Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

naunga mkono hoja,jeshi letu liheshimiwe !! NI jeshi lenye sifa zilizotukuka Africa yote ,Sasa tusianze kulichukulia poa . Jeshi halifungamani na siasa zaidi lina monitor wanasiasa na siasa zao ,na kulinda mipaka ya nchi na raslimali za nchi!! CDF sawa anateuliwa na rais lkn baada ya uteuzi ,ni mtu mkubwa kuliko ,ameshika hatma ya rais na nchi pia .salute kwa ma generals na soldiers wote,kwa kulilinda taifa letu na kulipa heshima taifa letu ,kimedani!!
 
Watu ( Members ) walio Werevu ( Intelligent ) kama Wewe hapa JamiiForums mpo Wachache sana. Hongera kwa Ulichokiandika Mkuu.
 
Tatizo hp jamii forums unaweza ukawa una-argue na mtu ambaye hajamaliza hata darasa la saba, Tutafutieni namna ya kuwa na forum zinazoendana na viwango vya elimu na uelewa tunaweza kuchangia vizuri na kuelewana vinginevyo tutaishia kutukanana na wa watu ambao siku ukibahatika kuwaona utajutia ulichokifanya. Huyu mtu hajuia hata muundo wa serikali, hajui maana ya wizara. Hajui kuwa taasisi yoyote nchi hii lazima iwe chini ya wizara fulani na kila wizara bosi wake ni waziri. Sahv ameishia kutukana tu. Hana anachoelewa pengine amelewa.
 
Kuchanganya siasa na jeshi ni kama kuchanganya mafuta na maji, lazima moja itakuwa juu na nyingine chini na siku zote mwanajeshi hawezi kukubali kuwa chini hiyo ni asili (Nature) nenda kokote duniani hata kama atakubali kujifanya chini ni ile ya kinafiki, unapoapa jeshini wewe unakuwa jamii nyingine ndio maana wanatengwa, siasa isipokuwa na mipaka inaleta muingiliano wa majukumu na kufundishana kazi ambazo sio utaratibu ndiposa mara nyingi jeshi linaamua kuasi.
Nawasilisha
 
Genta hivi unajua kuwa waziri wa ulinzi akifa anapigiwa mizinga 17? au umejisahaulisha! halafu unajisahaulisha kuwa hili ni jeshi la wananchi! wananchi ndio wanamchagua Rais ambaye anakuwa ndio Amiri jeshi mkuu!?
pia nafkiri huelewi vizuri majukumu ya mawaziri wewe
 

anajizima data.

waziri ni msimamizi wa sera wa wizara.
utakuwa ni upunguani kumzidi protocal mtu anayepigania maslahi yako.
waziri wa ulinzi ni incharge wa CDF ila sio boss wa CDF,anachanganya huyu.

CDF ana wakubwa wake kiutendaji wizarani,ana katibu mkuu wizara ana waziri wake pia,hao watu huwapelekea mipango na maombi yake ya matumizi mwaka mzima.
 
Mkuu you are dead WRONG!
CDF siku zote yupo chini ya Waziri wake wa Ulinzi kiserikali.
Hii ni licha ha ukweli kwamba Waziri wa Ulinzi hana mamlaka wala madaraka ya kumuingilia CDF na jeshi kwa ujumla.
Waziri wa Ulinzi ni kama muwakilishi wa jeshi kiserikali ila hawezi kuliamrisha jeshi kwa aina yoyote.
Kiutendaji CDF yupo chini ya Commander in Chief moja kwa moja.

Waziri Maokola Majogo alijaribu kuliamrisha jeshi wakati fulani, cha moto alikipata, na akaondolewa unceremoniously uwaziri.
 
Hii taasisi ya Jeshi ni ya kipekee inayotakiwa kuheshimiwa.
Jeshini kuna kila taaluma iliyoko uraiani kasoro taaluma ya Magereza japo wana jela zao. wana mahakama zao zinaitwa court martial kule hakimu ni mkuu wa kikosi na hakuna kujitetea wala wakili

Jeshini wapo ma prof na ma dr wa phD.Ukitaka kujua jeshini kuna kila taaluma kuna siku ma dr Muhimbili waligoma wanajeshi wakaenda kuchukua hatamu kusaidia maisha ya watu.Kuna siku waongoza ndege waligoma wataalamu wa jeshi wakaenda uwanjani kukamata hatamu.
Jeshini kuna madaktari wa kutibu,wahasibu,walimu,ma injinia wa umeme,majengo mechanical,chemical nk wataalamu wa IT.Iddi Amini alivobomoa daraja la Kagera ma injinia wa Jeshi walijenga la muda kwa mda wa chini ya wiki moja kazi ikaendelea ingekuwa ma injia wa uraiani wa 10% lingechukua muda mrefu na Iddi Amini angeikalia Kagera vizuri zaidi.
Nchi ya Marekani na Urusi pia mambo makubwa ya kiutafiti yanafanywa na wanajeshi.Hata waliokuwa wanakwenda anga za mbali hadi mwezini walikuwa wanajeshi kina Neil Armstrong huyu alikuwa ni profesa na mwanajeshi na alikuwa ndio mission commander ya kwenda mwezini.

Nimeona niongezee haya kuonyesha msisitizo taasisi hii ilivyo muhimu sio taasisi ya kuchukuliwa ki spot spot kwa waziri ulinzi kupigiwa salute hapo sina objection ninachokataa mkuu wa wilaya eti CDF anampigia salute kisa tu eti ni mkuu wa ulinzi na usalama kwenye wilaya yake wakati CDF ni mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa nchi nzima kwa maana changa vikorokoro vingine polisi,magereza,uhamiani, vyote yeye ndio mkuu.
Hili halijakaa sawa mkuu wa wilaya kupigiwa salute na CDF
 
Safi Mkuu, ila ni Court Martial!
 


CDF awe chini ya Waziri aliyetokea wapi mkuu.?

Ni heshima TU lakini sio kiuhalisia na haitakuja kuwa hivyo. CDF ni habari nyingine kabisa. Achana na hicho cheo mkuu. Mawaziri wapo kwenye level ya mabrigadier General hata stahiki zao zinaendana lakini sio General.

Uzuri tunao magenerala wastaafu wengi TU angalia heshima walizotununukiwa kimataifa na kitaifa.

Waziri si Mbunge TU.
Waziri anaweza akapigwa hata vibao na Polisi unasema Nini wewe mkuu.
Kama unabisha kamuulize Aliyekua Waziri wa Sanaa ,utamaduni na Michezo. Alishikiwa bastola akaufyata. CDF ukimshikia bastola unachapwa risasi on the sport na hakuna hata kesi itakayofunguliwa popote itakua kama mbu TU amepukuziwa rungu. Mambo mengine tuyaache mkuu.
Achana kabisa na habari ya mkuu wa majeshi. 4 Star General ni habari nyingine kabisa. Ile ni serikali Mbadala muda wote na ipo standby kushika nchi muda wote. Ukiona nchi Ina Jeshi la hovyo hovyo ambalo halijajianda kuilinda katiba Muda wote ujue hiyo ni nchi ya manyani wanayoishi mwituni. Utulivu wa nchi ni pale Jeshi linapokuwa na raia mmoja TU anayetia amri Kwa CDF na sio wanasiasa wengine. Rais wa awamu ya Tano JPM alipoapishwa aliendesha nchi vizuri sana bila wabunge wanaoitwa Mawaziri alikaa karibu Mwezi mzima. Haiwezi kutokea nchi kuendeshwa bila mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama hata Kwa dakika Moja. Anaweza kukosekana Waziri wa Ulinzi bila athari yoyote.
Nchi sio Mawaziri mkuu ,Nchi ni Jeshi mkuu. Ni amiri Jeshi peke yake mwenye mamlaka juu ya CDF . Peke yake , yaani Rais peke yake ,unajua maana ya peke yake.? Ndio hivyo mkuu. Hizo zingine ni stori za vijiweni.
 
Vijana msome katiba, mtu pekee ambae yupo juu ya CDF ni raisi wa nchi ambae ndie amiri jeshi mkuu
 
Uwe na Iq ndogo au kubwa jukumu lako raia ni kutii sheria bila shuruti na hutapata matatizo mpaka unazikwa. Mengine yote ni mbwembwe tu.
 
Maelezo mengi ila..Umepuyanga.
 
Vijana msome katiba, mtu pekee ambae yupo juu ya CDF ni raisi wa nchi ambae ndie amiri jeshi mkuu
Soma tena post yangu uilewe na si kukariri .
Halafu rudi ukaisome tena katiba uniambie mahali na lini CDF anaingia kwenye Cabinet.
 
Hapa nadhani maoni mengi ni ya Hisia.

Uko utawala wa Kijeshi-Dunia haitamani Serikali iwe na utawala wa Kijeshi..isipokuwa tu pale ambapo kuna mazingira yasiyokuwa na Amani.

Serikali ya Wananchi ni Serikali inayowapa Raia kujitawala kadiri wanavyoona inafaa.

Jeshi ni Nguvu ya Serikali.

Nguvu ni Nguvu siyo lazima ukunje misuli.

Nguvu hutumika wakati inahitajika.

Wakati mwingi wa utawala wa serikal ya wananchi ni utawala bila Nguvu.

Kwa hivo Nguvu iko kutizama ni wapi inahitajika...lakini kama haihitajiki basi maisha ya kiraia yanapendeza kuendeshwa kuraia.

Serikali ya Kiraia inakuwa na Katiba...

Hiyo katiba ndiyo hulindwa na Vyombo vyenye Nguvu!

Wanaotekeleza katiba ni wawakilishi wa wananchi waliounda Serikali yao kulingana na katiba waliyoikubali.

Waziri wa ulinzi ndiye kiungo kikubwa cha Serikali ya wananchi na Vyombo.

Serikali ndiyo yenye uwezo wa kusababisha mapato...

Mapato yanatokana na wananchi
..

Mwisho wa saa wananchi ndiyo wenye Jeshi lao...

Vyombo vipo chini ya Serikali yao iliyoundwa kutokana na wananchi.

Hata mwili una jeshi...

Lakini kinachoongoza mwili siyo jeshi...

Jeshi lina tii Serikali!
 
Safari umechemsha kwa busara zako. Hujui kabisa itifaki. Waziri ni mwakilishi wa kisiasa wa taasisi hiyo. Na siasa ndio inatawala nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…