Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 47
Alijikuta akiingiwa na wasiwasi. Alikuwa peke yake, katikati ya kiza katika eneo ambalo mchana huo lilikuwa la maafa. Akawaza kurudi, lakini alijikongoja hadi alipofika kando ya vifusi vya jumba hilo. Alitupa macho kila upande, hakuonana dalili yoyote ya mlinzi. Baada ya mizunguko kadhaa, aliamini kuwa sehemu hiyo haikuwa ikilindwa. Akasononeka moyoni.
Mara likamjia wazo jingine. Yawezekana katika jumba hili mlikuwa na vitu vya thamani ambavyo angevichukua na kuviuza! Wazo hili likamtuma Unono kuanza kuchungulia, akashika kile na kujipenyeza pale. Alipata mwanya ambao ulimwingiza ndani ya kifusi hicho. Mikono yake iliendelea kupeleleza kwa makini, macho yakifanya juhudi kutazama.
Ghafla Unono aligusa kitu ambacho kilimshitua. Kitu chenye dalili ya uhai. Nyoka? alijiuliza baada ya kuutoa haraka mkono wake. Baada ya kutulia kwa makini, aligundua kuwa alichogusa ni mwili wa binadamu. Ugunduzi wake ulimshitua zaidi. Maiti nyingine! aliwaza akiinuka na kuanza kuondoka.
Kisha ushujaa ukamwingia na kumfanya ahairishe safari yake na kuuinamia mwili huo kwa uchunguzi zaidi.
Inspekta Kombora alikuwa mgonjwa mahututi, ingawa hakuwa tayari kumweleza daktari wake kuhusu kuumwa kwake wala hakutaka kujieleza mwenyewe ni maradhi gani yanamsumbua. Alijiona tu yu hoi bin taaban, hali ambayo ilimtokea ghafla baada ya kuviona vile vipande vya mwili wa binadamu vilivyotawanywa kwa bomu. Lakini kilichomuuguza zaidi ni kuokotwa zile ndevu za bandia alizokuwa amevaa Joram Kiango.
Joram kafa! lilikuwa wazo lililomtesa zaidi ya ukweli Inspekta Kombora. Joram ambaye jina lake lilikuwa tishio kwa waovu wote wenye nia mbaya kwa nchi na wananchi wake! Joram ambaye alikubali kuiweka roho yake hatarini mara kwa mara kwa lengo la kuwakabiri maadui wenye nguvu na uwezo wa kutisha! Joram, kijana mwenye moyo wa jiwe na mwili wa chuma! Joram amekufa?...
Miaka mingi ilikuwa imepita, kiasi kwamba Inspekta Kombora hakumbuki siku gani aliyotokwa na machozi. Leo hii, akiwa peke yake ofidini, akiitazama meza yake, alihisi chozi likipenya kwenye vipingamizi vyote na kuelea juu ya
Alijikuta akiingiwa na wasiwasi. Alikuwa peke yake, katikati ya kiza katika eneo ambalo mchana huo lilikuwa la maafa. Akawaza kurudi, lakini alijikongoja hadi alipofika kando ya vifusi vya jumba hilo. Alitupa macho kila upande, hakuonana dalili yoyote ya mlinzi. Baada ya mizunguko kadhaa, aliamini kuwa sehemu hiyo haikuwa ikilindwa. Akasononeka moyoni.
Mara likamjia wazo jingine. Yawezekana katika jumba hili mlikuwa na vitu vya thamani ambavyo angevichukua na kuviuza! Wazo hili likamtuma Unono kuanza kuchungulia, akashika kile na kujipenyeza pale. Alipata mwanya ambao ulimwingiza ndani ya kifusi hicho. Mikono yake iliendelea kupeleleza kwa makini, macho yakifanya juhudi kutazama.
Ghafla Unono aligusa kitu ambacho kilimshitua. Kitu chenye dalili ya uhai. Nyoka? alijiuliza baada ya kuutoa haraka mkono wake. Baada ya kutulia kwa makini, aligundua kuwa alichogusa ni mwili wa binadamu. Ugunduzi wake ulimshitua zaidi. Maiti nyingine! aliwaza akiinuka na kuanza kuondoka.
Kisha ushujaa ukamwingia na kumfanya ahairishe safari yake na kuuinamia mwili huo kwa uchunguzi zaidi.
Inspekta Kombora alikuwa mgonjwa mahututi, ingawa hakuwa tayari kumweleza daktari wake kuhusu kuumwa kwake wala hakutaka kujieleza mwenyewe ni maradhi gani yanamsumbua. Alijiona tu yu hoi bin taaban, hali ambayo ilimtokea ghafla baada ya kuviona vile vipande vya mwili wa binadamu vilivyotawanywa kwa bomu. Lakini kilichomuuguza zaidi ni kuokotwa zile ndevu za bandia alizokuwa amevaa Joram Kiango.
Joram kafa! lilikuwa wazo lililomtesa zaidi ya ukweli Inspekta Kombora. Joram ambaye jina lake lilikuwa tishio kwa waovu wote wenye nia mbaya kwa nchi na wananchi wake! Joram ambaye alikubali kuiweka roho yake hatarini mara kwa mara kwa lengo la kuwakabiri maadui wenye nguvu na uwezo wa kutisha! Joram, kijana mwenye moyo wa jiwe na mwili wa chuma! Joram amekufa?...
Miaka mingi ilikuwa imepita, kiasi kwamba Inspekta Kombora hakumbuki siku gani aliyotokwa na machozi. Leo hii, akiwa peke yake ofidini, akiitazama meza yake, alihisi chozi likipenya kwenye vipingamizi vyote na kuelea juu ya