajili ya kumuangalia Erica na kufanya maombi pamoja nao,
“Kwahiyo utafika muda gani?”
“Nitafika nadhani mchana sababu nahitaji tufanye maombi na tusome neno kiasi”
“Karibu sana”
Bite alishukuru na kuagana nae, mama yao alivyofika alimwambia jinsi alivyoongea na Yule mwanamaombi,
“Oooh afadhali aje, nahamu sana ya kumfahamu huyo mama maana kanitia moyo sana yani sana kwa kipindi hiki cha Erica, namshukuru sana kwakweli, amakweli Mungu kamtumia huyu mama”
“Basi kesho anakuja mama”
Basi mama Erica alikaa na mwanae Erica huku akifurahi tu maana alivyoambiwa Yule mama anafika alijikuta akipata amani ya moyo kabisa.
Jioni yake alifika Erick kama kawaida ila kumuuliza chochote hawakuweza na walimwambia tu kuwa Yule mwanamaombi anafika kesho, akauliza tu ni muda gani,
“Kwahiyo kesho saa ngapi?”
“Kasema mchana”
“Kesho kuna kazi nilikuwa nataka kuzimalizia ila nitakuja kwaajili ya hayo maombi kwani hata mimi najiona nikihitaji maombi pia”
“Karibu sana”
Basi Erick aliendelea kuongea ongea na Erica pale kwani yeye ilikuwa fahari tu kwake kila anapoongea na Erica.
Ila Rrick na siku hiyo aliporudi hotelini alijaribu kumpigia tena Rahim kwani alitaka kujua ukweli wa ile hela.
Leo ndio ilikuwa siku ambayo Dora na Sia walipanga kwenda kwa babu wa Bagamoyo, kwahiyo walikutana na kuanza safari ya kwenda kwa huyo Babu ambapo alianza kuingia Dora na kueleza azma yake kisha akaonyeshwa wabaya wa Erica walioshiriki kumletea ule ugonjwa alishangaa kuona Derick nae aliungana na wale wanawake, Yule mganga akamueleza,
“Yani ni hivi, huyu mwanamke wa kwanza alienda kwa huyu mwanaume kuchukua majina ya huyo binti na kisha alipotajiwa akamtumia huyu mwanamke wa pili kisha huyu mwanamke wa pili ndio alimuendea kwa huyu mzee na kumfanya walivyomfanya, lengo lao walitaka awe chizi na mwisho wa siku rafiki yako angegongwa na gari na kufa, sema haijawezekana kuwa chizi maana rafiki yako ana imani kubwa sana na Mungu. Ila mimi nitakusaidia kukupa dawa ya kumponya kabisa na tunaweza kuwarudishia wale makombora”
“Ila ndugu zake wamekazana na maombi”
“Hii dawa waambie waache hayo maombi yao maana miungu ndio itamsaidia huyo mgonjwa wao”
“Sasa sitaweza maana hata wakiniona wananitimua, hivi nitawezaje kuwaambia waache maombi na waamini hizi dawa?”
“Najua unanijua dawa zangu huwa haziongopi na hakuna kinachoshindikana kwangu, vyote vinawezekana kuna dawa ya kunywa nitakupa ambapo muda nitakayokupa utainywa, na leo ukirudi kwako unainywa halafu kesho jiandae nenda kwa huyo rafiki yako, ukiwa unakaribia kwao inywe baada ya hapo hakikisha unaingia kwao saa saba mchana, ukiingia tu kwanza watakuwa na mshangao wa ulivyopendeza, kitendo cha wewe kuwapa salamu kitafanya wasikilize kila utakacho waambia ndio utaanza kufanya dawa kama nilivyokuelekeza na keshokutwa mtamleta huyo mgonjwa hapa kwangu ili apone kabisa maana akija hapa ndio funga kazi, yani usijali hao wenyewe watambeba mgonjwa wao na kumleta hapa, yani kwangu hakuna kinachoshindikana yani wasiokusikiliza watakusikiliza, mimi ndio kila kitu, ukisikia wananisifia babu wa Bagamoyo ujue kuna kitu kwangu ambacho wengine hawana”
Kwakweli Dora alifurahi sana kwani alitamani siku zote kupata dawa ya kusikilizwa kila anachosema, alimshukuru Yule mganga ambapo alimpa kwanza dawa hiyo ya kusikilizwa na kuinywa kama alivyoelekezwa kisha nyingine aliambiwa anywe akifika na nyingine akifika kwakina Erica, kisha akampa dawa za kumfanyia Erica na maelekezo kuwa nyingine amnyweshe na nyingine amuogeshe. Dora alishukuru sana na kuulizia ile dawa ya kusikilizwa vizuri,
“Kwahiyo nitasikilizwa na kila mtu?”
“Yani hii dawa inaenda kulainisha matamshi yako, hakuna utakachosema kisisikilizwe, hii ndio hutumiwa na wanasiasa wengi sana. Sababu wewe umekuwa mteja wangu mzuri ndiomana nimekupa, unaweza shangaa mtu kaja kakwambia jambo la ajabu tu ila umemfuta kumbe sababu yah ii dawa, matapeli wengi huitumia ndiomana anamlainisha mtu kwa maneno na mtu anatoa kila kitu baada ya hapo anajuta maana maneno yale hayana ukweli hata kidogo”
“Kwahiyo hata hawa wanaojifanya wanapenda maombi”
“Achana na habari za maombi kwangu, wewe ukifika anza na salamu ili sauti yako yenye kivutio iwaingie masikioni na hapo unajikuta umewalainisha na gafla wanaanza kukusikiliza wewe”
“Oooh asante sana babu, nashukuru sana”
Kisha akatoa laki tatu kwenye chungu cha babu kama hela ya shukrani halafu akatoka na Sia kuingia, aliambiwa aweke kifungua kilinge akatakiwa kuweka elfu hamsini sababu ya swala lake, basi Sia aliweka ile pesa, Yule babau akamwambia,
“Usishangae pesa ndefu ni sababu kazi yangu ni ya uhakika yani ukitoka hapa, leo ukimfanyia huyo mtu hiyo dawa basi nakwambia hafurukuti kwako”
Kisha akampa dawa kama alizopewa Dora za kumvuta James, ila yeye alitaka na dawa nyingine ya kumuita Erick ili aweze kumpa hiyo dawa,
“Sawa sawa, hapa hakuna kinachoshindikana ila kukuongeza dawa nyingine inabidi uandae elfu hamsini nyingine ya shukrani”
“Sawa hakuna tatizo”
Basi Yule mganga akampa dawa nyingine Sia ya kuchoma ili kumvuta Erick na akifika ampe tunda atakalokuwa ameweka dawa kisha ampe Erick na baada ya hapo ndio ampe chakula chenye dawa ili awe wake kabisa,
“Kwahiyo hii ya kuchoma uwe unachoma huku unasema Erick njoo yani unasema hivyo mpaka utakapomaliza, utaona mwenyewe yani atakuja bila kumuita sasa ndio umpe hilo tunda ale yani jitahidi kumlaghai ale hilo tunda. Ila ni vizuri uchome mchana ili jioni afike maana anaweza akalala huko huko na inakuwa rahisi kumpa chakula chenye dawa”
“Sawa, nashukuru sana”
Basi akatoa na ile hela ya shukrani na kutoka nje kisha kuongozana na Dora huku wakiondoka, yani njia nzima alikuwa akimshukuru Dora kwa kumpeleka kwa Yule mtaalamu,
“Yani sina la kukwambia nashukuru sana”
“Wewe usijali, mambo yakishakamilika niite nije nimuone shemeji”
“Sawa, hata usijali”
Muda huo Dora hakuelewa kuwa anayefanyiwa hizo dawa ni Erick Yule Yule mchumba wa Erica.
Bite alitulia na mdogo wake akiendelea kumfanyisha mazoezi mazoezi ya baadhi ya vitu, akapiga simu Yule mwanamaombi na kuwaambia kuwa amesharudi kwahiyo ataenda kesho yake kwaajili ya kumuangalia Erica na kufanya maombi pamoja nao,
“Kwahiyo utafika muda gani?”
“Nitafika nadhani mchana sababu nahitaji tufanye maombi na tusome neno kiasi”
“Karibu sana”
Bite alishukuru na kuagana nae, mama yao alivyofika alimwambia jinsi alivyoongea na Yule mwanamaombi,
“Oooh afadhali aje, nahamu sana ya kumfahamu huyo mama maana kanitia moyo sana yani sana kwa kipindi hiki cha Erica, namshukuru sana kwakweli, amakweli Mungu kamtumia huyu mama”
“Basi kesho anakuja mama”
Basi mama Erica alikaa na mwanae Erica huku akifurahi tu maana alivyoambiwa Yule mama anafika alijikuta akipata amani ya moyo kabisa.
Jioni yake alifika Erick kama kawaida ila kumuuliza chochote hawakuweza na walimwambia tu kuwa Yule mwanamaombi anafika kesho, akauliza tu ni muda gani,
“Kwahiyo kesho saa ngapi?”
“Kasema mchana”
“Kesho kuna kazi nilikuwa nataka kuzimalizia ila nitakuja kwaajili ya hayo maombi kwani hata mimi najiona nikihitaji maombi pia”
“Karibu sana”
Basi Erick aliendelea kuongea ongea na Erica pale kwani yeye ilikuwa fahari tu kwake kila anapoongea na Erica.
Ila Rrick na siku hiyo aliporudi hotelini alijaribu kumpigia tena Rahim kwani alitaka kujua ukweli wa ile hela.