Sisi Wakristo masikini tunanufaika vipi na shule za Kanisa?

Sisi Wakristo masikini tunanufaika vipi na shule za Kanisa?

MAKULUGA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2011
Posts
7,828
Reaction score
10,527
Leo matokeo ya Mitihani ya Darasa la nne na Form Four yametoka!

Kama kawaida shule zinazoongoza nyingi ni zile zenye Uhusiano na Kanisa, iwe kwa umiliki au kwa njia nyingine! Hii bila shaka inatoka na misingi Bora iliyowekwa!

Pamoja na mafanikio haya, Shule nyingi za Kanisa gharama zake za masomo ni ghali sana! Pengine kuliko hata shule za watu binafsi!

Hali hii huwafanya Wakristo wengi masikini wasinufaike na hizi shule! Kwangu mimi nafikiri hiki ni kinyume na misingi ya Ukristo na hata ubinadamu!. Ilitarajiwa basi wenye shule nao wanufaike!

Wote ni mashahidi Kwa mfano, upande wa KKKT kumekuwa na michango ya kuchangia Seminary kadhaa hapa nchini! Lakini ni vipi hawa masikini Wananufaika ambao ndio wanaochanga kuku na mbuzi wao na wengine huchangia kwa maombi ilhali ada za shule hizi ni sawa na kipato Cha familia masikini kwa mwaka mzima!

Je, hao hawana haki ya hii Elimu Bora!
Je, Kanisa linaona hii hali!?

Hali haipo tofauti pia ktk Hospitali za Kanisa,Waumini wengi hawana ubavu wa kuingia hospitali kadhaa za ambazo ni ghali.

Ni vipi Msharika Maskini wa Loita Dayasisi ya Meru anaweza kupata huduma Bora za afya ktk Hospitali ya Selian aliyaoichangia kwa miaka mingi!

Nafikiri kuna kitu hakipo SAWA! Ndani ya Kanisa na Sisi Waumini pia!

Tutafakari!
 
Simple calculation ni kuacha kuchangia maana hakuna matokeo ya moja kwa moja kwa muumini ndio maana nashangaa wanaowasakama akina Gwajina etc.

Wote wanafanya kwa njia tofauti, unatoa pesa ananunua helicopter unatoa sadaka wanajenga shule na hostels lakini manufaa yake yananufaisha wenye “jiko”

Faith Based Orgs hazina tofauti na NGOs au mashirika mengineyo 😃😃
 
Simple calculation ni kuacha kuchangia maana hakuna matokeo ya moja kwa moja kwa muumini
Ndio maana nashangaa wanaowasakama akina gwajina etc. Wote wanafanya kwa njia tofauti, unatoa pesa ananunua helicopter unatoa sadaka wanajenga shule na hostels lakini manufaa yake yananufaisha wenye “jiko”
Faith Based Orgs hazina tofauti na NGOs au mashirika mengineyo 😃😃
Kweli kabisa! Hiyo sadaka tutunze tupeleke watoto shule zao.

Wao wajenge kwa vyanzo vingine!

Niliumia sana binti mmoja alikuwa analalamika anakatwa mshahara LAKI 2,Kuchangia ujenzi was kitega Uchumi wcha Kanisa Fulani jijini Dodoma!
Huu ni wizi!
 
Dini yetu ya ukristo imekaa kiupigaji zaid. sio elimu tu hata huduma zao zingine mfano za hospital ni gharama mno, dini ni baishara tu kama biashara nyingne.. ngoja maskin wafia dini watavyokuja kukushika mashati hapa.
Waje na hoja ....tumepumbazwa Santa!
Halafu unakuta tunawacheka wanaopeleka Kwa kina Gwajima,na Mzee was Upako ...tofauti n ndogo sana!
 
Kuna shule Fulani ya Kidini ipo Ruaha Mbuyuni, mtoto wako akiwa na uwezo darasani ...wanakuruhusu ulipe ada hata kwa awamu Sita😂😂😂

Ila kama mtoto ni zile kuunga Sheriaa msumeno...unalipa ada awamu mbili TU!
Hawa ni Wakristo...wanainajisi Injili !
 
Kuna shule Fulani ya Kidini ipo Ruaha Mbuyuni,mtoto wako akiwa na uwezo darasani ...wankuruhusu ulipe ada hatq kwa awamu Sita


😂😂😂

Ila kama mtoto ni zile kuunga Sheriaa msumeno...unalipq ada awamu mbili TU!
Hawa ni Wakristo...wanainajisi Injili !
 
ikibidi wewe jitoe sadaka, fanya kazi kama mtumwa mtoto wako asome huko unakolalamika ni bei.

kuna wazazi wanasomesha watoto wao hizo shule, wanajinyima sana aisee.

uwe unaamka hata saa kumi alfajiri unapambbana hadi saa nne usiku, osha magari, uza mifuko, uza uji, n.k.
 
Wakisomesha bure masikini elimu yao itashuka. Kanisa linafanya biashara na halipo tayari kupata hasara nendeni huko kayumba
Kama mnafanya biashara, SI mfaanye biashara nyie matajiri ,sisi maskini mnatuchangisha za Nini!

Unajibu kama umevimbiwa baada ya kula nje ya kaamba yako!😂😂
Na Hali ndio inauporomomosha UKRISTO DUNIANI, inaonekana ni biashara TU!
 
Kuna vitu vinashangaza.

Nimezikumbuka harambee ujenzi wa SAUT miaka ya 2000 mwanzoni

Kuna seminari toka zianzishwe miaka 20+ mpaka leo waumini jimbo zima wanachangishwa gharama za uendeshaji kila mwaka na wakati huo zinatoza ada kubwa tu.

Kama Biashara hiyo haina faida au wameshindwa kuisimamia si bora madarasa wakafugia hata kuku!

Kama vipi pawepo namna ya kuwatambua waumini wachangiaji ili wapate discount wakifuata huduma pale.
 
ikibidi wewe jitoe sadaka, fanya kazi kama mtumwa mtoto wako asome huko unakolalamika ni bei.

kuna wazazi wanasomesha watoto wao hizo shule, wanajinyima sana aisee.

nnda huko kilosa ndani ndani ukodishe mashamba ulime
Hii ndiyo Prof Chachage aliita Collective Imbelization....!
Ambayo Kanisa na CCM wanaitumia sana kuwachezesha Sindimba!
 
Kuna vitu vinashangaza.

Nimezikumbuka harambee ujenzi wa SAUT miaka ya 2000 mwanzoni

Kuna seminari toka zianzishwe miaka 20+ mpaka leo waumini jimbo zima wanachangishwa gharama za uendeshaji kila mwaka na wakati huo zinatoza ada kubwa tu.

Kama Biashara hiyo haina faida au wameshindwa kuisimamia si bora madarasa wakafugia hata kuku!

Kama vipi pawepo namna ya kuwatambua waumini wachangiaji ili wapate discount wakifuata huduma pale.
Mkuu nenda Kwa Manka kula Bia 2,naa kilo mojaa ya nanii...mwambie bill yangu!
Nitalipia sadaka niliyopanga kupeleka kessho,ya ujenzi was shule.
 
Back
Top Bottom