Simulizi: Nini maana ya mapenzi

Simulizi: Nini maana ya mapenzi

SEHEMU YA 406

Baada ya mama yake Rahim kuambiwa na Rahim kuhusu Zainabu aliamua kumuita Zainabu ili kuongea nae, na kiukweli alivyofika Zainabu alijikuta nay eye akimpenda Yule binti na alihisi huenda akamfaa mtoto wake zaidi na jinsi alivyokuwa anaongea na Zainabu alimuhisi kuwa ni binti mwenye busara sana,
“Hongera Zainabu, sijawahi kuzaa mtoto wa kike ila wewe umelelewa haswaa yani wazazi wako inaonyesha wanajivunia uwepo wako”
Zainabu alikuwa akitabasamu tu, Neema nae alikuwa mule ndani kwahiyo akaongezea,
“Ni kweli Zainabu ni binti mpole na mcheshi sana ingawa binadamu hawakosi maneno huwa wanasema kama mzuri mbona haolewi”
Basi Mrs.Peter akachangia hapo,
“Yani watu bhana, kwani ambao hawajaolewa ni wabaya jamani! Huwa muda haujafika tu. Kwani Zainabu una umri gani?”
“Nina miaka thelathini na tatu”
“Una mtoto?”
“Hapana”
“Miaka thelethini na tatu, hujaolewa na huna mtoto yani hujazalia nyumbani mmh wewe ni binti wa kuigwa kwakweli. Zainabu tafadhali uwe mkwe wangu nakuomba, nakuomba sana uolewe na mwanangu”
Zainabu akauliza,
“Mfano ningekuwa na watoto je?”
“Hata ungekuwa na watoto bado ningekuomba hili maana busara yako nimeipenda, nakuomba ukubali kuwa mke wa mwanangu”
Gafla mlango wa pale ndani ulifunguliwa na aliyeingia alikuwa ni Salma kumbe alikuja kusalimia siku hiyo, ila kitendo cha kumuona Zainabu ndani kwa mkwe wake kilimchukiza sana, alijikuta akimuweka mwanae pembeni na kusema,
“Nilijua tu kuwa wewe mwanamke huna jema kwangu muone vile. Kujifanya umeshika dini huku unavizia waume za watu”
Kisha akamsogelea karibu Zainabu na kumkunja ili apigane nae huku maneno ya ajabu ajabu yakiendelea kumtoka mdomoni.

Nasma alivyoona Bahati harudi nyumbani kabisa aliamua kuaita washauri ambao walimshauri Bahati ili arudi nyumbani, Bahati alirudi kwake ila kwa shingo upande sana yani hakutaka kurudi kwake maana hakutaka kurudi pale wakati mkwe wake yupo.
Basi siku ya leo, Nasma alikuwa ameenda kununua mahitaji ya nyumbani na ndani alibaki mamake pamoja na Bahati basi Yule mama alienda chumbani kwake kujipumzisha kidogo baada ya mjukuu wake kuwa amelala.
Alishangaa bahati kuingia mule chumbani, alimuuliza kwa mshangao,
“Mwanangu umeingia bila hodi?”
“Nimeshindwa kuvumilia”
“Umeshindwa nini?”
Bahati alimvamia huyu mama na kutumia nguvu na kumbaka sababu huyu mama hakuwa na nguvu za kumzidi Bahati na alipomaliza tu kumbaka mama mkwe wake alitoka pale ndani na kukutana na Nasma mlangoni akiwa anaingia ndani.
Alimkuta mama yake analia, alimuuliza kuwa tatizo ni nini,
“Nasma, mumeo kanibaka”
“Kheee kakubaka!”
“Yani mimi madawa yenu niliwakataza, hebu ona nilivyodhalilika”
Muda huo alifika dada yake Bahati pia, na kugonga mlango bila kufunguliwa aliamua tu kufungua na kuingia ndani. Alimkuta Nasma akimbembeleza mama yake huku mama yake akielezea jinsi alivyobakwa na Bahati.
Dadake akashtuka na kusema,
“Kheeee kumbe Bahati katimiza kweli hilo swala la kubaka?”
Wakashangaa kuwa kumbe Bahati alipanga, Nasma alimfata kwa hasira dada yake Bahati na kumwambia
“Kumbe mliyajua yote haya ila mliacha ili mama abakwe jamani! Sio utu kabisa”
“Ila mlichofanya nyie cha kumtia kaka yangu uchizi na madawa ndio vizuri! Hujui kama madawa yako ndio yamesababisha yote hayo, mwambie baba yako amtolee ndugu yetu madawa hayo la sivyo na yeye atabakwa”
Nasma akachukia sana na kuanza kupigana na huyu dada wa bahati sema kwavile huyu dada ni ana nguvu sana ni alimbamiza Namsa hadi akaanguka chini na kuzimia.

Mzee Jimmy hakufurahishwa kabisa na habari ya kusema Erica ana mimba basi aliamua moja kwa moja kwenda kwakina Erica, ambapo aliyemfungulia mlango alikuwa mama Erica mwenyewe,
“Haya wewe mzee usiyekuwa na haya umefata nini leo? Si ulizimia wewe! Kumbe hukufa eeeh na mke bado unamfatilia”
“Nimfatilie mwanao wa kazi gani? Ila mwambie mwanao maswala ya kumsingizi mwanangu mimba sio mazuri”
“Mimba gani aliyomsingizia?”
“Mimba ambayo mwanao anayo sasa, kashaanza kumsingizia mwanangu wakati ana wanaume wengi”
Mama Erica alishangaa kwanza na kuuliza kwa makini,
“Erica ana mimba?”
“Ndio Erica ana mimba”
Mama huyu alihisi kama kizunguzungu.
 
SEHEMU YA 407

Mama Erica alishangaa kwanza na kuuliza kwa makini,
“Erica ana mimba?”
“Ndio Erica ana mimba”
Mama huyu alihisi kama kizunguzungu.
Ni Bite alitokea nyuma yake na kumshika mama yake, kisha kumwambia Yule mzee aondoke zake, yani huyu mama aliingia ndani kwa kushikiliwa na Bite ni wazi alipata mawazo sana, hakutegemea kama mwanae kapata maamuzi ya kuzalia watoto wawili nyumbani yani alijihisi vibaya sana, alikaa chini na kuwa kimya kwa muda kidogo kisha alipopuma akaanza kuongea,
“Hivi huyu mtoto ananitakia nini mimi jamani? Anataka kunifanya nini Erica? Kila siku naimba wimbo hapa asibebe mimba kumbe ananicheka kuwa utaona jamani! Kuzaa imekuwa shida eeeh! Bite, sikuwazaa nje ya ndoa nyie, iweje mwanangu awe mtu asiyejielewa, ni mapenzi gani anayoyaendekeza yeye jamani!”
“Mama, punguza jazba”
“Siwezi Bite, yani siwezi kwakweli. Nimemkubali Angel kama mjukuu wangu ila Erica hathamini kujua ni aibu gani mama yake naipata mtaani, kuishi na mtoto kisiri siri hata unatoka nae unajua kabisa utasemwa ila upo tu, na mtaani walishaanza kusema kuwa tumeleta mtoto wa kiarabu na wanacheka balaa, halafu leo aonekane na mimba nyingine jamani! Hivi jamii itaniangaliaje mimi, watu watanitazamaje, itaonekana sijui kulea kabisa jamani, mbona dada zake hampo hivyo, huyu Erica ni mapenzi gani yanayomsumbua yeye hadi anakuwa hivyo?”
“Mama, angalia afya yako, usiongee sana ukapata presha. Tumsubiri huyo Erica arudi na tumuulize pengine ni uongo”
“Sidhani kama ni uongo”
Kisha mama yao akainuka na kwenda chumbani kwa Erica kupekua na kwa bahati nzuri au mbaya, akakiona kile cheti cha hospitali ambacho kinaonyesha kuwa Erica ni mjamzito, yani hapo ndio alihisi presha kupanda zaidi, Bite alipata kazi ya kumtuliza tu mama yao na alipoona kuwa inakuwa ni ngumu aliamua kumpigia simu Mage ili kumueleza na Mage aende nyumbani.
“Unasema Erica mjamzito? Kasema mwenyewe au nani kawapa hizo habari?”
“Ndio mjamzito na mama kachanganyikiwa kabisa maana habari hizo kuzipokea kwake imekuwa ngumu si unajua ni swala la aibu! Yule mzee wake alifika hapa na kusema huo ujinga wa Erica”
“Huyu mtoto anatia aibu kwakweli, mara nyingine bora angekuwa mbuzi tu tungekunywa supu yake kuliko kwa mambo anayoyafanya. Kachanganya ndugu weee kaona haitoshi, katembea na kaka yake, haitoshi, kaenda kutembea na baba na mwana haitoshi, kazaa nyumbani bado haitoshi na sasa kuleta mimba nyingine nyumbani kweli! Si bora hela ya kumsomesha mjomba angetugaia tu tujilie zetu raha kuliko kusomesha kichaa kama Erica jamani! Jitu linakatazwa kufanya mapenzi bado tu yumo, ni hamu gani alizonazo yeye anayeshindwa kuzizuia! Nimechukia sana, nakuja huko hata kama muda umeenda nakuja. Kwanza yuko wapi?”
“Unafikiri yupo nyumbani basi! Asubuhi asubuhi kamvalisha Angel kamdanganya mama kuwa anaenda kliniki, alipoondoka badae kapiga simu kuwa atachelewa kurudi na mpaka mida hii yani saa mbili usiku saivi hajarudi, kashindikana Yule”
“Nakuja huko”
Akakata simu na kuendelea kumbembeleza mama yao pale,
“Mama, Mage kasema anakuja pia kwahiyo mama shusha presha. Huyu Erica safari hii hata ndoa ya mkeka tutamfungisha kwakweli maana si kwa aibu hii anayotutia”
“Nakwambia Bite, sijawahi kumpiga Erica toka akue maana neno nisamehe ndio humtoka upesi kuliko maneno yote ila leo hata aseme nisamehe mara mia nitampiga tu, yani leo nitampiga sana mpaka akili imkae sawa”
“Sasa mama, ukimpiga hivyo na mjamzito si mimba itatoka?”
“Na itoke tu, asiniletee ujinga nyumbani kwangu”
Bite alielewa kuwa mama yake ana hasira sana na anaongea yote yale sababu ya hasira maana alichukizwa vilivyo kwa kilichotokea nyumbani kwake, walikaa wakimngoja kwa hamu huyo Erica arudi.

Nyumbani kwakina Rahim, yani mrs.Peter alichukizwa sana na kitendo cha Salma kumparamia Zainabu ili apigane nae mpaka ilibidi waamulie tu huku Neema akimshika Salma ila Salma aliendelea kuongea maneno ya ajabu,
“Na wewe Neema hebu niache, mwanamke una roho mbaya wewe kama mchawi muone vile. Ndiomana kutwa kucha kujifanya unanifundisha jinsi ya kuishi na mume kumbe unanionea wivu na unataka kumleta mtu wa kunirithi, mwanamke una roho mbaya wewe niachie”
Alipoona Neema hamwachii alimng’ata mkono ili amuachie ilibidi Neema amuachie na kuelekea tena kwa Zainabu ila Zainabu alitulia tu kumuangalia Yule binti akimparamia mwilini, Mrs.Peter alishindwa kuamulia na kuamua kwenda kumuita Rahim.
Zainabu alipoona Salma anazidi kumsumbua alimshika mikono na kumnasa vibao, yani kitendo kile ndio kama kilimtia ukichaa Salma maana alijikuta akianza kutupa vitu vya kwenye nyumba ya mama mkwe wake bila kujali ni vitu vya kwa mama mke.
Basi Rahim na John walifika na siku hiyo alikuwepo Babuu ambaye alikuwa akiongea na Rahim, walipoingia ndani kile kitendo cha Salma kiliwachukiza sana yani walichukia mno, Rahim alienda kumshika Salma na kutaka kumpiga sana ila ndugu zake wakamzuia kuwa asifanye hivyo, basi alimkalisha chini kwa hasira, kwakweli mrs.Peter aliangalia mule ndani kwake na kusikitika sana kisha akasema,
“Salma, sikutegemea kama upo hivi kwakweli sikutegemea kabisa kumbe mwanangu alikuwa hakosei kukupiga, mwanangu hakukosea kukupa talaka yani sikutegemea kama tumemuolea Rahim mwanamke chizi kama wewe. (Kisha akamuangalia Zainabu na kumwambia) Zainabu mama hata tusizunguke mbuyu nahitaji sana uwe mke wa mwanangu na kesho tutakuja kwenu kujitambulisha ili kufanya mambo haraka haraka”
Muda ule ule Salma alianza kulia kama amefiwa vile, kwakweli iliwashangaza sana na mara alinza kusema anacholilia,
“Mmenipotezea muda wangu kusubiria toto lenu malaya, nimemvumilia kwa kipindi chote kwanza linaumiza balaa ila nimevumilia halafu mananifanyia hivi! Sikujua kama familia hii ina roho mbaya kiasi hiki, na wewe Zainabu yatakukuta tu maana hii sio familia ya kuishi nayo ni makatili hawa”
Akainuka na kumchukua mwanae halafu akaondoka, hakuna aliyemfata kwani kile kichaa chake hakuna aliyekitaka kwa muda huo kwani alikuwa ashaharibu vya kutosha pale sebleni.

Mage nae alipokuwa anaenda kwao alijikuta kuwa na hasira sana na mdogo wake na kuamua kumpigia simu kwanza ili kuyabwaga ya moyoni.
Muda huo, Erick na Erica walikuwa njiani kurudi nyumbani ambapo Angel alikuwa amelala, kwahiyo Erica alipoona kuwa dada yake anapiga simu sana aliamua kupokea ili kujua tatizo ni nini, alipokea na kumsalimia dada yake ila dada yake hakupokea ile salamu na kuanza tu kumshushia maneno,
“Wewe mtoto usiye na akili hata moja yani kwako moja haikai mbili haisogei, hivi unafikiriaga kwa kutumia nini? Huwa unatumia ubongo wewe au makalio yako ndio yanakutuma kufanya ujinga”
“Ujinga gani tena dada?”
“Hivi wewe ni wa kumuaibisha mama kiasi hiki, uzalie Angel nyumbani na bado unabeba mimba nyingine nyumbani”
“Dada, mbona mimi sina mimba”
“Huna mimba wapi mjaa laana wewe, wakati zee lako limekuja kusema kuwa una mimba, na mpaka muda huu hujarudi nyumbani ushaanza kumuhangaisha Angel kwa wanaume zako huko, na mimi naenda nyumbani nikukute wewe, urudi muda huu huu nyumbani mjinga wewe”
Kisha dadake akakta simu na hapo Erica akajua kuwa siri ya mimba yake imefichuka kwao, kwa jinsi alivyokuwa akionge kwa mshangao ilifanya Erick aweke gari pembeni ili amsikilize kuwa tatizo ni nini, alimuona Erica akiinama chini huku akiwa na mawazo tele, alimuuliza
“Mpenzi, nini tatizo?”
“Nyumbani wamejua kama nina mimba yani sijui itakuwaje”
“Kwani kuwa na mimba ni tatizo?”
“Si tatizo kwa mtu aliyeolewa ila kwa mimi ambaye sijaolewa ni tatizo kubwa sana, unajua mimba ni kielelezo tosha cha uzinzi. Yani ukiwa na mimba huwezi kukataa kuwa hujazini, na mama kila siku ananikataza habari za kuzini, aliniambia mpaka niolewe maana nishamtia aibu kwa Angel. Nilijiapia kufanya hivyo na ndiomana sikutaka hata kutumia uzazi wa mpango sababu nilijua nitaweza kujizuia hadi ndoa”
“Sasa swala la uzazi wa mpango limekuja vipi hapo? Inamaana Erica hukupenda kuzaa na mimi?”
“Sio hivyo Erick, yani sijui kama unanielewa mpenzi. Swala ni hivi, nyumbani huko kimewaka moto maana wamejua nina mimba yani leo nahisi mama atanipiga kipigo kisichoelezeka, yani nimechanganyikiwa”
“Mmmh akikupiga si mimba yangu itatoka? Erica, sitaki itokee ya kipindi kile kutoa mimba yangu”
“Kwani kipindi kile nilipenda Erick, ila dada zangu ndio walinishikilia bango nitoe ile mimba ili mama asijue yani hospitali na kila kitu walifanya wao. Sasa leo nyumbani, uwiiii sijui nifanyeje”
Erick akafikiria kidogo na kusema,
“Erica, hata mimi nahitaji kuwa na damu yangu, nahitaji kupata mtoto kutoka kwako na hata hivyo sihitaji upate matatizo sababu ya starehe zangu. Kuna jambo nawaza hapa, naomba unikubalie”
“Jambo gani hilo?”
“Naomba leo usirudi kwenu, tukatafute hoteli ukakae huko kwanza halafu mimi nifanye harakati za kuwasiliana na kwenu kisha tufunge ndoa. Si mama anahitaji uzalie ndani ya ndoa? Basi itawezekana tukifanya hivyo mpenzi au unaonaje? Ila usikatae tafadhali”
“Erick umeongea jambo jema ila sasa nisiporudi nyumbani si ndio balaa zaidi?”
“Erica, waswahili husema heri nusu shari kuliko shari kamili, ushasema kwenu wana jazba leo hivi wakikuona si ndio balaa zaidi, kwanza ni Mungu tu kafanya huyu dada yako akupigie simu huku akiwa na hasira hivyo zilizokuchanganya na wewe maana wangeweza wasubiri urudi tu na upate kipigo, ni heri kusubiri hasira zao zipoe kuliko kuchukua maamuzi kwasasa, kubali Erica tafadhali, nami sitaondoka tutakuwa wote hapo hotelini na kesho nitaenda kuwatafutia nguo wewe na Angel, huku tukiendelea kujadili cha kufanya, kwasasa kubali swala hili”
Erica alifikiria kwa kina na kuwaza akirudi kwao sokomoko atakalokutana nalo, akaona ni bora akubaliane na wazo la Erick tu maana hakuwa na jinsi kwa wakati huo.
Basi Erick aligeuza gari yake na kuanza kwenda kwenye hoteli ambayo alihisi itawafaa kwa siku kadhaa.
 
SEHEMU YA 408

Mage alifika nyumbani kwao akiwa amechukia sana, na alipogonga na kuingia ndani alishangaa kuambiwa kuwa Erica hajarudi hadi muda huo,
“Kheee mpaka saa hizi hajarudi? Mtoto ana wazimu huyu si bure, hivi jamani alitoka na nani?”
Bite akajibu,
“Nadhani ni kale katahira kenzie, kale ka Erick sijui yani nimejikuta nakachukia kale kavulana. Wanajifanya kutulia hapa wakati mwanamaombi anaomba kumbe anasubiri kwa hamu Erica apone wakafanye uzinzi”
“Ila mi nilikuwa nawaangalia tu mnavyomuachia Yule kijana na Erica, mi niliwashangaa kwakweli yani mnawaacha utafikiri wanandoa, kijana kutwa kucha yuko hapa, sijui kutafuta hadi madaktari wa kumuhudumia Erica ndio amuoe sasa”
“Atamuoa waishije unadhani? Huyo Erica si ndio atakuwa mboga ya kwao yani baba na mtoto na jinsi aivyoweza kujitetea mjinga Yule”
Mama yao ingawa alikuwa na hasira ila kwa muda huo alimtetea kidogo Erica,
“Jamani, Erica kama hawezi kujitetea basin i huko kwingine ila mkumbuke kuwa Erica alijitetea kwa shemeji yake. Kwa yale majaribu ya James, ingekuwa Erica yupo legelege basi angeshatembea nae jamani. Yote sina habari nayo mimi ila inayoniumiza kichwa ni kwanini abebe tena mimba nje ya ndoa? Yani hapo ndio ninapoumia kichwa”
Mage na Bite kwa upande mwingine waliona kama mama yao anampendelea sana Erica kwahiyo waliamua kunyamaza kwa muda kwanza kisha Mage akasema,
“Mama, watoto wako kwasasa tumekuwa na tunapokuja kwenye swala kama hili tuache tuongee ya moyoni, Erica ni mdogo wetu na tuna haki ya kuongea chochote juu yake kwahiyo mama acha tuongee sio kila siku kutukatisha tu. Kumbuka mimi ni mtoto wako wa kwanza yani kifungua tumbo lako ila sijawahi kutenda ujinga kama huu unaofanywa na Erica, inatuuma mama na tuna haki ya kuongea”
Basi walijadiliana huku wakiendelea kumsubiri Erica, ila waliona saa sita usiku inawafikia pale pale bila ya Erica kurudi nyumbani.
Muda kidogo walishangaa kuona kuna namba inaita kwenye simu ya mama yake Erica, basi Bite alipokea simu ile kumbe mpigaji alikuwa ni mzee Jimmy, na kuanza kuongea nae,
“Erica hapokei simu zangu, yuko hapo niongee nae”
“Hapana hajarudi, labda uniambie mimi mwenyewe”
“Sasa akirudi mwabieni asiitoe hiyo mimba, anataka amsingizie mwanangu wakati ni mimba yangu. Mwambieni nitamuoa, nilichukia sana ila nitamuoa asiitoe hiyo mimba”
Kisha akakata simu na Bite alimueleza mama yake ambaye alihisi presha zaidi kuwa licha ya Erica kuwa na mimba ni mimba yam zee asiyempenda kabisa katika maisha yake.

Erick alikuwa na Erica hotelini na mtoto alikuwa amelala, kiukweli Erica alishindwa kulala kabisa kwani aligubikwa na mawazo sana. Erick alimuuliza,
“Erica, hupendi hivi tupo pamoja? Furahi bhana, mimi ndio mumeo, na ndoa yetu inanukia sasa maana kipo cha kufanya nikuoe haraka”
Erica alitabasamu tu kisha Erick alimkumbatia na kuweza kumbembeleza alale.
Kulipokucha ni Angel alikuwa wa kwanza kuamka na kumsogelea mama yake ambaye aliamka pia, Angel alianza kumdai mama yake uji maana alishazoea akiamka asubuhi basi anakunywa uji yani hilo swala ndio likampa mawazo zaidi Erica na kumuuliza Erick kuwa watafanyaje, ila Erick akaamua kuondoka kidogo na baada ya muda alirudi na uji kwenye chumba na kikombe kwaajili kumuwezesha Angel anywe uji. Kwakweli Erica alifurahi sana na kuona kuwa Erick ana moyo wa upendo na kujali, basi alimmiminia ule uji Angel na kumpoozea kisha kuanza kumnywesha ambapo muda huo Erick alimuaga na kuondoka kwani alitaka akatafute nguo za kubadilisha kwaajili ya Erica na Angel.
Alivyoondoka Erick tu basi Erica aliendelea kumnywesha uji Angel na alipomaliza alichuua simu yake na kumpigia Dora kwani kwa muda huu alihisi kuwa Dora ndio msaada pekee alionao.
“Erica, niambie mama yangu nini tena?”
“Safi tu, nilikuwa nakusalimia”
“Mmmh salamu tu hiyo Erica au nije kwenu tuongee vizuri”
“Hapana usije nyumbani ila nitakwambia vizuri badae subiri kidogo”
Alikata simu kwani alitaka ajipange kwanza ndio aongee na Dora ili aweze kupanga nae mipango, na muda huo Erick aliingia mule ndani kwahiyo hakuweza kuongea nae jambo lolote lile zaidi ya kukata ile simu.
Erick alikuwa amewaletea nguo Erica na Angel ili wakioga wapate za kubadilisha kisha alimuachia hela pale na kumuaga,
“Naenda nyumbani mara moja Erica maana kuna kitu nawaza”
“Kitu gani Erick?”
“Nitakwambia tu, ila ngoja niende nyumbani mara moja si unajua uamuzi huu tumeuchukua kwa muda mfupi!”
Erica alimuelewa na kukubaliana nae, basi Erick aliondoka na kwenda nyumbani kwao.

Mzee Jimmy alichukia sana nyumbani vile kijana wake hakurudi kabisa, aliona Erick kaanza kutokuwa na heshima kabisa, ingawa siku za nyuma ilikuwa ni kawaida kwa Erick kukaa hata wiki bila kurudi kwao na hakuna aliyekuwa akimfatilia ila siku hiyo alionekana kuchukizwa sana na swala la Erick kulala nje ya nyumba yao.
Ile asubuhi alimuita Tumaini na kuongea nae,
“Huyu mdogo wako kaanza tabia gani ya kulala mbali na nyumbani?”
“Ila baba, Erick ndio zake yani hii sio mara ya kwanza ni kawaida yake. Anaweza kukaa hata wiki hajarudi nyumbani”
“Huwa anafanya huo ujinga wakati mimi nipo wapi?”
“Baba, ulikuwa unarudi usiku na kulala hata hatuonani kwahiyo Erick alikuwa halali hapa na wala hugundui”
“Sawa nimekubali nilikuwa siwaangalii ila huu anaoufanya kaka yako ni upuuzi na akirudi mwambie nimegundua habari za mimba ya Erica, mwambie kaka yako akae mbali na Erica maana kwa vyovyote vile atamuoa Sia nimemaliza”
Baba yao muda huo akatoka na kuondoka ila muda sio mrefu sana alifika Erick na kumkuta dada yake Tumaini akiwa anajiandaa pia kutoka na baada ya salamu alimueleza kile ambacho baba yake amesema,
“Aaah Tumaini achana na hayo maneno ya baba ila kuna jambo lingine limetokea bhana”
“Jambo gani tena?”
Bali Erick alianza kumueleza dada yake kwa kifupi jinsi ilivyokuwa,
“Kheee kwahiyo balaa kwakina Erica na mimba ya Erica!”
“Ndio hivyo, kwahiyo jana tumelala hotelini maana nimeshindwa hata kumrudisha kwao”
“Mmmh na bora mmejihami uwiii mamake Erica ana nguvu balaa, Yule mama angewachakaza. Mimi aliwahi kunipiga vibao hivyo huwa sivisahau hadi leo maana hadi nilihisi kizunguzungu na mbele sioni, weee mama ni noma Yule”
“Sasa mimi nilitaka niende kwao ili nijaribu kuongea na mama yake na kuomba msamaha”
“Erick, hujipendi mdogo wangu yani Yule mama muone vile vile, ana nguvu jamani balaa nakwambia mimi nilipigwa vibao tu ila nilijihisi kizunguzungu halafu wewe uliyemtia mimba binti yake ndio ukajifanye kuongea nae mmmh utachakazwa mdogo wangu tukusahau maana najua kumrudishia mama mkwe unaanzaje. Yani tafuta tu njia nyingine”
“Njia gani sasa?”
“Tafuta wazee wa busara wakaongee na wazazi wa Erica, yani tafuta kama washenga”
“Sasa washenga bila baba itakuwaje?”
“Yani hapa ndio kwenye mtihani mkubwa ila mdogo wangu ndoja tufikirie cha kufanya yani usiende kabisa kwakina Erica, nakupenda mdogo wangu Yule mama namfahamu sijui ujana wake alikuwaje, ana nguvu sana Yule mama”
Basi alikubaliana na dada yake huku akimuelekeza chumba walichopo kwenye hiyo hoteli ili hata kama akimtafuta ajue ni wapi pa kumpata kisha akachukua baadhi ya nguo zake ili aende kuzipeleka kule hotelini maana aliona ndio njia pekee kwa kipindi hiko kuishi na Erica tu.
 
SEHEMU YA 409

Familia ya Erica kiukweli walizidi kuchukizwa na kitendo cha erica kutokurudi nyumbani kwao, na vile Mage alisema kuwa alimuuliza wakajua ndio sababu kuwa huenda Erica ameogopa kurudi nyumbani,
“Erica anasahau kuwa laana ya mzazi ni kubwa sana maana nahisi hela za Yule mvulana ndio zimemzuzua mama mpaka hajarudi hadi leo”
Muda kidogo kuna mtu aligonga, walipomfungulia na kuingia ndani alikuwa ni Dora maana hakuelewa ni kwanini Erica kamwambia kuwa asiende kwao nay eye alienda tu akiamini huenda rafiki yake ana matatizo, ila alikuta pale kwao tofauti kwani mamake Erica alianza kwa kumbana Dora kuwa Erica yuko wapi,
“Sijui mama ila asubuhi nimeongea nae kuwa yuko salama, nikamuuliza nije kwenu akakataa yani mimi sijui lolote. Kwani imekuwaje?”
“Imekuwaje nini si mnajifanya mnafichiana siri, mwenzio ana mimba ya Yule mzee”
“Erica ana mimba?”
“Unashangaa nini sasa, kwani ndio mara ya kwanza kwa Erica kubeba mimba?”
“Hapana ila nimeshangaa tu ila hiyo mimba haiwezi kuwa ya mzee Jimmy, kama amejisifia hivyo mjue ni muongo. Hiyo mimba itakuwa ya Erick tu ila imekuwaje, nani kaleta hizi habari?”
“Imekuwaje kuhusu nini? Mzee wenu kaja hapa na kasema kuwa Erica ana mimba yake”
Dora alishangaa tu ila akaona kuwa huyu mzee kawalaghai hawa watu.
“Kwahiyo Erica yuko wapi?”
“Sijui mwenyewe”
Basi Dora aliamua kuondoka tu pale kwakina Erica ila kitendo cha mzee Jimmy kusema kuwa mimba ya Erica ni yake hakukipenda kabisa.
Alipofika kituoni aliamua kumpigia simu Erica ili kumuuliza vizuri alipo na kumwambia kuwa ametokea nyumbani kwao,
“Ila Dora, si nilikwambia kuwa usiende nyumbani!”
“Ni kweli uliniambia Erica ila sikujua ni nini kimekupata, niambie ulipo nije nikueleze na yaliyonikuta nyumbani kwenu.”
Basi Erica akamtajia hoteli aliyokuwepo na baada ya muda tu Dora alifika kwenye ile hoteli na kwenda kukaa nae kwenye bustani ya ile hoteli wakinywa vinywaji na kuzungumza ambapo Dora alimueleza rafiki yake kitu ambacho kilijiri nyumbani kwao, basi Erica naye alimwambia uamuzi ambao yeye na Erick wameuchukua, basi Dora alianza kumshauri Erica pale,
“Sasa Erica nikushauri kitu rafiki yangu”
“Nishauri”
“Kwa nionavyo ni kuwa Erick anakupenda sana, na kama anakupenda basi hii ndio nafasi ya kutimiza lile mlilokuwa mkilihitaji kwa muda mrefu sana. Ili mradi mmeshaamua hadi kukaa hotelini bila kurudi nyumbani basi ndio ujue maisha yako mapya yameanza hapo, sasa kuishi hotelini siku zote itawagharimu sana kwanza kumbuka mnaenda kuwa na familia, kuna mtoto huyu na huyo anayekuja kwahiyo lazima muwe makini kwanza”
“Eeeeh tufanyeje?”
“Mshauri Erick mkapange chumba, yani huko mtapata zaidi akili ya maisha kuliko kuishi hotelini maana hakuna mtakachofanya. Pangeni chumba na muanze kupanga maisha yenu, Erick hela anayo kwahiyo hapo kitu kinawezekana tu. Tafuteni nyumba ya kuishi, hela ipo kwahiyo mtapata kiurahisi halafu mnanunua vyombo vya ndani na kitanda na godoro yani taratibu mnaanza kupika na kuishi wenyewe hadi mnakuja kuoana mpo vizuri kuliko kuishi hotelini hadi ndoa maana kwasasa huwezi kurudi kwenu na kuishi kama zamani yani ukithubutu kurudi itakucost sana, kwahiyo fanya hivyo rafiki yangu.”
“Unajua sijawahi kufikiria kuwa Dora unaweza kuwa na ushauri mzuri kama huo, kwakweli leo nimeshangaa sana. Asante kwa huo ushauri na nitaufanyia kazi”
“Erica bhana, unahisi mimi ni wa kuongea pumba tu muda wote, kuna muda nina ya maana pia. Kwa maelezo yako uliyowahi kuniambia ni kuwa penzi lako na Erick lina vikwazo sana nah ii ndio njia pekee ya kuepeka hivyo vikwazo, muishi pamoja huku mipango ya ndoa ikiendelea”
“Asante sana”
“Halafu leo nita kusurprise rafiki yangu”
“Na nini tena?”
“Subiri tu utaona, si upo hapa hotelini? Subiri utaona”
Erica alicheka sababu hakujua kuwa rafikia yake anaongelea kitu gani kisha Dora akamuaga Erica pale na kuondoka zake.

Erica alirudi chumbani ila ushauri wa Dora ulimuingia vilivyo, Erick alirudi na kufurahi nae sana kisha Erick alimueleza jinsi alivyoongea na Tumaini kuhusu baba yao alichosema huku akiendelea kusema,
“Ila Yule mzee ana wazimu sana, jana usiku nilikuwa naona anapiga simu yako nikawa naikata yani Yule mzee bhana loh! Anaacha kuoa wazee wenzie anaanza kuibuka na vijana kweli?”
Erica aliachana na habari za mzee Jimmy na kuanza kumwambia ushauri Erick ambao alipewa na Dora ila hakumwambia kuwa Dora ndio amempa ushauri huo, Erick alitabasamu na kusema,
“Hakika nimepata mke mwenye akili sana, yani licha ya uzuri wako Erica ila bado una akili sana. Asante Mungu, kwakweli dah sijaamini kama ungeongea maneno ya akili kiasi hiko, ni kweli tutakuwa tunatumia gharama kubwa sana hapa hotelini wakati hii pesa tungeanzisha maisha yetu tu tufike mbali, dah mke wangu una akili sana. Nafurahi kukupata katika maisha yangu yani kesho tutakuwa tumepata nyumba ya kuanza na maisha yetu, Erica wewe ni mke bora katika wanawake wote duniani”
Erica alitabasamu na kufurahi sana kwani alikuwa anajua kuwa lile wazo kapewa na Dora ila yeye kafanya kama kalileta yeye.
Muda ule ule Erick alianza kuwasiliana na madalali kuhusu kupata nyumba maana baada ya lile wazo la Erica alitaka kesho yake wawe wameshaanza hayo maisha.
Basi kuna dalali muda ule ule alimuambia kuwa aende kuangalia mahali kwahiyo aliondoka na Erica pale na kumbeba Angel.
Walifika na kuonyeshwa nyumba hiyo, kwa hakika Erica aliipenda ile nyumba hata kutamani tu kuanza kuishi siku hiyo ila Erick alitaka watu waifanyie kwanza usafi na wao kwenda kesho,
“Erick jamani, usafi gani wa hadi watu wafanye? Si nitafanya mwenyewe!”
“Hebu acha zako Erica, unajua hali yako kabisa halafu unataka kufanya usafi, acha wafanye na kesho nitaagiza watu wa kutusaidia kuchukua vitu na kupanga ndani humu ila kwa leo acha wafanye usafi.”
“Mmmh sawa, hakuna shida”
“Sitaki uhangaike Erica hata kupanga napo ni kukuhangaisha tu ila sitaki upate manyanyaso yani nitajitahidi nijenge tu nyumba yangu maana sitaki baba atunyanyase kwa nyumba zake ingawa najua ana nyumba nyingi tu tungemwambia angetugaia moja”
Basi wakaongea ongea kule na kusimamia simamia vijana wa usafi, walipomaliza walianza kuondoka.
Njiani Erick alipitia sheli kuweka mafuta kwenye gari yake, wakati wanamuwekea mafuta pale sheli kumbe alikuwepo na James ambaye aliwaona Erica na mtoto wake kwenye gari ya Erick, alishuka na kuwafata, wakiwa ndani ya gari aliwagongea kioo ambacho Erica alifungua, kisha James alimuuliza,
“Kwenu wanajua?”
“Wanajua kuhusu nini?”
“Msichana unapenda wanaume wenye hela wewe, nadhani ulikuwa unatamani sana shemeji yako nikuoe”
Erica alimuangalia Erick na kumwambia kuwa Erick aondoe gari kwani hakutaka kabisa kuongea na Yule James. Kiukweli Erick hakupendezwa na kauli za Yule James na walipofika hotelini alitaka Erica amueleze vizuri ambapo Erica alimueleza kila kitu ila muda ule ule ujumbe uliinbgia kwenye simu ya Erica, na Erick aliichukua na kuusoma,
“Nimekumbuka sana utamu wako Erica, by James”
Erica pia alichukia ila kabla hajasema chochote alishangaa mtu kugonga mlango wao, Erick aliinuka na kwenda kufungua akashangaa ni Tumaini ameingia,
“Kheee Tumaini umekuja kufanya nini?”
“Kuna habari nimepata Erick?”
“Habari gani?”
“Twende”
Erick alitoka na kufatana na Tumaini, kuna mlango wa chumba kwenye ile hoteli wakagonga na akatokea mwanamke kuwafungulia, Erick alishangaa sana kwani mwanamke huyo alikuwa ni Dora na kuwakaribisha huku kajifunga taulo, walipoingia walishangaa zaidi kuona baba yao akitoka bafuni na taulo.
 
SEHEMU YA 410

Erick alitoka na kufatana na Tumaini, kuna mlango wa chumba kwenye ile hoteli wakagonga na akatokea mwanamke kuwafungulia, Erick alishangaa sana kwani mwanamke huyo alikuwa ni Dora na kuwakaribisha huku kajifunga taulo, walipoingia walishangaa zaidi kuona baba yao akitoka bafuni na taulo.
Ila mzee Jimmy wala hakuwa na habari kabisa kama kuna watu wameingia mule ndani, kisha Dora akaenda nyuma yake na kumbusu ambapo huyu mzee alianza pia kumbusu yani yale matendo watoto wake walikuwa wakiyashuhudia kwa macho yao, si Erick wala Tumaini walioweza kuendelea kumtazama baba yao, yani walitoka muda huo huo na kubamiza mlango, mzee Jimmy alishtuka na kumuuliza Dora,
“Inamaana hukufunga mlango?”
“Aaah kuna muhudumu alikuja kuchukua vitu humu”
“Jamani Dora kwahiyo katuona?”
“Hata akituona tatizo liko wapi, nilishindwa kujizuia kukuona ukitoka chooni yani nikajikuta nakutamani zaidi ndiomana nikaja nyuma yako upesi hata sikujali kuhusu muhudumu ila ngoja nikaufunge sasa”
Kisha Dora akainuka na kwenda kuufunga mlango kwa funguo za pale mlangoni halafu wakaaendelea na mambo yao sasa ila mzee Jimmy hakujua lolote kama watoto wake wamemshuhudia.

Erick na Tumaini walirudi kwenye kile chumba ambacho yupo Erica maana hakufatana nao, kwakweli Erick alikuwa na hasira zaidi kuona baba yake akiwa na Dora, alikuwa na hasira kiasi cha kumwagikwa na machozi, Erica alikuwa akimbembeleza bila kujua nini kimetokea, Tumaini alikaa chini akimtuliza mdogo wake,
“Hebu Erick acha hasira hizo ndugu yangu?”
Erica akauliza,
“Kwani nini kimetokea?”
Basi Tumaini akaanza kumuelezea,
“Unajua Dora nilikutana nae leo akaniambia kuwa anataka kunihakikishia kuwa anatoka na baba yangu, nikamwambia ni uongo maana baba hawezi kuwa nae. Sasa nikiwa nyumbani Dora akanipigia simu kuwa nifike hoteli hii akanitajia na chumba ambacho yupo, nilijua masikhara na kwavile Erick aliniambia pia chumba mlichofikia ndiomana nilikuja moja kwa moja na kuwagongea kwanza kisha ndio tukaenda kwenye kile chumba, jamani kwa macho yetu tumemshuhudia baba na Dora ila baba hajatuona maana alitoka bafuni kuoga, halafu Yule rafiki yako mshenzi sana yani ili kutuhakikishia kaenda kumbusu baba na kuanza kulambana nae midomo”
Erica akaelewa kuwa ndio ile surprise ambayo Dora alimwambia kuwa atamfanyia, kwakweli alizishangazwa sana na akili za Dora maana huwa anazijua mwenyewe, basi Tumaini alimtuliza kaka yake pale, ambapo Erick alikuwa akiongea kwa hasira,
“Baba, katuaibisha sana, yani kweli kabisa baba yetu wa kutembea na Dora! Si aibu hii! Hivi ni nani hamjui Dora alivyo jamani, kweli baba atembee na Dora loh!”
Tumaini akamwambia kaka yake,
“Sasa na wewe Erick una vituko loh! Ni kweli baba katudhalilisha kuwa na Dora, sasa baba anavyomng’ang’ania Erica je huoni kama hiyo ni zaidi ya kudhalilishwa? Yani mwanamke umtake wewe halafu baba nae amtake mmh ni hatari ujue”
Erick alinyamaza kwa maneno yale ya dada yake maana akifikiria anaona ni kweli, aibu ambayo baba yao kawaonyesha na kuwa na Dora ni zaidi ya aibu ile ya kutaka kuwa na Erica, ilibidi awe mpole na kuanza kupanga na ndugu yake pale.
Erica aliamua awe pembeni tu maana hakutaka kuingilia mipango ya ndugu asije onekana ana kiherehere bure, Tumaini akaanza kumwambia ndugu yake,
“Sasa Erick cha kufanya, mimi leo siondoki hapa ila nitamtumia ujumbe Dora kuwa akimalizana na baba yetu atuambie yani wakiwa wanataka kutoka ili twende ashuhudie kuwa tumejua”
“Eti eeeh Tumaini tufanye hivyo?”
“Ndio, ila kwanini tusingemshtua baba palepale?”
“Tusingefanya vizuri, sisi wanaume tupo tofauti na nyie wanawake yani pale baba tungemkata stimu ndiomana mimi nikaona aibu na kuondoka”
“Kwamaana hiyo wewe hata Erica akikufumania basi aondoke tu akuache uendelee na mamabo yako akihofia kukukata stimu?”
“Weee ushindwe na ulegee, Erica anifumanie kwa lipi? Erica hawezi kunifumania”
“Sababu utakuwa unajificha ukienda kumsaliti eeeh!”
“Hilo swala la mimi kumsaliti Erica halipo kabisa, yani siwezi kumsaliti sasa atanifumania vipi wakati kumsaliti siwezi”
Erica alijifanya kama hasikii vile ila hii kauli ya Erick ilimfanya kutabasamu sana maana alinihisi raha, Erick alimuangalia na kumuuliza,
“Erica mbona unacheka?”
“Hamna kitu, basi tu”
Erick akainuka na kusogea alipo Erica kisha akambusu na kumkumbatia, Tumaini akaguna na kusema,
“Mmmh mmeanza mahaba sasa, mnataka kunifukuza au?”
Erick akamwambia dada yake,
“Hatukufukuzi ila nakuonyesha dada yangu kuwa mapenzi ni kitu kizuri sana nan i matamu mno ukiwa na mtu mnapendana yani umpende akupende. Unajua kupendwa ni raha sana ila raha zaidi ni pale mkipendana. Dada ni wakati sasa na wewe kumpata shemeji jamani”
hili swala hata Erica alicheka maana toka amfahamu Tumaini hakuna hata siku moja aliyosikia kuwa Tumaini ana mpenzi au kuna mtu ana mahusiano nae ya kimapenzi.
Tumaini akawaangalia na kutabasamu kisha akasema,
“Haya nimesikia myasemayo na nimekubali ila jamani mahaba yenu subirini nitoke”
“Mmmh Tumaini hata kubusu tu tusubiri utoke kweli? Mbona wazungu huwa wanakiss hadharani”
“Ushasema wazungu, nyie waswahili msiniletee mambo ya baba na Dora mie. Ngoja nimtumie ujumbe Dora kabisa maana ndio tushapata mama mdogo”
“Maswala ya kumuita Dora mama mdogo siyataki”
“Kama hutaki basi mama mdogo atakuwa Erica”
Hapo Erick alikaa kimya kisha Tumaini akatuma ujumbe kwa Dora.
Ila muda ule Erica alimwambia Erick,
“Natamani ningepata chungwa, ila basi muda umeenda”
“Hapana bhana, naenda kukutafutia”
“Usihangaike Erick”
“Aaaah ni kazi yangu hii, nitakupa chochote unachohitaji ilimradi kipo kwenye himaya yangu”
Basi Erick alitoka na kuacha ndani amebaki Tumaini na Erica, walikaa tu kila mmoja akiendelea na simu yake yani hakuna aliyemuongelesha mwenzie hadi Erick aliporudi na machungwa, kisu na sahani akisema vile vyombo kavitoa mapokezi, Tumaini akasema,
“Mmmh kweli mahaba, hadi umeenda kuomba kisu na sahani ukatie machungwa!”
“Ndio, haya ni mahaba. Nampenda Erica, sitaki kuona apate shida wakati mimi nipo. Sasa nisingeenda kuomba kisu na sahani hayo machungwa tungekataje?”
Basi Erick alianza kumenya yale machungwa na kumpa Erica ayale ila kile kisu alisema kuwa atakirudisha akipata muda, basi Erica alikula chungwa moja wapo na kuridhika kisha akalala.

Nyumbani kwaina Rahim walipanga kuwa siku hii waende kwakina Zainabu na kweli jioni ya siku hiyo mrs.Peter alichukua na ndugu zake wawili pamoja na mshenga na kwenda kwakina Zainabu kwa lengo la kuzungumza na familia yake na kweli walikaribishwa vizuri kabisa na kuweza kuzungumza huku wakipanga mipango mbalimbali na kuonyesha nia ya kuwa kijana wao anataka kuoa pale.
Basi walipokuwa wanaaga wakati wanatoka walishangaa kumuona Salma amefika eneo lile kumbe aliulizia kwakina Zianabu hadi alifika ukizingatia jana yake alimsikia huyu mama akisema kuwa leo ataenda kwakina Zainabu.
Alikuwa amebeba mtoto wake ambaye bado alikuwa mdogo mgongoni, ma walipokuwa wanatoka tu akaenda kumuinamia mama mmoja aliyeonyeshwa kuwa ni mama yake Zainabu, wote wakamshangaa yani Mrs.Peter alitamani amtimue ila atamtimuaje kwa watu? Hakuweza kwakweli ila alichukia sana. Yule mama ambaye alikuwa ni mama yake Zainabu aliinama na kumuinua Salma aliyekuwa amelala kwenye miguu yake huku akilia, huyu mama alimuuliza
“Tatizo ni nini binti?”
“Huyo Rahim anayetaka kumuoa Zainabu alikuwa ni mume wangu, amenipa talaka baada ya kumuona Zainabu. Huyu mtoto niliyembeba mgongoni ni mtoto wetu, sasa Rahim na ndugu zake wananifukuza sina pa kwenda kwakweli na huyu mtoto na maisha haya naumia mimi. Sina raha jamani, nihurumie mama, naomba uwe kama mama yangu, mimi nilifiwa na mama sina mama kabisa na wote waliokuwepo wananikandamiza tu, nitaenda wapi na mtoto huyu? Nihurumie mama yangu”
Salma alikuwa anaongea kwa masononeko sana, yani kama mtu ambaye maisha yamemuonea sana mpaka ametia huruma kiasi kile, kwakweli mama Zainabu alimuhurumia sana Salma na kujikuta akiingia nae ndani kwake kuongea nae vizuri tena bila hata ya kuaga wale wageni, moja kwa moja wale wageni walijua hapo ni habari nyingine basi Mrs.Peter na wenzie wakaondoka.
Wakarudi nyumbani kwao tu kwa siku hiyo.
Salma hakuondoka hapo kwenye nyumba hiyo na alimueleza Yule mama matatizo mengi sana ambayo amewahi kufanyiwa na Rahim,
“Mama yangu, mimi sikujua laiti kama ningekuwa najua basi nisingekubali kuolewa na Rahim maana imekuwa ni mateso kwangu. Kwanza mimi nilitafutwa tu kuwa niolewe na kwavile mama wa kambo hapendi kuniona basi akanichagua mimi, nikaolewa na kuishi kwa mume wangu kwa adabu zote ila ndani ya nyumba nisithubutu kumuuliza kitu ni kipigo yani ananipiga hadi nachanganyikiwa, nishalazwa mara tatu kwa kipigo chake, halafu kweli ananiacha na mtoto mdogo hivi niende wapi mimi? Sijasoma mimi kusema labda nitatafuta kazi ya kufanya yani mimi sina mbele wala nyuma ila mtu ananifanyia hivi kweli na mtoto, ni haki hiyo?”
Mama Zainabu alizidi kumuonea huruma Salma na kumtaka siku hiyo alale hapo kwake halafu kesho yake aende nae kwa wakwe zake,
“Watakupokea mwanangu maana nitatafuta Sheikh akawaambie na maneno ya Mungu maana wanachokufanyia hakistahili kabisa kabisa”
Basi Salma alishukuru pale na siku hiyo alilala nyumbani kwakina Zainabu.
 
SEHEMU YA 411

Dora alifanya kama alivyoambiwa na Tumaini kwahiyo alipokuwa anataka kutoka na mzee Jimmy alimtumia ujumbe Tumaini kisha akafungua mlango na kutoka naye, pale nje alikuwepo Tumaini na Erick na kusema kwa pamoja,
“Baba!”
Mzee Jimmy aliona aibu sana na kuwaacha pale watoto wake kisha kuondoka zake, ambapo Dora nae aliondoka zake.
Kwakweli Tumaini na Erick walizidi kushangaa sana na muda huo Erick ndio akaamini vizuri zaidi kuwa mpaka alfajiri ile baba yao alikuwa amelala na Dora, basi baada ya hapo ndio Tumaini nae akaondoka zake kurudi kwao huku wakipanga kukutana kesho ili kumuhoji vizuri baba yao maana kukutana badae Erick alisema kuna kazi ambayo atafanya siku hiyo.
Tumaini akaondoka zake kisha Erick akarudi chumbani alipomuacha Erica na Angel, kisha alimsogelea na kumkumbatia na kumwambia,
“Usijali leo kukesha na Tumaini humu tulitaka kujua ukweli mke wangu”
“Hapana mimi sina tatizo, ila tulikuwa tunamkwaza Tumaini”
“Tunamkwaza nini? Ndio muda nay eye awe na mpenzi sasa, sie tunapendana na hilo tunawezaje kuficha? Yani mimi nikae bila kukukumbatia kidogo au kukubusu, nitajihisi vizuri kweli? Hapana Erica, muda wote natamani uwe karibu yangu mpenzi, wewe ndio furaha yangu hata katika kipindi kigumu kama hiki.”
“Asante sana Erick”
“Sasa, mimi nitaondoka hapa na kwenda kuangalia kule kwenye nyumba halafu nitakuja kuwachukua”
“Mmmh kwanini tusiende wote?”
“Hapana Erica, naomba upumzike nikarekebishe nitakuja kuwachukua hakuna shida”
Erick alioga na kujiandaa kisha akamuaga Erica kwa kumbusu na kwenda kule akafatilie usafi wa ile nyumba waliyoipanga.
Baada ya Erick kutoka tu Erica aliamka na kuoga kisha kulala tena sababu usiku hakulala vizuri kwani Tumaini na Erick walikuwa na mipango mingi kwahiyo walikuwa wanaongea ongea na kufanya usiku ule uwe kama wa mkesha, alilala usingizi mzito sana.
Gafla alisikia mtu akigonga mlango wao ule, alihisi huenda ni muhudumu wa ile hoteli au Erick karudi, aliinuka na usingizi usingizi wake na kwenda kufungua mlango, mara aliyekuwa anagonga akaingia mzima mzima ndani, Erica alifikicha macho na kumuangalia vizuri, alikuwa ni James, Erica alishangaa sana na kusema kwa mshangao,
“James”
“Ndio ni mimi Erica, nina kuhitaji sana. Nina kiu na penzi lako Erica, nimekufatilia sana yani huwezi amini toka muda ule tumeonana nilikuwa nakufatilia na leo nililala kwenye hii hotel na kwa bahati nzuri nilichungulia muda Yule jamaa yako akitoka ndiomana nimeamua kuja. Nakuhitaji Erica, nakupenda sana. Nilifanya makosa kumuoa dada yako, hata sikumpenda ni wewe nikupendae”
Muda huu Erica alikuwa mbali kabisa na James kwani alihisi kuwa huyu James hana nia njema na yeye, James akaanza sasa kumsogelea Erica yani kile kitendo kilimfanya Erica ashikwe na hofu huku akisema,
“Ondoka James”
Kwani James hata alisikia lile swala la ondoka, hakusikiliza kwakweli kwani muda ule ule alimvamia Erica na kutaka kumbaka huku akisema,
“Siku zote unaninyima na leo nitakubaka tu”
Ubaya wa ile hoteli, hata mtu apige kelele chumbani basi chumba cha pili haitasikika ile sauti maana Erica alianza kupiga kelele hata Angel aliamka na kuanza kulia, ila James hakujali kabisa zile kelele maana alimsukumia Erica kitandani na kuchana ile nguo aliyoivaa Erica ambapo Erica alipiga kelele na kujitahidi kumtoa James mwilini mwake ila alishindwa kwani James alikuwa na nguvu kuliko yeye, ila Angel alipoona kama mama yake anakandamizwa aliinuka na kuchukua kile kisu ambacho Erick alikiacha jana yake akajikuta akimpiga nacho James, kwahiyo James alijikuta akiruka pembeni kabla hata ya kumuingilia Erica, wakati James anajishangaa Erica alimchukua mwanae na kukimbilia bafuni ambako wakajifungia sasa.
James alikuwa akishangaa bado kuwa ni kitu gani cha ncha alichochomwa nacho, kuangalia nyuma yake akaona damu kwahiyo aliumia mgongoni, na alipoangalia pembeni akaona kisu kwakweli alishangaa sana,
“Yani kile kitoto ndio kimenichoma na kisu? Kile kitoto nilichokifanyia birthday ndio kimenichoma na kisu!!”
Akasogea kwenye mlango wa bafu na kumwambia Erica,
“Jifungia huko salama ila roho yako mbaya na mwanao nae umemrandisha roho mbaya, mtoto mdogo huyo na anajua kuua, nyie ni wabaya sana ila huu ni mwanzo tu”
Kisha akaondoka ila Erica alishindwa kutoka mule bafuni kabisa kwa kuhofia kuwa huenda bado yupo.

Mama Zainabu aliongozana sasa na Salma pamoja na Sheikh aliyemchukua kwenda nae nyumbani kwakina Rahim pamoja na wababa wengine wawili ambao pia ni watu wa dini, na walifika na kumkuta mama yake Rahim ambapo baada ya salamu wakaanza nae kikao, kisha akaenda kuitwa Rahim ili wazungumze nae, alipofika tu alichukia sana kuona kuna watu wameenda kumleta Salma, aliwasalimia na kukaa kisha mama yake akamtambulisha kwa watu wale kama yeye alivyotambulishwa ila alivyomaliza utambulisho tu yani kabla wale watu hawajaanza kuongea alifoka Rahim,
“Huu ni ujinga, mwanamke ananisumbua na wote mnatambua hili halafu bila aibu mnaniletea viongozi wa dini sijui wazungumze nami, niongee nao nini? Huu ni ujinga, siwezi kupewa mawaidha nisikilize wakati kuna mwanamke nisiyemtaka, mngekuja hapa na Zainabu sawa ila kwa huyu mwanamke niwasikilize siwezi”
Rahim akainuka na kutoka, mama yake alijaribu kumita ila Rahim hakuitikia na kuondoka zake.
Yani mama yake pale aliona aibu sana, ikawa hakuna namna waongee tu na huyu mama maana toka mwanzo alikiri wazi kuwa alimpenda Salma alivyoambiwa kuwa kachaguliwa kwaajili ya mwanae,
“Sasa kama ulimpenda hutakiwi kumchukia kwasasa, kama ana mapungufu ni kumrekebisha tu”
“Jamani, mimi mwenyewe sikujua kama huyu Salma ni msumbufu hadi jana alivyovunja vitu hapa kwangu na kufanya fujo”
Salma alijitetea kuwa ile ilikuwa ni hasira tu maana hata kwao hawamtaki sababu ana mtoto, kwamaana hiyo wakamwambia Mrs.Peter kuwa aishi tu na Salma walee Yule mtoto kama Rahim atajirudi basi ataishi na mke wake, na asipojirudi basi talaka itaendelea ila kwa kipindi hicho wakae nae tu walee mtoto. Mrs.Peter hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali tu kumlea Salma pamoja na mjukuu wake.

Erick alirudi pale hotelini jioni, na kuingia mule chumbani akashangaa kuona damu na kisu chini, alihisi kuchanganyikiwa kwakweli na kuita kwa uoga,
“Erica, Angel”
Erica aliitika akiwa bafuni ila kwavile ni sauti ya Erick alifungua mlango na kutoka, alimkimbilia na kumkumbatia huku akilia, Erick alimuuliza kuwa tatizo ni nini, basi Erica alianza kumsimulia ilivyokuwa yani Erick alijilaumu sana kwa kutokuondoka muda ule na Erica,
“Hivi kwanini mbwa mwitu kama hao wanakunyemelea sana mke wangu jamani! Kwani tatizo nini dah!”
Basi akapiga simu mapokezi ili waje kusafisha pale na kuchukua kisu, aliendelea kusema
“Yani baya lingekukuta leo sijui ningejionaje jamani, ningejiona sina thamani kabisa. Asante sana kwa mwanangu Angel, mtoto ana akili huyu kama mamake, nitakutafutia zawadi kubwa mwanangu. Tujiandae sasa tuondoke.”
Ila alimuhurumia Erica kuwa alijifungia bafuni bila kula chochote kwahiyo alikuwa anamwambia wale kwanza ndio waondoke ila Erica alikazana kuwa waondoke na wakale huko huko, Erick alielewa kuwa mahali hapo pameshamkera Erica hivyobasi wakajiandaa pale na kuondoka huku wakimuacha Yule wa mapokezi akifanya usafi, pale hawakumuhoji sana Erick sababu ni mteja wao mkubwa sana kwenye ile hoteli.
 
SEHEMU YA 412

Waliondoka na kwenda hadi kwenye nyumba ambayo Erick aliitafuta, kwa muda huo nyumba ile ilikuwa imefanyiwa usafi wote na ilikuwa imeshawekwa kila kitu kumbe Erick alivyoondoka ile asubuhi alienda kununua vitu vya kuweka ndani kwahiyo Erica aliipenda zaidi ile nyumba maana ilikuwa na muonekano wa kuvutia kutokana na vitu vilivyowekwa ndani.
Kwa muda huo Erick aliagiza chakula tu na kilipofika walianza kula.
Walipomaliza kula, Erick alikuwa amechoka sana hivyo akaamua kuoga na kulala maana siku hiyo alikuwa na kazi nyingi sana, kwahiyo kwa mara ya kwanza aliingia chumbani kwenye nyumba kwa lengo la kulala maana hawakuwahi kuishi hapo, Erica nae aliingia chumbani maana Angel alidai anataka kulala pia kwahiyo Erick na Angel walikuwa fofofo.
Wakati Erica amekaa tu simu yake ilianza kuita na alipoangalia mpigaji aliona kuwa ni Dora, aliamua kutoka sebleni na kuongea na simu ile.
“Eeeh niambie Dora”
“Samahani Erica, hivi babake mzazi Angel anaitwa nani?”
“Mmmh anaitwa Rahim, kwanini umemuulizia?”
“Anafananaje?”
“Sijui nikuelezeje, ila ingia facebook andika Rahim Shombeshombe utamuona, kwani vipi wewe?”
“Leo bhana katika pitapita zangu, nimekutana na huyo mtu anaitwa Rahim ni anakunywa pombe huyo balaa, ila nilipomuangalia nimemuona anaufanano kidogo na Angel.”
“Nasikia lakini anakunywaga, inawezekana akawa ni yeye”
“Unampenda?”
“Mmmh swali gani hilo Dora? Ninayempenda mimi ni Erick pekee sio huyo Rahim”
“Kama humpendi mbona ulizaa nae?”
“Dora, unajua mahusiano yalivyo, kipindi tupo kwenye mahusiano ilishapita hiyo hali ila kwasasa ni Erick tu ndio yupo kwenye moyo wangu”
“Na kwanini Rahim hakukuoa?”
“Aaaah Dora jamani loh! Hakuweza kunioa sababu alisema sifai kuolewa nae”
“Mmmh ila mzuri huyo, huwa napenda kweli wakaka shombeshombe jamani sema sijawahi kuwa na bahati nao”
“Hebu acha zako Dora, yani kwako kila mtu mzuri loh!”
“Ndio mzuri, anavutia ila hajamzidi Erick wako yani huyo Erick asingekuwa shemeji ungekuta nishamshawishi ila ni shemeji namuheshimu sana halafu mgumu huyo maana hata Sia aligonga mwamba na vidawa vyake. Sema Erick mzuri huyo, shoga yangu unafaidi wewe”
Erick alitoka chumbani na kufanya Erica aikate ile simu, Erick alimsogelea Erica
“Mbona umekuja kukaa mwenyewe mpenzi jamani! Yani umeacha sisi tutale wenyewe kweli!”
“Aaaah mmmh aaah”
Hakuwa na maelezo ya kujieleza, basi Erick akamshika mkono na kwenda nae chumbani na kumwambia akae tu hata kama halali ila akae nao karibu, kwahiyo kwa muda huo ilibidi Erica nae aanze kutafuta usingizi tu.

Mage alipoona mdogo wake hajarudi nyumbani hadi siku hiyo ilibidi amwambie mama yao kuwa yeye anaondoka zake,
“Mama, inaonekana mwanao kashajiozesha. Kwakweli mimi naondoka zangu akija mtaniambia”
Ila Bite akatoa wazo,
“Hivi kwanini tusimpigie simu huyo Erica?”
“Hakuna kumpigia simu wala nini, muacheni hivyo hivyo, si kaamua bhana. Mwacheni tu”
Basi wakakubaliana na lile swala la kutokumpigia simu wala nini maana amewadhalilisha sasa, muda ule walipigiwa simu na Tonny na aliwaeleza kuwa amepata mchumba anataka akamtambulishe.
“Usituletee tena yale mauza uza yako ya Dora”
“Hamna mama, safari hii nimepata mwanamke msomi na mwenye kazi yake inayoeleweka”
“Kwani Dora hakuwa msomi?”
“Alikuwa msomi ila sio kama huyo wa sasa, maana ni mwanamke haswaa nimempata”
“Haya, tunayasubiri hayo mauzauza yako utakayotuletea”
Aliwaahidi kuwa mwisho wa wiki ataenda kumpeleka mchumba wake nyumbani kwao wamfahamu.
Kwa muda ule walianza kujadili habari za Tonny na kuacha habari za Erica kwa muda.

Rahim alikuwa amechukizwa sana na kitendo cha kupelekewa viongozi wa dini,kwahiyo kwa hasira alizokuwa nazo alienda kunywa sana pombe na alikunywa siku hiyo kupita siku zote akajikuta anaanza kutongoza tongoza wanawake hovyo yani siku hiyo hadi wahudumu aliwaona kuwa ni wanawake waliovutia na alikuwa anaenda na mwanamke ndani na akitoka nae bado hajaridhika anachukua mwanamke mwingine, mpaka muda huo alikutana na Dora ambapo Dora aliamua kumpetipeti sasa.
Rahim akampata Dora na kwenda nae chumbani, Dora alimwambia
“Najua umelewa ila mimi sio malaya kama wale uliokuwa unawachukua zamu zamu, mimi ni mwanamke na heshima zangu. Nimekuhurumia na hayo unayoyafanya sio sawa kwakweli, mimi ni rafiki wa Erica”
“Ooooh Erica mrembo wangu yuko wapi?”
“Yuko wapi nini? Erica yupo na Erick kwasasa na wanapendana sana, yani wewe baba mzima unaanza kuhangaika na wanawake badala uwaze maisha ya badae ya watoto wako”
“Halafu wanwake kama nyie ndio huwa mnabakwa, sasa maisha yangu yatakusaidia nini?”
“Mimi sio wa kubakwa ila ni swala la kuelewana tu, mtu gani usiyejali familia yako wewe. Hivi unafikiri wanawake uliozaa nao wakisikia habari yako ya kubadilisha machangudoa huku watakufikiriaje?”
Rahim hakupenda maneno ya Dora, na ili kumuonyesha kuwa yeye ni mwanaume aliamua kumbaka Dora ila alishangaa mwanamke huyu amembaka ila amempa ushirikiano wa kutosha kabisa na alipomaliza nae alilala usingizi mzito sana ambapo Dora nae alilala.
Kulipokucha, Rahim aliona kabisa kuwa alichokifanya hakikuwa sawa na alifanya sababu alikuwa amelewa, alimwambia Dora wasahau tu kilichotokea,
“Sawa hakuna shida, ila swali langu ni kuwa wanawake wote wale hutumiagi kinga kweli?”
“Aaah wewe nae sijui umetumwa”
Rahim aliinuka na kujiandaa kisha kuondoka zake, Dora nae alijiandaa na kuondoka zake ila ilikuwa furaha sana kwake kuweza kulala na huyo makaka mshombeshombe.
 
SEHEMU YA 413

Erick alienda nyumbani kwao kama alivyopanga, na alienda mapema sana ili aweze kumkuta baba yao na wamuhoji kwa yale aliyokuwa ameyatenda.
Alifika na kumkuta Tumaini, akamsalimia na kumuuliza,
“Baba kashatoka?”
“Hamna bado yupo ndani, sijui ndio presha zimempanda”
“Asitutanie sie, presha baada ya kufanya maovu. Hebu twende tukaongee nae”
Erick aliongozana na Tumaini na kwenda kumgongea mlango baba yao ambapo aliwakaribisha na kudai kuwa anajisikia vibaya, Erick alielewa wazi kuwa baba yake kafanya vile sababu anaogopa kuulizwa na watoto wake, ila pale pale Erick aliamua kuongea,
“Baba, licha ya kuumwa ila umetudhalilisha sana watoto wako”
“Naumwa jamani, hivi nyie watoto hamuelewi?”
Ila Erick akawaza jambo kuwa pengine baba yao alifanyiwa dawa na Dora huku akikumbuka zile dawa ambazo alizompeleka Sia ili amletee yeye na jinsi alivyoanguka kwakina Erica na kuangusha dawa kwahiyo alihisi huenda baba yake karogwa na Dora. Basi akaamua kumshauri,
“Baba, naomba nikushauri kitu”
“Kitu gani? Ila kumbuka naumwa”
“Sawa unaumwa baba yangu ila naomba twende kwenye maombi, maana labda wamekutupia mavitu mabaya”
Sababu mzee Jimmy alikuwa akiona aibu kwa watoto wake, aliamua kukubaliana na Erick kwenda huko kwenye maombi huku na yeye akikubali kuwa huenda amerogwa.
Basi akajiandaa na kuondoka pale akiongozana na Erick pamoja na Tumaini kuelekea kwa mwanamaombi.
Walifika na Erick kugonga mlango wa Yule mama, wakati Yule mama anatoka nje, mzee Jimmy alionekana kumshangaa sana na kumuita kwa mshangao,
“Ester!! Ni wewe”
Yule mwanamaombi nae alionekana kumuangalia mzee Jimmy kama mtu anayemfahamu, hata Erick alishangaa kuona wanafahamiana wale watu


Walifika na Erick kugonga mlango wa Yule mama, wakati Yule mama anatoka nje, mzee Jimmy alionekana kumshangaa sana na kumuita kwa mshangao,
“Ester!! Ni wewe”
Yule mwanamaombi nae alionekana kumuangalia mzee Jimmy kama mtu anayemfahamu, hata Erick alishangaa kuona wanafahamiana wale watu.
Mzee Jimmy bado nay eye alikuwa na mshangao wa kumuona Ester inaonyesha hakutarajia kumuona tena katika maisha yake, kwahiyo kitendo cha kumuona kilimshangaza sana.
Alimsogelea karibu na kumwambia,
“Ester upo?”
“Nipo Jimmy, za siku?”
“Nzuri tu, ni muda mrefu umepita ila bado unapendeza tu”
“Utukufu kwa Mungu”
Ndio hapa mzee Jimmy alipogundua kuwa kweli Ester ulokole umemkaa, akawaangalia wanae na kuwaambia,
“Huyu ndio Yule mwanamke ambaye habari zake niliwagusia kidogo tu, ndio huyu mwanamke wa kilokole, kipindi hiko alikuwa binti na nilimpenda sana ila alinipa masharti mengi na kushindwa kuwa nae”
Erick na Tumaini walitamani wajue kiundani kabisa ila hawakuweza kumdadisi baba yao pale, na kabla hata Erick hajamueleza Yule mwanamaombi matatizo ya baba yao Yule baba aliwaambia wakamsubiri kwenye gari aongee nae mwenyewe.
Waliguna tu na kwenda kwenye gari kumngoja.

Baada ya muda baba yao alirudi na kuwataka warudi nyumbani, hawakujua ni kwanini baba yao kawaambia vile ila walikubali na kurudi nae nyumbani.
Ambapo waliingia ndani na kukaa nae sebleni kisha akaanza kuongea sana,
“Yule mwanamke anajua vitu vingi sana, yani anaonekana kufahamu vitu vingi sana na mimi sijaoa hadi leo sababu yake yani kila mwanamke namuona hafanani na yeye”
Erick alimuuliza baba yake,
“Kwani imekuwaje? Na yeye ulimfahamu vipi?”
“Ngojea niwaeleze kwa kifupi huenda mkafahamu kinachonitatiza baba yenu. Miaka ya nyuma huko wakati nimekua zangu na akili timamu, nikawa nisimamia mashamba ya babu yangu yani babu yangu alikuwa ana mashamba mengi sana ya kahawa kwahiyo nilikuwa nasimamia, kipindi hiko nilianza kunywa pombe na kuvuta sigara tena nilikuwa mpenzi mzuri wa mpira yani mpira mpira na mimi, na pia nilipenda sana kusikiliza mziki yani nikikaa shambani basi utanikuta na redio yangu pembeni nakula mziki taratibu tu. Sasa huyu Ester alikuwa ni mmoja wa vibarua kwenye shamba la babu, nilimpenda kwakweli na kama hela nilikuwa nayo, ila mwanamke huyu alikuwa wa ajabu sana machoni pangu, hela anayotaka nimpe ni ile aliyofanyia kazi tu na si vinginevyo yani Yule mwanamke hapendi hela jamani ndiomana haendelei hata huku mjini itakuwa kaja na mbio za Mwenge maana kama mtu hupendi hela basi mjini umekuja kwa mguu, ndio Yule na ndiomana maisha yake ni ya kawaida sana, ila alikuwa ni mzuri kweli, natumai mnanielewa, ni mtu mzima sasa ila uzuri wake bado haupotei, ni mzuri wa sura na umbo. Nilimpenda sana, nilimuhitaji sana, nilisema akinikubali tu naoa ila haikuwa hivyo. Baada ya kumfatilia sana nikajua ni mlokole, kuna jamaa akaniambia kumpata binti mlokole ni kujifanya na mimi ni mlokole pia, basi nikaanza kwenda kanisani na kuhudhuria mafundisho yote ya dini, nilianza kuwa vizuri kwakweli ila pombe, sigara, mpira na mziki ni vitu ambavyo sikupanga kuviacha kabisa. Basi nilivyokuwa vizuri nikawa namfata Ester na ananiambia maneno ya dini tu, nikamwambia mimi nimeokoka sababu yako, nahitaji uwe mke wangu, akanipa masharti magumu huyo kuwa niache pombe, sigara, mpira na mziki, nikamuuliza jamani hata mpira una tatizo gani? Akaniambia anataka mume ambaye atatangaza nae kazi ya Mungu ila mume mwenye upenzi na kitu kingine atashindwa kufanya nae kazi ya Mungu, jamani ilikuwa ngumu sana kwangu nilijitahidi vyote ila pombe na sigara sasa ukawa mtihani mkubwa, akaniambia yani bora hata ingebaki mpira kuliko pombe na sigara, nikajitahidi nikionana nae sivuti sigara wala sinywi pombe, nikamuomba jambo moja kuwa walau aniachie mpira, akubali basi nikafanya mipango ya kujitambulisha kwao na kutoa posa, kiukweli sikuwa na nia ya kumchezea nilitaka kumuoa, tulienda kwao kujitambulisha kila kitu na wakatuambia tupeleke mahari, ambapo ilikuwa ng’ombe jike watatu na dume moja, halikuwa tatizo kwangu maana kwetu tulikuwa na uwezo wa kutosha tu, tulipanga iwe haraka sana.
Siku hiyo bhana ambapo kesho yake ilikuwa ndio siku ya kupeleka posa, yani sijui Ester alitokea wapi muda huo uwiii akanikuta mahali shambani navuta sigara, yani huwezi amini ni pale pale alikataa mahari yangu na kesho yake tulirudishiwa posa yetu. Roho iliniuma sana ten asana, sijawahi kupata furaha hadi leo nimejikuta nachukia sana sigara maana ndio imesababisha nimkose Ester. Baada ya hapo sikuweza tena kukaa pale kijijini, nilimwambia babu anipe changu na kuja kufanya maisha mjini, basi kila mwanamke niliyemuona nilitamani tu kumpitia na sio kumuoa. Ninachojutia ni kushindwa kuomba msamaha kwa Ester pengine ningemuomba msamaha na kuahidi kubadilika angenielewa ila sikuwa na wazo la kuomba msamaha kabisa kwani nilisikiliza jamaa zangu waliniambia mwanamke anayekupangia pangia mambo ya kufanya si mzuri kuoa, na kule kwetu ilikuwa kumuomba msamaha mwanamke ni kujidhalilisha”
“Kheee baba, pole sana. Pengine Yule Ester ndio angekuwa mama yetu sasa”
“Ni kweli Tumaini ila Yule Ester hawezi tena kunikubali kwasasa, anasema ishapita tayari, niende kwake kufanyiwa maombi tu lakini sio kumuoa. Ndiomana nimeondoka kwa hasira. Ila kuna jambo naomba mnkisaidie wanangu”
“Jambo gani hilo baba?”
“Nimewapa hiyo story kwasababu maalumu kabisa mjue kwanini namng’ang’ania Erica, mwanamke niliyempenda maishani ndio huyo Ester na hakunitaka labda ningetumia nguvu ningempata. Sasa cha kunisaidia ni kimoja, baba yenu nahitaji mwenzangu, nahitaji mke nimechoka kuwa mpweke na katika wake hao kuna watu wawili tu hadi sasa kwenye kichwa changu, kuna Ester na Erica”
Hapo Erick alishtuka kidogo maana huwa hapendi kabisa baba yake kumng’ang’ania Erica, ila alitulia na kumuuliza,
“Sasa baba tukusaidie nini hapo?”
“Mnisaidie kumpata Ester nimuoe ili niache kusumbua kuhusu Erica, naomba mnisaidie nimuoe Ester ila nikimkosa huyu Ester kwa hakika hata wewe Erick hutoweza kumuoa huyo Erica, nampenda sana na nishagharamia hela zangu nyingi kwake. Kwaherini”
Muda huu mzee Jimmy aliinuka na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 414

Tony akawaza kumpeleka mchumba wake mpya nyumbani kwao ila asipate vikwazo kama alivyopata wakati anaenda kumtambulisha Dora, akakumbuka kuwa mdogo wake Erica ndio alimletea hivyo vikwazo yani ndio alikuwa kikwazo cha yeye kutokuwa na Dora pia akakumbuka kuwa vikwazo vya mdogo wake havikuwa vya wivu ila alikuwa akimuokoa kaka yake kutoka kwa mwanamke asiyefaa ambaye alikuwa Dora, kwamaana hiyo aliona Erica ni mdogo wake ila ana maono ya mbali zaidi kwahiyo aliamua mchumba wake mpya kabla ya kwenda kumtambulisha kwao basi amtambulishe kwanza kwa mdogo wake yaani Erica amuone kwanza kabla hajampeleka kwa wengine wamfahamu, halafu Tony hakujua kuwa ndugu yake kuna madudu kashafanya nyumbani kwao na kutoroka. Hivyobasi akampigia simu bila kujua chochote kile kinahoendelea kwa Erica,
“Hellow Erica, upo nyumbani?”
“Hapana, kwani kuna tatizo gani?”
“Hakuna tatizo mdogo wangu,ila kakako nimepata mchumba ambaye badae nataka aje kuwa mke wangu. Naomba nikufahamishe kwanza wewe umuone”
“Kheee jamani Tony, kwahiyo unataka nimuone mimi kwanza?”
“Ndio nataka wewe umuone kwanza, maneno yako ya mwanzo kunikataza nisimuoe Dora bado yananiingia akilini, najua mdogo wangu utakachochagua kitakuwa kizuri machoni pa wengine, si unaona mwanaume uliyechagua kuzaa nae! Hahaha umechagua haswaa ili uzae mrembo”
Erica alicheka tu ila alijua ni kwajinsi gani kakake hajui kinachomchukiza Erica kwa huyo mwanaume aliyezaa naye. Kisha Erica akamwambia kaka yake,
“Sasa mfano simpendi tu huyo mchumba wako kwasababu zangu binafsi itakuwaje?”
“Erica, kwasasa wewe ndio sijui nisemeje yani wewe ndio kama mchaguzi wangu mkuu. Nyumbani nimewaambia kuwa nitapeleka mchumba wamtambue ila nataka umtambue kwanza wewe, na kama humtaki au hanifai niambie kabisa, kwa hakika sitamuoa, nakumbuka ushauri wako uliopita kwa Dora na umeniokoa na vingi sana mdogo wangu, hivyo nakuomba nikuletee huyo mchumba wangu umfahamu na unipe viwango kama anafaa au hafai”
“Sawa kaka yangu hakuna shida, sasa utakuja nae moja kwa moja nyumbani?”
“Hapana, nataka tukutane mahali, labda hotelini hivi umfahamu”
“Sawa, hakuna shida kaka yangu. Basi utaniambia”
“Sawa hakuna shida”
Basi wakaagana pale ila Erica alielewa kuwa kakake hajui kuwa yeye hayupo nyumbani kwao.

Erick aliona babake kamuachia mzigo mkubwa sana yani hakuhisi kama mzigo huo watauweza na Tumaini, akamwambia dada yake
“Hivi huyu mzee yupo serious au ni nini jamani?”
“Hata mimi namshangaa”
“Mwanamke aliyemfuma kwa sigara tu na kumuacha atamkubali sasa akimfuma na wakina Dora?”
“Hapo sasa, huyu mzee anatubabaisha tu. Mke wake Dora”
“Aaaah acha maneno yako hayo”
“Sasa Erick, mi nilikwambia toka mwanzo kumshinda baba dhidi ya Erica ni sisi kuwa kitu kimoja. Baba katupa mtihani ambao hata yeye alifeli miaka ya nyuma huko, alikamwatwa na sigara tu na Yule mama hakutaka kuolewa nae, je baba wa sasa hivi anayekazana kuwataka wakina Erica yani watu wenye umri sawa na watoto wake, sijui wakina Dora unadhani Yule mama atamkubali? Yule mama sio mjinga kiasi hicho, yani hawezi kumkubali baba yetu hata iweje, kwahiyo tunatakiwa kujiandaa kisaikolojia kuwa baba lazima ataendelea kumtaka Erica tu, cha msingi tushirikiane tumwambie baba amuoe Dora tu, na zile habari zake tukitaka kumuuliza kuhusu Dora anajifanya presha imepanda ziishe, tuwe na ushirikiano yani ni Dora tu ndio anamuweza baba, akigoma tumlete Dora hapa nyumbani”
“Unajua mara nyingine unaongea kama si wewe uliyekuwa unamchukia Erica!”
“Hayo yalishapita Erick, tufikirire mapya tu kwasasa”
Basi Erick alipotaka kurudi kwake, Tumaini alimwambia kuwa ampeleke kwake ili apafahamu. Erick hakuona kama ni tatizo hilo na kuamua kwenda nae siku hiyo.
Kiukweli walifika na alipapenda pia na kuona mdogo wake kaanza mambo ya maendeleo na kumsifia kuwa amefanya jambo jema sana kuamua kuanza maisha na Erica, ila bado Tumaini alikuwa hayupo karibu na Erica kama zamani kuwa wanaongea, wanacheka na kufurahi yani alionekana kuwa kimya tu anapobaki mwenyewe na Erica, na muda kidogo aliaga na kurudi kwao.

Kesho yake Rahim akiwa kwao ilibidi mamake amseme sana maana ilikuwa ni aibu aliyoifanya majuzi mbele za wageni,
“Na Salma kaachwa hapa, wametusema na nimejitahidi kuelewa walichotusema. Mwanangu hakuna namna inabidi tu uendelee kuishi na Salma kama mke wako”
“Aaaah mama, huyu Salma simuhitaji kabisa, ninayemuhitaji mimi ni Zainabu”
“Sasa mwanangu wazazi wa Zainabu wamegoma sababu umemfukuza mkeo labda Salma aendelee kuwa mke wako na tukawaombe kuwa Zainabu awe mke wa pili”
“Huyo Salma atakubali?”
“Atakubali ndio, niliongea nae, nimemsema sana na amesikia atakubali tu. Dini inaruhusu wewe kuoa wawili, kuliko kumuacha atangetange ni bora uwe na wake wawili, na hakika utaweza kuwatunza.”
“Je Zainabu atakubali kuwa mke wa pili kwangu?”
“Uzuri wa Yule binti ameishika dini vizuri kwahiyo anaelewa sunah ya kuolewa wake wawili, hawezi kukataa maana na mimi nitaenda na masheikh kuzungumza nae, hata hivyo binti umri umeenda Yule, miaka thelethini na tatu unafikiri hatamani ndoa yule? Anatamani sana sema mambo ya dini yamemfunga, pale anatamani nay eye angekuwa na mume wake, angekuwa na watoto wake, anatamani sana na umri ushamtupa mkono anakaaje kwa mfano? Atakubali tu niachie mimi hilo swala”
“Sawa mama, hakuna tatizo kama ndio hivyo niko tayari kuishi na Salma maana nitamuoa na Zainabu pia”
Basi mama yake alikubali na wakati huo huo alijipanga kwenda kwenye familia ya wakina Zainabu ili aongee nao.
Na hakuchukua muda, alienda kuongea kwanza na wale Masheikh kisha kwenda tena kwenye familia ya Zainabu na Zainabu mwenyewe akasema kabla ya posa anahitaji kuongea kwanza na muhusika, kwahiyo mamake aliona mambo yameenda vizuri kabisa kama walivyopanga.

Kwa upande wa ndugu wa Bahati, walijikuta wakijilaumu tu kwani mambo aliyokuwa akiyafanya Bahati kwa kipindi hiko hayakuwa mambo ya kawaida kabisa, ilibidi ndugu zake wamuite tena wakae nae na wazungumze nae. Mama yake aliongea kwa uchungu sana,
“Bahati mwanangu, kweli umefikia hatua ya kumbaka mama mkwe wako kweli? Yule si sawa na mimi mama yako jamani!”
“Mama, kuna mambo huwa nayatenda hata mimi mwenyewe najishangaa na sipendi kuyatenda kabisa, Yule mama nilisema kwenye kikao siku ile kuwa sirudi kwangu sababu Yule mama mkwe namtamani, ila wakaja watu kunibembeleza kuwa nirudi kwangu. Nimejaribu kujizuia ila nimeshindwa na kujikuta nimembaka”
“Na ulivyo na mbegu kali mwanangu, mama wa watu ni mtu mzima ila kaanza kujihisi vibaya kama mjamzito, Bahati mwanangu kwanini umekuwa hivyo?”
Dada yake aliamua kumtetea kidogo,
“Mama, tutamlaumu sana Bahati ila na sisi pia tuna makosa tena makosa makubwa sana, hivi kwa mfano tungemuacha Bahati aoe mwanamke anayemtaka kungekuwa na tatizo hapa? Hivi Bahati angeishi na Yule mwanamke haya yaliyotokea yangetokea? Ila tulitumia hasira sana na hata kushiriki kutafuta dawa za kumfanya Bahati amsahau Yule mwanamke, na tulifanya vile sababu hatukumtaka Yule mwanamke. Ila mama kumbuka aliyetushauri kufanya hivi ni Yule babake Nasma kwanza ndio alikuwa mshenga wa Bahati, nasikia Yule baba sio mtu mzuri kumbe ni mchawi balaa, mtaa mzima wanamfahamu. Ila dawa za kumchanganya Bahati za mwanzo tumeshiriki wenyewe yani tusikatae kuhusu hilo, yani na sisi ni sehemu kubwa sana ya kuharibu maisha ya Bahati hata kafikia hiyo hali ya kumbaka mama mkwe wake. Hatukujua kuwa dawa tunazofanya tunajenga kitu kibaya kwa bahati maana hajampenda mke wake kwa mapenzi, siku zote watu wanaimba na kusema kuwa mapenzi ya dawa hayadumu na tunalijua hilo je tulihisi Bahati angedumu kwa Nasma? Yani mapenzi ya dawa huwa hayadumu unashangaa tu siku mambo yamebumbuluka kila kitu hadharani na ndio kilichotokea, nasikia Bahati baada ya kumuona Yule ampendaye dawa ziliruka na kupotea pia, alijikuta akaanza kumfatilia tena hiyo ni kwa mujibu wa Nasma na ndipo alipoamua kumfanyia dawa nyingine ili ampende kwa bahati mbaya ile dawa alikosea kidogo maana dawa zingine Bahati hakuzitumia ndio hivyo Bahati kawa kama Jogoo, maana hiyo dawa aliyofanyiwa ni anakuwa kama Jogoo, si unajua Jogoo anabaka kila anayemuona, kwahiyo usishangae kukuta Bahati anatutamani hadi sisis, hapa tufanye kitu jamani tusibaki kumlaumu Bahati tu au kulaumiana”
Bahati alikuwa kimya kabisa ila hata yeye alihisi kuwa hayupo sawa maana mambo aliyokuwa nayafanya hayakuwa ya kawaida, mama Bahati alipumua kidogo na kuanza kujadili na wanae cha kufanya,
“Sasa tufanyeje maana hii hali inatakiwa tuifanyie tiba mapema kabla huyu Bahati hajafungwa kwa makosa ya kubaka maana anapoelekea pabaya jamani, ila wanawake loh yani kale kaNasma kumfanya mwanangu awe kama Jogoo jamani loh!”
Dada mkubwa wa Bahati akashauri,
“Sababu ile dawa ya kwanza iliisha nguvu baada ya kumuona Erica, basi tumpeleke kwa mtaalamu Yule tuchukue dawa atumie halafu twendeni kwakina Erica amuone na awe huru”
“Sawa sawa, tusipoteze muda basi, le oleo atumie dawa za Yule mtaalamu halafu kesho twendeni kwakina Erica ili tuonane nae”
Wakakubaliana na muda huo wakaondoka na Bahati kwenda kwanza kwa mtaalamu ambaye walienda akawapa dawa ila hazikumsaidia kwahiyo wakaenda tena ili wachukue hizo dawa na kesho yake waende kwakina Erica pengine yale madudu yamtoke kabisa Bahati.
 
SEHEMU YA 415

Usiku ulipofika Erick aliamua kumueleza Erica kuhusu baba yake kufahamiana na Yule mwanamaombi, kwakweli alishangaa sana.
“Unajua katika maisha kuna mambo huwa yanatokea unajiuliza kwanini yametokea, mara ya kwanza wakati nakutana na Yule mama na kuhitaji namba yangu nilishangaa na kusema kwanini Yule mama ananifatilia sana, nikashangaa akawa ananipigia pigia simu kumbe kuna kitu kinamvuta kuhusu mimi, sasa nikaumwa kumbe Mungu anazidi kutuweka karibu na Yule mama, akaniombea na mpaka kupona kabisa, na nyie mkapenda na kufanya muende kwake na sasa mmempeleka muhusika kwake kwahilo hilo ni jambo la kushangaza sana, muache Mungu aitwe Mungu tu”
“Sasa tatizo baba katupa mtihani mkubwa sana, kuwa tumsaidie amuoe Yule mama, la sivyo hawezi kuruhusu mimi nikuoe wewe, yani hapo ndio pagumu hadi nawaza kwanini tumempeleka kwa Yule mama sababu kumuoa haitawezekana na kuhusu kunizuia mimi nisikuoe wewe hiyo haipo maana nakupenda sana Erica”
“Erica wala msijilaumu kumpeleka kule, ile ni pona ya baba yenu na ataweza kuondokana na yanayomtatiza kwasasa.”
“Ila baba yangu analalamika umemlia pesa nyingi sana, ni hela gani hizo?”
“Hakuna hela ya baba yako niliyokula”
Erica alianza kumueleza Erick kuhusu mchakato wa baba yao toka siku aliyokutana nae na alivyotaka kumuhonga simu jinsi alivyoiacha na kuondoka, na jinsi baba yake alivyopeleka milioni mbili, jinsi alivyorudisha pesa hiyo akiwa na mama yake na jinsi ya ile milioni kumi aliyoituma kwa Dora,
“Ile hela yote niliiweka kwa Dora, nilikwambia ni mke wa Yule mzee ila haikuwa hivyo alikuwa ni hawara yake na Dora alisema nimpe yeye maana ndio anastahili kula pesa yam zee Jimmy”
“Aaah nimekuelewa ila baba yangu huwa analalamika swala lingine kuwa kwenu alishatoaga posa, sasa ni posa gani hiyo?”
“Tena umenikumbusha kitu, huwa anasema hivyo na madai yake aliacha hiyo hela mlangoni kwetu ila hakuna aliyeiona, na kama tungeiona basi tungemrudishia kwakweli. Yani hata nyumbani huwa wanashangaa kuhusu swala la yeye kutoa posa”
Erick alikumbuka pesa ambayo aliikuta mlangoni kwakina Erica na karatasi ndani la kuonyesha upendo ambapo alijua ni Rahim ametuma, ila kwa maelezo ya Erick alihisi ni lazima baba yake ndio muhusika, aliamua kumuuliza
“Alisema ni pesa ngapi?”
“Eti zilikuwa milioni tatu”
“Oooh kumbe!”
Erick akamueleza Erica jinsi alivyochukua zile pesa akidhani kuwa ni Rahim kaziacha, kwahiyo alichukua kumkomesha.
“Kumbe kweli ulichukua wewe, Dada Bite kila siku alikuwa anasema nikuulize ila sikufikiria kuwa wewe unaweza kuchukua pesa hiyo, nilijua ungechukua ni lazima ungerudisha”
“halafu ninazo ndani kwangu kule hadi leo, kama ndio hizo zinamchanganya akili yake nitampeleka na ujumbe wake, yani mzee wangu jamani kwanini lakini? Hivi naweza hata dakika mbili kumuacha karibu yako, si atakubaka jamani loh! Erica nakupenda sana, sijawahi kumpenda mwanamke yeyote duniani kama ninavyokupenda wewe”
Erica alikuwa akitabasamu tu, ni kweli bado hakuoana na Erick ila alijihisi raha sana kuishi nae pamoja.

Rahim alivyopewa ujumbe na mama yake hakutaka hata kupoteza muda yani alitamani kesho yake ifike upesi ili akaongee vizuri na Zainabu, siku hiyo alianza kuishi na Salma tena, alikubali sababu aliona dalili ya yeye kumuoa Zainabu inaonekana kwahiyo alikubali swala aliloambiwa na mama yake kuwa aishi na Salma. Basi jioni hiyo alimuaga Salma na kutoka ila alienda kuongea na Babuu ili kesho yake waende wote kuongea na Zainabu kwani alimuona Babuu kuwa na busara zaidi yake.
Salma alikaa nyumbani na kuwaza sana, kiukweli hakupenda mume wake kuoa mke wa pili kwani alihitaji ndani aishi mwenyewe tu, ila hakuwa na namna maana ndio ilishaamriwa hivyo kuwa Rahim atamuoa huyo Zainabu, basi alikaa kidogo kisha akajaribu kuongea na washauri mbalimbali akiwepo Yule mama kwenye simu,
“Yani makubwa yalinipata mama yangu na mume wangu anataka kuoa mke wa pili, nimekubali maana sina namna na siwezi kumkatalia ila naona kabisa mume wangu atampenda sana huyo mke kushinda mimi”
“Anaenda kuoa lini?”
“Sijui ila kuna uelekeo maana huyo mwanamke washakamilisha mambo ya kujitambulisha na kesho anaenda kuongea nae ili aweze kumuoa kabisa”
“Sasa mwanangu usiwe na presha, mimi ndio kungwi wa makungwi yani ukiwasiliana na mimi basi ndoa haiwezi kuwa tatizo kwako tena. Sasa basi usichukie kwa swala la mumeo kutaka kuoa mke wa pili wala nini, ila unatakiwa kufanya hivi”
“Eeeeh kufanya nini?”
“Basi leo mumeo hakikisha unampa mapenzi ambayo hujawahi kumpa, yani kama hujui kukatika basi leo jifunze kukatika yani mpe mapenzi hadi mumeo awaze kwanini anaenda kuoa tena wakati wewe upo! Kiu kubwa ya wanaume ni mpenzi tu, yani mwanaume anahangaika kulia na kushoto ila shida yake ni ngono basi. Kwahiyo wewe mwanangu leo jitahidi, nenda kanunue udi ujifukize kisha mumeo akute unanukia na umpe mapenzi ambayo hujawahi kumpa”
“Asante sana, ngoja nifanyie kazi ushauri wako maana saa hizi katoka”
“Basi mwali wangu huu ndio muda wako, kanunue udi, oga vizuri jifukize na akija muandalie maji ya kuoga yawe ya uvuguvugu uweke na iliki yanukie, kwahiyo akifika tu aoge halafu akimaliza, mfute na umpetipeti kiasi kisha muandalie chakula, hakikisha umepika chakula anachopenda ili akikiona aweze kula hiko chakula halafu akishiba mmalizie na chakula hiko kinachopendwa na wanaume wote yani muda wa kumpa hiko sasa nakutumia ujumbe namna ya kufanya hadi huyo mumeo leo ahisi umekuwa mpya”
Salma alifurahi sana na kuagana na huyu mama kisha kwenda dukani kununua udi na vitu vingine alivyoelekezwa, kisha alivyorudi akafanya kama alivyoambiwa ambapo alipika chakula ambacho mumewe anakipenda lipomaliza akaenda kuoga na kujifukiza ule udi halafu alimsubiria mume wake sasa huku akisoma ule ujumbe aliotumiwa na Yule mama halafu akifanya mazoezi aliyoelekezwa na Yule mama ya jinsi ya kumvutia zaidi mumewe.
Kwenye mida ya saa tatu usiku Rahim alirudi nyumbani kisha Salma akafanya kama alivyoelekezwa na Yule mama tena zaidi ya pale hadi Rahim alishangaa kweli kuwa mke wake kabadilika kiasi hiko, baada ya hapo alimfurahisha mumewe kwenye tendo, kwakweli leo Rahim alijishangaa hata huwa anaenda kutembea na machangudoa wa nini, sema kwavile alishaweka ahadi ya kumuoa Zainabu akaona hakuna namna inabidi tu kesho aonane nae na apange nae mipango ya ndoa, ila siku hiyo alilala akiwa na tabasamu zito kwa jinsi alivyofanyiwa na mkewe.
 
SEHEMU YA 416


Kesho yake mzee Jimmy alienda kwenye kazi zake na alipokuwa kazini akawaza swala la Yule mwanamke aliyesema kuwa na mimba ya Erick yani Sia, akaona kuna umuhimu wa kumtunza hata kama mwanae anakataa kufanya hivyo kwahiyo alijiandaa na kutoka kazini ili akamuangalie.
Alipofika anapoishi Sia, alishangaa kumuona Steve nje akisombelea maji, huyu mzee alimuulizia Sia kwa Steve maana mara ya mwisho anakumbuka kuwa Sia alimtambulisha kuwa Steve ni mdogo wake akamuuliza,
“Yuko wapi dada yako?”
“Dada yangu yupi?”
“Dada yako Sia, yuko wapi?”
“Sia sio dada yangu ni Mke wangu, na muda huu ametoka”
“Unasema ni mke wako?”
“Ndio ni mke wangu”
Mzee Jimmy alishangaa sana kuwa kuna nini pale maana Yule aliambiwa ni mdogo mtu, sasa kusikia mke tena alishangaa sana hapo, wakati anashangaa vizuri alitokea Dora kumbe naye alienda kwa lengo la kumfata mdogo wake kwahiyo alipomkuta mzee Jimmy pale alichowaza moja kwa moja huenda huyo mzee Jimmy anatoka na Sia maana kama aliendelea kutaka Erica anayetoka na Erick mtoto wake ni wazi anaweza kumtaka Sia ingawa anajua wazi kuwa Sia amewahi kuwa na mahusiano na mwanae, alimfata na kumuuliza kwa mshangao,
“Wewe mzee vipi muda huu hapa?”
“Nimekuja hapa kwa lengo la kuonana na huyu binti wa hapa Sia, maana alisema ana mimba ya Erick”
“Kheee Sia ana mimba?”
“Ndio, na cheti alinionyesha”
“Hata usihangaike, hiyo mimba sio ya Erick ila ya mdogo wangu huyo Steve”
Kisha Steve alivyosogea karibu, Dora alimtambulisha vizuri,
“Huyu ni mdogo wangu anaitwa Steve”
“Kheee basi huyu binti hafai kunidanganya mtu mzima hivi!”
Mzee Jimmy alionekana kusikitika sana, ila Dora alimuangalia mdogo wake na kumwambia,
“Hongera sana Steve huo ndio uanaume, kajipendekeza umemjaza mimba atalea mwenyewe na midawa yake”
Kisha Dora akamuangalia mzee Jimmy na kumshawishi waondoke hapo, kwahiyo waliondoka bila hata kumchukua tena mdogo wake na bila ya kuonana na Sia.

Ndugu wa Bahati kama walivyokubaliana waliongozana na Bahati siku ya leo hadi kwakina Erica, walifika na kugonga ambapo Bite ndio aliwafungulia mlango. Walikaribishwa ndani na kuingia, kiukweli mamake Erica alishangaa uwepo wao na walieleza azma yao ya kutaka kuonana na Erica, mama Erica aliwauliza kwa mshangao,
“Mnataka nini leo, nyie si ndio mliondoka hapa kwa mnbwembwe!”
Mama Bahati akaanza kujitetea,
“Ni kweli tuliondoka na tumekiri makosa, tunaomba kwa huruma yenu tuweze kuonana na Erica”
“Kwa taarifa yenu, Erica kajiozesha yupo huko kwa mwanaume alikojipeleka”
Wale ndugu wa Bahati walishangaa sana, ila mama Erica hakutaka hata kuongea mengi zaidi ya kuwatimua tu kwahiyo ilibidi waondoke maana hawakuwa na namna zaidi ya kufanya.
Walipoondoka, mama Erica aliamua kumpigia simu Erica ili amseme, Erica alipokea ile simu
“Hivi wewe mtoto huna hata aibu, hayo mambo ya kujiozesha yameanza lini? Unajua laana wewe!”
“Mama sikutaka kukukosea tena kwa mimba niliyonayo”
“Mjinga wewe, unajua kabisa kubeba mimba nje ya ndoa ni dhambi na bado ukajibebesha na sasa umeamua kuishi na mwanaume ili kudhihirisha uzinzi wako. Sasa nakwambia ubaki huko huko yani hapa kwangu usirudi”
“Jamani mama”
“Nimemaliza, si wewe ndio mama basi jiite mwenyewe mama mie sitaki huo ujinga kabisa”
Mama Erica alikata ile simu na kuanza kuongea na Bite,
“Yani hili dogo lako halina akili hata kidogo, nadhani limechukua akili za Mage ambaye huwa wanashauriana kwenda kwenye matambiko maana naye alikimbilia kwa mwanaume, kuna mitoto kama imerogwa loh! Kujiozesha mwishowe ni kujuta, Mage anavumilia tu pale maana mwanaume mwenyewe hana mbele wala nyuma.”
“Kweli mama, yani Erica kasoma ila kama hajasoma vile, mambo yake hakuna msomi anayeweza kufanya kama yeye. Bora Mage hajasoma kivile lakini Erica ni msomi ila mjinga kabisa yani”
Walijikuta siku nzima wakisema kuhusu Erica tu maana aliwaudhi sana.
 
SEHEMU YA 417

Leo Rahim na Babuu walikutana na Zainabu na katika maelezo ya Zainabu alitaka kwanza waende kupima ukimwi na Rahim kabla ya kukubali kuolewa nae, hilo kwa Rahim hata halikuwa swala la shida maana hata wakati Salma ana mimba changa walienda kupima na alikuwa mzima kabisa kwahiyo alijiamini kuwa ni mzima kabisa, basi wakaondoka yeye, Babuu na Zainabu hospitali kupima tena walipima wote watatu.
Walisubiri majibu huku wakiwa na furaha sana, majibu yalipotoka daktari alisema kila mtu apewe majibu yake ila Rahim alikuwa wa kwanza kupinga,
“Daktari kwanini unataka kututenganisha hivyo? Sisi tumekuja pamoja kupima na tunataka majibu kwa pamoja”
“Kama mmoja wenu kaathirika je!”
“Sio tatizo maana tutampa moyo tu kuwa ni hali ya kawaida maana hatokuwa wa kwanza kuathirika”
“Ila haitakiwi kufanya hivyo”
“Mimi kama mkubwa wao hawa naomba utupe majibu kwa pamoja, huyu ni mdogo wangu kwahiyo ni muhimu mimi kujua afya yake, na huyu ni mke wangu lazima nijue afya yake na wao ni muhimu kujua afya yangu”
“Na nyie wengine mnasemaje?”
“Sawa hakuna tatizo”
Walijibu kwa pamoja maana walijikuta wakijiamini sana ila walijua ile kusema kama mmoja wenu kaathirika je, ndio kauli za madaktari ili kuwatisha tu.
Basi daktari hakutaka kubishaba nao sana na kuamua kuwapeleka ofisini tu kuwapa majibu yao.
Waliingia ofisini wote kwa pamoja yaani Babuu, Rahim na Zainabu. Daktari aliwapa majibu yao ambapo Babuu na Zainabu walikuwa wazima ila Rahim alikutwa kaathirika yani baada ya majibu yale Rahim alizimia bila hata kusikiliza ushauri wala nini.

Basi Erica alikosa raha kabisa tangu muda amepokea simu ya mama yake yani alijihisi vibaya sana kwenye moyo wake, ila siku hiyo alifikiwa na mgeni aliyekuwa ni Tumaini na kushangaa maana ni muda sana hakuweza kuongea na Tumaini kutokana na chuki ambayo ipo kati yao na hata haijulikani ni nini chanzo, ila siku hiyo ambayo Tumaini alienda mwenyewe akaona ndio siku pekee ya yeye kuweza kuongea nae na kumaliza tofauti zao ambazo ziliibuka tu.
Ila kabla hajaongea na Tumaini alipigiwa simu na kaka yake kuwa waonane aweze kumtambulisha huyo wifi yake, ila kwavile hakuweza kumwambia Tumaini kuwa aende nae au amwache halafu aende akaamua kwa muda huo amwambie tu kaka yake aende kule na huyo wifi yake,
“Mbona unaniambia huko Erica?”
“Wewe njoo tu na maelezo mengine utayapata huku huku”
Basi kaka yake alikubali kufanya hivyo na kwavile eneo walilokuwepo halikuwa mbali sana na pale kwahiyo alichukua muda mfupi sana kufika pale nyumbani kwa Erica.
Waligonga mlango na Erica kwenda kufungua, akaingia Tony na mdada mwingine, ila Erica alipomuona huyu mdada alijikuta akijawa na chuki isiyo na mfano kabisa maana huyu dada alikuwa ni Doroth yani yule daktari aliyemdai Erica laki moja ili amfichie siri.
 
SEHEMU YA 418

Waligonga mlango na Erica kwenda kufungua, akaingia Tony na mdada mwingine, ila Erica alipomuona huyu mdada alijikuta akijawa na chuki isiyo na mfano kabisa maana huyu dada alikuwa ni Doroth yani yule daktari aliyemdai Erica laki moja ili amfichie siri.
Erica alimkaribisha yule dokta kwa kinyongo sababu alikuwa na chuki nae sana ila kwavile yule dokta alionyesha kama kutokumkumbuka Erica, basi akaamua amkaribishe ndani ili amkumbushe vizuri.
Walipokuwa wanaingia ndani walikuta Tony akikumbatiana na Tumaini sababu Tony alitangulia kuingia ndani utafikiri nyumba yake, ilionyesha kuwa Tony na Tumaini wanafahamiana, Erica na Doroth walikaa tu wakiwaangalia.
Tumaini na Tony walikaa huku wakicheka kwa furaha, Tony akaanza kumwambia Tumaini,
"Kheee umebadilika, umependeza, umenenepa. Siri ya mafanikio Tuma?"
"Hamna bhana ni kuridhika tu"
"Unajua sikutegemea kukuona kabisa, duh ni kitambo sana jamani yani sikutegemea Tumaini"
Kisha akamuangalia Erica na kumuuliza,
"Erica, umefahamiana vipi na huyu?"
Erica akamjibu kaka yake,
"Nitakwambia tu maana lazima utamfahamu zaidi ya hivyo unavyomfahamu, ila kwanza tuongelee kuhusu uliyefika nae hapa, nitambulishe tafadhari"
"Aaaah hadi nimesahau jamani, (akamuangalia Tumaini na kusema) unaona Tumaini hadi umenisahaulisha mada yangu niliyokuja nayo loh! ( kisha akamuangalia Doroth na kusema) Sorry kipenzi yani kuna mtu amenichanganya hapa, sikutegemea kumuona. Ila huyu ndio yule mdogo wangu niliyesema nataka umuone anaitwa Erica, halafu Erica huyu ndio yule wifi yako niliyesema nataka ufahamiane nae anaitwa Tumaini oooh sorry jamani ni anaitwa Doroth"
Erica akacheka, wakati huo Doroth aliinuka ili kupeana mkono wa kufahamiana na Erica.
Ila Erica aligoma kupokea mkono huo kisha akasema,
"Hivi nikuulize unanikumbuka?"
"Hapana"
"Wewe ni Dokta! Nimejuaje kazi yako na Tony hajaisema?"
"Ni kweli mimi ni dokta, unaweza kunifahamu sababu nahudumia wagonjwa wengi sana ila ni ngumu kwa mimi kukumbuka kila mgonjwa"
"Hata unaowatapeli na kuwafanyia roho mbaya huwakumbuki pia?"
"Hakuna ninayemfanyia roho mbaya"
"Sawa umejibu vyema sana, basi hao wagonjwa huwa unawahumiaje?"
"Vizuri tu"
"Wewe Dokta hebu muogope Mungu jamani, unahudumia vizuri wagonjwa wewe!"
Tony aliingilia kati na kumuuliza dada yake
"Kwani tatizo nini Erica eeeeh!"
"Ngoja niseme, Doroth sina siri tena kwasasa maana nitaeleza hapa ili wajue ulichonifanyia halafu kaka utaamua yani kama kuendelea na huyo mwanamke au la! Sisemi umuache ila nataka kusema kile alichonifanyia mimi, sijui kwa wagonjwa wengine ila nazungumzia mimi."
"Sema Erica, sema kila kitu ili nisikie vizuri kakako"
"Siku moja nilipata matatizo ikabidi nijifanye naumwa ila sikuwa naumwa kweli yani nilifanya vile ili kuepuka matatizo, nikapelekwa hospitali na kumkuta dokta huyo Doroth, ila nilimuomba amwambie Erick atoke ili nibaki mimi na yeye, na alifanya hivyo. Nilimwambia ukweli kuwa siumwi ila amwambie Erick kuwa nina vidonda vya tumbo, akakubali na kusema nimpe laki moja, nikamwambia mimi nina elfu thelathini tu akaikataa katakata lakini nikampa ile elfu thelathini nikamwambia nyingine nitaenda kummalizia, akagoma kabisa akasema hadi niache simu yangu, ikabidi niache simu ndio akaweza kuniruhusu. Sasa wakati naondoka na Erick, aliulizia simu yangu nikamwambia nimeisahau hospitali, Erick akasema lazima tukaifate. Tulivyofika hospitali nikaenda kwa dokta huyu na kumueleza kila kitu ila akagoma kutoa ile simu najua alinifanyia mimi makusudi tu maana hakujua kama kuna kitu ambacho mimi naweza kumsaidia. Basi ilibidi nimpigie simu kijana mmoja ambaye alituma ile laki moja kwa huyu dokta ndio akaniruhusu niondoke na simu yangu, nikamuomba zile elfu thelathini zangu za mwanzo akagoma kabisa eti akasema zile ni za usumbufu, niliumia sana roho ila sikuwa na la kufanya. Nikaondoka ila tulivyofika hoteli kula na Erick nikaona si vyema niendelee kuongopa, bora nimwambie Erick ukweli, nikamweleza naye akachukia sana na kuondoka, sasa na mimi nilivyotaka kuondoka ndio nikaletewa bili ya pale na sikuwa na hela yoyote, kumbuka huyu dokta amezikomba zote. Siku ile siwezi kusahau, nilidhalilishwa mimi pale hotelini, niliosha vyombo usiku kucha. Ila chanzo ni huyu dokta asiye na huruma, kila siku namuota kwa ujinga wake alionifanyia"
Tony alimuangalia mdogo wake, kisha akamuangalia Doroth aliyekuwa kajiinamia tu, akamwambia
"Siku zote waswahili husema usimtendee mtu kitu ambacho hupendi wewe kutendewa, Erica mdogo wangu pole sana. Nimejaribu kujiweka kwenye nafasi yako ila imeniuma, laki moja kuficha siri? Kwani anatoa mimba au?"
Tumaini akaongea,
"Tena sio laki moja ni laki na elfu thelathini"
Tony akamuangalia Doroth na kumwambia,
"Kwanza mpe mdogo wangu laki mbili kwa ukatili uliomfanyia, kisha mlipe hela yake"
Doroth alibaki kimya tu kwani alihisi kama kuonewa vile ingawa alikumbuka fika alichomfanyia Erica, basi Erica akasema tena,
"Yani wewe nadhani hujui ethics za udokta, yani ulichonifanyia siku ile hakikuwa sawa kabisa. Madokta huwa ni marafiki wakubwa sababu inajulikana kuwa wanaifahamu saikolojia vizuri, sasa wewe ni dokta gani usiye na huruma jamani! Halafu mpaka muda huu upo kimya tu yani hujui hata kusema samahani, kaka ndio mwanamke wa kuoa huyu!! Hapana kwakweli"
Kikweli Doroth alihisi aibu sana na kuamua kuongea,
"Jamani sikia wifi yangu, sikujua kama nitalutana tena na wewe na sikujua kama utakuja kuwa wifi yangu. Naomba tusahau yaliyopita"
"Kirahisi rahisi hivyo eeeeh! Eti tusahau yaliyopita, yani unaongea au unatapika? Nilitamani sana siku moja uingie kwenye anga zangu"
Yani leo hata Tumaini alimshangaa Erica kama huwa ni muongeaji kiasi kile maana kila siku huwa anaishia kulia tu ila siku hiyo alikuwa kama kalishwa pilipili vile.
Doroth aliona aibu na hakutaka kuumbuka zaidi, kwani akainuka na kutoka, Tony akainuka pia ili kumfata ila Erica alimshika mkono na kumrudisha ndani na kumwambia,
"Kaka, unaenda wapi? Yule kajionyesha wazi kuwa si mwanamke wa kuolewa na wewe yani hata neno samahani halijui! Kaka ndio mwanamke gani wa kuolewa na wewe yule!"
Ila Tony yalimuingia akilini yale maneno ya Erica, muda huo Tumaini nae akaongea,
"Ila Erica ulisema unatuambia kisa cha huyo dokta na uamuzi wa kuendelea nae au kutokuendelea nae atafanya mwenyewe Tony au maneno yako ya mwanzo umeyasahau?"
"Hamna sijayasahau ila Tumaini umemuona mwanamke mwenyewe mambo yake yalivyo, haya Tony kaa kwanza unieleze kufahamiana na Tumaini imeanzia wapi"
Tony alikaa chini kwani hakwenda tena kumfatilia Doroth, kisha Erica aliinuka na kusema
"Ngoja niende jikoni niandae kidogo chakula"
"Sasa Erica, mbona hujaniambia hapa ni wapi?"
"Nitakwambia tu Tony usijali"
Kisha Erica aliinuka na kwenda jikoni.

Ikabidi Babuu na Zainabu wamsubirie Rahim akipewa huduma ya kwanza, kwahiyo walitoka nje na kukaa kwenye mabenchi ila ilionyesha kuwa Zainabu alikuwa na mawazo sana, kitu kilichofanya Babuu asogee na kuongea nae,
"Mbona una mawazo hivyo Zainabu? Unajua sio vizuri kuwaza kiasi hiko?"
"Aaah hamna bhana, ila nina mawazo sana sababu imekuwa kama nina mkosi vile, akitokea wa kunioa tu basi namkuta na majanga"
"Majanga gani? Na wangapi walipatwa na hayo majanga?"
"Yani huyu ni wa pili, wa kwanza nilimkuta kaathirika hivi hivi"
"Hivi Zainabu hujawahi kuwa na mpenzi wewe?"
"Ninahitaji mume ila sio mpenzi"
"Nikwambie kitu Zainabu"
"Niambie"
"Yani Zainabu ni kwavile ndugu yangu aliwahi kusema ila nilitamani sana ungeolewa na mimi. Naona ni binti unayejielewa sana ndiomana umechagua kupima kwanza. Nakuomba mipango ya ndoa iendelee baina yetu maana kama kupima tushapima na vilevile tunaendana kwahiyo bora tuoane tu"
Zainabu alitabasamu tu bila ya kujibu chochote kile. Babuu aliendelea kuongea,
"Jamani mpenzi, umetabasamu tu. Naomba tuwe pamoja"
"Yani wewe Babuu, swala la Rahim halijaisha na tayari ushaweka mada yako jamani! Ngoja kwanza haya yapite"
"Wakati tunangoja nikubalie, jua mimi ndio mumeo kwanza sijawahi kuoa na wewe hujawahi kuolewa, sina mtoto na huna mtoto huoni kama ni vizuri mimi na wewe kuwa pamoja?"
Rahim aliruhusiwa na daktari na alienda nae hadi alipokaa Babuu na Zainabu na kuanza kuongea nao kuwa ile hali waione ya kawaida na wawe wanampa ushauri. Basi walipomaliza kuongea na yule dokta, waliongozana na kurudi nyumbani ambapo getini tu Rahim aliwaambia waondoke na wamuache mwenyewe aingie ndani kwake,
"Nyie ondokeni, niacheni men yea niende ndani ila yaliyotokea hospitali ibaki kuwa siri yenu jamani yani sitaki mmwambie yeyote kuwa nimeathirika. Tumeelewana?"
"Ndio tumekuelewa"
Kwahiyo ilibidi wafanye hivyo tu na kuondoka.
Rahim aliingia ndani na kupokelewa na mke wake Salma, kwakweli alikuwa anaona ajabu sana sababu Salma alikuwa akitenda mambo ambayo hajawahi kuyafanya kabisa kabisa, aliona mke wake kabadilika ila atamwambia vipi swala la yeye kuwa na ukimwi? Aliona hilo ni jambo baya sana kwake.
Alimwambia amechoka na anaenda kupumzika ila Salma akamuuliza,
"Mume wangu, mke mwwnzangu Zainabu hajambo?"
Rahim akatikisa kichwa kisha akamjibu,
"Sio mke mwenzio tena yule, mimi sioi tena mke wa pili. Unanitosha wewe tu"
Salma hakuamini ile kauli, alienda kumkumbatia mume wake kisha kumuacha akapumzike, kwakweli Salma alijiona ni mshindi kwa siku hiyo yani aliona hajawahi kushinda kama hivyo, alimpigia simu na yule mama kumwambia habari zile,
"Nilikwambia mwali wangu, hapa ndii mwisho yani mambo yote ya kumfanyia mumeo uwe unaniuliza, sijui kuna chakula huwezi kupika niulize nikufundishe"
"Asante sana yani sana, umeokoa ndoa yangu. Nakutafutia zawadi mama nitakuletea"
Salma aliongea kwa furaha sana na mama huyu.
 
Back
Top Bottom