Acha upumbavu bana!..
.
Ukame upi?
Wewe unagizaga mafuta ya kula toka ukrein na urusi?
Mahitaji ya mafuta ya kula Afrika Mashariki yanafikia mpaka tani 2.5 milioni kwa mwaka. Kwa Tanzania mahitaji ni wastani wa tani 650,000 licha ya uzalishaji wa ndani ni wastani wa tani 290,000.
Uganda mahitaji kwa mwaka ni wastani wa tani 120,000 ingawa yenyewe inazalisha tani 40,000 tu.
Kwa nini bei ya mafuta ya kula imezidi kuwa mwiba Afrika Mashariki?
Nchi za Afrika Mashariki zinahitaji angalau wastani wa tani 2.5milioni za mafuta ya kula kwa mwaka kutosheleza mahitaji ya wananchi wake wanaokadiriwa kufikia milioni 300 hasa baada ya DRC kujiunga kwenye ukanda huo wa Afrika Mashariki.
Pamoja na mahitaji hayo makubwa, uzalishaji wa ndani wa mafuta ya kula haukidhi mahitaji hivyo kulazimika kuagiza mafuta kutoka katika mataifa ya nje.
Hata hivyo taifa kama Ukraine ambalo ni msambazaji mkubwa wa mafuta ya alizeti duniani imesimamisha shughuli na usafirishaji wa bidhaa hiyo kutokana na vita inayoendelea sasa nchini humo.
"Hapa kwetu, mambo ya Covid yalikuwa tayari yamesababisha bei ya mafuta kupanda kutoka 2,200Ksh mpaka 4,500Ksh ndani ya miaka miwili. Baada ya uvamizi (wa Ukraine) bei imepanda mpaka 5,100Ksh (dola 44$) ndani ya wiki moja", alinukuliwa na chombo cha habari cha Busness Daily cha Kenya, Mmoja wa viongozi wa sekta hiyo ya mafuta Abdulghani Alwojih.
Ukiacha vita vya Ukraine na sababu zingine za kiusalama pamoja na zile za kiuchumi na kisera, zipo sababu zingine kubwa mbili zinazotajwa wazi kuwa na mkono wake kwenye hili la kupanda kwa bei ya mafuta ya kula katika ukanda huu; mabadiliko ya hali ya hewa katika baadhi ya maeneo yanayozalisha malighafi ya mafuta ya kula pamoja na uwepo wa janga la Corona.
Kutokana na Covid-19 Malaysia pia ilipunguza uzalishaji wake kama ilivyo kwa Indonesia. Hilo limeongeza kuni za kupanda kwa 'moto' wa bei kutokana na uzalishaji wake kwenye soko la mafuta hayo.
Aghalabu kukuta sababu zote zinasadifu ukweli wa hali halisi ulivyo, wapo wanaotumia mwanya huo huo kwa manufaa binafsi kama anavyoeleza mtaalam wa masuala ya biashara kutoka chuo kikuu cha Ushirika, Moshi, Daktari Izack Kazungu; "Corona sawa, hali ya hewa sawa na vita ya Ukraine ni kweli imeendelea kuleta athari nyingi, lakini wapo wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakitumia mwanya huo kuongeza bei kiholela".
Kwa nini ni muhimu kushughulika na mafuta ya kula sasa?
Mwiba wa mafuta ya kula haupaswi kuachwa ukaozea ndani. Unapaswa kutolewa mapema hata kama utalazimika kutolewa kwa maumivu.
Wiki iliyopita Rais wa Tanzania, alimtaka waziri wake wa fedha, Mwigulu Nchemba kushughulikia suala la mafuta ya kula.
Mara kadhaa pia viongozi wa nchi zingine kama Uhuru Kenyatta wa Kenya na Paul Kagame wa Rwanda wamewahi kusikika wakizungumzia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo na bidhaa zingine za vyakula.
"Serikali za Afrika Mashariki, hazina namna ya kukwepa kulivaa hili, kwa manufaa ya muda mrefu, hata kama litawakosesha mapato ama kuwafanya kuingia gharama kubwa, hakuna njia ya mkato", anasema Dr. Izack Kazungu.
Wataalam wanataja mambo matano makubwa yanayoweza kusaidia kuleta suluhu ya muda mrefu na kuboresha sekta ya mafuta ya kula; kuwekeza katika uzalishaji wa mafuta kupitia kilimo cha kisasa cha mazao ya mafuta kama alizeti, pamba, nazi, mawese, karanga, korosho na ufuta. P
ili kuboresha sekta ya mifugo na uvuvi kwa ajili ya kupata kwa wingi mafuta yatokanayo na wanyama na samaki.
Suala lingine ni kuondoa tozo ama kodi zinazoongeza mzigo kwenye biashara ya mafuta ama shughuli za sekta ya mafuta ya kula wakati la nne ni kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya umeme na tano ni unafuu wa mafuta ya petroli na dizeli na kuboresha miundo mbinu ya usafirishaji.
"bado kuna mambo mengi ya kufanya hasa kwa upande wa serikali (Kenya) kwa mfano, kwa kupunguza 3% ya tozo ya RDL na IDF, kupitia gharama za mafuta (Petrol na Dizeli) na nishati ya umeme kama hatua zinazoweza kuchukuliwa', alisema Alwojih.
Kwa upande wa Tanzania, Juhudi za kupunguza pengo la mahitaji ya mafuta ya kula lilishaanza kwa msukumo wa waziri mkuu, Kassimu Majaliwa. Pamoja na zao la alizeti linalotiliwa mkazo, nchi hiyo imeanza kutekeleza mikakati ya kuendeleza zao la michikichi kwa kuanzisha Kituo Maalum cha Utafiti wa Mchikichi cha Kihinga.
Waziri mkuu huyo alisema kuwa hadi kufikia Mei, 2021 jumla ya mbegu 5,630,376 za chikichi na miche milioni 1.5 imezalishwa na kusambazwa katika Mikoa ya Kigoma, Katavi, Kagera, Rukwa, Mbeya, Pwani na Ruvuma.
Wakati hatua zinazofanana na hizi za Serikali za Afrika Mashariki zikendelea kuchukuliwa na kusubiriwa matokeo yake, je kwa sasa wananchi takribani 300 milioni wa ukanda huu waanze kufikiria kula 'vyakula vya chuku chuku" kwa maana ya visivyoungwa na mafuta na waendelee kuumia kwa bei za mwiba?
Pengine vyakula vya kuchemsha tu, kuoka, kuchoma ama vinavyotengeneza mafuta yake wakati wa kupika vinaweza kuwa mbadala kwa wakati huu. Ingawa matumizi ya karanga za kusaga, korosho au nazi hayawezi kupuuzwa
Chanzo BBC swahili 5/4/2012