Sisi Wakristo masikini tunanufaika vipi na shule za Kanisa?

Sisi Wakristo masikini tunanufaika vipi na shule za Kanisa?

Kumbe hili swali tunajiuliza wengi...
Pamoja na mafanikio haya ,Shule nyingi za Kanisa ,gharama zake za masomo ni ghali sana! Pengine kuliko hata shule za watu binafsi!
Hali hii huwafanya Wakristo wengi masikini wasinufaike na hizi shule!


Mmechangia kweli kanisa au mnalalamika tu kwa kuwa wengine walichangia? Mara nyingi wanaohojihoji matumizi ya kanisa ni wale ambao huwa hawachangi au wakichanga basi ni kwa mbinde na kwa masimango
 
Unajua watu kama wewe mnafikra za hovyo sana hivi mnafikiri sadaka ndio zinazofanya makubwa yote hayo kwenye kanisa???!hivi hamuonagi vitega uchumi vya makanisa? Sadaka ni ndogo sana usifikiri wanafaidika kiivyo, maendeleo ya makanisa mengi ni misaada ya wazungu kama hamjui hilo uliza mchungaji yoyote akueleze
Vitega uchumi vinatokana na nini ?
 
Unajua watu kama wewe mnafikra za hovyo sana hivi mnafikiri sadaka ndio zinazofanya makubwa yote hayo kwenye kanisa???!hivi hamuonagi vitega uchumi vya makanisa? Sadaka ni ndogo sana usifikiri wanafaidika kiivyo, maendeleo ya makanisa mengi ni misaada ya wazungu kama hamjui hilo uliza mchungaji yoyote akueleze
Msingi wa maendeleo ya kanisa ni michango ya waamini iwe zaka iwe sadaka vyote viko termed kama michango yao. Msingi wa ujenzi wa chuo, zahanati,benki, kanisa etc vyote hivyo % kubwa inatokana na michango ya waumini.
Swali fikirishi, je, hiyo michango baada ya kulinufaisha kanisa muumini wa kawaida ananufaika na nini?!
Au anaishia kupata ibada ya kuzikwa na kubatiza watoto wake?!
 
Ndio mjifunze makanisa sio taasisi za yesu ni taasisi za ujasiriamali kupitia jina la Mungu na Yesu !!!!na wajinga ndio waliwao!!ni pamoja na hao wanaopeleka watoto wao kwenye hizo shule!!
 
Leo matokeo ya Mitihani ya Darasa la nne na Form Four yametoka!

Kama kawaida shule zinazoongoza nyingi ni zile zenye Uhusiano na Kanisa, iwe kwa umiliki au kwa njia nyingine! Hii bila shaka inatoka na misingi Bora iliyowekwa!

Pamoja na mafanikio haya, Shule nyingi za Kanisa gharama zake za masomo ni ghali sana! Pengine kuliko hata shule za watu binafsi!

Hali hii huwafanya Wakristo wengi masikini wasinufaike na hizi shule! Kwangu mimi nafikiri hiki ni kinyume na misingi ya Ukristo na hata ubinadamu!. Ilitarajiwa basi wenye shule nao wanufaike!

Wote ni mashahidi Kwa mfano, upande wa KKKT kumekuwa na michango ya kuchangia Seminary kadhaa hapa nchini! Lakini ni vipi hawa masikini Wananufaika ambao ndio wanaochanga kuku na mbuzi wao na wengine huchangia kwa maombi ilhali ada za shule hizi ni sawa na kipato Cha familia masikini kwa mwaka mzima!

Je, hao hawana haki ya hii Elimu Bora!
Je, Kanisa linaona hii hali!?

Hali haipo tofauti pia ktk Hospitali za Kanisa,Waumini wengi hawana ubavu wa kuingia hospitali kadhaa za ambazo ni ghali.

Ni vipi Msharika wa Maskini wa Loita Dayasisi ya Meru anaweza kupata huduma Bora za afya ktk Hospitali ya Selian aliyaoichangia kwa miaka mingi!

Nafikiri kuna kitu hakipo SAWA! Ndani ya Kanisa na Sisi Waumini pia!

Tutafakari!
Mfumo uliopo ni wa kinyonyaji 100%. Shule hizo zinajenga kupitia sadaka Za maskini. Shule ikikamilika wanaoweza kusoma huko ni Watoto wa matajiri ambao pia hawakuijenga hiyo shule.
 
Sasa kama unaona hupendezwi si utoke??!mijitu mingine hovyo sasa unawaambia din nyingine ili iwaje??🙄🙄🙄 umasikini utawauwa nyie nyumbu, nenda kwenye din nyingine
Collective Imbecilization victim....pole sana!
 
Leo matokeo ya Mitihani ya Darasa la nne na Form Four yametoka!

Kama kawaida shule zinazoongoza nyingi ni zile zenye Uhusiano na Kanisa, iwe kwa umiliki au kwa njia nyingine! Hii bila shaka inatoka na misingi Bora iliyowekwa!

Pamoja na mafanikio haya, Shule nyingi za Kanisa gharama zake za masomo ni ghali sana! Pengine kuliko hata shule za watu binafsi!

Hali hii huwafanya Wakristo wengi masikini wasinufaike na hizi shule! Kwangu mimi nafikiri hiki ni kinyume na misingi ya Ukristo na hata ubinadamu!. Ilitarajiwa basi wenye shule nao wanufaike!

Wote ni mashahidi Kwa mfano, upande wa KKKT kumekuwa na michango ya kuchangia Seminary kadhaa hapa nchini! Lakini ni vipi hawa masikini Wananufaika ambao ndio wanaochanga kuku na mbuzi wao na wengine huchangia kwa maombi ilhali ada za shule hizi ni sawa na kipato Cha familia masikini kwa mwaka mzima!

Je, hao hawana haki ya hii Elimu Bora!
Je, Kanisa linaona hii hali!?

Hali haipo tofauti pia ktk Hospitali za Kanisa,Waumini wengi hawana ubavu wa kuingia hospitali kadhaa za ambazo ni ghali.

Ni vipi Msharika wa Maskini wa Loita Dayasisi ya Meru anaweza kupata huduma Bora za afya ktk Hospitali ya Selian aliyaoichangia kwa miaka mingi!

Nafikiri kuna kitu hakipo SAWA! Ndani ya Kanisa na Sisi Waumini pia!

Tutafakari!

Kwanza ungejiuliza umekuwaje masikini wakati Bibilia inasema uliumbwa utawale? Ungejiuliza Kwanini huyo Mungu awanague? Wachache wawe matajiri huku nyie wengi ndo masikini?
 
Una hoja unayopaswa kujibiwa basi zama zimebadilika pesa imetamalaki hadi altareni
 
Ukiwa na pesa na ukaoa na kuzaa nje ya ndoa utazikwa na padre ila ukiwa kapuku hata katekista haji utazikwa kiongozi wa kwaya.
 
Dini siku hizi ni bihashara.... Michango iliyopo makanisani kwa nyakati hizi aisee ni mtihani kwa kweli, Kuna michango ya Kila aina na huelew matumizi yake.

Lkn kuwepo na michango hii, si chanzo cha waamini kupoteza Imani yao katika dini. Tuendelee kumuabudu na kumtukuza Mungu wetu, maana ufalme wa mbingu unakaribia.

Ukipata nafasi ya kuchangia na moyo umekusukuma kuchangia bs ww changia tu, ukiona bado hujabarikiwa bs maisha yanaenda pia. Lkn km una uwezo wa kumsomesha mtt wako ktk shule nzuri na akapata elimu bora kbs, bs unampeleka tu. Na sie tusio na uwezo bs tutaendelea na kayumba. Lkn kukaa na kutegemea kanisa aah tutachelewa Sana.
Na usipochanga halafu wanakujua una kakipato wananuna kishenzi hawajui tu watu wanapitia mangapi mtaani!?
 
Kwanini uwe masikini tuanzie hapo..?pia tambua hizo taasisi hazijiendeshi bure..kuna bills wanalipa kama mishahara..maji..umeme..ulinzi..chakula..n.k
Unadhani sadaka yako ya buku kila siku ya ibada inatosha kulipia hizo gharama?

Kama uonaona elimu ni gharama jaribu ujinga.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
huu ni mfano wa majibu yanayotolewaga na viongozi wetu wa dini
Majibu ya kikauzu balaa 😀😀😀😀
 
Shule za dini zinazofaulisha vizuri ada ni kubwa hivyohivyo, za kiislamu nazo ni hivyo ila tofauti ni kwamba hazijengwi kwa michango ya waumini. Taasisi inayoanzishwa ndiyo inajenga, huku Tanga zipo zilianza kama madrassa, wanafundisha kwa ada na baadaye wakaja kufikia kuanzisha chekechea na kisha msingi mtaji ulipopanuka. Hatimaur wakaja kuleta sekondari zao.

Pia zipo taasisi zingine zilianzishwa na waislamu wanaojiweza, zikaja kumiliki shule zao.

Mfano Tanga kuna shule ya sekondari ada ni Sh Mil 5, na sijawahi kusikia imetoa div 4 au zero. Mwaka huu ina div 1 53, 2 zipo 19 na 3 zipo 5 tu.

Shule za kidini kuwa na ada kubwa si tatizo balo tatizo ikiwa inaendeshwa kwa michango na wanaotoa kiwa hawanufaiki. Ila kama iliundwa kwa nguvu za taasisi wakawekeza pesa ya kutosha si jambo baya hilo. Maana taasisi ni watu na hao watu wana maisha pia, inabidi wapate riziki kupitia huko.
 
Toa mfano wa hiyo ada kubwa. Ninacho kifahamu mimi kuna watoto wazaxi wao wana pesa lkn watoto zero brain wameshindwa kusoma hizo shule.

Sidhan kama ada ni kubwa kuliko shule binafsi sema tu wasajili watoto wazuri na wanakulia malezi ya Ki Mungu ndo maana wanafaulu.
Kuna shule inaitwa St.Joseph Cathedral, St. Francis hio ya mbeya hapo bila 4.5m kwa mwaka mtoto wako hasomi, shule za kanisa zote ada zao ni ghali sana...
 
Wakisomesha bure masikini elimu yao itashuka. Kanisa linafanya biashara na halipo tayari kupata hasara nendeni huko kayumba
Kwani yesu haangushi manoti kanisani?
 
Nyie masikini mnapata sifa shule zenu zimeongoza na kuwacheka waislam, kwani kwenye mpira timu yako ya ulaya ikishinda wewe shabiki wa nanjilinji unapata nini?
 
Back
Top Bottom