Siwezi kuficha furaha yangu kwa Yanga kula kichapo

Siwezi kuficha furaha yangu kwa Yanga kula kichapo

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001


Nipo hapa kuueleza umma kwamba mimi nisiwe mnaa. Furaha yangu kwa Utopolo kula kichapo haiwezi kufichika kwa uzalendo uchwara.

Nawaombea mkienda huko Algeria mchakazwe kama mbwa koko mkirudi msitamanike kabisa. Mna midomo sana

Nimefurahi sanaaaaaa
 
Hunishindi mimi. Kwa upuuzi huu lazima tufurahie.

IMG-20230528-WA0015.jpg
 
Haijaisha mpaka iishe!

Waarabu wanafungika, hawana mpira wowote bahati tu imewabeba!

Nabi kachelewesha sana sub. Leo kachemka! Alitakiwa half time irudi timu ingine baada ya kuwa Nyuma kwa goli moja!

Tumemiliki mpira asilimia 60, ila mtu wa kuwaunganisha Mayele na Musonda alikosekana!

Aziz Ki hakuwa makini alikazana kutaka kufunga badala ya kawaida yake kutoa mapande, anao anao sana badala ya kuharakisha kutoa pasi , c Morisson alielewa alichokosea Aziz Ki.

Mayele hakupata usaidizi akawa anacheza pembeni, Ambundo au Denis Nkane wanajua kukimbia na Mayele ,

Kibwana hakupanda inavyotakiwa!

Timu haikukaba kama kawaida yake, waarabu walirelax wakiwa na mpira!

Pengo la Aucho lilionekana timu ilikosa balance!
 
Back
Top Bottom