Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Sokomoko la zawadi ya gari ya Rais mstaafu Mwinyi

Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Tatizo hamsomi Biblia
Jana Rais Samia kwenye uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Mwinyi, alitangaza kuwa katika pia kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa Rais wetu huyo wa zamani aliyetimiza miaka 96, serikali imempatia gari [jipya?] aina ya Mercedes Benz iliyo chini [sedan] kwa sababu aliyokuwa akiitumia [nadhani ni SUV] ilikuwa inampa shida kuipanda na kushuka kutokana na umri wake mkubwa kwa sasa pamoja na kimo chake [hapa nahisi Rais Samia alisema kwa utani].

Tangazo hilo la Rais Samia limezua sokomoko kubwa, hususan mitandaoni.

Mimi sina tatizo na ‘zawadi’ hiyo kwa Rais wetu huyo mstaafu. Kwa maelezo machache aliyoyatoa Rais, sina pingamizi lolote lile.

Ila kuna wengine hawakufurahishwa na jambo hilo. Wamehoji kwamba iweje mtu kama Rais Mwinyi, ambaye katumikia taifa kwa muda mrefu na katika nafasi za juu kabisa, mtu mwenye istihaki nyingi hivyo, ashindwe kujinunulia gari linalomfaa kwa matumizi yake.

Rais Mwinyi keshawahi kuwa waziri. Keshawahi kuwa Rais wa Zanzibar. Na alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Sina hakika kama pia huwa anapata marupurupu ya utumishi wake kama Rais wa Zanzibar au la. Naamini ya urais wa Jamhuri ya Muungano anayapata.

Sasa mimi nina maswali kadhaa:

1. Je, hilo gari alilopewa hivi sasa ni la kwake? Limesajiriwa kwa jina lake? Yeye ndo analilipia bima?
Mimi muda wote huu nimekuwa nikidhani kuwa marais wastaafu huwa wanapewa gari ya matumizi na serikali na kwamba magari hayo huwa ni mali ya serikali.
Yaani, Rais mstaafu huwa anapewa gari, ofisi, watumishi wa ofisi, walinzi, na kadhalika.

2. Kama hivyo ni ndivyo, ni kapewa au wamembadilishia tu gari ya matumizi na siku atayoacha kuitumia itarudishwa ilikotoka?

3. Kama wamembadilishia tu gari, Rais angesema ‘tumembadilishia’ gari la matumizi kuliko kusema ‘tumempa’ gari jipya kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa, ingekuwa ni bora zaidi na isingezua sokomoko?

Tatizo nilionalo hapa ni kuhusu timing, optics, na word choice tu.

Zaidi ya hapo kelele zilizopigwa sizioni kama ni hoja zilizo compelling.

Rais Mwinyi siyo raia wa kawaida. Hawezi kulinganishwa na wazee wengine ambao hawajawahi kuwa marais.

Rais Samia kusema ile majuzi kuwa serikali haina hela za kutosha kuwapa posho wazee, hiyo haina maana serikali haina hela za kuwatunza marais wa zamani.

So this is much ado about nothing.

Go ahead and click that ‘Like’ button if you agree with me. Even if you don’t agree but you appreciate the content, go ahead and smash that button.

Happy Sunday and most importantly, have a very happy Mother’s Day!
Luka 19:26
 
Hawezi kupinga Wazenji wenzake kupeana zawadi!

Kumbuka kuwa mbaya hakuwa CCM. Mbaya alikuwa Magufuli..
Ndio maana naona kimya siku hizi, halafu kuna issue ya Rais ni mwanamke mwenzao naona hata Mange nae anatetea kila jambo kisa rais ni mwanamke mwenzake.
 
Mwinyi kupewa hilo Benzi wewe unaona ni tatizo?
Sana. Hahitaji zawadi ya Benz. Mafao yake na stahili zake zina mruhusu aishi vizuri sana. Kuna watumishi muhimu sana ambao wanaambiwa wajinunulie yunifom kwa sababu hamna pesa.

Amandla...
 
Kwenye hili sakata nimegundua watu wanaomchukia Mother wapo wa makundi 3:
1. Wasiotaka Rais mwanamke, hawa ni jamaa wasiotaka kukubali kuwa dunia imebadilika sana
2. Watanganyika wanaochukia kutawaliwa na Mzanzibari, hawa ni wengi zaidi
3. Wakristo wasiopenda kutawaliwa na mwislamu, hawa wengi vile vile.
Sababu zingine ndogo ndogo na ni wachache ni vyama vya upinzani na watu walioumizwa sana na kifo cha JPM
Hawa walioumizwa sana na kifo cha mwendazake ni wachache zaidi na hasa wale aliowapendelea kwa 7bu ya ukabila na ukanda (nepotism)
 
Sana. Hahitaji zawadi ya Benz. Mafao yake na stahili zake zina mruhusu aishi vizuri sana. Kuna watumishi muhimu sana ambao wanaambiwa wajinunulie yunifom kwa sababu hamna pesa.

Amandla...
Anahitaji zawadi gani sasa kama siyo Benzi?
 
Kutoka kwa yeyote yule…hata wewe Fundi Mchundo..
Hahitaji zawadi ya aina yeyote. Ila rafiki na ndugu zake wanaweza kumpa zawadi ya kitu ambacho wanajua anakipenda au atakifurahia. Wanaweza kumpa hata Rolls Royce. Serikali ingempa kadi na maua kama zawadi na sio zaidi.
Fundi Mchundo angempongeza tu kwa kutimiza miaka 96 bila zawadi yeyote. Sana ningetoa mchango kwenye kituo cha watoto yatima kilichopo jirani yetu.

Nyani unajua huko uliko mambo ya zawadi za magari ni watu kama wakina Kardashian. Watu wenye heshima zao huwa wanasema kama unataka kunipa zawadi basi changia charity hii na hii. Zawadi za magari ya kifahari waachiwe wakina Daimondi, sio serikali.

Amandla..
 
It's a law of nature. Mwenye nacho huongezewa. Asiyekuwa nacho, basi anaweza kunyang'anywa hata kidogo alichobahatika kuwa nacho ili achukue mwenye nacho kingi tayari...

Mwinyi anapewa zawadi ya gari aina ya Germany Technology Mercedes Benz na serikali na siyo Mama Samia Suluhu Hassani...

Inashangaza kidogo kwa sababu kiongozi mstaafu kama Mwinyi mwenye privileges na marupurupu kibao na mwenye familia nzuri yenye watoto wenye nyadhifa kubwakubwa na uwezo Mkubwa wa kiuchumi ktk jamii, anashindwaje kujinunulia yeye mwenyewe gari atakalo kwa mahitaji yake kwa gharama zake toka ktk fedha nyingi anazolipwa na serikali wakati wote...?

It doesn't make any sense at all, ... right...?

Mama Samia Suluhu Hassani, Rais wa JMT umeanza kuboronga mapema sana. Unaanza kulewa madaraka mapema sana. Unaanza kuanza kuyatumia madaraka yako ya Urais vibaya mapema sana...!

I am afraid to say that, this is very dangerous move to your presidency...

Nakuhakikishia kuwa, unaweza kuishia kuwa Rais wa hovyo sana pengine kuliko hata Mwendazake Pombe Magufuli...!!

LABDA UNASAHAU HARAKA SANA....

Kumbuka, ni wiki jana tu umetoka Mwanza kwenye sherehe za Mei Mosi. Wafanyakazi waliitaka serikali yako ingalau iwaongezee mshahara ingalau hata Shilingi 50,000 tu kwa kila mfanyakazi. Ulijitetea vizuri, ukaeleweka na wakasema watakuvumilia hadi mwakani sawasawa na ombi lako...

Aidha kumbuka jana tu pia ulikusanya walioitwa "wazee wa Dar". Wakaiomba serikali yako unayoingoza ifanye vitu vidogo kadhaa vinavyohitaji fedha...

"Malkia wa maneno matamu" ukajitetea vizuri sana kwa maneno yako matamu kwelikweli huku ukisingizia hali mbaya ya uchumi wa nchi kama sababu...

Ukawaomba wakupe muda ili ujipange na kuona hali itakuwaje. Wazee wale kwa nilivyowatazama nyuso zao, ni kama walikuelewa na wakakupa " benefit of doubt..."

Lakini leo katika hali ya kushangaza unaamua kumzawadia fedha za wazee na wafanyakazi hawahawa wa nchi hii Mzee Ally H. Mwinyi uliyoiita "zawadi ya birthday" gari aina ya Mercedes Benz yenye thamani ya kiasi cha fedha za kitanzania kati ya 900,000,000 hadi 6,900,000,000 (bilioni 6.9)....!!

Are you really serious Madam President..?

Labda Madam President wewe na watu wako mnadhani Watanzania ni wajinga sana, hawajui gharama za magari hayo kama ni mapya. Ngoja tukueleze...

Binafsi niliposikia tu unachotaka kufanya kwa Mwinyi, haraka haraka nimetembelea soko la aina hii ya magari mapya mtandaoni, nimeshangaa kwa sababu bei yake ni kubwa sana..

Mercedes Benzi ya bei ndogo kabisa kwa kuzingatia muundo na toleo ni USD 400,000 sawa na Tshs. 920,000,000...!!

Ya bei ya juu kabisa ni USD 3,000,000 sawa na Tshs 6, 900,000,000 (bilioni 6.9..!!!)

Hapa chini ni baadhi ya picha ya magari haya..
Screenshot_20210509-211918.png
Screenshot_20210509-211326.png


Hivi unadhani kuna sababu gani ya Watanzania kuendelea kuamini kuwa wewe mama kama kiongozi wa nchi hii unakwenda kufanya tofauti na aliyekutangulia nawe kwa bahati tu umejikuta ni Rais wa nchi hii...?

It's a wrong decision at a wrong time...

Achana na hii kitu. Hizo fedha unazoziona hapo siyo zako. Ni fedha za Watanzania zaidi ya 60,000,000. Tafadhali usuanze kupagawa mapema hivi, utaharibikiwa. Tumia busara na hekima kuzitumia fedha hizo ili kila Mtanzania aone impact yake..

Unapata wapi ujasiri wa kumzawadia mtu mmoja Tshs. 900,000,000 (huku tayari akiwa fedha zake nyingi tu) kati kati ya kundi kubwa la wananchi unaowaongoza ambao zaidi 30% wanaishi katikati ya umasikini uliotopea...??


Screenshot_20210509-211947.png


Screenshot_20210509-211918.png


Screenshot_20210509-211918.png


Screenshot_20210509-211918.png


Screenshot_20210509-211918.png
 
Hahitaji zawadi ya aina yeyote. Ila rafiki na ndugu zake wanaweza kumpa zawadi ya kitu ambacho wanajua anakipenda au atakifurahia. Wanaweza kumpa hata Rolls Royce. Serikali ingempa kadi na maua kama zawadi na sio zaidi.
Fundi Mchundo angempongeza tu kwa kutimiza miaka 96 bila zawadi yeyote. Sana ningetoa mchango kwenye kituo cha watoto yatima kilichopo jirani yetu.

Nyani unajua huko uliko mambo ya zawadi za magari ni watu kama wakina Kardashian. Watu wenye heshima zao huwa wanasema kama unataka kunipa zawadi basi changia charity hii na hii. Zawadi za magari ya kifahari waachiwe wakina Daimondi, sio serikali.

Amandla..
Acha roho ya korosho Fundi!

Mzee umri umeenda. Na ni mtu mwenye kimo kifupi. Anahangaika kuzipanda SUV.

Kwa hali yake ya sasa, sedan ndo inamfaa.

I can’t begrudge a 96 year old man getting a Mercedes Benz sedan for his use.

To me it’s a no biggie!

Una roho mbaya wewe Fundi Mchundo 😁 kama yule rafiki yako Kuhani!
 
Tunahitaji kuona picha ya aina ya benz alilopewa Mzee Dr Ally Hassan Mwinyi. Yawezekana kapewa la bei ndogo!
 
It's a law of nature. Mwenye nacho huongezewa. Asiyekuwa nacho, basi anaweza kunyang'anywa hata kidogo alichobahatika kuwa nacho ili achukue mwenye nacho kingi tayari...

Mwinyi anapewa zawadi ya gari aina ya Germany Technology Mercedes Benz na serikali na siyo Mama Samia Suluhu Hassani...

Inashangaza kidogo kwa sababu kiongozi mstaafu kama Mwinyi mwenye privileges na marupu rupu kibao na mwenye familia nzuri yenye watoto wenye nyadhifa kubwakubwa na uwezo Mkubwa wa kiuchumi ktk jamii, anashindwaje kujinunulia yeye mwenyewe gari atakalo kwa mahitaji yake kwa gharama zake toka ktk fedha nyingi anazolipwa na serikali wakati wote...?

It doesn't make any sense, right...?

Mama Samia Suluhu Hassani, Rais wa JMT umeanza kuboronga mapema sana. Unaanza kulewa madaraka mapema sana. Unaanza kuanza kuyatumia madaraka yako ya Urais vibaya mapema sana...!

I am afraid to say that, this is very dangerous to your presidency...

Nakuhakkikishia kuwa, unaweza kuishia kuwa Rais wa hovyo sana pengine kuliko hata Mwendazake Pombe Magufuli...!!

LABDA UNASAHAU HARAKA SANA....

Kumbuka, ni wiki jana tu umetoka Mwanza kwenye sherehe za Mei Mosi. Wafanyakazi waliitaka serikali yako ingalau iongeze mshahara hata Shilingi 50,000 tu kwa kila mfanyakazi. Ulijitetea vizuri, tukakuelewa na tukasema tutakuvumilia sawasawa na ombi na maneno yako...

Aidha kumbuka jana tu pia ulikusanya "wazee wa Dar". Wakaiomba serikali unayoingoza ifanye vitu vidogo kadhaa...

Ukajitetea wewe " Malkia wa maneno matamu" huku ukisingizia hali mbaya ya uchumi wa nchi...

Ukawaomba upewe muda. Wazee wale kwa nilivyotazama nyuso zao, wakakuelewa na kukupa " benefit of doubt "..

Lakini leo katika hali ya kushangaza unaamua kumzawadia fedha za wazee na wafanyakazi hawahawa wa nchi hii Mzee Ally H. Mwinyi kiasi cha fedha za kitanzania kati ya 900,000,000 hadi 6,900,000,000 (bilioni 6.9) kama zawadi ya birthday yake....!!

Are you really serious Madam President..?
Labda hujui na wewe na watu wako mnadhani Watanzania hawajui gharama za magari hayo iwapo ni mapya. Ngoja tukueleze...

Binafsi nilipopata tu unachotaka kufanya, haraka haraka nimetembelea soko la aina hii ya magari mapya mtandaoni, nimeshangaa kwa sababu bei yake ni kubwa sana..

Mercedes Benzi ya bei ndogo kabisa kwa kuzingatia muundo na toleo ni USD 400,000 sawa na Tshs. 920,000,000...!!

Ya bei ya juu kabisa ni USD 3,000,000 sawa na Tshs 6, 900,000,000 (bilioni 6.9..!!!)

Hapa chini ni baadhi ya picha ya magari haya..
View attachment 1779132View attachment 1779134

Hivi unadhani kuna sababu gani ya Watanzania kuendelea kuamini kuwa wewe mama kama kiongozi wa nchi hii unakwenda kufanya tofauti na aliyekutangulia nawe kwa bahati tu umejikuta ni Rais wa nchi hii...?

It's a wrong decision at a wrong time...

Achana na hii kitu. Hizo fedha unazoziona hapo siyo zako. Ni fedha za Watanzania zaidi ya 60,000,000. Tafadhali usuanze kupagawa mapema hivi, utaharibikiwa. Tumia busara na hekima kuzitumia fedha hizo ili kila Mtanzania aone impact yake..

Unapata wapi ujasiri wa kumzawadia mtu mmoja Tshs. 900,000,000 (huku tayari akiwa fedha zake nyingi tu) kati kati ya kundi kubwa la wananchi unaowaongoza ambao zaidi 30% wanaishi katikati ya umasikini uliotopea...??

View attachment 1779135

View attachment 1779136

View attachment 1779137
Kwa hiyo na wewe ulitaka Mzee Ruksa apewe IST?
Mtu mmoja alipata kusema "maskini wana roho mbaya sana!!"
 
Back
Top Bottom