HADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL:
thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 81
"We mjinga umepitaje na mwili huu mpaka huku? ebu utoe haraka sana kwa sababu nitakufanyia jambo baya ambalo haujawahi kulifikiria kabisa kwenye maisha yako yote. Unakuja kumtisha raisi wa nchi Ikulu kwa sababu tu ni mkurugenzi wa shirika la kijasusi, nafasi ambayo naweza kukutoa muda wowote ule nikitaka?" aliongea kwa ukali sana raisi Justin Mtadei.
"Mazungumzo ambayo nahitaji tuyafanye mimi na wewe yanahusisha huu mwili kuwepo hapa na uwe unauona vizuri kwa sababu kile ambacho wewe unaogopa kukiona na kuona kinyaa muda huu kuna watu huwa wanakiona kila siku kwenye maisha yao kwa sababu tu ya kauli zako za kishamba na kipumbavu kuhamasisha mauaji na matendo mabaya sana ambayo yanawafanya wananchi wasiokuwa na hatia wakiteseka huku wewe ukiendelea kukuza kitambi chako tu na wanao wakiwa wanaringa na magari ya gharama sana mitandaoni wasijue kwamba hizo ni kodi za wananchi ambao wewe unatumia muda mwingi kuwadhihaki na kuwatukana" likuwa ni kauli ya kijasiri sana kuweza kuitamka mbele ya raisi wa nchi.
Raisi alishtuka baada ya kumuona mwanamke huyo amebadilika sana maana hakuwahi kumuona kwenye hali kama hiyo, siku zote alikuwa mtiifu sana kwake na msikilizaji mzuri sana lakini siku hiyo mambo yalikuwa tofauti mno, mwanamke huyo alikuwa siriasi sana na yeye ndiye alikuwa mwongeaji mkuu na raisi alitakiwa kuwa msikilizaji mkubwa. Mheshimiwa alimuita mlinzi wake kwa nguvu lakini lango hilo lililokiwa kwa ndani akiwa na mkurugenzi huyo na wanaume wa kazi wawili na mlinzi wake mkuu nje ya huo mlango alibebwa na wanaume wanne baada ya kupokea kipigi kizito sana kisha wakaondoka naye kwenda kumuua huku wengine wanne wakiwa wamebakia hapo kuhakikisha ulinzi unakuwepo na kama mtu mgeni angekatiza hapo hakuna ambaye angejua kwamba kuna tatizo maana walijipanga kama ilivyokuwa siku zote za kazi walinzi wa kawaida wakiwa hapo.
"Unamaanisha unataka kuipindua nchi?" raisi aliuliza kwa hasira kali sana
"Hapana mheshimiwa, ila wewe ndiye unatakiwa kuondoka kwenye hiyo nafasi na sio kwa hiari bali kwa lazima"
"We malaya una kichaa sio? unatishia kumtoa raisi kwenye nafasi yake, unayajua madhara yake? unahisi nchi na jeshi watakubali juu ya hili? Chuki usije ukafanya hili kosa ambalo hautaweza kulibeba kwenye maisha yako yote" aliongea akiwa anamsogelea mwanamke huyo, alikuwa ana hasira sana kudhalilishwa na mwanamke ambaye yeye ndiye alimuweka kwenye hiyo nafasi lakini alisimama baada ya wanaume ambao walikuwa karibu na Chuki kumsogelea bosi wao kuhakikisha hakuna mtu yeyote alikuwa anapitisha hata kidole chake kwenda kwa huyo mwanamke.
"Upo sahihi kuniita mimi malaya kwa sababu ya hilo jeshi ambalo unajisifia nalo hapa saivi. Lakini hali ambayo itatokea endepo ikiwa hivyo ni kama hiki ambacho unakiona hapa mbele yako kwenye huo mwili wa Dax. Watu watakufa sana, mauaji mengi sana yatatokea na huo hautakuwa mwafaka kwa sababu utaongeza zaidi matatizo, huenda hata mkuu wa majeshi ananitegemea zaidi mimi kuliko hata mimi ninavyo mtegemea au wewe unavyo mhitaji kwa ajili ya usalama wa taifa hili na usalama wako pia. Mimi ndiye mtu ambaye nina taarifa nyingi sana za siri za taifa hili, mimi ndiye mwenye taarifa za ndani sana kujua kwamba ni nani na nani wanahitaji kulivamia na kulipoteza taifa hili, je unahisi mimi na hilo jeshi yupi wa mhimu zaidi? jibu baki nalo kwenye moyo wako"
"Kitu pekee ambacho mimi nakijutia kwenye maisha yangu ni kushindwa kutambua yale ambayo yalikuwa yanaendelea mapema. Sikujua kwamba nilikuwa nimewekwa hapa kama toi la kuchezewa mpaka hili sakata lilipokuja kwenye njia yangu ndipo nilielewa kwamba hii nchi haikuwa sawa kama nilivyokuwa nadanganywa bali msaada wangu kama kiongozi wa usalama ulikuwa unahitajika sana"
"Chuki umesahau mahali ambako tumekutoa na kukuweka kwenye hiyo nafasi mpake leo unakuja kuingia kwenye njia zetu?"
"Najua sana mliko nitoa, najua kwamba mmenitoa nikiwa mtu wa kawaida tu ndani ya jeshi nikaingizwa huku na kwa sababu ya manufaa yenu mkanipa nafasi hii mtu ambaye mlijua kabisa kwamba sisitahili kwenye nafasi hii. Najua mlinipa hii nafasi kwa sababu mimi ni mwanamke na mlikuwa na uhakika kwamba mtaweza kuniendesha kirahisi sana kuliko kama mngemuweka mwanaume kwenye hii nafasi, ila unatakiwa kuelewa kwamba kuniweka mimi hapa hili ni kosa kubwa zaidi wewe kuwahi kulifanya kwenye maisha yako na huyo bosi wako ambaye amekuweka wewe kama kivuli hapo ulipo ukiwa hauna maamuzi yoyote yale" dharau zilizidi raisi huyo alimkimbilia Chuki kwa hasira sana lakini alirudi akiwa anayumba yumba baada ya kupokea kibao kikali sana kutoka kwa moja ya wanaume ambao walikuwa pembeni yake, mtu huyo alikuwa anacheza na bosi wao ambaye ndiye alikuwa ameshika hatima ya maisha yao.
"Chuki unathubutu kuruhusu huyo kijana anipige mimi, huo mkono ndani ya dakika kumi na tato zijazo naenda kuuchoma niule. Ngoja niite walinzi wote wa nje wafike hapa kisha hii taarifa imfikie mkuu wa majeshi"
"Pole sana mheshimiwa, Ikulu yote kuanzia hivi ninavyo ongea ipo chini yangu na wewe upo chini ya ulinzi kwa sababu za kiusalama wa nchi na nina hiyo haki ya kukukamata kama naona kwamba nchi haipo salama kutokana na wewe kuwa huru"
"Whaaaaat?"
"Najua kwamba wewe ndiye kiongozi mkuu wa hili shirika langu lakini kwa maslahi mapana ya taifa langu siwezi kukuacha ukiwa huru kwa sababu utaleta matatizo makubwa sana" mwanamke huyoa alimalizia maelezo yake huku akiwa anawaachia nafasi wanaume ambao walikuwa karibu yake hapo waweze kumfunga vyema kabisa mheshimiwa.
"Chuki una uhakika na hiki unacho kifanya? utajutia sana kwa kuichezea nafasi ambayo nimekupa uache mara moja hiki"
"Naelewa kwamba unategemea Denis Kijazo atakuja kukuokoa akipata taarifa ila nataka nikuhakikishie yeye mwenyewe kuanzia muda huu ana masaa ambayo hayazidi ishirini kuweza kuyanusuru maisha yake na kama anaweza anatakiwa kuikimbia nchi kwa sababu kuna uwezekano akafa au akaishia sehemu ambayo hatakuja kuliona jua mpaka siku ya mwisho ya kufa kwake. Sehemu ambayo atawekwa, atatamani ni bora angejiua yeye mwenyewe ila hataipata hiyo nafasi. Usiku nitakuja kukuonyesha nini maana ya hofu kwa huyo ambaye unategemea kwamba atakuja kukusaidia katika hili" aliongea akiwapa ishara wanaume hao waweze kuondoka na mtu huyo hilo eneo haraka sana.
Rasmi Ikulu ilikuwa imechukuliwa na mkurugenzi mkuu wa shirika la kijasusi la nchi ya Tanzania, raisi alikuwa amekamatwa kwa sababu ambazo zilisemekana kuwa za kiusalama zaidi sasa kazi ilikuwa imebakia kwa Denis Kijazo, mwanamke huyo hakutaka kufanya makosa kama ambayo waliyafanya wenzake. Jambo hilo lilifanyika kwa siri kubwa sana na hakuna mwananchi au mtu yeyote wa raisi huyo ambaye alikuwa ana hizo taarifa kwamba Ikulu haikuwa kwenye mikono ya raisi tena bali kwa watu wa usalama.
Nchi ilikuwa imechafuka kwa habari mbaya ambazo zilikuwa zinaendelea nchini. Wananchi walikuwa wakipiga sana kelele kuhitaji kusikia chochote kutoka kwa raisi wao kitu ambacho kilikuwa nyuma kabisa na matarajio yao kwani waliamini kwamba angetoa kauli zozote zile za kuridhisha. Mauaji mengine ya kikatili ambayo yalianza kusambaa asubuhi hiyo hususani kutoka kwa watu ambao aalikuwa wapinzani wa serikali ambayo ilikuwa madarakani yalianza kuleta tafrani kubwa sana nchini huku baadhi ya watu wakiwa wanatishia kuondoka nchini maana haikuonekana kuwa sehemu ya amani tena kama walivyokuwa wameizoea miaka na miaka.
Watu hao walisambaza taarifa za upotevu wa makomando saba ambao walidaiwa kuuawa wote na kibaya hawakufa kwa ajili ya kulipambania taifa bali kuyapambania maslahi ya watu fulani. Watu hao pia kwa kutumia mitandao ya kijamii walianza kusambaza habari kama utani kwamba serikali ilikuwa imepinduliwa na ili kuthibitisha hilo walimtaka raisi ajitokeze au mkuu wa majeshi ajitokeze hadharani ili kupinga tuhuma hizo zikiwemo ya makomando wake kupoteza maisha.
Hizo habari zilimkuta Denis Kijazo akiwa kwenye mawazo sana, alikuwa anayatafakari sana yale ambayo alifanikiwa kuyaongea na Profesa Mande. Akiwa kwenye hayo mawazo mazito ya kuamua hatima yake ingekuwaje ndipo alipata hizo habari ambazo zilimshtua mno na kumfanya aanze kutokwa na jasho huku akitetemeka kwa hasira sana. Aliitoa simu yake na kuhitaji kuipiga kwa mkuu wa majeshi lakini kabla ya kufanya hayo yote, mlinzi wake alifika humo ndani na kumsihi kwamba mkuu wa majeshi alikuwa amefika. Alikuwa na hamu sana na mtu huyo na alifika kwa muda mwafaka kabisa hivyo alimtaka aingie ndani haraka sana.
"Ni kipi kinaendelea nchini ambacho hata mimi sina taarifa nacho?"
"Makomando wote saba wamepotea"
"Umechanganyikiwa?"
"Hapana mheshimiwa, jana wakati nakupa taarifa kuhusu Dax ni kweli walifika alipokuwa anaishi na kukuta ameuawa hivyo waliamua kwenda alikokuwa anaishi mkewe kwa kuhisi kwamba mtu huyo angekuwa huko hivyo ingewezekana wakampata huko"
"Enhe"
"Walienda na kumkuta lakini aliwaua kikatili sana"
"Whaaaaat? Makomando wote saba?"
"Hapana waligawana, kule walienda wanne na watatu walikuwa wanakuja kuniletea mwili wa yule bwana mdogo ili niufanyie uchunguzi"
"Sasa unasemaje kwamba wamepotea wote?" mkuu wa majeshi hakuongea lolote, aliitoa simu yake na kuifungua video ambayo waliipata kutoka nyumbani kwa mke wa Dax. Ni video ambayo ilikuwa inaonyesha jinsi makomando watatu walivyouawa kikatili sana lakini mmoja aliachwa.
"Huyu kwanini aliachwa?"
"Hakuna na nia ya kumdhuru Max ndiyo maana hapo alikuwa na nafsi ya kumpiga risasi lakini alimuacha na mtu huyo alionekana kumpa maagizo ambapo hatukusikia kinacho ongelewa lakini baadae komando huyu alionekana akiondoka na mtoto, ni wazi kwamba alimpa nafasi ya kuishi ili akamlee huyo mtoto"
"Sasa kwanini aliua baba na mama na akamuacha mtoto?"
"Kwa sababu mtoto hana hatia yeye alikuwa anadili na wahusika wake tu"
"Na hao watatu wako wapi?"
"Hao waliokuwa wanakuja kuuleta mwili kwangu mpaka sasa hawapatikani, nimewaagiza vijana wawatafute lakini wamezunguka kila sehemu ya jiji na hakuna kitu wamekiona hivyo ni ishara kwamba kama hawajauawa wametekwa"
"Hapana, hili jambo haiwezekani alifanikishe mwenyewe, lilikuwa ni jambo la haraka sana sasa kivipi ayafanya mambo yote haya kwa wakati mmoja? maana yake lazima nyuma yake ana mtu mwenye nguvu sana ndiye anamsaidia. Familia yake imesafirishwa kwenda Arusha, namhitaji akiwa hai, nina imani leo Ted anaenda kumpata haraka sana ila kabla ya hili nahitaji kukutana na mkurugenzi wa shirika la kijasusi huyu atakuwa na taarifa nyingi sana juu ya hili na siku hizi simuelewi sana"
81 inafika mwisho.