Somo la 'Historia ya Tanzania' alilotaka Magufuli lasitishwa

Somo la 'Historia ya Tanzania' alilotaka Magufuli lasitishwa

Magufuli alikuwa sawa, achaneni kupinga kila jambo:
Tuachane na mtaala wa kikoloni tufundishe watoto wetu historia yetu na ya mababu zetu, tamaduni zetu, mila zetu, ili tukuze uzalendo kwa vizazi vya sasa na vijavyo
Hakuna haja ya kufundisha historia kwa Kiingereza,
Magufuli alikuwa sawa, ProfesaNdalichako harakisheni huo mtaala mpya
swali langu ni je nn malengo ya mtaala huo?
is it applicable in modern world employment market?

kama waziri ameona haiko sawa? ww ni nani ?
 
"Mimi na Magufuli ni kitu kimoja" dadavua sentensi hii
... dah! Hii ikifanyiwa qualitative exploratory case study research unatoka na conclusions kali sana! Wanazuoni waifanyie research hii kauli ya Mama Samia; imebeba jumbe nyingi muhimu sana zilizofichika.
 
imagine unafundishwa historia ya mkwawa kiingereza[emoji16][emoji16],sijui ukasimulie wazungu ama!!!

wakati mwingine kuna watu wanayapa matako kazi ya kichwa,mmoja wapo mleta mada.na anacheka cheka tu.
Lengo la Magufuli alitaka aingizwe kwenye mtaala wa somo la historia na wala siyo suala la lugha! Hivi historia ya Mkwawa ikifundishwa kwa kiingereza inakuwa tofauti na ikifundishwa kwa kiswahili?
 
Magufuli alikuwa sawa, achaneni kupinga kila jambo:
Tuachane na mtaala wa kikoloni tufundishe watoto wetu historia yetu na ya mababu zetu, tamaduni zetu, mila zetu, ili tukuze uzalendo kwa vizazi vya sasa na vijavyo
Hakuna haja ya kufundisha historia kwa Kiingereza,
Magufuli alikuwa sawa, ProfesaNdalichako harakisheni huo mtaala mpya
Ndiyo umepigwa teke hutaki kajinyonge!
 
Hivi ni mazuri gani ya Mwendazake zake yanayosemwa.?
hayapo ni wazi waweza fikiri kuwa walikuwa wakimchukia hasa na wote wa karibu yake maana kila jambo alilofanya linaongelewa kwa ubaya na walewale walilo sifu hii ina maana hata samia yaweza kumkuta toka kwa watu wale wale maana kikwete naye watu walewale walimuongelea kwa ubaya wakatiwa magufuli nakumponda ni walewale walewale walikuwa waki msifu kwa kasi ileile na ari mpya ile ile na na wengi ni walewale wa CCM ileile maana huu ni utamaduni wao wanajua wanachokifanya
 
Hivi hili lilikuwa liwe somo kabisa kama vile ilivyo kiswahili au ni topic tu katika somo la historia (kitu ambacho nadhani topic hio/hizo zipo)....

Au alitaka kuanzisha somo la Propaganda...
... Kaka, tulikuwa tayari kwenye direction ya NK. Vikosi maalumu (wasiojulikana) vilishaundwa; ilikuwa kukamilisha mambo fulani fulani before full enforcement! Tusiache kumshukuru Mungu kila wakati kwa neema zake zisizo na kipimo!
 
Yaani hadi Professor Ndelichako anamsaliti Magufuli? Kweli?
Ni Magufuli aliyemuinua Professor Ndelichako kutokea benchi, akampa ubunge wa bure na zawadi ya uwaziri, leo hii bila aibu anaizika legacy ya Magufuli kirahisi.

Nimeamini adui wa mtu ni watu wa karibu yake. Magufuli alizungukwa na wanafiki watupu, akawakumbatia huku akiwaangamiza wapinzani.
nafikiri umeshindwa kutofautisha mtu na mamlaka.
linapokuja suala la maamuzi kwa maslah ya nchi.. humuangalii aliekuweka hapo.
ungaalia unapangaje kwa ajili ya nchi ... si mtu fulani.

hapo hakuna usaliti. marehem hana faida.. akienda ameenda
 
Ila Profesa Ndalichako aliyapokea maagizo kwa heshima na unyenyekevu mkubwa! Ilikuwaje alishindwa kumshawishi Bosi wake kuhusu huo upuuzi!

Na kama Bosi angemkatalia, si angejiuzulu! Au kukubali kufukuzwa Uwaziri na ikibidi hata Ubunge wake wa kuteuliwa kwa heshima! Ila kwa sababu ya njaa, akaamua kuweka taaluma yake pembeni na kuamua kupokea kila aina ya maagizo! Yakiwemo haya ya hovyo!

Njaa na unafiki ni vitu vibaya sana.
Njaa haimpendezi mtu ndugu
 
Sio kweli lakini Hayati alisisitiza Historia ya kweli ya Taifa letu sio kwa bahati mbaya cos kuna mambo mengi yanamkanganyiko mpaka leo moja wapo kifo cha Mkwawa na pia Mapinduzi ya Zanzibar
Sasa hayo mambo si yangeweza kurejebishwa kwenye syllabus iliyopo kuliko kuanzisha kitu kipya?
 
Sio anageukwa ndio uhalisia na ndio kipindi kizuri kujifunza..

Watu walipokua wanasema makosa yake hamkuamini?

Haiwezekani analala anaamka anakuja na mawazo yake binafsi yasiyo na kichwa wala miguu na hajashauriana na mtu yeye anataka litekelezwe
Tatizo lake alijiona anajua kila kitu...hata ule mchakato wa kubadili lugha ya mahakama kuwa kiswahili nadhan wataachana nao tu
 
We utakuw a umesoma debit ma credit ambavyo siyo vigumu ukilinganisha na history. Hata tundu lisu alisoma hgl lakini ni mweledi sana. So sayansi ni utopolo tu ukiwa unaweza kukalili unaweza andika A zote
"So sayansi ni utupolo tu"
sorry unamaanisha all scientist walioleata mabadiliki dunian walikariri text books?

nitakupa mfano : can you crame calculus?
 
Sio kweli lakini Hayati alisisitiza Historia ya kweli ya Taifa letu sio kwa bahati mbaya cos kuna mambo mengi yanamkanganyiko mpaka leo moja wapo kifo cha Mkwawa na pia Mapinduzi ya Zanzibar
somo la historia la sasa halizungumzii hilo?
 
Waziri wa elimu Prof. Ndalichako amesitisha maboresho ya mtaala wa somo historia ambao ulianzishwa na Magufuli. Mtaala huo wa somo la historia ungeanzisha kufundisha somo la historia kwa kiswahili tangu madarasa ya awali hadi chuo kikuu. Waziri Ndalichako ameagiza kuendelea kutumia mtaala wa zamani hadi mtaala mpya utakapoandaliwa kwa kushirikisha wadau.

Source: ITV

Sijui Magufuli anajisikiaje huko aliko kwa sababu maagizo yake yanatupiliwa mbali kila kukicha!
Makosa ya mwendazake yasameheni bure maana tumejiridhisha kuwa alikuwa ni mgonjwa wa akili,msisumbue vichwa vyenu
 
Somo la Historia ni kutuwezesha kujua tulikotoka na tulipo kwa sasa ili tujue tunakokwenda kama ni sahihi kama nchi na kama dunia. Vijana wetu wa sasa hawajui tulikotoka. Na sasa ndiyo ma DC na RC wetu, tutegemee watatupeleka wapi kama si kule akina Chalamila na Ole Sabaya walikokuwa wanatupeleka licha ya kuwa na madigiri ya uzamifu? Hata akina Ndalichako ni wale wale.
 
swali langu ni je nn malengo ya mtaala huo?
is it applicable in modern world employment market?

kama waziri ameona haiko sawa? ww ni nani ?
pamoja na yote bado historia inabeba dhima nzima ya maendeleo ya binadamu kujua alipo leo kwa kuamgalia ya jana na ndiyo maana mpaka leo hata nchi zilizoendelea bado zinawekeza mabilioni kwenye eneo hili kwa kufanya tafiti mbalimbali duniani. historia hutupa data na nadharia ambazo zaweza kusaidia kutengeneza sheria kwa kuangalia matukio yaliopita yawe ya ,kisayansi kijamii NK ila tatizo hapa kwetu hata ukiisoma haikupeleki kuwa mbobezi katika eneo lolote na wala si jambo la kipaumbele ndio maana waweza sema hakuna employment market. miaka kadhaa watafitiwa kihistoria waligundua mji maarufu wa Rhapta chini ya bahari hapa Tanzania ambao ulikuwa kwenye maandiko ya Ptolemy kama Africa's first metropolis, kwa nchi zenye kujua hii licha ya kuwa eneo la kitalii bali wangewekeza kwenye tafiti zaidi na kujua zaidi ni kwa vipi ulizama je janga kama hilo laweza kujirudia?
 
Back
Top Bottom