Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

Simulizi ya kijasusi: Nafsi zilizotelekezwa

HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 56

MADAM KATE
Lilikuwa nina maarufu ndani ya Black Market, jina ambalo liliheshimika na kuogopwa isivyokuwa kawaida. Ni kutokana na mambo ambayo alikuwa ameyafanya, mafanikio ambayo wengi waliamini kwamba ameyapata kutokana na biashara hizo zipatikanazo ndani ya soko jeusi. Licha ya kuwa maarufu sana huko lakini hakuwa akifahamika kwenye maisha halisi kwamba Madam Kate ni nani hasa.
Cersie Mhina ndilo lilikuwa jina halisi la mwanamke huyo, mwanamama ambaye alikuwa akiimbwa kila kona ya nchi kwa sababu alikuwa ni moja kati ya wanawake ambao walikuwa na mafanikio makubwa mno tofauti na mitazamo ya wengi ambavyo huwa ipo kwenye jinsia hiyo. Alikuwa amejikita zaidi kwenye biashara ya gesi pamoja na mitandao ya simu lakini pia alikuwa akijishughulisha na madini ya dhahabu. Mafanikio yake yalimfanya kuwa na ukaribu na viongozi wakubwa wa kiserikali kiasi kwamba akawa anahusishwa kwenye mipango mingi ya maendeleo ya nchi na hata kwenda kuiwakilisha nchi ilipokuwa inapata nafasi za uwekezeaji kimataifa kwa sababu alikuwa na uzoefu mkubwa kwenye biashara na uwezo mkubwa wa mikakati ya biashara kubwa ambapo hakuna mpango wake hata mmoja ambao ulikuwa umewahi kufeli chini yake.
Baada ya kutoka Bulgari mwanamama huyo alikuwa anahitaji kufanya mkutano, mkutano wa siri kati yake yeye na watu wake ambao alikuwa amewapa majukumu pamoja na viongozi kadhaa wa serikali. Usiku wa saa saba ndio ulikuwa muda wa kufanyika mkutano ndani ya jengo lake kubwa la biashara ambalo lilikuwa limejengwa maeneo ya Mikocheni Dar es salaam.

MHINA TOWER, majina ambayo yalikuwa yanang’aa yalilipamba jengo hilo na kuyafanya yasomeke vyema wakati huo wa usiku kiasi kwamba hata kama mtu angekuwa mbali basi maandishi hayo angeyaona kwa usahihi bila shaka. Ndani ya eneo la chini kabisa la jengo hilo, yalianza kupaki magari ya kifahari mno, ilikuwa ni ishara ya watu hao kuweza kukutana na kiongozi wao kujadili mambo mbalimbali yakiwemo maseke seke ambayo bado yalikuwa yanaendelea kutokea.
Zilipaki gari kadhaa na watu walikuwa wakionekana kuelekea kwenye lifti na kupandisha maghorofa ya juu. Zilipita kama dakika tano baadae ndipo ukaonekana msafara wa gari tatu ukiwa unaelekea eneo hilo, msafara huo ndio ulikuwa wa boss lady mwenyewe akiwa na walinzi wake kumi. Mmoja wa watu ambao walikuwa kwenye huo msafara alikuwa ni mwanaume Yohani Mawenge.
“Baadae natakiwa kuongea na wewe unipe mrejesho wa kazi zote ambazo nimekupatia uzikamilishe” mwanamama huyo aliongea kwa sauti ya taratibu akiwa anamwangalia kijana wake huyo mtu kazi Yohani Mawenge.
“Sawa bosi”
Chumba kikubwa ambacho kilipambwa na marashi ya kutosha pamoja na samani za bei ghali mno, kilikuwa kina wana wanaume watano ambao walikuwa wametangulia kabla yake madam Kate. Yeye aliingia humo ndani akiwa ameongozana na Yohani ambaye alikuwa ameishika begi ya mwanamama huyo. Baada ya kufika wote waliinuka kumpatia heshima kwani walionekana kumuogopa isivyokuwa kawaida, waliketi baada ya yeye kuketi kwenye kiti ambacho kilikuwa mbele ya hao wote tena katikati kabisa.
“Ni muda umepita sasa tangu niwe nje ya nchi, kuna mambo yanaendelea hapa nchini ambayo ni hatari kwa biashara yetu na kwa jamii yetu kwa ujumla na hatutakiwi kuruhusu kabisa yaendelee kutokea ndiyo maana nimewaiteni hapa leo tuweze kuyaweka sawa haya mambo kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyokuwa kimepangwa” aliongea akiwa anaivua miwani yake na kuiweka juu ya meza. Umri ulikuwa umekwenda lakini pesa ilimfanya bado aendelee kuvutia kwenye macho ya watu ambao walikuwa wanamtazama.
“Hili jambo ni kweli kwa sababu tangu lile tukio ambalo lilitokea pale uwanja wa ndege, ni kama lilikuja kwa wakati mbaya zaidi kumteka binti yule maana ujio wake umekuwa chanzo cha matatizo mengi hivyo naona anatakiwa kufa” Aliongea mwanaume mmoja mtu mzima lakini kwa bahati mbaya hakujulikana ni nani kwa sababu nyuso zao wote watano zilikuwa zimefunikwa kasoro mwanamama huyo pekee ndiye ambaye uso wake ulikuwa wazi. Hao wote hawakutakiwa kabisa kujuana ili kila mtu kuwa na amani na kila ambacho kilikuwa kinafanyika.
“Unamaanisha yule binti ambaye aliiba mzigo wetu?”
“Ndiyo madam”
“Yule atakufa ila sio kwa sasa”
“Kwanini?”
“Kwa sababu nafanya naye kazi”
“Hilo ni jambo ambalo haliwezekani bosi, inawezekanaje mtu ambaye ameiba mzigo wa mabilioni ya pesa ufanye naye kazi kirahisi tu hivyo?” aling’aka mwanaume mwingine kwa jazba ambayo ndani yake ilikuwa na heshima kwa mwanamke huyo.
“Kwa sababu naye anamtafuta mtu ambaye tunamtafuta sisi, alinihakikishia kwamba alikuwa anahitaji kuonana na mimi ili nimsaidie ndiyo maana akafanya lile jambo la kujikamatisha na sio mtoto wa Patrick Magembe kama alivyokuwa amedanganya bali ni mtoto wa mwanasheria wa zamani Aidan Semzaba na ni miongozi mwa watu ambao wana mafunzo ya kikomando”
“Unamaanisha kwamba yule komando Daniel ambaye alifia Somalia ni kaka yake wa damu?”
“Ndiyo”
“Kwahiyo hii ndiyo sababu ambayo imefanya amtafute Clyton Lameck?”
“Ndiyo hivyo kwa namna moja ama nyingine atatusaidia kazi kwa kiasi kikubwa na baada ya hapo atanipa mzigo wetu kisha nitamuua kwa mkono wangu mwenyewe” kauli hiyo ilionyesha kuwafurahisha wote humo ndani ambapo waligongesha mikono yao juu ya meza kuunga mkono jambo hilo lakini mmoja wao ambaye alivaa suti ya gharama ya kijivu alijikohoza kwa nguvu ili wenzake wampe umakini wa kumsikiliza.
“Bosi tunasubiri utupatie muongozo wa hatua zilizo chukuliwa, tulipo na tunapo elekea kwa sababu kama unavyo ona hali imekuwa mbaya hususani kwa yule mwanasheria yule ambaye hata jana amefika nyumbani kwa dokta Namaki Prasad hivyo kama tungechelewa kidogo basi huenda angepata siri nyingi ambazo hatakiwi kuzipata. Yule mtu huwa hazushi jambo bila kuwa na ushahidi hivyo mpaka anaongea hayo yote mitandaoni na kwenye vyombo vya habari basi ana mengi ambayo anayajua, tunataka kujua maamuzi ya jamii yetu ni yapi kuhakikisha sisi wote tupo sehemu salama na haya yanaisha” Mzee huyo aliuliza swali la maana kabisa ambalo huenda ndiyo ilikuwa sababu ya msingi zaidi ya kuweza kuwafikisha hapo usiku huo.
“Najua hicho ndicho kimetuleta hapa usiku wa leo, mambo yote yameenda kama yalivyopangwa, Keneth Lawi amekufa tayari Yohani aliifanya kazi vizuri nchini Uganda lakini wanatuma majasusi wao kuja kupeleleza na majasusi hao wanatakiwa kufa bila kuacha ushahidi wowote. Tukija hapa nyumbani, daktari tayari amekufa hivyo moja ya siri kubwa zinaendelea kuwa salama lakini shida ipo sehemu moja kwa yule kijana Damasi, yule alifanya kosa kubwa kuweza kuruhusu sura yake kuonekana jambo ambalo sasa gharama yake itakuwa kubwa kwani inatulazimu kuhakikisha shirika la kipelelezi la nchi haliendelei na habari yake ambayo kama ikija kuwa wazi zaidi itakuwa ni hatari kwetu. Nitalishughulikia lakini kama likifeli kabisa basi nitamuua mwenyewe hivyo msiwe na shaka kuhusu yeye” maelezo yake yalikuwa yamenyooka na kuwapa amani watu hao ambao walikuwa wameanza kupata wasiwasi kwenye mioyo yao.
“Sasa jambo la mhimu zaidi ni hatima ya huyo Lameck pamoja na JACK THE LAWYER, kuna kipi kitafanyika juu yao?”
“Hayo yote mimi nitawashughulikia ila ninacho kitaka kwa sasa, kama kuna mtu kati yenu bado ana biashara ambazo anaona sio sawa basi azisimamishe zote mara moja, nitawapa ratiba ya kuanza kuzifanya kwa mara nyingine. Hakuna kosa la kijinga ambalo linatakiwa kufanyika ila hao wawili ambao mmewaulizia ni kwamba wanatakiwa kufa mapema iwezekanavyo”
“Sawa bosi, na viongozi wakuu uliahidi kwamba tutawaona!” aliuliza mwanaume mmoja ambaye tangu aingie hapo ndani hakuwa ameongea jambo lolote lile. Madam Kate alimwangalia kwa muda kisha akatabasamu.

UKURASA WA 56 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 56

MADAM KATE
Lilikuwa nina maarufu ndani ya Black Market, jina ambalo liliheshimika na kuogopwa isivyokuwa kawaida. Ni kutokana na mambo ambayo alikuwa ameyafanya, mafanikio ambayo wengi waliamini kwamba ameyapata kutokana na biashara hizo zipatikanazo ndani ya soko jeusi. Licha ya kuwa maarufu sana huko lakini hakuwa akifahamika kwenye maisha halisi kwamba Madam Kate ni nani hasa.
Cersie Mhina ndilo lilikuwa jina halisi la mwanamke huyo, mwanamama ambaye alikuwa akiimbwa kila kona ya nchi kwa sababu alikuwa ni moja kati ya wanawake ambao walikuwa na mafanikio makubwa mno tofauti na mitazamo ya wengi ambavyo huwa ipo kwenye jinsia hiyo. Alikuwa amejikita zaidi kwenye biashara ya gesi pamoja na mitandao ya simu lakini pia alikuwa akijishughulisha na madini ya dhahabu. Mafanikio yake yalimfanya kuwa na ukaribu na viongozi wakubwa wa kiserikali kiasi kwamba akawa anahusishwa kwenye mipango mingi ya maendeleo ya nchi na hata kwenda kuiwakilisha nchi ilipokuwa inapata nafasi za uwekezeaji kimataifa kwa sababu alikuwa na uzoefu mkubwa kwenye biashara na uwezo mkubwa wa mikakati ya biashara kubwa ambapo hakuna mpango wake hata mmoja ambao ulikuwa umewahi kufeli chini yake.
Baada ya kutoka Bulgari mwanamama huyo alikuwa anahitaji kufanya mkutano, mkutano wa siri kati yake yeye na watu wake ambao alikuwa amewapa majukumu pamoja na viongozi kadhaa wa serikali. Usiku wa saa saba ndio ulikuwa muda wa kufanyika mkutano ndani ya jengo lake kubwa la biashara ambalo lilikuwa limejengwa maeneo ya Mikocheni Dar es salaam.

MHINA TOWER, majina ambayo yalikuwa yanang’aa yalilipamba jengo hilo na kuyafanya yasomeke vyema wakati huo wa usiku kiasi kwamba hata kama mtu angekuwa mbali basi maandishi hayo angeyaona kwa usahihi bila shaka. Ndani ya eneo la chini kabisa la jengo hilo, yalianza kupaki magari ya kifahari mno, ilikuwa ni ishara ya watu hao kuweza kukutana na kiongozi wao kujadili mambo mbalimbali yakiwemo maseke seke ambayo bado yalikuwa yanaendelea kutokea.
Zilipaki gari kadhaa na watu walikuwa wakionekana kuelekea kwenye lifti na kupandisha maghorofa ya juu. Zilipita kama dakika tano baadae ndipo ukaonekana msafara wa gari tatu ukiwa unaelekea eneo hilo, msafara huo ndio ulikuwa wa boss lady mwenyewe akiwa na walinzi wake kumi. Mmoja wa watu ambao walikuwa kwenye huo msafara alikuwa ni mwanaume Yohani Mawenge.
“Baadae natakiwa kuongea na wewe unipe mrejesho wa kazi zote ambazo nimekupatia uzikamilishe” mwanamama huyo aliongea kwa sauti ya taratibu akiwa anamwangalia kijana wake huyo mtu kazi Yohani Mawenge.
“Sawa bosi”
Chumba kikubwa ambacho kilipambwa na marashi ya kutosha pamoja na samani za bei ghali mno, kilikuwa kina wana wanaume watano ambao walikuwa wametangulia kabla yake madam Kate. Yeye aliingia humo ndani akiwa ameongozana na Yohani ambaye alikuwa ameishika begi ya mwanamama huyo. Baada ya kufika wote waliinuka kumpatia heshima kwani walionekana kumuogopa isivyokuwa kawaida, waliketi baada ya yeye kuketi kwenye kiti ambacho kilikuwa mbele ya hao wote tena katikati kabisa.
“Ni muda umepita sasa tangu niwe nje ya nchi, kuna mambo yanaendelea hapa nchini ambayo ni hatari kwa biashara yetu na kwa jamii yetu kwa ujumla na hatutakiwi kuruhusu kabisa yaendelee kutokea ndiyo maana nimewaiteni hapa leo tuweze kuyaweka sawa haya mambo kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyokuwa kimepangwa” aliongea akiwa anaivua miwani yake na kuiweka juu ya meza. Umri ulikuwa umekwenda lakini pesa ilimfanya bado aendelee kuvutia kwenye macho ya watu ambao walikuwa wanamtazama.
“Hili jambo ni kweli kwa sababu tangu lile tukio ambalo lilitokea pale uwanja wa ndege, ni kama lilikuja kwa wakati mbaya zaidi kumteka binti yule maana ujio wake umekuwa chanzo cha matatizo mengi hivyo naona anatakiwa kufa” Aliongea mwanaume mmoja mtu mzima lakini kwa bahati mbaya hakujulikana ni nani kwa sababu nyuso zao wote watano zilikuwa zimefunikwa kasoro mwanamama huyo pekee ndiye ambaye uso wake ulikuwa wazi. Hao wote hawakutakiwa kabisa kujuana ili kila mtu kuwa na amani na kila ambacho kilikuwa kinafanyika.
“Unamaanisha yule binti ambaye aliiba mzigo wetu?”
“Ndiyo madam”
“Yule atakufa ila sio kwa sasa”
“Kwanini?”
“Kwa sababu nafanya naye kazi”
“Hilo ni jambo ambalo haliwezekani bosi, inawezekanaje mtu ambaye ameiba mzigo wa mabilioni ya pesa ufanye naye kazi kirahisi tu hivyo?” aling’aka mwanaume mwingine kwa jazba ambayo ndani yake ilikuwa na heshima kwa mwanamke huyo.
“Kwa sababu naye anamtafuta mtu ambaye tunamtafuta sisi, alinihakikishia kwamba alikuwa anahitaji kuonana na mimi ili nimsaidie ndiyo maana akafanya lile jambo la kujikamatisha na sio mtoto wa Patrick Magembe kama alivyokuwa amedanganya bali ni mtoto wa mwanasheria wa zamani Aidan Semzaba na ni miongozi mwa watu ambao wana mafunzo ya kikomando”
“Unamaanisha kwamba yule komando Daniel ambaye alifia Somalia ni kaka yake wa damu?”
“Ndiyo”
“Kwahiyo hii ndiyo sababu ambayo imefanya amtafute Clyton Lameck?”
“Ndiyo hivyo kwa namna moja ama nyingine atatusaidia kazi kwa kiasi kikubwa na baada ya hapo atanipa mzigo wetu kisha nitamuua kwa mkono wangu mwenyewe” kauli hiyo ilionyesha kuwafurahisha wote humo ndani ambapo waligongesha mikono yao juu ya meza kuunga mkono jambo hilo lakini mmoja wao ambaye alivaa suti ya gharama ya kijivu alijikohoza kwa nguvu ili wenzake wampe umakini wa kumsikiliza.
“Bosi tunasubiri utupatie muongozo wa hatua zilizo chukuliwa, tulipo na tunapo elekea kwa sababu kama unavyo ona hali imekuwa mbaya hususani kwa yule mwanasheria yule ambaye hata jana amefika nyumbani kwa dokta Namaki Prasad hivyo kama tungechelewa kidogo basi huenda angepata siri nyingi ambazo hatakiwi kuzipata. Yule mtu huwa hazushi jambo bila kuwa na ushahidi hivyo mpaka anaongea hayo yote mitandaoni na kwenye vyombo vya habari basi ana mengi ambayo anayajua, tunataka kujua maamuzi ya jamii yetu ni yapi kuhakikisha sisi wote tupo sehemu salama na haya yanaisha” Mzee huyo aliuliza swali la maana kabisa ambalo huenda ndiyo ilikuwa sababu ya msingi zaidi ya kuweza kuwafikisha hapo usiku huo.
“Najua hicho ndicho kimetuleta hapa usiku wa leo, mambo yote yameenda kama yalivyopangwa, Keneth Lawi amekufa tayari Yohani aliifanya kazi vizuri nchini Uganda lakini wanatuma majasusi wao kuja kupeleleza na majasusi hao wanatakiwa kufa bila kuacha ushahidi wowote. Tukija hapa nyumbani, daktari tayari amekufa hivyo moja ya siri kubwa zinaendelea kuwa salama lakini shida ipo sehemu moja kwa yule kijana Damasi, yule alifanya kosa kubwa kuweza kuruhusu sura yake kuonekana jambo ambalo sasa gharama yake itakuwa kubwa kwani inatulazimu kuhakikisha shirika la kipelelezi la nchi haliendelei na habari yake ambayo kama ikija kuwa wazi zaidi itakuwa ni hatari kwetu. Nitalishughulikia lakini kama likifeli kabisa basi nitamuua mwenyewe hivyo msiwe na shaka kuhusu yeye” maelezo yake yalikuwa yamenyooka na kuwapa amani watu hao ambao walikuwa wameanza kupata wasiwasi kwenye mioyo yao.
“Sasa jambo la mhimu zaidi ni hatima ya huyo Lameck pamoja na JACK THE LAWYER, kuna kipi kitafanyika juu yao?”
“Hayo yote mimi nitawashughulikia ila ninacho kitaka kwa sasa, kama kuna mtu kati yenu bado ana biashara ambazo anaona sio sawa basi azisimamishe zote mara moja, nitawapa ratiba ya kuanza kuzifanya kwa mara nyingine. Hakuna kosa la kijinga ambalo linatakiwa kufanyika ila hao wawili ambao mmewaulizia ni kwamba wanatakiwa kufa mapema iwezekanavyo”
“Sawa bosi, na viongozi wakuu uliahidi kwamba tutawaona!” aliuliza mwanaume mmoja ambaye tangu aingie hapo ndani hakuwa ameongea jambo lolote lile. Madam Kate alimwangalia kwa muda kisha akatabasamu.

UKURASA WA 56 unafika mwisho.
Inanishawishi kuona ni kama maisha halisi uko vyema FEBIANI BABUYA
 
U

ULIMWENGU WA WATU WABAYA, GEREZA LA HAZWA, INNOCENT KILLER (THE REVENGE), IDAIWE MAITI YANGU, THE ODYSSEY OF GAVIN LUCA

Hizo Zina hizo panga za kutosha ambazo unazihitaji.
Pamoja sana,... Kweny Sanaa ya kuelezea Mapigo we ni noma sana ( manguli wengi walishindwa kuelezea martial skills kwa Njia ya maandishi)
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 57

“Wakihitaji muwaone watakuja wao wenyewe hivyo hilo sio mimi wa kupanga”
“Sawa bosi” mkutano ulikuwa umeisha, wote walitoa heshima kwake na kutoka humo ndani ambapo yeye alibaki na Yohani pekee. Alimgeukia mwanaume huyo na kumwangalia kwa umakini kwenye macho yake.
“Kuna ushahidi wowote uliacha kwenye kazi zote ambazo umezifanya?”
“Hapana bosi”
“Kwa sasa nahitaji umfuatilie Damasi kwa umakini lakini kabla ya kufanya hilo nahitaji uwe karibu na yule mwanasheria wakati huo Nicola najua atakuwa msaada mkubwa kutusaidia kumpata Edison kwani yeye ana uchungu naye na wakati anaendelea na hilo mwambie Saimoni amfuatilie kwa umakini ili tuweze kujua mahali ambako aliuficha ule mzigo na mzigo ukipatikana basi hakikisheni Nicola analetwa kwangu”
“Sawa bosi”

Tangu akutane na JACK THE LAWYER, Aaliyah Beka alikuwa na mawazo mengi kwenye kichwa chake, mawazo kutokana na vitu ambavyo aliambiwa na mwanasheria yule. Bado havikuwa vikimuingia akilini wala kuamini kwamba yule ambaye alikuwa anaongea naye alikuwa ni yule mwanasheria ambaye mikono yake iliaminika kwa ulaini zaidi kwa sababu ya kuishika kalamu kwa muda mrefu lakini haikuwa hivyo bali mtu yule alikuwa na upande wake wa siri ambao huenda ni yeye pekee ndiye ambaye alikuwa anaujua vyema.
Hakuwa na budi zaidi ya kuupeleka mrejesho huo kwa wenzake watatu ambao walikuwa wanasubiria taarifa yake kwani walikuwa na siku mbili tu pekee za kuweza kupeleka mrejesho kwa mkurugenzi wao. Aaliyah alikuwa mbele ya wenzake akiwa amezama mbali kifikra, wenzake wote walibaki wanamshangaa kwani ni yeye ambaye alikuwa anasubiriwa ili kuweza kujua ni hatua gani ambayo walikuwa wamefikia.
“Yule sio yeye” ndiyo kauli ambayo aliitoa kwenye kinywa chake.
“Unamaanisha nini kusema hivyo?” aliuliza mwanaume Jumapili Magawa.
“Nina uhakika yule sio yule komando ambaye alipotea Somalia”
“Kivipi na hizo bahari inadaiwa kwamba kavujisha yeye! Unataka kuniambia kwamba anataka kujitoa sadaka kubeba mzigo wa mtu mwingine?”
“Mpaka sasa hilo ndilo jibu sahihi, majibu yake yanaonyesha kwamba sio yeye ila huyo mtu yeye ana mfahamu”
“Amekwambia hivyo?”
“Hapana baada ya kumtisha kuna kauli ambayo ameniambia ndiyo imenihakikishia hili”
“Itamke hiyo kauli”
“HII KAULI IISHIE KWANGU TU NA SIO KWAKE, ATAKUUA BILA KUKUULIZA CHOCHOTE” Wote walibaki wanaangaliana usoni wasijue ni jambo lipi ambalo lilikuwa linazungumzwa.
“Hili jambo linaniingia akilini, hiyo ni kauli ambayo ni wazi alikuwa amemlenga huyo mtu wake mwingine hivyo tunaweza kuhitimisha kwamba yule sio yeye kama ambavyo taarifa za awali zilidai. Nadharia ya kusema ni yeye inagoma kwa kutumia kipimo cha nyakati, wakati wale makomando wanaenda Somalia na Kongo ni kipindi ambacho mwanasheria huyu alikuwa anashinda mahakamani kila siku kushughulikia kesi ya mauaji ya wale wanafamilia ambao waligongwa na gari ya mfanya biashara mkubwa wa madini ila ni siku moja tu ambayo yule komando alidaiwa kuua wenzake kule Somalia na kupotea ndiyo ambayo mwanasheria huyu hakutokea mahakamani hali iliyo pelekea kesi kuahirishwa. Hivyo ni kwamba huyu sio yeye ila anamjua mhusika kwa asilimia miamoja na huenda naye alihusika kwa namna moja ama nyingine na kama watu hawa tutengeneze nadharia kwamba walivamiwa kuuawa basi huyu ndiye alienda kumuokoa” Maelezo ya David Mbatina mtu mjivuni yalifungua mambo mengine kwenye mazungumzo yao.
“Mbona hii habari inaanza kunichanganya! Tuchukulie kwamba alienda kumuokoa komando huyu ambaye damu yake ilikutwa eneo la tukio maana yake ni lazima alijeruhiwa vibaya. Kama ni hivyo yeye alijuaje kwamba watu hawa watavamiwa na akawahi kufika kwa muda mwafaka na kufanikiwa kumuokoa mtu huyu? Lakini pia yeye ni nani kwa mtu huyo kiasi kwamba aache kazi zake za mhimu na kusafiri mpaka Somalia kwa ajili ya kumuokoa mtu ambaye hamhusu? Hapana kuna jambo tunalikosa hapa katikati huenda ndipo habari yenyewe ilipo” Ruben Magesa naye aliongezea jambo ambalo lilizidi kuipa uzito nadharia ambayo walikuwa wanaitengeneza kwenye hiyo kesi yao huku wenzake wakiwa wana utulivu wa kutosha kwa sababu waikuwa wanadili na mtu mwenye akili nyingi zaidi yao na mtu huyo kwenye kila muondoko wake alikuwa anawazidi hatua mbili mbele.
“Huyu mtu ana siri nyingi ambazo hata sisi hatuna” Aaliyah alivunja ukimwa kwa mara nyingine
“Kama zipi labda?”
“Kama mnakumbuka miaka kadhaa huko nyuma iliwahi kusambaa habari juu ya uwepo wa jamii ya siri kwenye nchi hii, jamii ya LS na tulipo anza kufuatilia kuhusu jambo hilo wakubwa walidai kwamba ni nadharia ya kufikirika ambayo haipo kwenye maisha halisi na tukaamua kuifunga. Nadhani wote mnaikumbuka?”
“Ndiyo, hiyo inahusiana vipi na hii kesi?”
“Basi huenda majibu ya maswali yetu yote yapo hapa”
“Aaliyah wewe ndiye umeongea na huyo bwana ebu tufungukie kila ambacho amekwambia ili tujue tunaanzia wapi kama kwake au kwa mtu mwingine ambaye anaweza kuwa msaada wa sisi kuweza kufikia mwafaka kwenye hili”
“Huyu mtu anaamini kwamba jamii hii ipo kwenye maisha ya kweli na inaendeshwa na jasusi wa zamani wa KGB ambaye anaitwa IRINA ESPANOVICH. Mwanamke huyu alikuja Tanzania baada ya umoja wa nchi za kisovieti kudondoka na hakuja kwa wema bali alikimbia kwao kwa sababu shirika hilo lilikuwa linamtafuta akiwa ni moja ya watu ambao waliuza taarifa zao kwa Marekani. Sasa ujio wake hapa nchini ndio ambao ulizalisha jamii hii ya siri ambayo aliianzisha kwa mlengo wa kuweza kujilinda yeye mwenyewe na kujitengeneza kuwa na nguvu kubwa kiasi kwamba hakuna mtu ambaye atakuwa anaweza kumgusa” Aaliyah alitulia kidogo na kuendelea;
“Baada ya kuanzisha umoja huo mwanamke huyo alitafuta namna sahihi ya kuweza kuotesha mizizi hususani kwenye ngazi za juu za serikali hivyo akamrubuni mdogo wa raisi wa zamani wa Tanzania Novack Nyangasa wakaingia kwenye mapenzi. Raisi alipokuja kupata habari hizo hakuwa tayari kukubaliana na jambo hilo hivyo wakaamua kumuondosha, walimuua kwa sumu na ndipo makamu wa raisi wa kipindi kile akaingia madarakani na taifa letu kuongozwa na mwanamke kwa mara ya kwanza. Yule raisi alikuwa ni pandikizi lao na hapo sasa wakaanza kuingiza watu wao kwenye mfumo hususani nafasi za juu zaidi kimamlaka ili waweze kuendesha kila sehemu ya taifa hili lakini tangu hapo watu hao wawili hawajawahi kuonekana hadharani tena huku ikisemekana kwamba kuna mtu mmoja ambaye anaweza kufanikisha kuwapata ila hajanitajia jina la mhusika mwenyewe” wenzake walibaki wameduwaa na kushangaa kwamba inawezekana vipi mwanasheria akawa na taarifa zote hizi ambazo zingine hata wao hawana? Walibaki wanakuna vichwa kwa sababu kazi iliyokuwa mbele yao ilikuwa ngumu isivyo kawaida.
“Tunamhitaji mwanasheria tena akiwa hai kuliko mtu yeyote yule kwa sasa” David aliongea kwa sauti ya juu ya matumaini ambayo haikuwa na uhakika na alichokuwa anakimaanisha.
“Kwanini?”
“Kwa sababu kama mtu huyu ana hizi taarifa na kama ni za kweli basi sisi tunahangaika kuwatafuta watu ambao hatutakiwi kuwatafuta. Ukijumlisha muunganiko wa historia ya maisha ya Edison, ambaye alidanganya kama Clyton Lameck, baadae akagundulika kwamba ndiye yule mtoto wa mwanasayansi Christian. Baadae akaingia kwenye mikono ya mchungaji ambaye naye alikuwa mpelelezi wa zamani na ndiye amemlea baada ya kukimbia kazi yake na kujipa mwonekano mwingine, baadae mtu huyu anauawa halafu katikati anajitokeza mwanasheria huyu! Maana yake huyu ndiye ana taarifa zote ambazo sisi tunazihitaji, huyu ndiye mtu ambaye anajua kila kitu na ana majibu yote ya mambo ambayo yametokea. Jioni ya leo pia ameonekana kwenye nyumba ya daktari Namaki Prasad kabla hajauawa na inadaiwa kwamba mke wa daktari yule ameongea naye kwa muda kidogo kabla ya mtu huyo kutoweka” sasa wote walisimama kwani kesi yao ingekuwa nzito mno bila kumpata mwanasheria huyo, waligundua kwamba yeye ndiye ambaye alikuwa daraja kwao.

UKURASA WA 57 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 58


“Amekubali kutusaidia kwa sharti moja” Aaliyah alitamka kauli hiyo kabla wenzake hawajakurupuka kwenye kumtafuta mtu huyo
“Tunakusikiliza”
“Amekubali kutusaidia kujua tunacho kihitaji na huenda kukifikia kama tukifanya kazi chini yake. Ukiacha hilo amesisitiza kwamba serikali inajaribu kuficha uchafu mwingi kuanzia sakata la kupotea kwa mwanasayansi Christian lakini hata wale makomando kumi ambao waliuawa na serikali moja kwa moja lakini sio hao tu watu wengine wataendelea kuuawa kama ambavyo mauaji kila siku yanatokea jijini hapa. Kulimaliza hilo inabidi tuyafumbue macho yetu na kuanza kuwashughulikia wahusika moja kwa moja na kufanya naye kazi kwa ushirikiano mkubwa ila kama tukigoma basi amenihakikishia kwamba hatakuwa na uwezo wa kutulinda kwa sababu tutakufa wote” mazungumzo yalizidi kuwa siriasi tofauti na walivyokuwa wameyaanza. Maelezo hayo yalimfanya Mbatina kucheka, ni mtu ambaye alizipenda mno sifa nazo zikamkubali hivyo kwake ilikuwa ni kama kichekesho.
“Yaani sisi tufanye kazi chini ya huyo mpuuzi? Hilo ni jambo ambalo haliwezekani, kama akigoma kutusikiliza kwa njia ya amani basi njia ya lazima itatumika hatuwezi kumbembeleza mpuuzi mmoja kama huyo wakati tuna mamlaka yote ya kufanya lolote kwa ajili ya taifa hili”
“Na vipi kama maelezo yake yapo sahihi?” Aliuliza Jumapili ambaye bila shaka alionekana alipenda kuyachambua mambo hayo kiweledi zaidi.
“Unamaanisha kwamba kama wakubwa ndio ambao wapo nyuma ya haya mambo?” wote waliguna kwa sababu hilo lilikuwa jambo lingine.
“Mhhhhh tunapo elekea na hili jambo linaweza kututokea puani sisi wenyewe, kama yanayo zungumzwa ni kweli! Basi hata huo umoja ambao unasemwa hapa upo na upo chini ya usimamizi wa wakubwa. Hili linatupa uhalisia kwamba hata mkurugenzi lazima atakuwa na hizi taarifa na kama anazo kwanini hajawahi kutupatia dodoso juu ya mambo haya? Tunako elekea nadhani tunaenda kuchagua kati ya kuusimamia ukweli halisi hata kama unaumiza ama kuamua kuufukia ukweli na kulinda maslahi ya wakubwa” Ruben aliongea kwa sauti ya kukata tamaa, jambo hilo kadri walivyokuwa wanazidi kulichimba kiundani basi waliona kabisa linaenda kuwa gumu kwa upande wao.
“Nadhani inatakiwa tumshirikishe mkurugenzi tujue yeye ana maoni gani juu ya hili”
“Mpaka hapa sina imani naye kabisa, tunaweza kumshirikisha na bado atahitaji mambo yafanyike kwa matakwa yake”
“Angalia huo mdomo wako Jumapili, usije ukairudia tena kauli yako, unaanza kumtuhumu bosi kwa hizi nadharia ambazo tunazitengeneza midomoni?” Aaliyah aliongea kwa sauti ya ukali kidogo, kuacha kumuamini bosi wao ingekuwa dosari nyingine kwao.
“Na vipi kama hizi taarifa ni za kweli?” lilikuwa swali lingine kutoka kwa Jumapili.
“Tuachane na hizi habari kwa muda, David umefikia wapi kufuatilia lile jambo ambalo lilitokea uwanja wa ndege?”
“Yule binti alidanganya jina lake kujiita Leyla Patrick, jina lake halisi anaitwa Nicola Aidan Semzaba. Huyu binti, kaka yake ni miongoni mwa wahanga ambao walifia kule somalia ambao walikuwa pamoja na Edison. Kwahiyo kwa nadharia hizo ni kwamba hakutekwa bali ni yeye alijikamatisha”
“Kwanini afanye hivyo?”
“Nimetengeneza nadharia kwamba huenda alisikia kwamba kuna watu wanamtafuta muuaji wa kaka yake ambaye ni Edison hivyo akahitaji kuweza kuungana nao ili aikamilishe kazi ya kulipa kisasi kwa mtu huyo”
“Unataka kuniambia kwamba kila ambacho kilitokea pale ni yeye alikipanga?”
“Sina uhakika ila mpaka sasa naweza kusema hivyo”
“Na maisha yake ya nyuma yapoje?”
“Amewahi kupata mafunzo ya kikomando”
“Whaaaat?”
“Ndiyo hivyo ni mtu makini ambaye anajua kila hatua ambayo anaipiga”
“Na kuhusu Damasi Kazimoto ni mtu alitumia sura yake bandia au kuna mchezo umefanyika kuhusu kifo chake?”
“Nina mashaka kwamba huenda yupo hai, kama kuna mtu alihitaji kuishi kwenye sura yake kwa siri basi asingejitokeza hadharani namna ile kwa sababu kuonekana kwake kungeleta utata”
“Kwahiyo unahisi ni yeye mwenyewe?”
“Ndiyo”
“Sasa kwanini afanye vile kama ni yeye na aliponaje?”
“Teknlojia ni kitu cha hatari, kama ni yeye kuonekana kwake huenda alijiamini kwamba watu wao wangezima kamera ila kwa bahati mbaya mambo yameenda nje na matarajio yao”
“Tunafanyaje kuhusu hili?”
“Nadhani inabidi tuanzie kwao kufanya uchunguzi”
“Kwa familia yake?”
“Ndiyo”
“Nadhani kwa sasa tuanze na hili la mwanasheria kwanza, kesho mmoja ataenda kwa akina Damasi wakati huo wengine tutaenda kwa mwanasheria, asubuhi nitaenda kuongea na mkurugenzi ili nimuulize baadhi ya maswali kama atakuwa na taarifa za kutosha kuhusu mambo hayo huenda anaweza kuwa na msaada mahali. Kwa sasa mnaweza kuondoka” kikao ambacho kiuhalisia bado hawakupata ule mwafaka ambao walikuwa wanautaka kilifika mwisho, kila mtu aliondoka kichwa chake kikiwa na mambo mengi mno.
Nicola tangu alipokutana kwa mara ya kwanza na mwanasheria Jack kwenye maisha yake akili yake ilikuwa inaenda mbio isivyokuwa kawaida, ilikuwa inaenda mbio kwa sababu alikutana na mambo ambayo moyo wake bado haukuwa ukiamini kama yalimtokea ni yeye au alikuwa ndotoni. Mwanaume yule alikuwa mkatili mno mbele yake, kwa namna alivyofanikiwa kuwaua wale vijana ambao alikuwa ameenda nao kule, hali ile ilimtisha isivyokuwa kawaida, yule mtu hakuwa kama ambavyo alikuwa akimkadiria yeye, yalikuwa maji marefu kwake kuyaogelea.
Mara nyingi alizoea kumuona mwanaume yule akiwa ndani ya suti amesimama mahakamani au kwenye vyombo vya habari akiwa anaichambua sheria kwa umakini mkubwa ila kwa siku ile ilijengeka sura tofauti kabisa kwneye macho yake na kuamini kwamba hakuna ambalo alikuwa analifahamu kutoka kwa mtu huyo. Hilo halikumshangaza zaidi, jambo ambalo lilimsafirisha mbali kimawazo ni ile sura ambayo aliiona kwa mara ya mwisho, sura ya mtu ambaye yeye alikuwa akimsaka mno kwenye maisha yake, sura ya mtu ambaye alikuwa tayari kupoteza chochote hata kufilisika ili kuweza kumpata na kumuua.
Siku ile sura ile ilikuwa mbele yake lakini alishindwa kufanya chochote, alikuwa na nafasi ya kufanya hivyo ila uwezo wake ukawa mdogo huenda ni kwa sababu ya kupigwa na butwaa ya kumuona kwa mara ya kwanza tena kwenye mazingira ambayo hakutarajia lakini mwanaume yule alimhakikishia kwamba hayupo tayari kufa kwa wakati ule kwa sababu kuna majukumu ambayo alikuwa hajayakamilisha bado na wakati ambao yangekuwa tayari huenda wangekuwa na mazungumzo mengine. Majukumu yapi hayo? Kivipi mtu huyo aishi kwenye sura ya mtu mwingine na hio sheria alijifunzia wapi kwa sababu muda mwingi wa historia yake alionekana kuwa mtu wa jeshi? Alichanganyikiwa Nicola.
Mwanaume yule licha ya kumshangaza kwa ile sura ambayo alimuona nayo pale lakini pia alimuongezea mzigo mwingine mkubwa kwenye akili yake, mzigo wa taarifa ambazo hakuwahi kuzijua mwanzo. Kuhusu ukweli wa kifo cha kaka yake, alimhakikishia kwamba yeye hakuhusika kwa sababu hata yeye pia alitakiwa kufa ila ulikuwa mpango wa serikali chini ya watu ambao walikuwa wanafanya naye kazi kwa wakati huo. Hilo ndilo jambo ambalo lilikuwa linamchanganya zaidi kichwa, kwamba alidanganywa? Kwanini adanganywe na kwa malengo yapi hasa? Alijicheka mwenyewe kwani alikuwa anaona anaelekea kuwewuka, jambo hilo liligoma kabisa kwenye akili yake kwamba alikuwa amedanganywa, lakini kama hakuwa amedanganywa na yeye kabisa alikuwa anaenda kumuua mwanaume yule, kwanini alimuacha yeye hai wakati alikuwa na nafasi ya kumuua? Kwamba Edison alijihisi hatia ya kumuua kwa sababu alimuua kaka yake? Jibu lilikuwa hapana, mwanaume kama yule anapo ifanikisha kazi yake hawezi kufanya makosa ya kijinga namna hiyo hivyo kwenye moyo wake akahisi kuna mambo ambayo hakuwa akiyajua bado hivyo alitakiwa kuyafahamu.

UKURASA WA 58 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 59

Aliinua simu yake kuelekea kwa mtu ambaye aliamini kwamba anaweza kumjibu baadhi ya maswali yake, Saimon. Huyu alikuwa ni miongoni mwa vijana wa kuaminika kwa madam Kate, alihitaji kukutana na mwanaume huyu kwani kuna maswali ya msingi alihitaji kumuuliza.
“Saimoni uko wapi?”
“Naongea na nani?”
“Nicola”
“Umeipata wapi namba yangu?”
“Tunafanya kazi pamoja, acha maswali ya kijinga”
“Unataka nini?”
“Uko wapi?”
“Tutaongea kesho”
“Ni jambo la mhimu kwenye hii kazi yetu hivyo tafadhali naomba unielekeze ulipo nikufuate muda huu”
“Shiit! Njoo Club poison mtaa wa Ohio. Ukifika mapokezi ulizia Sai the nightmare utaletwa nilipo” simu ilikatwa na mara moja mrembo huyo akaingia kwenye gari yake kuelekea ilipo club hiyo. Alitumia dakika kumi na nane pekee kutoka Mikocheni ambapo alikuwepo wakati huo kuweza kuwasili ndani ya club hiyo ambayo ilikuwa imechangamka mno.
Aliendesha gari yake mpaka ilipokuwepo parking kubwa, alizima gari na kushuka kwa mwendo wa madaha, alikuwa mrembo na alipendeza mno kiasi kwamba kila mwanaume ambaye alikuwa anamuona basi mate ya uroho yalikuwa yanamtoka kwa tamaa za kifisi lakini hakuwa na muda nao bali alijiendea zake ndani. Walinzi hata hawakuhangaika naye, uliwahi kusikia wapi warembo wanalipia gharama kuingilia sehemu hizo! Warembo ni bure bwana!
Aliingia mpaka mapokezi, ndani kulikuwa kumewaka usingehisi kwamba muda ulikuwa umeenda. Watu walikuwa wamejichanganya kucheza mziki ambao ulikuwa unapigwa kwa sauti za juu kiasi kwamba hata kusikiana kwa wale ambao walikuwa karibu na mziki ilikuwa ni changamoto.
“Karibu mrembo” alitabasamu baada ya kukaribishwa kwa tabasamu la sauti ya kiume
“Sai the nightmare nampata wapi hapa?”
“Una appointment naye?”
“Ndiyo, anajua kwamba nipo hapa”
“Huwa hapendi kabisa usumbufu, Richie mpeleke huyu” aliitwa kijana ambaye alikuwa karibu na bila shaka hata yeye hayo mazungumzo aliyasikia vizuri kabisa. Waliondoka hapo na kuelekea eneo ambalo liliandikwa VIP, huko kulikuwa na mziki mzito lakini haukuwa wa kuumiza, kila mtu alikuwa anaendelea na hamsini zake huku kwenye baadhi ya vyumba akiwa anawaona watu wakifanya mapenzi hadharani, haikuwa biashara yake kufuatilia mambo hayo kwani hayakuwa yakimhusu, kama angehitaji ustaarabu basi alitakiwa kwenda kanisani ama msikitini.
Maisha yaliwakubali watu, walikuwa wanamwaga radhi na kusahau shida za dunia kwa muda. Kijana huyo ambaye aliitwa Richie alimuonyeshea kidole sehemu ambayo alitakiwa kwenda kisha yeye akatoka zake kurudi mapokezi, eneo ambali alionyeshwa lilikuwa na uwazi mpana ambapo mbele yake kulikuwa na walinzi watatu waliokuwa eneo hilo. Alitembea taratibu akiwa anasogea bila presha lakini alipo karibia kuufikia mlango ambao alipaswa kuingia alizuiwa na mlinzi mmoja. Alichukizwa na kitendo hicho hali ambayo ilimfanya kuuvuta mkono wa mlinzi huyo na kumkutanisha na kiganja chake kwenye eneo la shingo, mlinzi huyo aliguna kwa maumivu kwa sababu ilikuwa ni ghafla hakujiandaa na hali hiyo, alichotwa mtama na kupigwa goti la kifua ambalo lilimzoa mpaka mlangoni.
Mwenzake mmoja aliichomoa bastola na kuhitaji kumnyooshea mwanamke huyo, buti lilitua kwenye goti lake ambapo aliinama chini bila kupenda, kuinama kwake kuliusiogeza uso wake karibu na alipokuwa Nicola ambaye aliurusha mguu wake na kiatu chake kikaufunika uso wa mwanaume huyo ambaye kwa bahati mbaya alidondokea kisogo chake na kuzimia hapo hapo. Aliyekuwa amebakia mmoja alihitaji kuinyoosha bastola yake kwani alitumia muda mwingi kushangaa ambacho kilikuwa kinatokea hapo akajisahau lakini alikuwa amechelewa, alikuwa anaangaliana na bastola usoni kwake hivyo akawa mpole.
“Nipeleke kwa bosi wako” hakuwa na namna zaidi ya kuongoza ndani ambako alimkuta Saimoni akiwa amezungukwa na wanawake wawili ambao wote walikuwa uchi, walikuwa ni wanawake warembo mno lakini pesa iliwafanya kutokuwa na thamani mbele ya Saimoni pesa ilikuwa inaununua utu wa watu, jiji lina joto kali nani ambaye angeweza kukubali kubaki kwenye umaskini na mwili mzuri anao? Nicola alibaki anaangaza angaza humo ndani ya jinsi chumba hicho kilivyokuwa kimepambwa kwa ustadi mkubwa.
“Kipi kimekuleta huku kiasi kwamba unavamia na kuharibu starehe za watu?”
“Hii ndiyo sehemu ambayo huwa unakuja mara kwa mara?”
“Maisha yangu binafsi hayakuhusu, ongea haraka nataka nikalale na hawa warembo”
“Nahitaji tuwe wawili tu kwa sababu nina maswali binafsi ambayo nahitaji majibu yake” Saimoni aliwaangalia warembo hao ambao walitoka humo ndani mara moja.
“Nakusikiliza”
“Una muda gani tangu uanze kufanya kazi na madam Kate na je unamfahamu kwa sura?”
“Unaniuliza maswali ambayo unajua kabisa kwamba siwezi kukujibu”
“Saimon najua hilo lakini jambo ambalo naliongelea hapa ni jambo la familia yangu, tafadhali sana nahitaji msaada wako kwa sababu najua wewe ni mtu ambaye unaweza kunisaidia kwa hili. Kaka yangu aliuawa na kesi akapewa Edison lakini kwenye ufutiliaji wangu nahisi kama kuna vitu nafichwa hapa na huenda nafanya maamuzi ambayo sio sahihi kabisa hivyo nahitaji kuujua ukweli”
“Ukweli upi huo labda wakati unajua kabisa huyo ndiye mtu ambaye alimuua kaka yako na makomando wenzake?”
“Vipi kama huu ni ukweli ambao kuna watu waliupika ili dunia iamini hivi lakini sio ukweli wenyewe?”
“Una maana gani Nicola?”
“Yule mtu anadaiwa kuwaua wenzake, sawa lakini haiingii akilini, alihusikaje kwenye mauaji ya wenzake wote ambao walienda Somalia na Kongo? Kwamba aliwauza wa Kongo na wale wa Somalia aliwaua mwenyewe? Jibu linaweza kuwa kweli kama alikuwa na sababu za msingi za kufanya hivi, je huyu mtu alikuwa na sababu ipi? Hakuna sababu yoyote ya kumfanya yeye awaua sasa ina maana kwamba alijisikia tu kuwauza na kuwaua na kama alifanya hivyo aliwauza kwa nani hasa? Jibu haliji kabisa, mtu ambaye alimuacha mkewe mjamzito tena mke wa ndoa ambaye kwa rekodi ni kwamba alimpenda sana hawezi kufanya jambo la kipuuzi namna hii labda kama kuna sababu nyuma yake ambayo mimi siijui unaweza ukanisaidia!” hayo maelezo kidogo yalimshtua Saimon kwani hakuyatarajia wakati kama huo.
“Hahaahaha Nicola, usiniambie kwamba zile porojo za yule mwanasheria kwenye mitandao zimekuingia kichwani?”
“Sina hakika na hilo lakini kwa rekodi ni kwamba mwanasheria yule hata siku moja hakuwahi kutoa habari za uongo wala za kubahatisha, mara nyingi habari ambayo anaiweka kwenye mitandao huwa ni ya kweli. Sasa vipi kama alicho kiongea ni kweli?”
“Nicola acha kuwaza mambo ya kijinga, huyu mtu ni msaliti kwa taifa hili na anatafutwa popote pale alipo na akikutwa inatakiwa kuuawa nadhani biashara yetu sisi na wewe itakuwa imeishia hapo kwa sababu utatakiwa kuurudisha mzigo kwa namna yoyote ile”
“Saimon ni kweli huyu mtu alihusika kwenye mauaji ya kaka yangu?”
“Ndiyo”

UKURASA WA 59 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 60

“Lazima kutakuwa na uthibitisho wa hizi habari, nahitaji kuona huo uthibitisho wa taarifa hizi” Saimon alibaki anamwangalia mwanamke huyo kwa mashaka.
“Kama ukinielekeza kwa mtu ambaye anaweza kunipa uthibitisho basi mimi nitakuamini wewe moja kwa moja na sitauliza tena hizi habari juu yenu ila kama utashindwa basi sitakuwa na imani na nyinyi tena na huenda hata mzigo wenu msiupate kwa sababu kunidanganya inaweza ikapelekea mimi kupotea na mzigo msije mkaupata”
“Anaitwa Maliki Jamei. Anaishi Upanga, mita mianane kutoka ilipo ofisi ya mkuu wa majeshi nyumba namba 77” Nicola alinyanyuka na kuanza kutembea, alipo ufikia mlango aligeuka ambapo alikuta bado Saimon amemkazia uso wake vibaya mno.
“Ni kweli kwamba Madam Kate ana mtoto ambaye alimpoteza?” ni swali lingine ambalo Saimon aliona uelekeo wa mwanamke huyo unaenda kuwa mbaya.
“Sina taarifa zozote kuhusu maisha binafsi ya bosi na sijawahi kuonana naye hata siku moja”
“Sawa Saimon, nina taarifa zako nyingi hususani za wewe kuwa moja kati ya wadunguaji hatari hapo zamani kwenye jeshi la nchi hii, sijui ni kitu gani hasa kilikupata mpaka ukaishia kwenye kazi ya hatari kama hii” maneno yalimgusa mno kwenye moyo wake na kumpatia hasira kwani mwanamke huyo alikuja kumharibia siku yake. Nicola hakukaa hapo akatoweka kuelekea huko ambako alikuwa ameelekezwa.
Saimon jasho lilikuwa linamtoka taratibu, alibamiza meza chini kwa hasira mpaka ikavunjika, Nicola alianza kuhoji maswali ambayo kiuhalisia hakutakiwa kuuliza. Saimon aliitoa simu yake akiwa anahema kwa hasira na kuipiga mahali.
“Bosi ameanza kuuliza maswali mengi akihitaji kutupima imani na ametishia kama nisingemwambia ukweli basi anaweza kupotea na mzigo”
“Maswali gani?”
“Anataka kuujua ukweli kuhusu kaka yake”
“Umamjibu nini?”
“Nimemuelekeza kwa Maliki ili aendelee kuwa na imani na sisi”
“Maliki akibanwa anaweza kuongea ukweli, huu upuuzi hautakiwi kutokea”
“Nimekupigia simu ili nipate ruhusa yako ya kumuua Maliki. Najua akifika kule atakuwa na imani na sisi hata kama Maliki atakufa atakuwa na uhakika kwamba nilimpa taarifa za kweli”
“Muue Maliki kabla hajaongea chochote kwake na kama akirudi kwako mwambie kwamba hakuna unalo lijua kwa sasa”
“Sawa bosi” maelezo yalimtosha mwanaume huyo kutoka ndani humo na kuwahi eneo la tukio kumuua huyo mtu wake kabla hajaropoka kwani aliamini kwamba kijana huyo kama angebanwa basi kuna siri ambazo angezitoa na siri hizo alitakiwa kufa nazo kwenye moyo wake. Maliki alikuwa moja ya vijana wao ambaye alikuwa anatumika kuhifadhi taarifa zao za siri.
Nicola alifika sehemu ambayo alikuwa ameelekezwa, alipaki gari yake umbali kadhaa kutoka eneo hilo. Alitembea kwa mguu wake na kufika ndani ya eneo hilo ambalo nyumba ilikuwa ndogo tu lakini ya ghorofa moja na ilijengwa kwa ustadi mkubwa mno. Aliruka kwenye fensi na kurukia ndani ya eneo hilo ambapo aligundua kwamba nyumba hiyo haikuwa na mlinzi wa nje ila alikuwa na uhakika kwamba mwenyeji wake alikuwa yupo ndani kwa sababu chumba cha juu mwanga ulikuwa unaonekana kwa mbali.

Alifungua dirisha moja la kioo kwa kisu chake na kudondokea ndani akiwa na bastola yake mkononi, alitembea kwa tahadhari mpaka alipo sikia sauti ya kishindo juu ya kile chumba ambacho kilikuwa kinatoa mwanga ndani ya nyumba hiyo. Hali hiyo ilimfanya akimbilie kwa kasi kwa sababu alihisi kwamba kulikuwa na tatizo, ni kweli wakati anafika ndani ya chumba hicho ambacho aliingia baada ya kuuvunja mlango wa mguu wake, alimkuta mhusika ambaye alimfuata hapo akiwa anagalagala chini na hakuchukua hata sekunde kumi akawa anapoteza maisha.
Alishangazwa mno na jambo hilo damu zikiwa zimesambaa chini kwenye sakafu kwa wingi. Alimtazama mwanaume huyo na kugundua kwamba alipigwa risasi kwenye koo lake ndiyo maana alidondoka chini kwa nguvu na kuvunja meza ambayo ilikuwa pembezoni mwa kitanda. Aliyainua macho yake kuelekea dirishani, hapo aligundua kwamba ndipo risasi ilipo pitia, palikuwa na tobo na ndipo ambapo ilipenyea na kwenda kuyachukua maisha ya Maliki. Kwa namna risasi hiyo ilivyo pigwa mtu wa kawaida asingeweza kufanya hivyo hivyo ni lazima alikuwa mdunguaji wa ngazi ya juu sana ambaye alifanikisha hilo, alianza kuwa na hisia mbaya na Saimoni hivyo ikamlazimu kumpigia simu haraka ili ajue kama yupo kwenye club ile na kama hayupo kule maana yake mhusika angekuwa ni yeye. Simu iliita kidogo na kupokelewa ambapo kwa mbali alisikia sauti ya muziki.
“Saimoni uko wapi?”
“Nipo ulipo niacha, siwezi kuwaacha warembo hawa mapema namna hii”
“Una uhakika haujatoka huko?”
“Ndiyo, vipi kwani?”
“Maliki ameuawa na mdunguaji”
“Acha utani”
“Nipo kwenye nyumba yake hapa saivi”
“Lakini si umefanikiwa kupata ambacho unakihitaji?”
“Hapapa, hili tukio limetokea kabla sihafanikisha hilo labda niangalie ndani kwake kama nitapata kitu”
“Watu wa hivyo taarifa zao zinahifadhiwa kichwani Nicola sio kwenye nyumba, ondoka hapo haraka kabla polisi hawajafika” Simu ilikatwa na wakati huo Saimoni alikuwa kwenye gari yake ambamo alifungulia mziki mkali ili aonekane yupo club, alikuwa anaendesha gari yake kwa kasi ili awahi eneo hilo ili hata kama Nicola angerudi basi asinge mshtukia kwa lolote. Ni kweli baada ya muda mfupi alisikia ving’ora vya polisi ambavyo vilimshangaza kwani ilikuwa ni ghafla mno, alishangaa polisi hao walipata wapi taarifa mapema yote hiyo? Hata hivyo hakupata majibu zaidi ya kuamua kutoweka ndani ya hilo eneo.

UKURASA WA 60 unafika mwisho.
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 61

SURA YA SITA
Kutoka gazeti la THE TRUTH habari zilisambaa tangu asubuhi ya mapema kwamba mwanasheria JACK THE LAWYER usiku wa saa tano angeongea na wananchi, ilikuwa ni siku ambayo hakuna mtu alitakiwa kuikosa taarifa yake hiyo kutokana na umuhimu mkubwa ambao ilikuwa nayo. Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya siku ambayo kila mtu alibaki anaiongelea kila sehemu, watu wengi walikuwa na hamu kubwa ya kusikia habari hiyo kutoka kwenye kinywa chake kwa kuwa mwanasheria huyo hakuwahi kuwa na jambo dogo kila anapokuwa anajitokeza hadharani kuongea.
Siku zote hausimami na usiku wa deni haujawahi kuchelewa kufika na ndivyo ilivyokuwa kwa watanzania. Kwa ambaye alikuwa na simu yake basi alihakikisha bando linakuwa la kutosha, kwa watu ambao walikuwa karibu na televisheni zao na mitandao mbalimbali walikuwa makini mno kusubiria taarifa ya mwaasheria huyo hata mamlaka za usalama zilikuwa makini kuweza kuisubiria taarifa hiyo ili wajue mtu huyo alihitaji kufanya nini asije kuharibu amani ya nchi.
Alikuwa mtu wa kwenda na muda isivyo kawaida hali ambayo ilifanya saa tano kamili awepo mbele ya kamera yake kwenye chumba ambacho hakuna ambaye alifanikiwa kujua kwamba alikuwa wapi kwa wakati huo. Mwanaume huyo alitokea mbele ya kamera akiwa amependeza kwa suti ya blue ambayo ilikuwa na mistari myeusi, alikaa kwenye kiti kwa dakika tano bila kuongea jambo lolote lile, alijiweka sawa na kuisogeza kamera karibu kabisa na alipokuwa amekaa;
“Moja kati ya vitu ambavyo nitajivunia hata pale ambapo nitakuwa ndani ya jeneza kwenye safari yangu ya mwisho, ni kuzaliwa Tanzania. Kuzaliwa ndani ya taifa hili ni moja ya jambo bora kuwahi kutokea kwenye maisha yangu mimi ndiyo maana siku zote nimekuwa adui mkubwa wa watu ambao wamekuwa wanapambana kuweza kulirudisha nyuma taifa letu hili kwa namna moja ama nyingine.;”
“Nchi hii inawahitaji watu wenye maono makubwa, inawahitaji vijana shupavu kwa sababu ndipo ilipo nuru ya kesho ya taifa hili, kupitia vijana ndipo ambapo kama taifa tunaweza kufika mahali ambapo tumekuwa tukipasoma tu kwenye vitabu ila kwa bahati mbaya taifa letu linawachukia watu wenye uwezo mkubwa. Watu ambao wana uwezo wa kulipeleka mbele taifa letu wanachukuliwa kama hatari hususani kwa wale mazuzu ambao wamedandia nafasi kubwa serikalini wakati hawastahili kuwa hapo wakiamini kwamba kama vijana hawa wakipewa nafasi basi watazibeba nafasi zao. Unahisi tunaweza kufika popote kama taifa kwa akili hizi? Hapana asilani!?”
“Nimezaliwa kwenye familia ya kawaida tu ambayo naweza kusema ilinifunza mabaya na mazuri tangu siku tu natoka tumboni mwa mama yangu. Maisha yangu yamenifunza ukatili nikiwa bado mdogo lakini sikuruhusu kuwa katili kwa watu wengine kwa namna yoyote ile ndiyo maana naweza kusimama hapa na kujisifia kwamba mimi ni miongoni mwa watu ambao wamejitahidi kwa kila namna kuwa bora mbele ya bendera ya nchi yangu, hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kunilipa mimi, ni Mungu pekee atafanya hivyo siku ya kugawa thawabu kwa wale ambao ni wake”
“Kupenda kwangu kulitumikia taifa langu na kuweza kuzipigania rangi nne za bendera ya taifa langu ndiko ambako kulinifanya nilazimike kulipenda jeshi bila kupenda mwisho wa siku nikazamia huko. Jeshi sikuwahi kulipenda kwenye maisha yangu ila nilifanya hivyo ili niweze kuishi na kujilinda mwenyewe lakini pia kupigania haki za watu wengine ila baada ya muda niligundua kwamba jeshi pekee haliwezi kuleta hicho ambacho mimi nakitaka, ukawa mwanzo wangu wa kuipambania sheria pia”
“Niliamini kwamba nikiwa na hivyo vyote viwili basi ningekuwa na uwezo wa kupambania haki za wengi hivyo nilisoma kwa nguvu na kwa hasira zote mpaka nilipofanikiwa kumaliza shule ya sheria na rasmi nikavikwa vazi hilo ambapo mpaka sasa historia itaandika kwamba mimi ndiye mwanasheria ambaye sikuwahi kupoteza kesi yoyote ile mbele ya mahakama na ndiye mwanasheria ambaye sijawahi kudhulumu haki ya mtu ambaye anastahili kuipata kwa gharama yoyote ile”
“Kama nilivyosema mwanzo watu kama mimi hawapendwi kwa sababu mfumo hauwapendi mashujaa, jambo hilo ndilo lilikuwa chanzo cha umauti wangu ambao huenda mtauelewa baada ya masaa kadhaa kupita kuanzia sasa. Watu wengi hawaujui ukweli wa maisha yangu, mimi ni mtoto wa damu kabisa wa mwanasayansi Christian Edison ambaye aliuliwa na serikali ya nchi hii kwa kigezo cha kudai kwamba anapelekwa Israeli kufanya kazi na MOSSAD kama makubaliano ya nchi hizo mbili lakini haikuwa kweli, baba yangu aliuawa kwa sababu alikuwa na akili kuliko binadamu yeyote kwenye taifa hili”
“Nimekuzwa kwenye mazingira ya hatari mno kiasi kwamba ililazimika mimi kupotezwa kumbukumbu ili nisikumbuke yale ambayo yalitokea nyuma na habari mbaya zaidi hata mama yangu mzazi alinikimbia na huenda ndiye sababu kubwa ya baba yangu kufa pamoja na familia yangu yote. Licha ya hayo yote bado niliamua kulipambania taifa langu kama komando mwenye mafunzo ya juu lakini kuna watu ambao waliona uwepo wangu mimi na wenzangu ni hatari hivyo wakaamua kutuua” Aliongeza kuongea maneno hayo huku akiivua ile sura yake ambayo aliishi nayo kwa muda mrefu ambayo watu walimzoea nayo akifahamika kama Chrispin Mwambano na kubaki na ile sura ya Edison Christian ambaye baadhi ya watu walimjua kama Clyton Lameck.
“Iliamriwa niuawe kwa sababu nilikuwa hatari kwao lakini wasingeweza kuniua pekeyangu ilitakiwa waue kikosi kizima ambacho mimi ndiye nilikuwa nikikiongoza. KILL ON MISSION (KOM) ndilo lilikuwa jina la kikosi changu, kikosi ambacho jumla tulikuwa makomando kumi ila kwa bahati mbaya ni mimi pekee ambaye nilifanikiwa kuishi. Watu hawa walituma kikosi cha pili nyuma kwa madai kwamba kinakuja kutupatia msaada lakini watu wale walikuja kutushambulia kwa risasi ni bahati tu wakati wanafika simu iliita ndani nikarudi kuipokea na wakati nikiwa naongea na mtu kwenye simu ambaye alikuwa ananipa taarifa za kunitaka nitoke na wenzangu pale kwani nchi imetusaliti, nilisikia milio ya risasi ikanilazimu nitoke nje. Nilifanikiwa kuwaua watu wale wote ila kwa bahati nyingine mbaya ni kwamba walitumwa watu wengine watatu ambao walitumwa kuhakikisha kazi inakamilika na ndipo nilipopigwa risasi mbili (alifunua suti yake na shati kifua kilikuwa na makovu mawili) wakati nikiwa kwenye hatua za mwisho za kuishi kwangu, alitokea mwanaume nisiye mjua na kunisaidia ambapo sikuwa na fahamu ila niligundua kwamba nipo hai baada ya kuamka kwa mara nyingine”
“Wakati naamka nilifutiwa kumbukumbu zote kichwani mwangu, sikujua ni nani ambaye aliniokoa wala nilikuwa wapi na kufanya nini kitu pekee ambacho nilikuwa nakikumbuka ni sura ya mtu ambaye alinilea. Mtu huyo alinitaka nikaishi maisha ya chini mno huko Kigogo mwisho huku nisijue ni kwanini nilitakiwa kufanya hivyo kwani sikuwa na kumbukumbu. Nimeyaishi maisha hayo mpaka nilipo vamiwa kwa mara nyingine na watu ambao walihitaji kuyachukua maisha yangu ndipo ambapo nimekuja kuujua ukweli mwingine baadae”
“Ukweli wa kwamba kutoka na na lile ambalo lilitokea kule Somalia hawakuukuta mwili wangu hivyo wakaamua kujumlisha kwamba huenda nilipona na kama nilipona basi wakaamua kunipa kesi nzito ya kuhusika na mauaji ya makomando wenzangu, kesi ambayo waliliaminisha taifa zima kwamba mimi ndiye chanzo wa kila jambo lakini haukuwahi kuwa ukweli kwa sababu ukweli ni kwamba hata mimi nilitakiwa kufa ila nikaishi kwa neema za mwenyezi Mungu. Hilo halikutosha wakati wananituma huko na kikosi changu walimuua na mke wangu ambaye alikuwa mjamzito akikaribia kujifungua. Huenda kila mtu anatamani kuijua sababu haswa ya msingi zaidi ya haya yote kutokea”
“Kuna mambo sitayaongea hapa kwa sababu ya kulinda usalama wa taifa hili ila nchi haipo salama kabisa, watu wanakufa na kila siku zinavyozidi kwenda mbele basi watu wataendelea kufa zaidi. Nchi inaongozwa na watu ambao sio watanzania, sio kwamba viongozi wa juu hawajui au mamlaka za juu hazitambui hilo, lahasha! Bali ni miongoni mwa vibaraka wa hao watu. Taifa lilianza kuingia dosari baada ya raisi Justin Nyangasa alipo uawa kwa sumu aina ya Polonium 204 kisha kuchomwa aina nyingine ya sumu ambayo iliyaondoka maisha yake mara moja wakaja kudanganya mbele ya vyombo vya habari”
“Juzi hapa nilitangaza kuishtaki serikali na moja kati ya makosa yao ambayo walitakiwa kuyatolea majibu ni hilo kwa sababu muuaji mwenyewe alikuwa bado yupo hai. Dokta Namaki Prasad ndiye ambaye aliikamilisha kazi hiyo ya kumuua raisi Nyangasa na jana nilienda kwake ili niweze kumuomba asaidie kutoa ushahidi kwa juu ya jambo hili lakini kwa bahati mbaya nilimkuta mkewe na watoto wake tu yeye akiwa ameuawa tayari. Wamemuua ili kuondoa na kulinda ushahidi. Hivyo mnatakiwa kujua kwamba haya yote ambayo yemetokea na yanayo endelea kutokea hakuna mchawi wa kumlaumu bali serikali wenyewe ndio wanahusika moja kwa moja”

UKURASA WA 61 unafika mwisho.
 
SIMULIZI TUTAIMALIZA HAPA...

Ila mwa wale wa kumaliza siku moja wikiendi yako unamalizia kwa 1500 upate burudani.


0621567672 (HALOPESA)

0745982347 (M-PESA)

0714581046 (TIGO-PESA)

0689440143 (AIRTEL MONEY)

36316279 (LIPA NAMBA (M-PESA) inapokea mitandao yote)

FEBIANI BABUYA
 
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 61

SURA YA SITA
Kutoka gazeti la THE TRUTH habari zilisambaa tangu asubuhi ya mapema kwamba mwanasheria JACK THE LAWYER usiku wa saa tano angeongea na wananchi, ilikuwa ni siku ambayo hakuna mtu alitakiwa kuikosa taarifa yake hiyo kutokana na umuhimu mkubwa ambao ilikuwa nayo. Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya siku ambayo kila mtu alibaki anaiongelea kila sehemu, watu wengi walikuwa na hamu kubwa ya kusikia habari hiyo kutoka kwenye kinywa chake kwa kuwa mwanasheria huyo hakuwahi kuwa na jambo dogo kila anapokuwa anajitokeza hadharani kuongea.
Siku zote hausimami na usiku wa deni haujawahi kuchelewa kufika na ndivyo ilivyokuwa kwa watanzania. Kwa ambaye alikuwa na simu yake basi alihakikisha bando linakuwa la kutosha, kwa watu ambao walikuwa karibu na televisheni zao na mitandao mbalimbali walikuwa makini mno kusubiria taarifa ya mwaasheria huyo hata mamlaka za usalama zilikuwa makini kuweza kuisubiria taarifa hiyo ili wajue mtu huyo alihitaji kufanya nini asije kuharibu amani ya nchi.
Alikuwa mtu wa kwenda na muda isivyo kawaida hali ambayo ilifanya saa tano kamili awepo mbele ya kamera yake kwenye chumba ambacho hakuna ambaye alifanikiwa kujua kwamba alikuwa wapi kwa wakati huo. Mwanaume huyo alitokea mbele ya kamera akiwa amependeza kwa suti ya blue ambayo ilikuwa na mistari myeusi, alikaa kwenye kiti kwa dakika tano bila kuongea jambo lolote lile, alijiweka sawa na kuisogeza kamera karibu kabisa na alipokuwa amekaa;
“Moja kati ya vitu ambavyo nitajivunia hata pale ambapo nitakuwa ndani ya jeneza kwenye safari yangu ya mwisho, ni kuzaliwa Tanzania. Kuzaliwa ndani ya taifa hili ni moja ya jambo bora kuwahi kutokea kwenye maisha yangu mimi ndiyo maana siku zote nimekuwa adui mkubwa wa watu ambao wamekuwa wanapambana kuweza kulirudisha nyuma taifa letu hili kwa namna moja ama nyingine.;”
“Nchi hii inawahitaji watu wenye maono makubwa, inawahitaji vijana shupavu kwa sababu ndipo ilipo nuru ya kesho ya taifa hili, kupitia vijana ndipo ambapo kama taifa tunaweza kufika mahali ambapo tumekuwa tukipasoma tu kwenye vitabu ila kwa bahati mbaya taifa letu linawachukia watu wenye uwezo mkubwa. Watu ambao wana uwezo wa kulipeleka mbele taifa letu wanachukuliwa kama hatari hususani kwa wale mazuzu ambao wamedandia nafasi kubwa serikalini wakati hawastahili kuwa hapo wakiamini kwamba kama vijana hawa wakipewa nafasi basi watazibeba nafasi zao. Unahisi tunaweza kufika popote kama taifa kwa akili hizi? Hapana asilani!?”
“Nimezaliwa kwenye familia ya kawaida tu ambayo naweza kusema ilinifunza mabaya na mazuri tangu siku tu natoka tumboni mwa mama yangu. Maisha yangu yamenifunza ukatili nikiwa bado mdogo lakini sikuruhusu kuwa katili kwa watu wengine kwa namna yoyote ile ndiyo maana naweza kusimama hapa na kujisifia kwamba mimi ni miongoni mwa watu ambao wamejitahidi kwa kila namna kuwa bora mbele ya bendera ya nchi yangu, hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kunilipa mimi, ni Mungu pekee atafanya hivyo siku ya kugawa thawabu kwa wale ambao ni wake”
“Kupenda kwangu kulitumikia taifa langu na kuweza kuzipigania rangi nne za bendera ya taifa langu ndiko ambako kulinifanya nilazimike kulipenda jeshi bila kupenda mwisho wa siku nikazamia huko. Jeshi sikuwahi kulipenda kwenye maisha yangu ila nilifanya hivyo ili niweze kuishi na kujilinda mwenyewe lakini pia kupigania haki za watu wengine ila baada ya muda niligundua kwamba jeshi pekee haliwezi kuleta hicho ambacho mimi nakitaka, ukawa mwanzo wangu wa kuipambania sheria pia”
“Niliamini kwamba nikiwa na hivyo vyote viwili basi ningekuwa na uwezo wa kupambania haki za wengi hivyo nilisoma kwa nguvu na kwa hasira zote mpaka nilipofanikiwa kumaliza shule ya sheria na rasmi nikavikwa vazi hilo ambapo mpaka sasa historia itaandika kwamba mimi ndiye mwanasheria ambaye sikuwahi kupoteza kesi yoyote ile mbele ya mahakama na ndiye mwanasheria ambaye sijawahi kudhulumu haki ya mtu ambaye anastahili kuipata kwa gharama yoyote ile”
“Kama nilivyosema mwanzo watu kama mimi hawapendwi kwa sababu mfumo hauwapendi mashujaa, jambo hilo ndilo lilikuwa chanzo cha umauti wangu ambao huenda mtauelewa baada ya masaa kadhaa kupita kuanzia sasa. Watu wengi hawaujui ukweli wa maisha yangu, mimi ni mtoto wa damu kabisa wa mwanasayansi Christian Edison ambaye aliuliwa na serikali ya nchi hii kwa kigezo cha kudai kwamba anapelekwa Israeli kufanya kazi na MOSSAD kama makubaliano ya nchi hizo mbili lakini haikuwa kweli, baba yangu aliuawa kwa sababu alikuwa na akili kuliko binadamu yeyote kwenye taifa hili”
“Nimekuzwa kwenye mazingira ya hatari mno kiasi kwamba ililazimika mimi kupotezwa kumbukumbu ili nisikumbuke yale ambayo yalitokea nyuma na habari mbaya zaidi hata mama yangu mzazi alinikimbia na huenda ndiye sababu kubwa ya baba yangu kufa pamoja na familia yangu yote. Licha ya hayo yote bado niliamua kulipambania taifa langu kama komando mwenye mafunzo ya juu lakini kuna watu ambao waliona uwepo wangu mimi na wenzangu ni hatari hivyo wakaamua kutuua” Aliongeza kuongea maneno hayo huku akiivua ile sura yake ambayo aliishi nayo kwa muda mrefu ambayo watu walimzoea nayo akifahamika kama Chrispin Mwambano na kubaki na ile sura ya Edison Christian ambaye baadhi ya watu walimjua kama Clyton Lameck.
“Iliamriwa niuawe kwa sababu nilikuwa hatari kwao lakini wasingeweza kuniua pekeyangu ilitakiwa waue kikosi kizima ambacho mimi ndiye nilikuwa nikikiongoza. KILL ON MISSION (KOM) ndilo lilikuwa jina la kikosi changu, kikosi ambacho jumla tulikuwa makomando kumi ila kwa bahati mbaya ni mimi pekee ambaye nilifanikiwa kuishi. Watu hawa walituma kikosi cha pili nyuma kwa madai kwamba kinakuja kutupatia msaada lakini watu wale walikuja kutushambulia kwa risasi ni bahati tu wakati wanafika simu iliita ndani nikarudi kuipokea na wakati nikiwa naongea na mtu kwenye simu ambaye alikuwa ananipa taarifa za kunitaka nitoke na wenzangu pale kwani nchi imetusaliti, nilisikia milio ya risasi ikanilazimu nitoke nje. Nilifanikiwa kuwaua watu wale wote ila kwa bahati nyingine mbaya ni kwamba walitumwa watu wengine watatu ambao walitumwa kuhakikisha kazi inakamilika na ndipo nilipopigwa risasi mbili (alifunua suti yake na shati kifua kilikuwa na makovu mawili) wakati nikiwa kwenye hatua za mwisho za kuishi kwangu, alitokea mwanaume nisiye mjua na kunisaidia ambapo sikuwa na fahamu ila niligundua kwamba nipo hai baada ya kuamka kwa mara nyingine”
“Wakati naamka nilifutiwa kumbukumbu zote kichwani mwangu, sikujua ni nani ambaye aliniokoa wala nilikuwa wapi na kufanya nini kitu pekee ambacho nilikuwa nakikumbuka ni sura ya mtu ambaye alinilea. Mtu huyo alinitaka nikaishi maisha ya chini mno huko Kigogo mwisho huku nisijue ni kwanini nilitakiwa kufanya hivyo kwani sikuwa na kumbukumbu. Nimeyaishi maisha hayo mpaka nilipo vamiwa kwa mara nyingine na watu ambao walihitaji kuyachukua maisha yangu ndipo ambapo nimekuja kuujua ukweli mwingine baadae”
“Ukweli wa kwamba kutoka na na lile ambalo lilitokea kule Somalia hawakuukuta mwili wangu hivyo wakaamua kujumlisha kwamba huenda nilipona na kama nilipona basi wakaamua kunipa kesi nzito ya kuhusika na mauaji ya makomando wenzangu, kesi ambayo waliliaminisha taifa zima kwamba mimi ndiye chanzo wa kila jambo lakini haukuwahi kuwa ukweli kwa sababu ukweli ni kwamba hata mimi nilitakiwa kufa ila nikaishi kwa neema za mwenyezi Mungu. Hilo halikutosha wakati wananituma huko na kikosi changu walimuua na mke wangu ambaye alikuwa mjamzito akikaribia kujifungua. Huenda kila mtu anatamani kuijua sababu haswa ya msingi zaidi ya haya yote kutokea”
“Kuna mambo sitayaongea hapa kwa sababu ya kulinda usalama wa taifa hili ila nchi haipo salama kabisa, watu wanakufa na kila siku zinavyozidi kwenda mbele basi watu wataendelea kufa zaidi. Nchi inaongozwa na watu ambao sio watanzania, sio kwamba viongozi wa juu hawajui au mamlaka za juu hazitambui hilo, lahasha! Bali ni miongoni mwa vibaraka wa hao watu. Taifa lilianza kuingia dosari baada ya raisi Justin Nyangasa alipo uawa kwa sumu aina ya Polonium 204 kisha kuchomwa aina nyingine ya sumu ambayo iliyaondoka maisha yake mara moja wakaja kudanganya mbele ya vyombo vya habari”
“Juzi hapa nilitangaza kuishtaki serikali na moja kati ya makosa yao ambayo walitakiwa kuyatolea majibu ni hilo kwa sababu muuaji mwenyewe alikuwa bado yupo hai. Dokta Namaki Prasad ndiye ambaye aliikamilisha kazi hiyo ya kumuua raisi Nyangasa na jana nilienda kwake ili niweze kumuomba asaidie kutoa ushahidi kwa juu ya jambo hili lakini kwa bahati mbaya nilimkuta mkewe na watoto wake tu yeye akiwa ameuawa tayari. Wamemuua ili kuondoa na kulinda ushahidi. Hivyo mnatakiwa kujua kwamba haya yote ambayo yemetokea na yanayo endelea kutokea hakuna mchawi wa kumlaumu bali serikali wenyewe ndio wanahusika moja kwa moja”

UKURASA WA 61 unafika mwisho.
Ni 🔥 🔥 🔥 🔥
 
Hii tayari imefikia tamati kwa hapa huu ndo uhalisia kwa sasa. 😅, SHUKRANI KWAKO NDUGU MTUNZI TUKUTANE TENA KWENYE VIGONGO VINGINE.
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 61

SURA YA SITA
Kutoka gazeti la THE TRUTH habari zilisambaa tangu asubuhi ya mapema kwamba mwanasheria JACK THE LAWYER usiku wa saa tano angeongea na wananchi, ilikuwa ni siku ambayo hakuna mtu alitakiwa kuikosa taarifa yake hiyo kutokana na umuhimu mkubwa ambao ilikuwa nayo. Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya siku ambayo kila mtu alibaki anaiongelea kila sehemu, watu wengi walikuwa na hamu kubwa ya kusikia habari hiyo kutoka kwenye kinywa chake kwa kuwa mwanasheria huyo hakuwahi kuwa na jambo dogo kila anapokuwa anajitokeza hadharani kuongea.
Siku zote hausimami na usiku wa deni haujawahi kuchelewa kufika na ndivyo ilivyokuwa kwa watanzania. Kwa ambaye alikuwa na simu yake basi alihakikisha bando linakuwa la kutosha, kwa watu ambao walikuwa karibu na televisheni zao na mitandao mbalimbali walikuwa makini mno kusubiria taarifa ya mwaasheria huyo hata mamlaka za usalama zilikuwa makini kuweza kuisubiria taarifa hiyo ili wajue mtu huyo alihitaji kufanya nini asije kuharibu amani ya nchi.
Alikuwa mtu wa kwenda na muda isivyo kawaida hali ambayo ilifanya saa tano kamili awepo mbele ya kamera yake kwenye chumba ambacho hakuna ambaye alifanikiwa kujua kwamba alikuwa wapi kwa wakati huo. Mwanaume huyo alitokea mbele ya kamera akiwa amependeza kwa suti ya blue ambayo ilikuwa na mistari myeusi, alikaa kwenye kiti kwa dakika tano bila kuongea jambo lolote lile, alijiweka sawa na kuisogeza kamera karibu kabisa na alipokuwa amekaa;
“Moja kati ya vitu ambavyo nitajivunia hata pale ambapo nitakuwa ndani ya jeneza kwenye safari yangu ya mwisho, ni kuzaliwa Tanzania. Kuzaliwa ndani ya taifa hili ni moja ya jambo bora kuwahi kutokea kwenye maisha yangu mimi ndiyo maana siku zote nimekuwa adui mkubwa wa watu ambao wamekuwa wanapambana kuweza kulirudisha nyuma taifa letu hili kwa namna moja ama nyingine.;”
“Nchi hii inawahitaji watu wenye maono makubwa, inawahitaji vijana shupavu kwa sababu ndipo ilipo nuru ya kesho ya taifa hili, kupitia vijana ndipo ambapo kama taifa tunaweza kufika mahali ambapo tumekuwa tukipasoma tu kwenye vitabu ila kwa bahati mbaya taifa letu linawachukia watu wenye uwezo mkubwa. Watu ambao wana uwezo wa kulipeleka mbele taifa letu wanachukuliwa kama hatari hususani kwa wale mazuzu ambao wamedandia nafasi kubwa serikalini wakati hawastahili kuwa hapo wakiamini kwamba kama vijana hawa wakipewa nafasi basi watazibeba nafasi zao. Unahisi tunaweza kufika popote kama taifa kwa akili hizi? Hapana asilani!?”
“Nimezaliwa kwenye familia ya kawaida tu ambayo naweza kusema ilinifunza mabaya na mazuri tangu siku tu natoka tumboni mwa mama yangu. Maisha yangu yamenifunza ukatili nikiwa bado mdogo lakini sikuruhusu kuwa katili kwa watu wengine kwa namna yoyote ile ndiyo maana naweza kusimama hapa na kujisifia kwamba mimi ni miongoni mwa watu ambao wamejitahidi kwa kila namna kuwa bora mbele ya bendera ya nchi yangu, hakuna mwanadamu mwenye uwezo wa kunilipa mimi, ni Mungu pekee atafanya hivyo siku ya kugawa thawabu kwa wale ambao ni wake”
“Kupenda kwangu kulitumikia taifa langu na kuweza kuzipigania rangi nne za bendera ya taifa langu ndiko ambako kulinifanya nilazimike kulipenda jeshi bila kupenda mwisho wa siku nikazamia huko. Jeshi sikuwahi kulipenda kwenye maisha yangu ila nilifanya hivyo ili niweze kuishi na kujilinda mwenyewe lakini pia kupigania haki za watu wengine ila baada ya muda niligundua kwamba jeshi pekee haliwezi kuleta hicho ambacho mimi nakitaka, ukawa mwanzo wangu wa kuipambania sheria pia”
“Niliamini kwamba nikiwa na hivyo vyote viwili basi ningekuwa na uwezo wa kupambania haki za wengi hivyo nilisoma kwa nguvu na kwa hasira zote mpaka nilipofanikiwa kumaliza shule ya sheria na rasmi nikavikwa vazi hilo ambapo mpaka sasa historia itaandika kwamba mimi ndiye mwanasheria ambaye sikuwahi kupoteza kesi yoyote ile mbele ya mahakama na ndiye mwanasheria ambaye sijawahi kudhulumu haki ya mtu ambaye anastahili kuipata kwa gharama yoyote ile”
“Kama nilivyosema mwanzo watu kama mimi hawapendwi kwa sababu mfumo hauwapendi mashujaa, jambo hilo ndilo lilikuwa chanzo cha umauti wangu ambao huenda mtauelewa baada ya masaa kadhaa kupita kuanzia sasa. Watu wengi hawaujui ukweli wa maisha yangu, mimi ni mtoto wa damu kabisa wa mwanasayansi Christian Edison ambaye aliuliwa na serikali ya nchi hii kwa kigezo cha kudai kwamba anapelekwa Israeli kufanya kazi na MOSSAD kama makubaliano ya nchi hizo mbili lakini haikuwa kweli, baba yangu aliuawa kwa sababu alikuwa na akili kuliko binadamu yeyote kwenye taifa hili”
“Nimekuzwa kwenye mazingira ya hatari mno kiasi kwamba ililazimika mimi kupotezwa kumbukumbu ili nisikumbuke yale ambayo yalitokea nyuma na habari mbaya zaidi hata mama yangu mzazi alinikimbia na huenda ndiye sababu kubwa ya baba yangu kufa pamoja na familia yangu yote. Licha ya hayo yote bado niliamua kulipambania taifa langu kama komando mwenye mafunzo ya juu lakini kuna watu ambao waliona uwepo wangu mimi na wenzangu ni hatari hivyo wakaamua kutuua” Aliongeza kuongea maneno hayo huku akiivua ile sura yake ambayo aliishi nayo kwa muda mrefu ambayo watu walimzoea nayo akifahamika kama Chrispin Mwambano na kubaki na ile sura ya Edison Christian ambaye baadhi ya watu walimjua kama Clyton Lameck.
“Iliamriwa niuawe kwa sababu nilikuwa hatari kwao lakini wasingeweza kuniua pekeyangu ilitakiwa waue kikosi kizima ambacho mimi ndiye nilikuwa nikikiongoza. KILL ON MISSION (KOM) ndilo lilikuwa jina la kikosi changu, kikosi ambacho jumla tulikuwa makomando kumi ila kwa bahati mbaya ni mimi pekee ambaye nilifanikiwa kuishi. Watu hawa walituma kikosi cha pili nyuma kwa madai kwamba kinakuja kutupatia msaada lakini watu wale walikuja kutushambulia kwa risasi ni bahati tu wakati wanafika simu iliita ndani nikarudi kuipokea na wakati nikiwa naongea na mtu kwenye simu ambaye alikuwa ananipa taarifa za kunitaka nitoke na wenzangu pale kwani nchi imetusaliti, nilisikia milio ya risasi ikanilazimu nitoke nje. Nilifanikiwa kuwaua watu wale wote ila kwa bahati nyingine mbaya ni kwamba walitumwa watu wengine watatu ambao walitumwa kuhakikisha kazi inakamilika na ndipo nilipopigwa risasi mbili (alifunua suti yake na shati kifua kilikuwa na makovu mawili) wakati nikiwa kwenye hatua za mwisho za kuishi kwangu, alitokea mwanaume nisiye mjua na kunisaidia ambapo sikuwa na fahamu ila niligundua kwamba nipo hai baada ya kuamka kwa mara nyingine”
“Wakati naamka nilifutiwa kumbukumbu zote kichwani mwangu, sikujua ni nani ambaye aliniokoa wala nilikuwa wapi na kufanya nini kitu pekee ambacho nilikuwa nakikumbuka ni sura ya mtu ambaye alinilea. Mtu huyo alinitaka nikaishi maisha ya chini mno huko Kigogo mwisho huku nisijue ni kwanini nilitakiwa kufanya hivyo kwani sikuwa na kumbukumbu. Nimeyaishi maisha hayo mpaka nilipo vamiwa kwa mara nyingine na watu ambao walihitaji kuyachukua maisha yangu ndipo ambapo nimekuja kuujua ukweli mwingine baadae”
“Ukweli wa kwamba kutoka na na lile ambalo lilitokea kule Somalia hawakuukuta mwili wangu hivyo wakaamua kujumlisha kwamba huenda nilipona na kama nilipona basi wakaamua kunipa kesi nzito ya kuhusika na mauaji ya makomando wenzangu, kesi ambayo waliliaminisha taifa zima kwamba mimi ndiye chanzo wa kila jambo lakini haukuwahi kuwa ukweli kwa sababu ukweli ni kwamba hata mimi nilitakiwa kufa ila nikaishi kwa neema za mwenyezi Mungu. Hilo halikutosha wakati wananituma huko na kikosi changu walimuua na mke wangu ambaye alikuwa mjamzito akikaribia kujifungua. Huenda kila mtu anatamani kuijua sababu haswa ya msingi zaidi ya haya yote kutokea”
“Kuna mambo sitayaongea hapa kwa sababu ya kulinda usalama wa taifa hili ila nchi haipo salama kabisa, watu wanakufa na kila siku zinavyozidi kwenda mbele basi watu wataendelea kufa zaidi. Nchi inaongozwa na watu ambao sio watanzania, sio kwamba viongozi wa juu hawajui au mamlaka za juu hazitambui hilo, lahasha! Bali ni miongoni mwa vibaraka wa hao watu. Taifa lilianza kuingia dosari baada ya raisi Justin Nyangasa alipo uawa kwa sumu aina ya Polonium 204 kisha kuchomwa aina nyingine ya sumu ambayo iliyaondoka maisha yake mara moja wakaja kudanganya mbele ya vyombo vya habari”
“Juzi hapa nilitangaza kuishtaki serikali na moja kati ya makosa yao ambayo walitakiwa kuyatolea majibu ni hilo kwa sababu muuaji mwenyewe alikuwa bado yupo hai. Dokta Namaki Prasad ndiye ambaye aliikamilisha kazi hiyo ya kumuua raisi Nyangasa na jana nilienda kwake ili niweze kumuomba asaidie kutoa ushahidi kwa juu ya jambo hili lakini kwa bahati mbaya nilimkuta mkewe na watoto wake tu yeye akiwa ameuawa tayari. Wamemuua ili kuondoa na kulinda ushahidi. Hivyo mnatakiwa kujua kwamba haya yote ambayo yemetokea na yanayo endelea kutokea hakuna mchawi wa kumlaumu bali serikali wenyewe ndio wanahusika moja kwa moja”

UKURASA WA 61 unafika mwisho.
 
Back
Top Bottom