Hussein Massanza
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 1,016
- 2,195
Asante sana masimulizi yenye hamasa na ya kizalendo, angalau umefika kileleni, na unaweza kueleza vema vilele vya aina zote ulivyowahi kufika bila kusimuliwa. Nimehamasika na nitaupanda huu mlima kwa heshima ya uzi huu. Nimesikitishwa tu na ukweli kuwa wapandaji wengi ni wageni.
Sawa mkuu.Kwa mimi nafikiria kuja kupanda tena miaka ya mbeleni uko ila bado sijapanga nitaenda lini ila kwa ushauri mdogo tu kwa wanaotaka kupanda mlima kilimanjaro hauhitaji mazoezi sana ili ufike kileleni labda uwe mtu wa kushinda kwenye gari kutembea huna kumbukumbu ulitembea lini hata nusu saa kwa siku hapo fanya mazoezi mepesi tu kinacho washinda watu wengi kufika kileleni ni kwa sababu mlima kilimanjaro unajitengenezea hali yake una zaidi ya hali3 utakazo kutana nazo equatorial,Savannah, mediteranian nk so unakuta mtu mwili wake unashindwa kuhimili hali hii nyingine anaweza ukiwa kwenye Savannah unaweza hata huumwi kichwa ila ukienda sehemu nyingine hali inabadirika unaanza kuumwa na kunakua na mgandamizo wa hewa so kunakushinda
Cha kufanya pima afya yako vaa na beba mavazi na vifaa rafki tokana na ushahuri wa watu wanaokuongoza naamini unaweza toboa maana kule wanaenda wanajeshi ila kunawashinda sababu ya hali ya hewa ila ma porters na tour guiders muda mwingine unakuta wamevaa t-shirts na suruali tu na they're fine ila wewe unavaa mikoti na mikoti ila bdo hali inakusumbua tu
Mimi pia nilipita njia nzuri ya marangu na baridi lipo kuanzia mandara me siku ya kwnza tu betri ya simu ilikata moto wakt sikuitumia hata
All the best kwa mwendaji yeyote mwaka huu
Sent using Jamii Forums mobile app
Lile ziwa naskia kuna sehemu kwa upande wa Tanzania lilihama kabisa likahamia pale lilipo sijui ni kweli au ni maneno ya watuLile ziwa nilishafika mkuu lipo chini sana ni kama unashukia kwenye kamgodi flan hivi
Unasema ukweli mie nilirudia hapaUle mlima hauna mwili wala nini cha msingi uwe umefanya mazoezi ya kutosha na uombe tu hali ya hewa isikukatate....hali ya hewa ikikugomea unarudishwa siku ya kwanza tu
Sent using Jamii Forums mobile app
Ujuzi ulio nao wa kupanda dushe unatosha![emoji4][emoji4][emoji4]
Aisee mkuu pale nimeenda ..kuna mandhari nzuri na ziwa ni la kipekee..lina kina zaidi ya 300 m..na utapata na historia ya jinsi hilo ziwa lilitokea. Jitahidi uende mkuu.(sehemu ambayo natamani niende ni Ziwa Chala.....
Jamani mnaisahau njia ya Umbwe njia ngumu na ndefu kuliko zote nimepanda kwa njia hio 3 timesHuyo Laini ,we kiboko.vipi ulitoboa
Machame njia yangu.
Tumezoea kupanda mara nyingi lakini hata sisi mara ya mwanza inakuwaga hellTulifika sehem (Tulitumia njia ya Machame) wakasema Mlima umepumua, unatoa gesi flani inaumiza vichwa sana, watu wengi wanakua na hali mbaya kuliko maelezo. Kuna mzungu kidogo amalize mitungi yote ya oxygen. Alishushwa kwa machela hadi chini.
Ila wale wagumu hawana mapafu ya kawaida. Kule sio kwa kuishi au kufanya kazi muda mwingi.
Yaani lile ni downwarped lake...mwanzoni palikua na mlima na juu ya mlima alikua anaishi mzee mmoja anaitwa mzee chala. Baadae mlima ukadissapear ndo likatokea hilo ziwa. Na wanadai chanzo cha maji yake ni mt. Kilimanjaro. Pia ziwa liko mpakani mwa kenya na tz. So tunashareLile ziwa naskia kuna sehemu kwa upande wa Tanzania lilihama kabisa likahamia pale lilipo sijui ni kweli au ni maneno ya watu
Liko wilaya ya Rombo -Kilimanjaro karibu na KenyaLipo sehem gani hilo ziwa aisee