Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Mwambie aache kutumia wasanii katika kampeni uone maajabu
20200912_081929.jpg
maajabu kama haya ya kusomba watu lissu asiaibike
 
Kusema kampeni za CCM ni ngumu ni vichekesho. Rais Magufuli hata asipopiga kampeni kuanzia leo ushindi ni 90%

Rafiki zetu wa CHADEMA mtaula wa chuya huu mwaka hampati hata mbunge.
Binti ulipotelea wapi,au mpini ulikukolea ukapasahau hapa?
 
Mambo mengine ni ya ajabu sana. Ukiangalia kwenye ratiba ya kampeni kwa mgombea wa ccm, imeonesha siku atakapo pumzika. Pia niwaambie cdm. Jembe litaendelea kuikanyaga nchi nzima kwa gari.
 
Ingawa ni mgombea, bado pia ni Rais wa nchi kwa hiyo hawezi kutumia muda wote kwenye kampeini na kusahahau majukumu ya uraisi. Halafu kama angekuwa na woga, ndipo angekuwa anafanya kampeini usiku na mchana lakini kwa vile hana hofu basi anaweza kuchukua time-off ili kufanya mambo mengine.

October 28 ndiyo fainali.
Hana woga, muulize Prof. Kabudi kutwa kucha kueleza balozi UK na US uchaguzi utakuwa huru na haki. Ingia control room utajua kunachoendelea hapa Tanzania.
 
Kumbuka uchaguzi ni mwezi ujao tena mwishoni na safari hii kampeni inafanywa na viongozi wakubwa wote katika mikoa tofauti tofauti.
Hakuna kiongozi yeyote wa ccm mstaafu na hata wa sasa mwenye ushawishi kwa wananchi , watu wametekwa na kuuawa hakuna aliyenyanyua mdomo kupinga , leo hii watasema nini mbele ya wananchi wanaopoteza ndugu zao kila uchao kwa kutekwa
 
Mambo mengine ni ya ajabu sana. Ukiangalia kwenye ratiba ya kampeni kwa mgombea wa ccm, imeonesha siku atakapo pumzika. Pia niwaambie cdm. Jembe litaendelea kuikanyaga nchi nzima kwa gari.
CCM wanafanya kampeni za kisayansi😁😁😁 kampeni zenye matokeo chanya.... na sio kampeni za kulalamika kuonewa kutwa na kutishana
 
Hahaha kampeni miaka mitano bado hueleweki, inakatisha tamaa sana.

2015 mpaka leo 2020 kampeni na hueleweki sio kupumzika angeacha kabisa.
 
Mwingine anaweza kusema mwaka 2015 alitumia nguvu kubwa na akapita maeneo mengi kwa sababu kazi ilikuwa ngumu hata matokeo ya Uraia yalisadifu hilo.
Mwaka huu kazi ni nyepesi mno, kila mtu anaona kinachotokea, mwitikio wa Raia kwake na kwa wapinzani wake. ACT wameshanyosha mikono, CDM ndiyo Kama hivo, Juzi uliona Raia wa pwani Kama vile hawamjui, Jana Morogoro mjini umeona hali mwenyewe, kule Mheza ilikuwa aibu. Hata Makamanda tangu Mlivyoposti picha za Mbeya, hamjaposti tena, utafikiri Mgombea wenu yupo likizo naye.
Sasa kwa namna hiyo kwanini asipumzike Budha. Game imekuwa nyepesi mno.
Kama umegundua, wanachokifanya CCM baada ya uhakika wa Kushinda, ni kuhakikisha mtu anapata kipigo cha mbwa koko, hicho ndicho kinachofanyika kwa Sasa.
Kuna ubaya gani mtu kupumzika? Ukijadili suala hili bila mwegemeo wa kisiasa utaona hakuna tatizo mtu kuamua kupumzika. Safari ya Dodoma mpaka musoma, Mwanza Geita wakati huo anaongea kula mahali Kuna shida gani hapo mtu akipumzika. Badala ya kujadili issue ya mtu kupumzika, ambayo ni kawaida,tungepiga kelele humu mitandoni jinsi ambavyo mawakala la tume ya uchaguzi( wakurugenzi) walivyoharibu uchaguzi huu kwa kuengua wagombea. Inaumiza kuona uchaguzi unageuka kuwa uteuzi. Inawezekanaje mnaenda kupiga kura kwenye kinachoitwa uchaguzi huku tayari almost theluthi ya madiwani ameshapita bila kupingwa? Kuna wabunge wameshapita pia. Hii mentality ya kuona Mambo mazuri katika wapési wa kifikra itatusaidia? Kujadili mtu kakata pumzi au napumzika kwangu Mimi ni dhana ya kukupa Mambo madogo kwa gharama ya Mambo muhimu. Let's change.
 
Wanafunzi ndio wapiga kura wa kesho, tatizo CHADEMA mmjezana wengi wenye fikara zisizo ona mbali
Kaka sijui Dada, vipi kuhusu malipo yetu ya leo huko? Tunapata ugumu sana kutetea chama chetu huku tukiwa na njaa ujue.
 

Attachments

  • Lumumba Buku 7.jpg
    Lumumba Buku 7.jpg
    20.8 KB · Views: 1
Mwacheni Mh Rais apumzike jamani kwanza amehakikishiwa na wapambe nuksi kwamba mwaka huu anashinda kwa asilimia 99.9.
 
Madukuduku ya watu wanajibiwa na rais kwa muda wote anaokuwa ikulu.

Msafara unaposimama njiani rais huongea na watu na kuwauliza shida zao,anachokifahamu katika vikao vya aina hiyo ni zaidi ya mbwembwe za midahalo.

Kwenye mdahalo ndio sehemu sahihi ya kuulizwa na kujibu kwa utaratibu mzuri. Huko barabarani anakutana na watu waliopangwa kumuuliza, na wale wote ambao hawajapangwa wakimuuliza huwa anawajibu kwa kejeli na dharau kubwa. Huwa tunaona anachokifanya wala hatuhadithiwi
 
Back
Top Bottom