Sitashangaa kuona Yanga inaanzia tena nyumbani na kumalizia ugenini

Red arrows tukamalizia Zambia na kuingia makundi CAFCC
nadhani Red Arrows walitolewa kwenye raundi ya awali na Agosto ya Malawi kwa hiyo hawapo kwenye shirikisho. Nadhani kiutaratibu Yanga atacheza na timu iliyoanza kwenye michuano ya shirikisho toka mwanzo na pia nadhani kikanuni Yanga ataanza ugenini.
 
nadhani Red Arrows walitolewa kwenye raundi ya awali na Agosto ya Malawi kwa hiyo hawapo kwenye shirikisho. Nadhani kiutaratibu Yanga atacheza na timu iliyoanza kwenye michuano ya shirikisho toka mwanzo na pia nadhani kikanuni Yanga ataanza ugenini.
Yanga anaanzia nyumbani kumalizia ugenini ndio kanuni ilivyo

Sent from my SM-G9650 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza kuanzia ugenini ukafa nyingi ukirudi nyumbani usipindue matokeo, kuanzia ugenini sio uhakika wa kumtoa mpinzani wako, hasa ikiwa uwanja wenu wa nyumbani hata kufunga magoli matatu hamuwezi.
Kumbuka Azam alichofanywa jana, alikula 3 ugenini.
 
Timu kuanza ugenini au nyumbani inategemea na points alizojikusanyia kwa kipindi cha miaka 5. Na utaratibu ni kua timu yenye points ndogo lazima icheze na giant mwenye points nyingi. Yanga hakuna points tulizovuna kwa kipindi hiki cha miaka 5 kwenye mashindano yeyote ya CAF, hivyo basi uwezekano wa kuanza nyumbani ni mkubwa sana kuliko ugenini.
 
yanga ina ubovu gani mkuu ama umesimuliwa mpira mtu kakimbizwa dk 600 sema haikuwa bahati kwa yanga
Mliachwa mcheze kwenye zone yenu (back passes nyinyi) halafu nyinyi mnajiona mmecheza bila kujua kama mliingia kwenye game plan yao.

Wale jamaa baada ya kupata goli hawakutaka kushambulia tean, ndiomaana ile siku pale Taifa walikuwa wanatafuta droo ila baada ya kuwafunga walifunguka wakawapelekea moto mpaka mkatamani mpira uishe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
huo mpira uliona peke yako tuliocheza kwenye eneo letu mkuu
 
Usidanganye, Simba ilipotolewa na jwanneng Galaxy ilianzia nyumbani na kumalizia ugenini[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787], taabu iko palepale.
Simba alianzia ugenini akashinda 2-0 Kwa mkapa Simba ikapoteza 3-1 ikatolewa Kwa gori la ugenini..
 
Hamna Akili za kucheza mechi kubwa
 
huo mpira uliona peke yako tuliocheza kwenye eneo letu mkuu
Mmepiga mashuti mangapi yaliyolenga goli kwa mkapa na huko Sudan? Leta takwimu hapa ili tuona kama mlikuwa na hatari yoyote kwenye goli la Hilal.
 
Duuu! Mwaka jana mlisema ni kombe la loser leo hii ni kombe muhimu #WajingaNyinyi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…