FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #41
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 25
Kwangu ilikuwa bahati ya mtende kuwa ndani ya idara, idara ambayo kila mwanajeshi kambini alikuwa akiiimba kila siku na kutamani kuwa huko ila ni mimi ambaye niliipata hiyo nafasi. Nilikumbuka nilikotoka sikutaka kufanya makosa, nilitamani kumfanya mama yule aliyenilea ajivunie huko aliko hivyo nilihitaji kufanya kazi kwa juhudi zangu zote na kweli nilitimiza hilo. Huko kwenye idara nilipewa kesi nyingi na nilizitimiza kwa asilimia zote miamoja na kwa moyo wote baada ya mafunzo ya muda mrefu.
Sikuwahi kumsahau baba yako, alikuwa ni mtu maarufu tayari nchini, niliona ni muda sahihi wa kumtafuta rafiki yangu wa damu. Kumpata kwake akiwa na mke na mtoto tayari alinitupia lawama nyingi kwa kuamua kumkimbia ila alinielewa kwa sababu maana yangu haikuwa mbaya. Maisha yangu ni siri kubwa ila niliamua kumuweka wazi juu ya kazi yangu mpaka nilipo fikia wakati huo, akanipongeza na kunifurahia rafiki yake, urafiki wetu ukarudi japo kwa siri kwani haikutakiwa kujulikana kwa mtu yeyote, wote tungekuwa hatarini.
Nikiwa ndani ya idara ndipo lilipokuja kutokea jina la mrembo IRINA ESPANOVICH, haikuchukua muda mezani likaja jina la LS (The LUNATIC SOCIETY) tukiwa tunaendelea kulifuatilia kwa ukaribu ndipo raisi akaja kufariki ghafla, ukawa msiba kwa taifa. Tulibaki tumeduwaa lakini viongozi wa ngazi za juu wakawa hawana presha yoyote kana kwamba walikuwa wanajua kilichokuwa kinaendelea, jambo hilo kama mzalendo lilinigusa mno, licha ya baba yako kunipa maelekezo juu ya kilichokuwa kinaendelea upande wake; kama mzalendo niliamua kuingia kwenye maktaba za taifa kuusaka ukweli ambao ulikuwa nyuma ya jambo hilo.
Nilicho fanikiwa kukijua kinatisha, hakikuwa salama kwangu hata kidogo kama ningeamua kukifikiria, jambo la kwanza nilishangazwa na ukweli kwamba raisi aliuawa na mdogo wake wa damu Novack Nyangasa ambaye alikuwa mpenzi wa mrembo ambaye aliiasi idara yake ya KGB, Irina. Ujio wake Tanzania ndio ulikuwa mwanzo wa kuanzishwa kwa jamii hiyo ya siri ambayo kwa wakati huo yeye na mpenzie Novack Nyangasa ndio walikuwa viongozi.
Hata baada ya raisi kufariki, walimpa nafasi hiyo aliyekuwa makamu wa raisi mwanamama Daniela Lopa akakaimu nafasi hiyo. Mwanamama huyo alikaa hapo kuwawakilisha wao hivyo taifa likaingia kwenye mikono yao rasmi kwa kutumia akili ya mwanamke huyo. Kwa bahati mbaya baadae ilikuja kugundulika kwamba hata mimi nilikuwa nawafuatilia kwa ukaribu hivyo nikawa nipo kwenye mahesabu yao ya kunifanya niwe mtu wao au wanipunguze duniani kwani kukusanya taarifa zao nyingi lilikuwa ni tatizo kubwa ambalo lingekuja kuwaharibia mbeleni kwenye hiyo mipango yao.
Wakati mambo yote hayo yanafanyika ndio wakati ambao baba yako alikuja kwangu na kutaka mimi nikutafute wewe na mama yako kwa kupotea ghafla huku yeye akidai anaelekea Israeli. Aliniachia mtihani mzito mbele yangu, mimi mwenyewe nilikuwa nimeshaharibu kwenye idara kwa kufukunyua taarifa ambazo hazikuwa zikinihusu halafu ndio wakati ambao rafiki yangu alinifuata na kuhitaji nimtafutie familia yake na kuihifadhi mahali ambapo ni salama. Nina uhakika ukikaa sehemu yangu utaona ni ugumu kiasi gani ambao nilikuwa nao, lakini ningefanyaje na mimi ndiye mtu pekee ambaye baba yako aliniamini kiasi cha kuniachia hata miliki zake na mali zake zote? Ningegoma nisingekuwa na cha kujibu mbele ya mwenyezi Mungu siku ya mwisho kikaoni, nikakubali kuifanya kazi ya kukutafuta wewe na mama yako, kazi ambayo ilinishangaza na kuyafanya maisha yangu kubadilika.
Nilifanya kila namna kuhakikisha nawapata japo sikuwa na mwanzo wa kujua mliko potelea wala kuwepo kwa wakati huo ila jambo ambalo lilinishangaza kwenye upelelezi wangu juu ya maisha yako ni baada ya kugundua kwamba mama yako alikuwa ni mwanachama wa jamii hiyo ya LUNATIC SOCIETY na ndiye ambaye alikwenda huko mbarali kuwapa sumu familia ya baba yako kwa sababu alikuwa akiaminika huko. Hilo ni jambo ambalo lilinishangaza na siwezi kusema niliamini bali nilibaki nimetahamaki nisijue ni kipi nilitakiwa kukifanya, mtu ambaye nilitakiwa kumlinda na mwanae ndiye alikuwa nyuma ya hiyo mipango. Ulimwengu uliwahi kunishangaza ila siku ile ulinipa somo kuhusu wanadamu. Sasa ni wakati wa wewe kujua sababu ya msingi hasa kwamba ni kwanini watu hawa wanaisaka roho yako kwa udi na uvumba kuliko hata pesa inavyotafutwa na maskini, wapo tayari kutumia mabilioni ya fedha kukuua wewe na kukupoteza ulimwenguni kwa sababu wewe ni miongoni mwa viumbe hatari vichache vilivyo bakia duniani na uhatari wako unawahusu wao wakiogopa kwamba siku ukiujua ukweli utafanya mambo ya kutisha kwa upande wao lakini pia wanaogopa zaidi wewe kuvujisha taarifa hizo ukizipata.
Simulizi ndefu imhusuyo yeye na maisha yake ya nyuma ilikuwa imefika kati kati, ilikuwa inasisimua, inaliza na kushangaza. Alikuwa amepewa nusu yake na sasa alikuwa anaelekea kwenye sehemu ya mhimu zaidi akiwa anashangaa kuambiwa kwamba mama yake mzazi alikuwa mwanachama wa jamii hiyo ya siri ambayo ndiyo kwanza alikuwa ameiskia kwa mara ya kwanza ambayo ilidaiwa kuwa nyuma ya mipango miovu ya serikalini ikiwepo kumuua raisi wa nchi, kumtoa baba yake kafara lakini kuiteketeza familia yake yote. Edison alihema kwa nguvu akiwa mwingi wa hofu, jasho lilikuwa linashuka usoni kwake akiwa hana uwezo wa kulizuia. Aligusisha kidole chake mdomoni ili kupata mate ya kufungulia kurasa mpya ambazo alitakiwa kuanza kuzisoma sababu za msingi za yeye kuishi maisha ya sasa, aliifunua kurasa hiyo iliyo fuata;
Juu iliandikwa KIFO CHANGU MKONONI MWANGU. Hakuelewa maneno hayo yalikuwa na maana gani na yalihusiana nini na simulizi ya maisha yake, kitabu alikuwa nacho, alichagua kuzizuia hasira na kuwa mpole ili aelewe mchezo mzima ulikuwaje.
“MAGAIDI WATISHIA AMANI TANZANIA KWA KUMWAGA DAMU ZA WATU, MMOJA ATEKWA. KUNANI NYUMA YA PAZIA? TANZANIA SI SALAMA TENA. JNIA HALI TETE”
Kichwa cha gazeti kilizipamba kurasa za mbele kabisa za magazeti ambazo zilifanya taasisi za usambazaji wa magazeti kupata wateja wengi siku hiyo kuliko ilivyo kawaida. Tukio la jana yake usiku lilikuwa la namna yake, tukio lilikuwa la kusisimua huku likitokea ndani ya uwanja ambao unategemewa na taifa zima.
Habari hiyo ilisambaa kwa kasi kila eneo na kuzua mijadala mikubwa, wengi walihusisha jambo hilo na shambulio la kigaidi wakiamini kwamba huenda Tanzania kuziunga mkono baadhi ya nchi ilikuwa inaenda kuleta matatizo makubwa nchini, kama kawaida ya wananchi wengi lawama walizielekezea upande wa serikali na kuona kama serikali haifanyi kazi sawa sawa kama inavyopaswa. Wengine hawakuishia hapo tu, walitaka wale ambao walikuwa wazembe kwenye hizo sehemu zao walitakiwa kuchukuliwa hatua kali kwani uzembe wao ulifanya watu wengi kuumia vibaya kwa kukimbia, ulileta shambulio na nafsi kwa wahanga ambao walikuwepo eneo hilo lakini lilikuwa shambulio hatari la kuhatarisha maisha ya watu hao.
Eneo la Banana njia ya kuelekea Kitunda, watu walikuwa wameketi pembezoni mwa barabara karibu na kilipo kituo cha dala dala za kwenda huko wakiteta yale ya jana.
“Mimi huwa nasema kila siku, hawa wajinga wanakula kodi zetu tu hakuna kitu wanakifanya huko zaidi ya kuwaza kuwavua warembo chupi na kujaza matumbo yao. Haiwezekani eneo kama lile ambalo sisi tunaamini kwamba ni moja ya sehemu ya kujivunia ya taifa, eneo ambalo tunaamini kwamba linalindwa na ni salama! Watu wanavamiwa na kuuawa halafu inasemekana hakuna hata mmoja aliye kamatwa? Huu ni ujinga mtupu, haki ya Mungu siji kwenda kupiga kura tena” Kijana mmoja alifoka! Hasira zilikuwa zimempanda huku akiwa anahema kwa jazba. Haikueleweka kama alikuwa na hasira zake za kupigwa na maisha au ni mtu ambaye alivurugwa asubuhi hiyo, ilibidi mwenzake mmoja ampe maji kwanza apooze koo, alipaniki isivyo kawaida mpaka akawa anawashangaza wenzake.
“Abraham Linkoln aliwahi kusema USIHUKUMU HAUTAHUKUMIWA, kabla ya kuwarushia lawama kwanza inabidi ukae kwenye nafasi yao halafu ujiulize kama ungekuwa wewe ungefanyaje! Hata wewe mwenyewe kuna mazingira familia yako tu inakushinda kuifanyia maamuzi sasa kwanini unavamia tu na kuanza kutukana kuwasema viongozi bila kutumia upembuzi mzuri wa hoja? Maliki punguza kukurupuka mwanangu. Hakuna taarifa kutoka mamlaka za usalama nchini hivyo subiri watoe taarifa zao walipo fikia ndipo ulaumu, ni ngumu kushindana na watu ambao hujui wanapanga nini dhidi ya nchi yako, ni sawa na wewe hapo uvamiwe na kuchomwa kisu ghafla ukiwa kwenye utafutaji wako badala ya kutafuta sababu iliyo mfanya mtu huyo akushambulie unaanza kujilaumu kwa kushambuliwa, huo ni ujinga mwanangu” kijana ambaye alionekana kuwa mwerevu alimpa somo mwenzake, alitakiwa kuacha kukurupuka bali kuwa mtu wa kutumia zaidi akili.
UKURASA WA 25 unafika mwisho.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 25
Kwangu ilikuwa bahati ya mtende kuwa ndani ya idara, idara ambayo kila mwanajeshi kambini alikuwa akiiimba kila siku na kutamani kuwa huko ila ni mimi ambaye niliipata hiyo nafasi. Nilikumbuka nilikotoka sikutaka kufanya makosa, nilitamani kumfanya mama yule aliyenilea ajivunie huko aliko hivyo nilihitaji kufanya kazi kwa juhudi zangu zote na kweli nilitimiza hilo. Huko kwenye idara nilipewa kesi nyingi na nilizitimiza kwa asilimia zote miamoja na kwa moyo wote baada ya mafunzo ya muda mrefu.
Sikuwahi kumsahau baba yako, alikuwa ni mtu maarufu tayari nchini, niliona ni muda sahihi wa kumtafuta rafiki yangu wa damu. Kumpata kwake akiwa na mke na mtoto tayari alinitupia lawama nyingi kwa kuamua kumkimbia ila alinielewa kwa sababu maana yangu haikuwa mbaya. Maisha yangu ni siri kubwa ila niliamua kumuweka wazi juu ya kazi yangu mpaka nilipo fikia wakati huo, akanipongeza na kunifurahia rafiki yake, urafiki wetu ukarudi japo kwa siri kwani haikutakiwa kujulikana kwa mtu yeyote, wote tungekuwa hatarini.
Nikiwa ndani ya idara ndipo lilipokuja kutokea jina la mrembo IRINA ESPANOVICH, haikuchukua muda mezani likaja jina la LS (The LUNATIC SOCIETY) tukiwa tunaendelea kulifuatilia kwa ukaribu ndipo raisi akaja kufariki ghafla, ukawa msiba kwa taifa. Tulibaki tumeduwaa lakini viongozi wa ngazi za juu wakawa hawana presha yoyote kana kwamba walikuwa wanajua kilichokuwa kinaendelea, jambo hilo kama mzalendo lilinigusa mno, licha ya baba yako kunipa maelekezo juu ya kilichokuwa kinaendelea upande wake; kama mzalendo niliamua kuingia kwenye maktaba za taifa kuusaka ukweli ambao ulikuwa nyuma ya jambo hilo.
Nilicho fanikiwa kukijua kinatisha, hakikuwa salama kwangu hata kidogo kama ningeamua kukifikiria, jambo la kwanza nilishangazwa na ukweli kwamba raisi aliuawa na mdogo wake wa damu Novack Nyangasa ambaye alikuwa mpenzi wa mrembo ambaye aliiasi idara yake ya KGB, Irina. Ujio wake Tanzania ndio ulikuwa mwanzo wa kuanzishwa kwa jamii hiyo ya siri ambayo kwa wakati huo yeye na mpenzie Novack Nyangasa ndio walikuwa viongozi.
Hata baada ya raisi kufariki, walimpa nafasi hiyo aliyekuwa makamu wa raisi mwanamama Daniela Lopa akakaimu nafasi hiyo. Mwanamama huyo alikaa hapo kuwawakilisha wao hivyo taifa likaingia kwenye mikono yao rasmi kwa kutumia akili ya mwanamke huyo. Kwa bahati mbaya baadae ilikuja kugundulika kwamba hata mimi nilikuwa nawafuatilia kwa ukaribu hivyo nikawa nipo kwenye mahesabu yao ya kunifanya niwe mtu wao au wanipunguze duniani kwani kukusanya taarifa zao nyingi lilikuwa ni tatizo kubwa ambalo lingekuja kuwaharibia mbeleni kwenye hiyo mipango yao.
Wakati mambo yote hayo yanafanyika ndio wakati ambao baba yako alikuja kwangu na kutaka mimi nikutafute wewe na mama yako kwa kupotea ghafla huku yeye akidai anaelekea Israeli. Aliniachia mtihani mzito mbele yangu, mimi mwenyewe nilikuwa nimeshaharibu kwenye idara kwa kufukunyua taarifa ambazo hazikuwa zikinihusu halafu ndio wakati ambao rafiki yangu alinifuata na kuhitaji nimtafutie familia yake na kuihifadhi mahali ambapo ni salama. Nina uhakika ukikaa sehemu yangu utaona ni ugumu kiasi gani ambao nilikuwa nao, lakini ningefanyaje na mimi ndiye mtu pekee ambaye baba yako aliniamini kiasi cha kuniachia hata miliki zake na mali zake zote? Ningegoma nisingekuwa na cha kujibu mbele ya mwenyezi Mungu siku ya mwisho kikaoni, nikakubali kuifanya kazi ya kukutafuta wewe na mama yako, kazi ambayo ilinishangaza na kuyafanya maisha yangu kubadilika.
Nilifanya kila namna kuhakikisha nawapata japo sikuwa na mwanzo wa kujua mliko potelea wala kuwepo kwa wakati huo ila jambo ambalo lilinishangaza kwenye upelelezi wangu juu ya maisha yako ni baada ya kugundua kwamba mama yako alikuwa ni mwanachama wa jamii hiyo ya LUNATIC SOCIETY na ndiye ambaye alikwenda huko mbarali kuwapa sumu familia ya baba yako kwa sababu alikuwa akiaminika huko. Hilo ni jambo ambalo lilinishangaza na siwezi kusema niliamini bali nilibaki nimetahamaki nisijue ni kipi nilitakiwa kukifanya, mtu ambaye nilitakiwa kumlinda na mwanae ndiye alikuwa nyuma ya hiyo mipango. Ulimwengu uliwahi kunishangaza ila siku ile ulinipa somo kuhusu wanadamu. Sasa ni wakati wa wewe kujua sababu ya msingi hasa kwamba ni kwanini watu hawa wanaisaka roho yako kwa udi na uvumba kuliko hata pesa inavyotafutwa na maskini, wapo tayari kutumia mabilioni ya fedha kukuua wewe na kukupoteza ulimwenguni kwa sababu wewe ni miongoni mwa viumbe hatari vichache vilivyo bakia duniani na uhatari wako unawahusu wao wakiogopa kwamba siku ukiujua ukweli utafanya mambo ya kutisha kwa upande wao lakini pia wanaogopa zaidi wewe kuvujisha taarifa hizo ukizipata.
Simulizi ndefu imhusuyo yeye na maisha yake ya nyuma ilikuwa imefika kati kati, ilikuwa inasisimua, inaliza na kushangaza. Alikuwa amepewa nusu yake na sasa alikuwa anaelekea kwenye sehemu ya mhimu zaidi akiwa anashangaa kuambiwa kwamba mama yake mzazi alikuwa mwanachama wa jamii hiyo ya siri ambayo ndiyo kwanza alikuwa ameiskia kwa mara ya kwanza ambayo ilidaiwa kuwa nyuma ya mipango miovu ya serikalini ikiwepo kumuua raisi wa nchi, kumtoa baba yake kafara lakini kuiteketeza familia yake yote. Edison alihema kwa nguvu akiwa mwingi wa hofu, jasho lilikuwa linashuka usoni kwake akiwa hana uwezo wa kulizuia. Aligusisha kidole chake mdomoni ili kupata mate ya kufungulia kurasa mpya ambazo alitakiwa kuanza kuzisoma sababu za msingi za yeye kuishi maisha ya sasa, aliifunua kurasa hiyo iliyo fuata;
Juu iliandikwa KIFO CHANGU MKONONI MWANGU. Hakuelewa maneno hayo yalikuwa na maana gani na yalihusiana nini na simulizi ya maisha yake, kitabu alikuwa nacho, alichagua kuzizuia hasira na kuwa mpole ili aelewe mchezo mzima ulikuwaje.
“MAGAIDI WATISHIA AMANI TANZANIA KWA KUMWAGA DAMU ZA WATU, MMOJA ATEKWA. KUNANI NYUMA YA PAZIA? TANZANIA SI SALAMA TENA. JNIA HALI TETE”
Kichwa cha gazeti kilizipamba kurasa za mbele kabisa za magazeti ambazo zilifanya taasisi za usambazaji wa magazeti kupata wateja wengi siku hiyo kuliko ilivyo kawaida. Tukio la jana yake usiku lilikuwa la namna yake, tukio lilikuwa la kusisimua huku likitokea ndani ya uwanja ambao unategemewa na taifa zima.
Habari hiyo ilisambaa kwa kasi kila eneo na kuzua mijadala mikubwa, wengi walihusisha jambo hilo na shambulio la kigaidi wakiamini kwamba huenda Tanzania kuziunga mkono baadhi ya nchi ilikuwa inaenda kuleta matatizo makubwa nchini, kama kawaida ya wananchi wengi lawama walizielekezea upande wa serikali na kuona kama serikali haifanyi kazi sawa sawa kama inavyopaswa. Wengine hawakuishia hapo tu, walitaka wale ambao walikuwa wazembe kwenye hizo sehemu zao walitakiwa kuchukuliwa hatua kali kwani uzembe wao ulifanya watu wengi kuumia vibaya kwa kukimbia, ulileta shambulio na nafsi kwa wahanga ambao walikuwepo eneo hilo lakini lilikuwa shambulio hatari la kuhatarisha maisha ya watu hao.
Eneo la Banana njia ya kuelekea Kitunda, watu walikuwa wameketi pembezoni mwa barabara karibu na kilipo kituo cha dala dala za kwenda huko wakiteta yale ya jana.
“Mimi huwa nasema kila siku, hawa wajinga wanakula kodi zetu tu hakuna kitu wanakifanya huko zaidi ya kuwaza kuwavua warembo chupi na kujaza matumbo yao. Haiwezekani eneo kama lile ambalo sisi tunaamini kwamba ni moja ya sehemu ya kujivunia ya taifa, eneo ambalo tunaamini kwamba linalindwa na ni salama! Watu wanavamiwa na kuuawa halafu inasemekana hakuna hata mmoja aliye kamatwa? Huu ni ujinga mtupu, haki ya Mungu siji kwenda kupiga kura tena” Kijana mmoja alifoka! Hasira zilikuwa zimempanda huku akiwa anahema kwa jazba. Haikueleweka kama alikuwa na hasira zake za kupigwa na maisha au ni mtu ambaye alivurugwa asubuhi hiyo, ilibidi mwenzake mmoja ampe maji kwanza apooze koo, alipaniki isivyo kawaida mpaka akawa anawashangaza wenzake.
“Abraham Linkoln aliwahi kusema USIHUKUMU HAUTAHUKUMIWA, kabla ya kuwarushia lawama kwanza inabidi ukae kwenye nafasi yao halafu ujiulize kama ungekuwa wewe ungefanyaje! Hata wewe mwenyewe kuna mazingira familia yako tu inakushinda kuifanyia maamuzi sasa kwanini unavamia tu na kuanza kutukana kuwasema viongozi bila kutumia upembuzi mzuri wa hoja? Maliki punguza kukurupuka mwanangu. Hakuna taarifa kutoka mamlaka za usalama nchini hivyo subiri watoe taarifa zao walipo fikia ndipo ulaumu, ni ngumu kushindana na watu ambao hujui wanapanga nini dhidi ya nchi yako, ni sawa na wewe hapo uvamiwe na kuchomwa kisu ghafla ukiwa kwenye utafutaji wako badala ya kutafuta sababu iliyo mfanya mtu huyo akushambulie unaanza kujilaumu kwa kushambuliwa, huo ni ujinga mwanangu” kijana ambaye alionekana kuwa mwerevu alimpa somo mwenzake, alitakiwa kuacha kukurupuka bali kuwa mtu wa kutumia zaidi akili.
UKURASA WA 25 unafika mwisho.