Soko la Machinga Dodoma, tumpe Rais Samia maua yake

Sahihi Kwa vyakula. Ulijaribu kugusa nguo na viatu🤔🤔
Hiyo ndo shopping niliyofanya.

Bei ya ushindani na unaweza kunegotiate.

Lakini kwa mfumo wa biashara usitegemee kukuta bei ya kariakoo
 
Nenda hapi baada ya miezi sita uje ulete mrejesho!! Mwafrika hajaweza kujitawala bado.
 
Nikweli tumpongeze saaana saaana. Tatizo ni Moja kwamba, haitakuja kutokea tujenge majengo ya machinga ya kutoshereza idadi Yao. Hapo walipojenga tayariii hapatoshi. Kwa nini hapatoshi sababu ni hiiii;
1. Machinga wanazalishwa Kila sikuuu kama ifuatavyo, Kila uchwao, machinga wanaongezeka Kwa Kasi kubwaa saaana kwani Kila unapoona darasa la Saba wamemaliza basi ujue tumepeleka machinga Tena,

2. Kila unapoona form4 na f6 wamemaliza ujue Kuna machinga wameingia mijini Tena. Kila unapoona vyuo vya in kati na vyuo vikuu wamehitimu, basi ujue tumepeleka machinga wengine wengi saana.

Pia Kila siku kunawasitafu wengine Tena wanaongezeka, hao nao ujue umeongeza machinga Tena mtaani na mijiniii, Bado watumishi wa umaa nao nimwachinga pia.

Kwahyo hakuna siku tutajenga majengo ya kutoshereza wimbi hili la machingaaa. Tutajenga majengo mangapiiio ya kutoshereza? Hivyo namuomba mama yangu kipenzi changu na shujaaa wa TANZANIA na Africa nzima afanye hiviii; wawepo machinga wakukaaa kwenye MAENEO hayoo, pia wawepo machinga watakao ruhusiwa kutembeza bidhaa zao MAENEO yote ya mjini. Au zitafutwee baadhi ya barabara zifungwee ili machinga hawa .
 
Tuna sapoti ujinga badala ya kuja na sera nzuri za Vijana kuwekeza tunawatengenezea nazingira ya wao kuendelea kuwa wajinga, Hao wana siasa kuna ndugu zao ni Machinga?

Nchi tuna risishana ujinga,
 
Pongezi nyingi sana Kwa Rais Samia alitoa pesa za COVID zikafanya kazi hii ku top up pesa za Jiji..

Pia Mtaka na yule alikuwa DED wa Dom walifanya kazi nzuri
Wasoko ya Wanyonge si ndio? Wapiga kura ili watu waendelee kufaidi mema ya nchi hii lazima wa hanasishe umachinga
 
Hakika hii ni neema kwa machinga
Neema ipi? Hilo soko linauza nini kama.sio asilimia 100 peoduct za kichina? Na nguo za mitumba kama Boxer na Sidiria? Badala ya nchi kuwekeza kwenge sera za viwanda viajana wapate ajira tunawekeza kwenye danganya Toto,
 
Mama Samia pokea mauwa yako kwa upendo, heshima na taadhima👇🏾




Mama Samia anaupiga mwingi Kimataifa.
 
Soko ni landmark lile.

Serikali ikiwekeza ktk ideas kama hizo tutaondokana na wamachinga kuvamia mabarabara na kutembeza bidhaa kwenye bars.

Mapato yataongezeka
Nnia pekee ya kuondokana na Macbibga ni uwekezaji kwenye viwanda, vijana wapate ajira, au uwekezaji mkubwa kwemye kilimo.

Hmachinga ni kutengeneza Taifa ka watu wasio waza wanao waza uchuuzi tu, Wamachinga wanakuza uchumi wa China
 
Limeanzwa na JPM na frem zipo WAZI hao unaowaona wanazuga tu huku mtaani wanavunja vibanda wakishikiza watu kuhamia hapo.

Ni kama machinga complex Dar kuna maajabu gani horofa kwanza tu wamejaa wauza simu na mafundi laptops
Hakuna kitu hapo, naumia sana kuona Taifa tuna risishana ujinga, wakati wenzetu wana risishana akili. Unachinga ni vitu ya ku descourage kwa gharama yoyote ile, ila Bongo tuna hamasisha Unachinga si kwa sababu za Kiichumi bali za kisiasa
 
Bidhaa zipi zimejaa za vuwanda vya Tanzania?
 
Hakuna kitu hapo, naumia sana kuona Taifa tuna risishana ujinga, wakati wenzetu wana risishana akili. Unachinga ni vitu ya ku descourage kwa gharama yoyote ile, ila Bongo tuna hamasisha Unachinga si kwa sababu za Kiichumi bali za kisiasa
Mkuu we ukichangia uchumi inatosha 😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…