KABURI LA MWANAMUZIKI (EPISODE 09)
Mtunzi; Robert Heriel
WhatsApp 0693322300
EPISODE 09
ILIPOISHIA
‘ Gibson! Kwema ndugu yangu” Nikamsogelea
“ Kwema, vipi!” Nikasema bila uchangamfu,
“ Naona umepambana mpaka umefika level hii, ngoja tuone” Akasema,
“ Huu ndio mwanzo tuu, hakuna wa kunizuia” Nikasema,
“ Ndio maana ukaimba nyimbo ya Lusifa, hahahah! “ akacheka kwa dharau huku akimuangalia mtu aliyekuwa akimuita, nafikiri alikuwa ni dereva wake.
“ Alice anakuja wiki ijayo, lakini kabla hajaja nataka nikupe maumivu kidogo, nataka nimchukue Neema kwa hii wiki ili ujisikie vile nilivyojisikia kipindi kile ulivyonichukulia Alice wangu” Akasema, akiwa ananitazama kwa macho ya hasira iliyojificha, Nikatabasamu bila ya kumjibu kitu, nikaondoka kwenda kwenye gari walipokuwa wananisubiri Neema na Kaka yake..
ENDELEA
*****************
Nilirekodi wimbo wangu wa kwanza, kisha nikatoa na video yake, ulikuwa wimbo mzuri uliovuma nchi nzima, karibu chaneli zote za Televisheni zilionyesha video ya wimbo wangu, redioni nako ngoma yangu ilipasua anga, mitaani na kwenye Bar kote ilikuwa ndio habari ya mjini, hiyo ilikuwa hatua muhimu ya mafanikio katika maisha yangu ya muziki, nilijua jina langu limeanza kujulikana kitaifa, kila nilipopita watu walikuwa wakiniita kwa jina langu, wengine wakinisumbua nipige nao picha, mwanzoni nilijivunia walivyokuwa wanafanya hivyo lakini kadiri siku zilivyokuwa zinaenda nilianza kuona ni usumbufu,
Maisha mapya ya kuishi kama mtu mashuhuri yalianza, umashuhuri unaraha zake, ikiwemo kibiashara kwani jina langu ningelitumia kutangaza biashara yoyote ikaenda, makampuni makubwa yalikuwa yakipigana vikumbo kuja kuomba kuingia mkataba na mimi ili nitangaze bidhaa zao, mawakala na meneja wa muziki walikuwa wakiomba niwe chini yao ili kuniongoza kwenye taaluma yangu ya muziki, baada ya kutoa ngoma yangu ya kwanza ikapokelewa vizuri, ilinibidi nihame pale kwa Riadi, nilitaka kuishi kwa uhuru zaidi nikiwa najitegemea, nikaongea vizuri na Riadi, alisikitika sana, licha ya kunisihi niendelee kuishi kwake lakini niling’ang’ania kuwa nahitaji kujitegemea, basi ikawa alivyoona nimechachamaa na msimamo wangu akaniruhusu huku akinisihi nisisite kurudi kwake ikiwa mambo yataenda tofauti, akaniambia pale ni kama nyumbani, na mimi ni kama mdogo wake, basi tukaachana,
Nilikuwa nimekodi nyumba nzima, maeneo ya Mwenge, sasa nilianza maisha mapya, kwa mara ya kwanza nilianza kuyala matunda ya kipaji changu, ilikuwa nyumba kubwa ya vyumba vinne, chumba kimoja kikiwa Master, sebule mbili, jiko na stoo, ilikuwa ndani ya uzio kukiwa na vigae pamoja na bustani nzuri, niliona itafaa kwa kuanzia maisha yangu, sasa nilitamani kuishi na Mama yangu, nikamtumia mama nauli akaja mjini, mama alifurahi sana kuniona mafanikio niliyoyapata,
“ Mwanangu hii nyumba yote ni yetu?’ Mama akaniuliza,
“ Ndio mama, hii ni nyumba yako mama” Nikasema,
“ Nashukuru sana mwanangu, Uzidi kubarikiwa na kuwa mtu mkubwa” Mama akasema akiwa anaendelea kuikagua nyumba yetu. Hakuna kitu kizuri kama kumuona mama yako mzazi akiwa na furaha, moyo wangu ulikuwa umechangamka ajabu, lakini mama akaniuliza swali ambalo liliondoa uchangamfu wangu,
“ Mwanangu hii sio nyumba yako, kitu ulichokikodisha hakiwezi kuwa chako mwanangu, nakuomba usibweteke, hela unayolipa si itakuwa nyingi sana?” Mama akasema,
“ Aaah! Mama, unajua kwa sasa mimi ni Star, siwezi kuishi nyumba ya kawaida Mama, lazima nikae nyumba inayoendana na jina langu Mama” Nikasema,
“ Yote ni sawa Kijana wangu, lakini nakuomba ufanye juu chini ujenge nyumba yako mwenyewe kabla mambo hayajawa mengi, unajua kila kitu ni kirahisi kama kitafanywa kwa wakati hasa mwanzoni kabla mambo hayajakutinga” Mama akasema,
“ Usijali Mama yangu, kwanza nataka nikujengee bonge la jumba, mama kwanza kisha mimi nitafuata, nataka pale kijijini watu waliokudharau wakuheshimu, na hili nitalifanya mapema mwaka huu” Nikasema, maneno hayo yalimfanya mama atabasamu huku akiniangalia kwa macho ya upendo. Juma lilelile nilinunua gari zuri la gharama, hiyo ilikuwa ndoto yangu kumiliki usafiri wenye hadhi, nilifanya hivyo kwa sababu, nisingeweza kuendelea kupanda magari ya kukodisha kama vile Uber au Bolt, nilistahili kuwa na usafiri wangu,
Wimbo wa pili nikarekodi nikishirikiana na Neema, ulikuwa wimbo mzuri sana ambao ulizidi kuimarisha majina yetu ndani na nje ya Nchi yetu, katika tasnia ya muziki wapo wa kongwe wengi ambao tuliwakuta kwenye Game, haikuwa kazi rahisi kutukubali kama wanamuziki wenzao, wengi wao walituchukulia kama washindani na hii ilipelekea uhasama wa kila mara baina yetu, fitina na majungu kwenye muziki ni jambo la kawaida, kila kitu kizuri kinahitaji kupiganiwa, kinahitaji mtu ajitoe kisawasawa.
Nikatafuta jina la kisanii ambalo litatumika katika kazi zangu za sanaa ya muziki, kiukweli kutafuta jina sikudhani kama ni jambo gumu kiasi kile, ilinichukua wiki nzima kupata jina nililoliona litanifaa katika kazi zangu, nikajiita Gstar(tamka JISTAA) Herufi ya “G” Ikibeba jina langu Gibson, Star ikimaanisha Nyota ing’aayo. Nilikuwa nikijiona kama Nyota yenye kung’aa, nilitaka nuru yangu iwaangazie watu wa nchi yangu na dunia kwa ujumla. Nilitaka muziki ukomboe watu wangu. Jina linamchango mkubwa katika kazi za sana, pia hata katika maisha ya kawaida jina la mtu huweza kuchangia kwa sehemu kubwa mapito yake, jina zuri linaweza badilisha mtu na kuwa mtu mzuri.
Nikampigia simu Neema tuonane katika Hotel Fulani iliyokatikati ya jiji, nilikuwa nina siku kadhaa sijakutana naye kutokana na shughuli nyingi za muziki pamoja na kukaa na Mama, nilitaka mama akae na mimi mpaka hamu yake iishe, na hilo lisingetokea kwani hamu ya mama kwa mtoto wake kamwe haiwezi kuisha, ingawaje angalau niliweza kuishusha, nikakutana na Neema Hotelini, Neema naye alikuja na Gari yake, alikuwa kapendeza sana, alivalia kigauni kifupi kilichoishilizia katikati ya mapaja, chenye rangi kama ya kijani kilichopauka,
“ Nimefurahi sana kukuona Neema” Nikasema,
“ Hata mimi pia Gstaa, jina lako zuri sana, unajua kujipendelea, mimi mbona hunitungii jamani” Neema akasema, hapo tukacheka.
“ Unahitaji nikutungie jina mpenzi?’
“ Unaniuliza tena jamani, nitungie bhana, hili nililonalo alinitungia Baba yangu, nataka la usanii unitungie wewe, si unajua kwa sasa wewe ndio Baba yangu uliyebakia” Neema akaongea kwa madeko huku akiyazungusha macho yake kwa kurembua, hapo tukapeleka glass za mvinyo kinywani kisha tukaendelea.
“ OoooH! Hivi hukuwahi kuniambia habari za wazazi wako, wako wapi?” Nikamuuliza, hapo nikauona uso wa Neema ukibadilika, huzuni yenye uchungu ilizikumbatia kwa nguvu misuli ya uso wake, macho yake yakashindwa kuhimili machozi yaliyokuwa yakibisha katika miimo ya macho yake, nikamuona akilia, nilijisikia vibaya sana kumuona katika hali ile.
“ I’m sorry Neema, sikuwa lengo la kukuumiza, nisamehe sana!” Nikasema,
“ Hujawahi kuniumiza Gibson, wala hujawahi kuniudhi hata kidogo, nilikuwa nimeshakata tamaa ya kuishi duniani, furaha ilinikimbia miaka mingi iliyopita, sikuwahi kufikiri siku moja nitakuwa na furaha, lakini tangu nimekutana na wewe siku ile ya kwanza pale TGT furaha yangu ikarejea” Hapo akameza fumba la mate kisha nikachukua kitambaa nimfuta machozi,
“ Ahsante Mpenzi” Akasema huku akiniangalia kwa upendo, alinishukuru kwa kumfuta machozi,
“ Kwa vile tumekuja kuinjoi nafikiri tuachane na hiyo stori, utanisimulia siku nyingine, leo tunywe, tule tufaurahi” Nikasema, hapo nikachukua lile chupa kubwa la Wine nyekundu na kumimina kwenye Bilauri ya kioo. Tukanywa na kula, mpaka tukahisi kulewa, nikaomba mhudumu atuandalie chumba kizuri, kisha tukaelekea chumbani, ilikuwa yapata majira ya usiku wa saa mbili hivi; nikiwa chumbani na mtoto Neema, ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana faragha, tulikuwa tumelewa lakini haikuwa sana kiasi cha kushindwa kutembea, tukabadilisha nguo na kuvaa taulo nyeupe kama makoti, kisha tukaenda bafuni, kila mmoja alikuwa na hamu na mwenzake, ulikuwa usiku mkubwa sana kwetu wa kihistoria, ndani ya bafu tulikuwepo viumbe viwili tukiwa uchi wa mnyama tukiwa tunachezea maji ya Jakuzi yaliyojaa mapovu mengi yenye marashi ya kuamsha ashki za ngono, tulichezeana kila mmoja akiufaidi mwili wa mwezake, Neema alikuwa mwanamke mzuri sana hasa mwili wake ukiwa umelowa maji, tena ukiwa na mapovu mapovu ndio ulizidi kupandisha mashetani yangu, sasa tulianza kulisakata rumba baada ya kila mmoja kumhitaji mwenzake, tulibinjuana na kuburuzana kwenye lile jakuzi huku Neema akitoa milio ya kike ya kunogewa na utamu uliomkolea, kuna saa alizungusha macho yake mazuri huku aking’ata ng’ata midomo yake kwa uhondo, nilimkunja alipokuwa kajinyoosha, nilimnyoosha pale alipokuwa amepinda, sikutaka mchezo ule uishie palepale, nilimnyanyua kwa nguvu kama mtoto na kumbeba, nikamleta chumbani na kumbwa kwenye sofa lilokuwa pale chumbani, hapo bila ya kumfuta mapovu nikambinua kisha vita vikaendelea, moyo wangu ulikuwa ukienda kasi sana, akili yangu ilikuwa haifanyi kazi sawia, nilipoteza ufahamu wa kufikiri kisawasawa, nikamnyanyua na kumtupia kitandani kisha nikawa namuangalia kama vile Jinni mla watu, yeye akawa anajiviringa viringa kama nyoka aliyejeruhiwa na kumwagiwa mafuta ya taa, ndio nilikuwa nimemjeruhi vilivyo na sasa alikuwa akinyonga nyonga akisikilizia utamu wa mapenzi yangu,
“ Come on Baby, Njoo unitese, nitese Bebe mpaka nife” Neema aliongea kisauti cha kiajabu ajabu kilichofanya Abdalakichwa wazi wangu apige guu pande kisha anyanyue kichwa juu kama Ile mijusi kafiri, kisha nikamrukia na kumsaga mpaka pale nilipoona ananing’ang’ania huku akiachia yowe kubwa ambalo lilipambana na sauti nyepesi ya muziki uliokuwa mule ndani, ukulele wake ulimaanisha kushangilia kufika mwisho wa safari ndefu, jasho lilikuwa likitutoka kama waoka mikate, sikutaka akinaiwe na ushindi wa bao moja, nikaendelea mpa mwisho alipofunga bao tatu mimi nikiwa nipo nyuma kwa bao mbili, lilikuwa ni pigano ambalo mpaka hivi leo ninalikumbuka,
Tulipumzika, Neema akiwa amelala katika kifua changu, hapoo nikamsikia akisema;
“ Wewe kweli ni mwanaume, leo umenikomba kila kitu, khaah! Sio kwa mikiki mikiki ile” Hapo nikamtazama kisha kukatokea ukimya, alafu akasema tena,
“ Furaha ya mwisho niliipata siku moja kabla wazazi wangu hawajauawa, ilikuwa miaka mingi iliyopita nikiwa mtoto, familia yetu tulikuwa mimi, mdogo wangu ambaye tumepishana mwaka mmoja hivi, ilikuwa miaka kumi na tano iliyopita ambapo familia yetu ilipatwa na tukio baya lililobadili maisha yangu, leo hata nisingekuwa hivi” Neema akasema, nikawa namtazama nikimsikiliza kwa utulivu. Akaendelea;
“ Nilikuwa nipo na Baba sebuleni, nikiwa ninamiaka kumi na nne tuu, ilikuwa likizo nikiwa nimetoka shule kwani nilikuwa kidato cha kwanza, Baba alikuwa akinipenda sana, sisemi kwamba mama hakuwa ananipenda, wote walikuwa wananipenda ila niliyekuwa karibu naye ni Baba zaidi, Mama yangu alikuwa anatumia muda mwingi na mdogo wangu wa kiume niliyemzidi mwaka mmoja” Hapo akameza mate kisha akaendelea,
“ Mama alikuwa akipenda kumsomea Mdogo wangu Bedtime Stori, hivyo alikuwa chumbani kwa mdogo wangu akimsomea stori, baada ya mdogo wangu kulala mama akarejea sebuleni akinikuta mimi na Baba tukicheza Game kwenye Tv, Mama aakawa ananisaidia tukimchangia Baba ili tumshinde” Nikaona akiachia tabasamu kwa mbali kama mtu aliyefurahishwa na kumbukumbu hiyo.
“ Wakati bado tunaendelea kucheza Ghafla mlango wetu wa sebuleni ukafunguliwa kwa nguvu kwa kuvunjwa, wakaingia wanaume wawili na wanawake wawili, wote wakiwa wameficha sura zao, wanawake wakiwa wamevaa hijabu, walikuwa wamebeba silaha, wakatuweka chini ya ulinzi” Alipofika hapo kwenye wanawake wawili waliokuwa wamevaa hijjabu nikakumbuka ile stori ya yule msela kule Jela, ni kama zilikuwa zinafanana lakini mbona yeye alisema miaka thelasini iliyopita, alafu Neema anasema miaka kumi na tano iliyopita, nikataka kumuuliza swali lakini akili yangu ikanionya na kuniambia niwe na subira.
“ Yule mwanamke akamfokea sana Mama yangu, nilikuwa najisikia vibaya sana kuona mama yangu akifanyiwa vibaya na wale majambazi, hata hivyo nilikuwa nikijiuliza sababu ya wale majambazi kutuvamia ilikuwa ni nini, kwani Baba alikuwa yupo tayari kutoa pesa zozote ili watuachie lakini hawakutaka, lakini nilimsikia mama akimwambia Baba, kuwa alimkanya Baba asiingie katika mahusiano na yule mwanamke, nikajua kuwa kumbe Baba alikuwa na mwanamke mwingine wa nje ambaye sikuwahi kumuona, yule mwanamke akanifuata mimi na kunikata kata na kisu, nilimuona Baba akijaribu kufurukuta lakini hakuweza, nikapoteza fahamu wala sikufahamu kilichokuwa kimetokea” Akameza mate, hapo nikawa nina maswali mengi sana, kisa cha Neema kilifanana kwa sehemu kubwa na kisa cha yule msela wa Jela, lakini utofauti pia upo, Dada yake yule msela alikuwa akiitwa Consolata ambaye wote walikuwa ni watoto wa Waziri, huyu anaitwa Neema, tukio la yule msela alisema Dada yake alichinjwa na kufa papo hapo, lakini Neema yeye anasema tukio lile alipoteza fahamu “ Itakuwa ni stori mbili tofauti zinazokaribiana na ukweli, kwanza Neema hajasema yeye ni mtoto wa Waziri” Nikawa nawaza, Neema akawa anaendelea,
“ Niliokolewa na Rafiki yake Baba ambaye alikuwa ni Luteni wa Jeshi, sijui ile siku alikuja kufanya nini, lakini anasema alikuwa akirudi kutoka kazini usiku ule, yeye alikuwa anakaa mtaa uliokuwa unafuata lakini barabara atakayoitumia inapita karibu na Geti letu, akiwa anakaribia kulifikia geti letu alishangaa kuona gari jeusi lenye vioo vya tinted likiwa limepaki karibu na geti letu alafu wakatoka watu wanne waliovalia kininja, wanawake wakiwa wawili na wanaume wawili, alisema, kitendo cha kuona watu wale kilimshtua akajua kuna hatari imetokea katika nyumba yetu, akapunguza mwendo wa gari wakati lile gari la wale majambazi likiondoka, akajaribu kusoma Platenumber lakini lile gari halikuwa na platenumber, akafika na kuingia katika geti letu, hapo akashtushwa na moto mkubwa uliokuwa ukiwaka katika nyumba yetu, wale majambazi waliichoma nyumba, pia alishtushwa na kuona Askari wawili wa ulinzi wakiwa wameuawa pale, hakuwa na muda wa kupoteza akaingia ndani ya Nyumba moto ukendelea kushika kasi, alipofika ndani kulikuwa na moshi mwingi huku moto mkubwa ukiunguza Masofa na mapazia, hapo alinikuta mimi nikiwa nimelala, Baba na Mama, alisema, alikuta mama na Baba akiwa amekufa, mimi nikiwa nimezimia lakini mapigo ya moyo yakiwa yanadunda kwa chini sana, akanitoa kwanza nje kisha akatako kurudi kumuangalia Mdogo wangu Paul, lakini hakuweza tena, Mdogo wangu alikufa na moto siku ile masikini” Neema akaanza kulia tena, uvumilivu ukamshinda alikuwa akitingishwa na Kwikwi kwa nguvu! Nikawa nambembeleza huku stori ile ikiwa imeniumiza sana, sasa nilihitimisha kuwa stori ya yule Msela na Neema ni stori mbili tofauti,
“ Walimchoma moto Mdogo wangu akiwa hai kalala chumbani, waliichoma miili ya wazazi wangu, Yule Baba mdogo aliniambia wakati anataka kurudi ili amuokoe Paul akashindwa kwani moto ulikuwa umechachamaa, akaondoka kinyemela akiwa kanibeba na kunipeleka nyumbani kwake ambapo kulikuwa na chumba cha matibabu, huko alikuwa akiita madaktari kwa siri hasa ambao hawanijui vizuri” Baba yangu alikufa huku uchunguzi ukipigwa danadana za kisiasa” Neema alisema machozi yakiwa yameulowanisha uso wake.
Ilikuwa simulizi yenye kusisimua sana, nilimuonea huruma sana Neema, kuna wakati nilitaka kumuuliza kuhusu kifo cha Waziri na mkewe pamoja na binti yake lakini nilipokumbuka kwenye stori ya Msela hakunielezea habari ya nyumba kuchomwa nikaona haina maana yoyote, lakini nikakumbuka kuwa Yule msela hakuwa amemalizia Stori yake, nikajikuta nataka kumuuliza Neema lakini ghafla simu ikaita, alikuwa Mama ananipigia, nikapokea, alikuwa akiniambia nipo wapi kwani usiku umeenda hivyo anawasiwasi, nikamuomba msamaha kwa kushindwa kumpa taarifa kuwa sitarudi siku ile hivyo tutakutana asubuhi.
***************************************
Kazi ya kumpeleleza Osman Midevu iliendelea, sasa nilijua yapo maficho mawili ya kuweza kumpata Bwana huyo, Ficho la kwanza ni kwake ambapo ni Mbezi Beach, Ficho la pili ni kule Tegeta walimpompeleka Kibadeni, tayari nilikuwa nimeripoti tukio la kushambuliwa kwa Kibadeni kwa Dr. Miranda wa Marekani kwa njia ya Email, nilijulishwa niendelee na kazi, suala la Kibadeni linashughulikiwa, nikaondoka mida ya saa moja hivi kuelekea Mbezi beach nikiwa na pikipiki wakati huu, sikutaka kutumia gari kwa kuhofia kukaririwa na wakazi wa eneo lile, nikavaa suruali ya jeansi, fulana nzito, na mabuti meusi, nikaiweka bastola yangu sehemu yake, kisha nikavaa miwani nyeusi usoni, kutoka Goba Mpaka mbezi shule sio mbali sana hivyo haikunichukua dakika chache kufika, giza lilikuwa limeshatawala, ungeshangaa ni kwa vipi niliendesha pikipiki kwa kasi nikiwa nimevaa miwani nyeusi usiku lakini miwani niliyokuwa nimeivaa ilikuwa ya kijasusi, hivyo ilikuwa inatumika hata kwenye giza unaona vizuri tuu. Nikaiegesha pikipiki yangu umbali wa mita thelasini nikiwa nimeipita nyumba ya Osman, nikaitoa sigara na kuipachika mdomoni, nikawa navuta huku nikitafakari jambo Fulani la zamani,
“ Taswira ta mwanamke aliyevalia nguo nyeusi zote ilikuwa ikipita kichwani mwangu, uso wake ukiwa na athari kubwa ya vipodozi, akaamka na kutoka, nami nikaamka nikaondoka pale nilipokuwa nimekaa, nikawa namfata kinyemela bila ya yeye kujua, kisha nikamuona akichukua simu yake na kubonyeza bonyeza, aalafu akairudisha simu kwenye mkoba wake, punde nikasikia kwa nyuma mtu anakuja, nikajibanza, nilishtuka kumuona Gibson akiwa anatembea kumfuata yule Mama’ Gibson anamfahamu vipi huyu Mwanamke? nikajiuliza“ Sikuamini kumuona yule mwanamke, nilifikiri nimeonana na mzimu, mara ya mwisho kumuona ilikuwa zamani kidogo kama miaka kumi hivi iliyopita” Nikawa nawaza, “ Kwa nini alimuita Gibson chobingo?” Nikawaza huku nikiwa navuta sigara yangu,
“ Mara ya mwisho kumuona yule mwanamke ilikuwa ni siku ambayo Baba yangu alinichukua tukaenda katika Hotel Fulani, alisema anaenda kukutana na mtu Fulani hivi, siku ile ilikuwa jioni ya saa kumi na moja hivi, tukafika katika Hoteli ile, tulimkuta Mwanamke mmoja wa makamo, mrefu kiasi, mweusi mwenye weusi mzuri wa kuteleza, anayejipenda, baada ya Baba kusalimiana naye, akaniambia nisogee nikakae pembeni kwenye meza ya mbali kidogo kuwapisha wazungumze, nikawapisha, nikiwa na maswali yule mwanamke ni nani, lakini kwa kazi ya Baba yangu nikaona swali langu ni lakijinga kwani Baba yangu ni kawaida kukutana na watu tofauti tofauti, nikaendelea na hamsini zangu nikishangaa bustani na miundombinu mizuri ya ile hotel, lakini kabla sijafika mbali kuufaidi uzuri wa mandhari yale nilishtushwa na maneno ya Yule Mwanamke akimuambia Baba;
“ Achana na jambo hili halitakufikisha popote, utajiingiza kwenye matatizo bure yasiyo na maana yoyote”
Baba akamjibu” Dora! Nisikilize vizuri kwa umakini. Aliyefanya jambo hili ni lazima atalipia kwa kile alichokifanya”
“ Kwa nini walikuwa wanagombana, ni jambo gani hilo ambalo Yule Mwanamke alikuwa akimzuia Baba kulifuatilia?” Nikawaza, jina la yule mwanamke ndiye Dora, sasa alikuwa anafanya nini na Gibson kule chobingo siku ile ya Tuzo za shindano la Tanzania Got Talent, “ Hapa lazima kutakuwa na jambo limejificha, itabidi nianze kumfuatilia huyu mwanamke” Nikawaza, lakini ghafla nikashtushwa na gari likitoka katika geti la nyumba ya Osman, lilikuwa gari jeusi lenye vioo vyeusi, la gharama na lenye kuvutia sana. Lile gari likaondoka nami nikalifungia Mkia kinyemela bila ya wao kujua, tukafika Bagamoyo Road tukakatisha mkono wa kushoto tukielekea Mjini, tulipofika Makumbusho lile gari likaingia kituo cha mafuta kujaza mafuta, kisha likaendelea na safari, ni mpaka tulipofika Maeneo ya Upanga, likakatisha kama linaingia barabara ya Kinondoni makaburini, kisha likakata kulia tena, hapo nikaliona likisimama kwenye Geti kubwa jeusi ambapo ndani yake kuna jumba kubwa la ghorofa, Geti likafunguka kisha lile gari likazama ndani, bila ya kupoteza muda nikaipaki Pikipiki yangu kisha nikaenda kwenye ule ukuta, nikazitengenisha nyaya za ulinzi zilizokuwa juu ya ule ukuta kwa kutumia kifaa maalumu cha kuzuia umeme usipite, kisha nikazama ndani, hapo nikapokelewa na uwanja wenye vigae maridadi na magari matatu, moja likiwa la ubalozi, la pili likiwa la binafsi na jingine ni lile nililokuwa nalifukuzia, jumba lilikuwa na giza kwa ndani isipokuwa sebuleni, nikaona Mbwa mkubwa mweusi akiranda randa kuzunguka lile jumba, Getini kulikuwa na kijumba cha mlinzi ambapo ndani yake nilimuona mwanaume mmoja aliyevalia sare ya rangi ya dark blue, nikajua alikuwa mlinzi, upande wa pembe ya kushoto wa ile nyumba kulikuwa na bustani yenye miti ya maua na ukoka, na viti kadhaa vya kupumzikia, pia kulikuwa na vyungu vikubwa vyenye maua ndani yake, nikashuka nikiteleza kama nyoka kwenye mwamba, nilipojihakikishia nipo salama nikaitoa bastola yangu mafichoni, nikawa nimeishika, nikakimbilia chungu kilichokuwa mbele yangu, nikajibanza, kisha nikapima mzunguko wa sauti na hewa eneo lile nikaona bado hali ni shwari, nikasonga kwenye chungu kilichokuwa mbele yangu nikijihami na kugundulika na yule Mlinzi na lile Jibwa kubwa aina ya Germany Sherperd. Nilikuwa nimefika kwenye Karibu na Kinoki ya ile nyumba, ambapo kulikuwa na taa ikimulika, hapo nikalisogelea dirisha nikiwa nimeinama lakini ghafla nikasikia sauti ya mbwa akija, nikageuka, alikuwa akija nilipokuwa lakini ghafla tena nikamsikia yule mlinzi akimuita kwa jina lake, akamfuata, “ Afadhali! Atakuwa hakuniona” Nikashusha pumzi nikiwa namtazama yule Mbwa mwenye mkia mnene wenye afya, nikachungulia tena dirishani, lilikuwepo pazia lililokuwa linanizuia nisione vizuri, nikawa nasikia watu wakizungumza bila ya kuwaona,
“ Imekuwa kheri mmekuja ndugu zanguni, nimepigiwa simu na mshirika wetu ambaye yupo katika ile hopsitali ya Waingereza, Kama ulivyoniambia jana Mkuu kuwa Mna mtu wenu mulimteka miezi kadhaa iliyopita, lakini mkashangaa haripotiwi kwenye vyombo vya habari tangu mlipojaribu kumuua, mkawa na hofu kuwa kama hajatangazwa basi atakuwa ameokolewa” Sauti ya kiume nyepesi ilikuwa ikizungumza, nilishtushwa na maneno hayo, tayari niliona Maisha ya Kibadeni yapo hatarini, nilijua wanamzungumzia yeye tuu wala asingekuwepo mtu mwingine.
“ Ni lazima atakuwa hai, tena ameokolewa na Yule mwehu anayeitwa Peter Mirambo, Siku ile Peter Mirambo alivyotutoroka tunahakika alienda kumuokoa Kibadeni kwa msaada wa maelekezo ya yule mlinzi wetu mwenyewe, kwa hiyo unasemaje Balozi” Sauti hiyo ilifanana kwa kiasi kikubwa na sauti ya Osman, nikajua ndiye mwenyewe, nikawa najiuliza huyo anayeitwa Balozi ni balozi jina au Balozi cheo,
“ Tayari nimefanya kama mlivyosema, nimeagiza kijana wangu niliyewapa aende akatekeleze mauaji, muda mfupi ujao” Maneno hayo yalinifanya niamke na kuondoka mbiombio bila kujali kuna mbwa au mlinzi, yule mbwa aliponiona nikikimbia akanikimbilia lakini tayari nilikuwa nimemzidi hesabu, nikauparamia ukuta na kupanda juu huku nikikoswa koswa na meno ya yule mbwa, nikatokea upande wa pili, bila kupoteza muda nikachukua pikipiki yangu na kutokomea nikimuwahi Kibadeni asije kuuawa, nusu saa nilikuwa nimesimama mbele ya Geti la Ile hospitali nikaingia ndani ya jengo kisha nikawa naifuata Lifti, wakati naikaribia Lifti nikapishana na mwanaume mmoja aliyekuwa kavaa kapero kuficha uso wake, akili yangu ikajua alikuwa ndiye muuaji aliyetoka kufanya mauaji, akawa anakuja kwa mbele yangu huku akijitahidi kuficha uso wake nisiuone, tukapishana hapo nikageuka nyuma kumtazama, naye akatembea kwa hatua kama saba hivi akageuka nyuma hapo tukatazamana alafu kwa haraka akageuka na kuanza kukaza mwendo, nikaona nimfuate, nikamfuata naye akawa anasonga zaidi, nikawa namuita, “ Oya! Wewe! Simama!” Akawa anaongeza kasi zaidi na zaidi akaifikia gari nyeusi iliyokuwa imeegeshwa akapanda nikiwa namuwahi akawasha gari akaondoka, hapo nami nikaiwahi pikipiki yangu na kupanda upesiupesi, kisha nikaitoa getini na kuanza kulifukuzia lile gari, nililkimbiza lile gari likawa linakata mitaa, yule mwanaume alikuwa anajua kuendesha gari sio utani, tutatokea Kariakoo kisha akanirejesha tena Posta, hapo akakatisha kulia kwa haraka kisha nilipokatisha nami nikakuta lile gari halipo ila kuna barabara mbili moja imekata kulia nyingine kushoto, nikafanya uamuzi wa haraka, nikakata kulia tena, hapo nikatembea na ile barabara nikiwa na pikipiki yangu, nikakata kushoto nikaikuta ile gari imepaki, nikashuka upesi nikatoa bastola yangu, nikawa naikaribia lakini kwa mbali kama hatua hamsini hivi nikaona mtu aliyevaa kofi akiwa anatembea, kisha akakatisha kushoto, nikamkimbiza kwa kasi nikiwa nimeiweka bastola yangu kuielekezea juu ikiwa mbele yangu, nikaikuta ile kona, nikamuona yule mwanaume aliyevalia kofia akiwa yule na mwanamke hivi, nilipowakaribia nikasema; “ Tulieni hivyo hivyo” Wakageuka nilishangaa kuona hakuwa yule mwanaume niliyekuwa namkimbiza niliyemuona kule hospitalini, nilibaki nimetekewa nikiwa nimechukizwa na kitendo kile cha kuzidiwa akili,
“ Mnatoka wapi usiku huu?” Nikasema, nikiwa nazuga, nikawaona wakitazamana wakiwa na hofu, ni kama mtu na mpenzi wake waliokuwa hawaelewi jambo lolote.
“ Kaka tusamehe, hatutatembea usiku tena” Yule mdada akasema akiwa anatetemeka kwa hofu, nikaona napoteza muda wangu bure, nikawaamrisha wakimbie, walitoka nduki sijawahi kuona, kidogo nicheke kwa jinsi mwanamke alivyokuwa anakimbia kwa kasi kuliko mwanaume, kwa jinsi alivyo mrembo wala usingetegemea kama anaweza kukimbia namna ile,
Nikarudi Hospitalini, baada ya kumaliza Lifti nikakuta Kibadeni akiwa ananitazama, kisha akatazama chini kama ananionyesha jambo Fulani, nikanona Dripu lililokuwa limepasuka kwa kukanyagwa, Nilifurahi kumkuta akiwa mzima, lakini kwa mazingira yale niliyoyakuta nilitamani kujua kilichokuwa kimetokea lakini Kibadeni hakuwa na uwezo wa kuongea, bado alikuwa anaumwa sana. Nikawasiliana na Dr, Miranda akaniambia ni mhamishe Wodi, alafu kuhusu walinzi haina shida atatuma usiku uleule.
“ Lakini Mkuu humu hospitali yupo Informer wao anayewapa taarifa” Nikasema,
“ Fanya nilichokuambia, mhamishe kwanza kisha mtafute huyo mtu, hakikisha umpate usiku huuhuu kabla hapajakucha” Dr, Miranda akasema, kisha simu ikakatika, tulikuwa tunawasiliana Kupitia Telegram, punde akaingia Daktari akiwa anapumua kwa woga,
“ Vipi Mkuu, imekuwaje?” Akaniuliza
“ Kama unavyoona kuna mwanaume alikuwa anajaribu kumuua Kibadeni”
“ Dr. Miranda kanipigia simu ndio kanipa taarifa, kasema nisubiri vijana wa ulinzi wakija atanipa maelekezo” Yule Dokta akasema, “ Kumbe timu ya Dokta Miranda ni kubwa kiasi hiki” Nikawaza.
“ Mimi ndio nimetoka kuongea naye sasa, hivi kasema niondoke sasa hivi”
“ Uondoke! Uende wapi?’ Dokta alikuwa akiongea kwa wasiwasi mpaka nikawa nahisi kuna jambo linamsumbua,
“ Ni lazima msaliti atafutwe, lakini sasa hivi naenda kukutana na huyo mwanaume aliyetaka kumuua Kibadeni” Nikasema,
“ Ni kweli haiwezekani watu wabaya wajue Kibadeni yupo hapa, wakati hii ni siri ya watu wachache sana, sasa utampata wapi huyo mwanaume muuaji?”? Akaniuliza,
“ Subiri utaona” Nikasema, kisha nikatoka nikimuacha anasemasema akitaka niendelee kubaki, mlangoni nikapishana na muuguzi wa kike, wala sikuongea naye jambo lolote nikaondoka,
“ Nani aliyeipasua lile Dripu” Nikawaza, nilikuwa narudi kwenye kule nilipowaacha wale vijana wawili wakike na wakiume, nilijua tuu lazima kuna mchezo walikuwa wameucheza kunizuga, nikafika mitaa ileile nilipowaona wameingia katika nyumba moja hivi baada ya kuwaamrisha wakimbie, nilikumbuka maneno ya yule dada kuwa wanaishi mtaa ule akaninyoshea kidole nyumba waliyokuwa wanaishi, nikafika palepale nikaigesha pikipiki yangu, nikabisha hodi, baada ya kugonga kwa mrefu bila kufunguliwa, nikatoa funguo maalum nikaufungua mlango na kuzama ndani, nikapokelewa na korido yenye kagiza hafifu kisha nikapokelewa na njia mbili, njia ya kwanza ilikuwa yakupanda ngazi, yapili ilikuwa inanielekeza kwenye Lifti, nikajiona mjinga nilipokumbuka nilivyokuwa napiga hodi, nilikuwa nimechanganyikiwa, unapigaje hodi kwenye nyumba ya ghorofa yenye wapangaji wengi, nikakumbuka yule mwanamke alikuwa amebeba funguo yenye kibao kilichoandikwa namba 15, nikabonyeza lifti mpaka kwenye floor ya kumi na tano, hapo nikapokelewa na mlango uliokuwa umefungwa wenye maandishi meusi yaliyosomeka Namba kumi na tano, nikatoa ile funguo nikaufungua mlango nikakutana na kelele za muziki, walikuwa wakicheza muziki, waliponiona wakapagawa, baada ya kuwaminya sana wakamtaja Dakatari ndiye aliyetoa siri ya kuwepo kwa Kibadeni hospitalini pale, walimtaja kwa jina moja Dokta Deus, nikampigia Miranda kuthibitisha jina la yule Daktari akaniambia jina lake ni Deus Zebaki, nikamuambia kuwa ndiye msaliti.
Hapo kumbukumbu zangu zilikatika nikiwa nimelewa tilalila, nilikuwa nakunywa pombe nikiwa Mbwii, zilikuwa kumbukumbu za mlevi zenye kujichanganya changanya, hata hivyo zilikuwa na ukweli kwa kiasi kikubwa, muda ule niliyekuwa nikimuwaza ni Dora, niliyemuona akiwa na Gibson siku ile ya Shindano la Tanzania Got Talent(TGT), nilikuwa nimelewa huku nikimtazama Dora aliyekuwa na Yupo na Binti mmoja aitwaye Semeni ambaye nilikuja kugundua alikuwa ni mtoto wake. Ingawaje nilikuwa nimelewa sana lakini bado akili yangu ilikuwa ikifanya kazi vizuri. Mwili pekee ndio ulikuwa hauna nguvu ya kusimama, hapo ilikuwa katika hoteli kubwa ya kitalii iliyokuwa Stonetown, Zanzibar.
*************************
ITAENDELEA, KESHO MCHANA,
Kitabu cha "Mlio wa risasi harusini" Kipo tayari
Softcopy 5,000/=
Hardcopy 15,000/=