Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Sipendezwi na jinsi inavyolazimishwa sasa CDF kuwa chini ya Waziri wa Ulinzi 'Kiprotokali' wakati Waziri wa Ulinzi ndiyo anapaswa kuwa chini ya CDF

Ni kwa sababu hujawahi kuona lakini utaratibu ndio uko hivyo kiprotokali majeshi yote yanamsalute CDF, Vivyo hivyo magereza na wengine wanamsalute IGP

Na ni sahihi kwamba CDF ni mkuu wa majeshi yote uliyoyataja kutia ndani bregade zake zote , ndio sababu anaitwa mkuu wa majeshi sio mkuu wa jeshi
Acha uongo. IGP hampigii saluti CDF.
 
Marekani hawana waziri wa ulinzi, wana secretary General ambae ni Lloyd
Uongo mwingine huu. Marekani wana waziri wa ulinzi. Mawaziri wao hawatumii title ya "minister" bali huitwa "secretary". Ndio maana kuna Secretary of State (waziri wa mambo ya nje), Secretary of Treasury (waziri wa fedha), Secretary of Defence (waziri wa ulinzi) n.k
 
Yani unataka waziri apokee order toka kwa CDF??? hapana waziri lazima awe mkubwa kuliko cdf kiliko IGP. Hii nchi sio ya kijeshii
 
sio jeshi tu inawezekana chanzo cha haya matatizo ie ujinga, maradhi na umasikini inatokana na hii kasumba kuweka siasa mbele ya utaalamu ndio maana mambo mengi tunafeli saana.
 
Wapi uliona MKUU WA MAJESHI ANAKUWA MKUBWA WA WAZIRI WA ULINZI? Hapo USA tu tunaona Waziri wa Ulinzi ndio Top.
Anakuwaje chini ya waziri wa ulinzi hebu tuelekeze wewe unaefahamu itifaki.
 
Kitu Ambacho watu hawaelewi ni neno MAJESHI kama linavyotumika Kwa Mkuu wa Majeshi,
MAJESHI kama ilivyo/inavyo tumika Kwa CDF ni Vile vikosi vyote vilivyochini ya JWTZ,
Mfano Kikosi cha Anga, Maji, Nchi kavu nk ni vikosi vyenye yadhi ya kuwa jeshi kamili na inatambulika hivyo, Kwa hyo Neno MAJESHI halina Maan ya kwamba ni Majeshi mengine kama Polisi,Magereza,Uhamiaji nk isipokuwa kama nilivyoandika hapo juu, na Wakuu wa vyombo hivi haviwajibiki wa CDF isipokuwa Kwa Mamulaka za uteuzi (Rais).
Kwa Kifupi CDF ni Mkuu wa JWTZ na si vinginevyo.
Hivi vyombo vyote vya ulinzi na Usalama vinafanya kazi Kwa Kushirikiana sana,
Na Kutokana na ushirikiano huo, JWTZ kikapewa Hadhi kubwa Kwa Sababu ya Ulinzi wa Katiba na Mipaka ya Nchi na CDF kama Mkuu wa JWTZ akapewa Hadhi ya kuwa Mwenyekiti wa hivi hasa pale vinapotekeleza Majukum yake.
Na Hata ukiangalia wanavyokuwa wamekaa kama (watakutana pamoja) anaanza Mkuu wa JWTZ anafuata wa Polisi nk,
Kama Polisi wamefanya kazi ambayo inahitaji Ushirikishwaji wa JWTZ basi watafanya hivyo Hali kadhalika na vyombo vingine,
Kwa hyo Hakuna Mkubwa Kati ya Wakuu wa vyombo hivi Ila Mkubwa wao ni Rais,
Isipokuwa CDF amepewa Hadhi Kwa Sababu ya Hadhi ya chombo anachokisimamia,
Ni kama Wakuu wa Mikoa,
Hakuna Mkuu wa Mkoa Mkubwa kuliko mwenzie,
Isipokuwa muda Mwingi Mkuu wa Mkoa DSM anapewa Hadhi Kutokana na Mkoa wake lakin haina Maan kwamba ni Mkubwa kuliko Wenzie,
Kuhusu CDF kuwa chini au kwenda kujitambulisha Kwa Waziri nafikili ni Kwa sababu ya Katabia kalikozuka Awamu iliyopita Maan Viongozi wa kisiasa ilifikia hatua wakaona kama wako juu ya kila kitu.
Na Katabia haka kanaendelea Kwa Kasi Sana japo Muanzilishi wake hayupo,
Miaka ya Huko nyuma hatukuwahi kuona Maajabu kama haya ya kujitambulisha,
Ila Kutokana na Kwamba CDF ni mwanajeshi itabidi Tu akajitambulishe Kwa waziri wa Wanajeshi,
Maan Wizara ya Ulinzi ni Wizara ya Wanajeshi.
Buruguja hongera kwa kujiamini saana ila umeenda speed umepitiliza kituo.

CDF.

Ni mkuu wa majesh ya ulinz na ni mkuubwa kwa majeshi yoote.

Ndio maana ukakuta mzee aliweza move na cheo chake toka tpdf hadi magereza, amran kombe alimove na cheo chake toka tpdf hadi tiss na mifano mengine miiiiingi.

But kinachotokea ni ugawanyajw wa madaraka tu... Training ya igp sio sawa na jwtz ndio maana kunakuwa na mipaka...
 
Duniani Kote nchi ni ya Jeshi . Nchi yenye Jeshi Kubwa ndiyo nchi imara. Tanzania hatuoni umuhimu wa majeshi yetu Kwa sababu Mwalimu alikua msomi Halisi wa siasa na jamii na Dunia aliijua vizuri Kwa alikua ni Msomi aliyeelimika Kwa kiwango kikubwa sana. Nyerere hakuwa mjinga alipokua analitumia Jeshi lake kwenye vita za Ukombozi na kusaidia nchi nyingine. Aliwaweka Wanajeshi Bize na mambo ya nje na kuwasaidia majirani. Na hicho ndicho wanachofanya Marekana ni nchi za NATO. Nchi za Kiraia zinapaswa kulitumia Jeshi Kwa umakini mkubwa. Huwezi ukasikia Rais wa Marekani anawakoromea wanajeshi Kwa lugha za kudhalilisha. Hata Kagame analiheshimu sana Jeshi lake ikiwemo Jeshi la Polisi. Huku Afrika na hata Tanzania ni rahisi kusikia Rais au mwanasiasa analidhalilisha Jeshi au Polisi wakati huo huo anategemea kuiba kura Kwa sababu Majeshi yatamlinda. Yani ni Hopeless kabisa.

Jeshi ni serikali Mbadala ndio maana imepewa jukumu la kulinda Katiba Muda wote. Kuna maana kubwa uliyojificha nyuma ya Jukumu Hilo . Wanasiasa UCHWARA HAWAWEZI KUELEWA MAANA YAKE. IPO SIKU AMBAYO HAIPO MBALI WATAJUA MAANA YAKE. Historia Duniani Kote hua inatabia ya kuwapitisha wanadamu kwenye nyakati zinazofanana endapo hawatajifunza Kwa waliowatangulia katika nyakati zinazofanana.
Afrika maendeleo ya pamoja yatatokea Kwa mapinduzi na sio Kwa kugonga meza. Afrika ikiwa na Marais 5O kama Kagame na Museveni na Museveni Hakika Kwa utajiri uliopo tungekua tunauza mtungi wa Gesi KG 15 Kwa sh. 20000 na mafuta Petroli Sh. 1200/- kwa Ltr.

Kutoliheshimu Jeshi na kulipa heshima yake inatokana na matatizo ya nchi jirani.Hali inayopelekea wanajeshi wetu angalau kupata sehemu wanapoweza kwenda kuweka roho zao rehani ili wapate anagalu fedha za kuboresha maisha yao na hivyo kutulia na kuwaachia wanasiasa wa ndani ya nchi zao wakilamba asali na kuwakejeli wanajeshi wao . Hiyo ipo pia Kwa majeshi ya Polisi Afrika wanaachwa kama Kuku wa Kienyeji waishi Kwa rushwa na kubambikia watu Kesi ili waweze kuendesha maisha yao na kusomesha watoto wao ili watoto wao wasije wakarithi matusi na kejeli Toka Kwa wanasiasa kuwa hawajasoma ,hawana uwezo wa kuchanganua mambo ,hawajui kupeleleza, ni wababaishaji,wasumbufu, hawajui Sheria n.k lakini ndio wanaowatumia kuiba kura na kuchafua Hali ya utulivu kisiasa na wakishaingia madarakani wanawakejeli na kuwaona hawana maana yoyote na hawastahili kulipwa mishahara ya kuwafanya waendeshe maisha yao Kwa misingi ya Haki na uadilifu . Matokeo yake ni kuwa na mifumo isiyoeleweka na yenye mikanganyiko mikubwa. CDF ni International Rank na vyeo vingine vyote vya Kijeshi chini yake. Hawatakiwi kuwa watumwa wa kisiasa . Wanapaswa kuwa huru mbali na siasa. Raia mmoja TU ndiye mwenye kauli juu ya Jeshi ,yaani Rais basi mana ana mamlaka ya kumteua CDF na Kumtengua muda wowote. Wengine wote hawana jambo lolote la kiutendaji juu ya Jeshi na hivyo hawana maelekezo yoyote Kwa Jeshi zaidi ya blabla za sijui ilani sijui Nini wakati Jeshi na ilani ni vitu visivyoendania Kwani Jeshi linapaswa kulinda Mipaka ya nchi na Katiba ya nchi hata kama hakuna Rais Wala Chama. Yaani hata ikatokea Serikali yote wakaangamia Kwa baridi Kali au Upepo mkali wa kisulisuki Ukalizoa Jengo la Bunge la Kameruni Bado Jeshi litalinda mipaka ya nchi na Katiba mpaka Hali itakapokaa sawa. Hivyo nakubaliana na wewe kabisa kuwa Jeshi linahitaji kuheshimiwa na kuepuka jambo lolote linaloweza kuwafanya wanasiasa kujiweka juu ya Taratibu za Kijeshi Kwa namna yoyote ndani ya nchi zetu za Afrika.

Ni bahati TU Afrika Kuna nchi zenye Vita kama Kongo ,Sudani,Somalia ,Msumbuji, Burundi n.k. Hali inayowapa fursa baadhi ya wanajeshi wa nchi nyingine kufadhiliwa na Mabeberu wa nchi za magaharibi Kwa kulipwa fedha ili wakalinde kile wanachokiita amani. Hapo wanaopata fursa hiyo wanajipatia nafasi ya kuboresha maisha yao na kuvumilia manyanayaso ya wanasiasa waliojaa dharau na kejeli Kwa kushiba asali na kujiona wao wanajua kila kitu mpaka Medani za kivita Kwa sababu TU ya kuangalia Move za Kina Rambo wanadhani kuwa kumbe inawezekana mtu mmoja akalinda mipaka ya nchi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]


Nakuunga mkono hata kama hawatakuelewa lakini Iko siku watakuelewa. Siku Sudani na Kongo wakipata amani akili zitakaa sawa Kwa wanasiasa wa nchi za Kiafrika ,Watajua kuwa hakuna Serikali bila majeshi,hakuna heshima ya mahakama bila Majeshi ,hakuna heshima ya Bunge bila Majeshi. Hakuna amani bila Majeshi. Hakuna kula Bata na starehe bila Majeshi. Watu wamwagilia mioyo yao Kwa sababu Kuna majeshi yanayolinda usalama wa nchi.
Nimeishia pale uliposema kuwa Afrika ikiwa na viongozi kama Kagame na Museven tungeendelea.

Mimi nakuuliza, hao Kagame na Museven si wapo na ni maraisi?! Nchi zao zimeendelea kuzidi nchi zingine? Au hadi wafikie Madkiteta 50 ndio tuendelee, sio kwamba akina Kaguta na swahiba wake Paulo wangeonyesha kwanza mfano?
 
Hakimu mfawidhi anapigiwa salute na CDF? you are joking.Ngoja vita ije au yatokee machafuko ndio utajua sio sawa mambo mengine ni siasa hazima mashiko waliotutangulia walikosea sana kama ni kweli hiko cheo kinachezewa
Hayo mambo ya kupiga saluti kwa mahakimu na majaji,wanayafanya polisi sijawahi kuona mwanajeshi anapiga saluti kwa jaji au hakimu.
 
Hakuna Kitendo Kimenishangaza na Kimeniuma kama kuona Juzi CDF na Chief of Staff wake wakienda Kiunyonge na Kiuhuruma kwa Waziri wa Ulinzi Kujitambulisha.

Sijawahi kuona popote pale Waziri wa Ulinzi anakuwa Juu ya Jeshi tena Kiprotokali wakati Jeshi ni Serikali Kificho ya Kimedani na inayojitegemea na ambayo ikiamua muda wowote ule ichukue hatamu ya nchi inaweza na huyo ( huyu ) Waziri wa Ulinzi anakuwa si lolote wala si chochote.

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Hayati Mkapa na kidogo Mzee Kikwete waliwaheshimu mno CDF's wa Vipindi vyao na walihakikisha hawalazimishi Jeshi kuwa ni sehemu ya Siasa na Utawala wa Kiserikali.

Hayati Rais Dkt. Magufuli alianza kwa mbaali kutaka Kummiliki CDF (japo alikumbana na Ugumu kidogo) kwakuwa CDF Mstaafu Mabeyo anajitambua na ameiva Kimedani (Kijeshi ) pamoja na Protokali zake zote.

Kama kuna Kitu kimenishangaza na naona HATARI fulani mbeleni huko ni kuona Awamu hii ya Rais Samia huyu Waziri wa Ulinzi Bi. Stegormena Tax akipewa Madaraka makubwa juu ya Jeshi na CDF wake kitu ambacho si Kizuri na siyo cha Kiutaratibu kabisa.

Kwa Kawaida ilitakiwa baada ya CDF Kuteuliwa basi Kiitifaki Waziri wa Ulinzi ndiyo alipaswa kwenda kwa CDF ila siyo CDF na Chief of Staff kwenda kwa Waziri wa Ulinzi huku wakiwa na Nyuso za Huruma kana kwamba Wameamrishwa na Mtu wakati Wao ndiyo wana Mandate ya Kuamrisha.

Namalizia kwa Kuwaasa na Kuwaonya enyi Watawala ( Wanasiasa ) kuwa chezeni na Vitu vyote ila msicheze na Taasisi Nyeti kama ya Jeshi na kutaka nao wawe Wanasiasa kama nyie wakati Kiuhalisia wao ni Wanamedani na wako kwa ajili ya Ulinzi na Usalama Uliotukuka wa Taifa letu hili la Tanzania.

Nichukieni, ila yafanyieni Kazi yote!!!
Umenena vyema kabisa, japo mi ningependa hata ikiwa Waziri wa ulinzi na usalama atakuwa juu ya CDF kimamlaka basi awe anateuliwa tokea humo humo kwenye Jeshi ili awe anasimamia inshu za Jeshi kimikakati sababu ya kuwa mzoefu wa kazi na kujua namna gani ya kukabiliana na changamoto zote za Askari.
 
Uongo mwingine huu. Marekani wana waziri wa ulinzi. Mawaziri wao hawatumii title ya "minister" bali huitwa "secretary". Ndio maana kuna Secretary of State (waziri wa mambo ya nje), Secretary of Treasury (waziri wa fedha), Secretary of Defence (waziri wa ulinzi) n.k
Huwa mnapata wapi muda Wenu wa Kupoteza Kuwaelimisha Watu Wapumbavu na Wendawazimu kama huyo?
 
Buruguja hongera kwa kujiamini saana ila umeenda speed umepitiliza kituo.

CDF.

Ni mkuu wa majesh ya ulinz na ni mkuubwa kwa majeshi yoote.

Ndio maana ukakuta mzee aliweza move na cheo chake toka tpdf hadi magereza, amran kombe alimove na cheo chake toka tpdf hadi tiss na mifano mengine miiiiingi.

But kinachotokea ni ugawanyajw wa madaraka tu... Training ya igp sio sawa na jwtz ndio maana kunakuwa na mipaka...
Mzee alimove na Cheo chake Kwa Sababu alitoka JWTZ,
Huku alikohamia hawezi na hakuweza kutambulika kama Mej Gen. Ila alitambulika kama CGP yaani Mkuu wa Jeshi la Magereza ambae Kwa wadhifa wake wa CGP anakuwa level moja na hawa Wakuu wengine (CDF,IGP,CGI na DTISS).
Kumbuka Kwa upande wa JWTZ, waliokuwa au wenye Cheo kama Cha Mzee wapo wengi ambapo Mzee alipokuwa huko JWTZ alikuwa level moja na Wenzie (wanatofautiana Tu seniority) na alivyohamia Magereza, automatic akawa level nyingine kulinganisha na hao aliowaacha JW ambapo Kwa vyovyote vile lazim wamsalute hata kama Hakuwa senior alipokuwa JW.
 
Buruguja hongera kwa kujiamini saana ila umeenda speed umepitiliza kituo.

CDF.

Ni mkuu wa majesh ya ulinz na ni mkuubwa kwa majeshi yoote.

Ndio maana ukakuta mzee aliweza move na cheo chake toka tpdf hadi magereza, amran kombe alimove na cheo chake toka tpdf hadi tiss na mifano mengine miiiiingi.

But kinachotokea ni ugawanyajw wa madaraka tu... Training ya igp sio sawa na jwtz ndio maana kunakuwa na mipaka...
Ushasema trainings ni tofauti,halafu mmoja awe mkubwa kwa mwenzake,how?
 
Back
Top Bottom