Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Uchaguzi 2020 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli na Samia Suluhu

Kwanza ni makosa na kuwanyima haki zao maana kwenye mkutano kuna watu wa aina mbili wafatao fiesta na wafatao sera sasa fiesta likiisha sioni kosa lao waamuapo kuondoka
 
Kuna mgombea urais inasemekana anachukiwa. Leo namfuatilia kupitia TBC naona kila anaposimama watu wanajaa na wanamshangilia sana. Nilitegemea watu wasijitokeze au wamzomee!

Tuache kudanganyana huku mitandaoni huko uraiani mambo ni tofauti. Naona uwanja wa Tanganyika Packers kumejaa kweli kweli na mitaani anakopita watu wamejipanga barabarani kumsubiri.

Happy Nyerere day!
 
Picha
 

Attachments

  • IMG_20201014_110449.jpg
    IMG_20201014_110449.jpg
    103.8 KB · Views: 2
Members, Sura za wana ccm wanaokaa mbele kwenye kampeni kila jimbo wanafanana sura na ni wale wale ,Je hii ni bahati mbaya au wanaccm wanazaa mapacha kila jimbo la uchaguzi

Hawa watu wanaozunguka kila jimbo la uchaguzi utawaona Mbeya,Iringa,Dodoma na sasa wanaonekana Dar es Salaam mfano Mburahati

Kwa muonekano huo,Je ccm imekosa ushawishi kwa wananchi?

Hao watu wana kazi gani?kila wakati wao wanazungushwa kila jimbo na kurukaruka mbele huku wakizungusha bendera wanapewa kitu gani?


Hii inachekesha sana kama ushawishi ni kuzungusha watu walewale ili kujaza uwanja na kuonekana watu wengi kumbe ni changa la moto
 
Nikiangalia mwenendo wa kampeni za uchaguzi mkuu hapo 28 Oct 2020 kwa chama fulani ni kama ule msimu wa Fiesta kama wafanyavyo CLOUDS FM au WASAFI FM n.k.

Bahati mbaya kuna mgombea amejinadi na kujikweza kuwa hajawahi kupata upendo mkubwa kwa watu kujitokeza kumsikiliza kwa mapenzi yao kwake licha ya mvua zinazonyesha

Sasa najiuliza mbona yule mgombea mwingine watu wanajitokeza kwa wingi katika mlingano uleule licha ya kuwa hakuna tamasha la muziki wala wasanii wanaovutia watu?

Sasa najiuliza yule aliendaa tamasha la muziki na kuwalazimisha wasanii wakubwa na wenye mvuto kushiriki kampeni zake, na yule ambae hafanyi matamasha ya muziki wala kushirikisha wasanii wanaojulikana ili kuleta mvuto ...

Lakini ukiangalia mahudhurio ya watu ni kama sawa kwa mlingano wa yule anaefanya tamasha kuvutia watu na yule asie fanya matamasha ...

Je, hapo ni nani aneonyeshwa upendo na wananchi

Kuna wakati binaadamu tunapenda kujipa moyo na kujifariji ...

Anyways two weeks down to go!!! #NI YEYE TU 2020
20201014_114347.jpg
20201014_114402.jpg
20201014_114422.jpg
20201014_114457.jpg
 
Habarini Wanajukwaa, poleni na kampeni. Nipende kumshukuru Mungu kwa Yote.

Mimi kama mwaccm kindakindaki nipende kusema tu CHADEMA WAMEJUA KUTUTESA KITESO TUSICHOTEGEMEA. Linapokuja jambo linaloitwa kampeni hawa watu wapo vizuri kushambulia sana yaani CCM IMEPAKI BASI kuzuia mashambulizi. Ukweli usemwe TUMEZIDIWA.

Labda tutegemee Tume Ituvushe vinginevyo kwa kampeni hizi dhaifu za mwaka huu tutakimbia mchana kweupe. CHADEMA kwa sasa ina wafuasi ama sawa na ccm au kuzidi CCM hilo halina ubishi.

Mungu Ibariki nchi hii Ameen
 
Habari wana JF,

CCM Imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya hii nchi sababu hata ukifannaisha na nchi zote za jirani na Tanzania, Bado Tanzania inang’ara kwa jitihada na maendeleo.

CCM inashindwaje kutumia kwa busara maendeleo walioyapata ambayo ni mazuri mno kuliko ahadi za Wapinzani!?

Kila kitu kipo wazi maendeleo yanaonekana ila kwanini wananchi wanapata muamko wa upinzani! Zaidi?

Ni Upumbavu na Uovu wa kiasi gani kwa vyombo vya dola kujidhihirisha mbele ya wananchi kua mnaminya demokrasia.

Hakuna haja ya mabavu kiasi icho na vikwazo vya kipumbavu kwenda upinzani vinavyozidi kuwapa wananchi huruma upinzani na hatimae kura yao kuwapa upinzani.

Naweza kusema kua safu ya intellegensia ya CCM hamkujipanga vyema kupambana kihoja na murua juu ya demokrasia.

Nashangaa zaidi hasa serikali ya magufuli ndio imefanya kazi kubwa zaidi katika maendeleo ila wapinzani wanazidi kupata nguvu, zinatoka wapi.

Safu ya intelligence ya CCM kama hamuwezi kutumia akili zaidi kuliko mabavu mnaikosesha CCM mwelekeo.
 
Kuna mgombea urais inasemekana anachukiwa. Leo namfuatilia kupitia TBC naona kila anaposimama watu wanajaa na wanamshangilia sana. Nilitegemea watu wasijitokeze au wamzomee!

Tuache kudanganyana huku mitandaoni huko uraiani mambo ni tofauti. Naona uwanja wa Tanganyika Packers kumejaa kweli kweli na mitaani anakopita watu wamejipanga barabarani kumsubiri.

Happy Nyerere day!
Tulichofuata hapo ni fiesta tu.
 
RAISI MAGUFULI AMALIZA HOJA ZA WAPINZANI

Na Mackdeo Shilinde

Ndugu Wana jukwaa la siasa wenzangu nawasalimu katika jina la Bwana wetu Yesu kristo wa Nazareth na mtume Muhammad (SAW)

Wana jukwaa wenzangu kwa Sasa ukiangalia hali ya kampeni zinazoendelea,wazi kabisa utaona kuishiwa kwa hoja kwa wapinzani.

Kuingia kwa hi ungwe ya mwisho kwa maana ya siku hizi 12 zilizo baki ,utagundua wapinzani wanachokifanya Ni kutembea na MAGUFULI,Maana yake Nini?

Wanachofanya wapinzani aswa huyu Lissu Ni kisubiria anacho zungumza MAGUFULI kwenye mikutano yake na yeye kutokea hapohapo, hi inaonesha wazi kuishiwa kwa hoja za kuzungumza bwana Tundu Lissu,lakini sio kuishiwa kwa hoja tu hi pia inatokana na CHADEMA kuwa na sera na ILANI mbovu.

Raisi alivyo kuwa dar alikuwa akizungumza Ni kwa namna gani atakwenda kutatua changamoto za wakazi wa jiji Hili.

Na kwa kuchanganyikiwa kwake mgombea wa CHADEMA na yeye huchukua hoja hizo na kwenda kuwalisha wananchi wa eneo lingine. Mfano raisi alipokuwa Temeke amesema atajenga flyover za kutoshaa ili aende akapunguza adha ya foleni jijini.

Lakini Cha kushangaza TUNDU LISU akiwa mkoani Singida alisikika akiwaambia wananchi wa huko kuwa hawatakula flyover kwa sababu haziwasaidi,kufanya hivyo haiwasadi chadema kupata kura na badala yake wanaendelea kumpaisha raisi kipenzi Cha Watanzania.

Lisu alitakiwa kujua changamoto za watu wa singida na kuwambia Ni kwa namna gani akiingia madarakani atakwenda kutatua changamoto za wakazi wa huko SINGIDA.

Na ndio maana Raisi MAGUFULI kila mahala anapokuwa kwenye kampeni anazungumzia changamoto za eneo husika na ata siku moja uwezi kusikia raisi MAGUFULI akizungumzia kutatua changamoto za wakazi wa Dar kwenye kampeni mkoa mwingine.

Sasa huyu wa kwao kwa kuonesha wazi kuchanganyikiwa kwake akiwa singida ataongea changamoto za Dar, akiwa mwanza ataongea changamoto za kagera na akiwa Mara ataongea changamoto za shinyanga.

Sera na Ilani mbovu ya Chadema ndio inapelekea mpaka mgombea wao kushindwa Ni kitu gani Cha kuzungumza kwenye kampeni zinazo endelea.
 


Utamchaguaje mtu ambaye huwezi kumshauri au kumtaka aache mara moja kwenda kinyume na utaratibu? Nani mwajiri wako? Upo juu ya sheria? Upo juu ya kila kitu?

Kama yeye hapangiwi inakuwaje sisi anatupangia mtu wa kumpigia kura.

Nileteeni Lisuu
Nileteeni Lisuuuuu
Nileteeni Lisuuuuuuuu
Nileteeni Lissuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Bajeti za Madawa kutoka Billion 34 mpaka sasa Billion 270

80% vijiji vyote vimepata Umeme

Tatizo la Umeme linakwenda kuwa historia kupitia mradi kubwa wa Stigles pale Rufiji ambao utatoa Megewati 2015

SGR itakwenda kuwa mkombozi kwa Nchi zaidi ya nane ambao baadhi yao miaka ya nyuma walitukimbia kwasababu ya ubabaishaji mkubwa Bandarini

Wafanyakazi hewa sasa ni Historia na Serikali kupitia Dr John Pombe Magufuli imekoa billion za kutosha ambazo sasa zinaingia sehemu nyingine

Ubasharifu wa pesa za umma na matumizi mabovu kwa watendaji sasa hakuna tena

Sector ambayo tuliumizwa vibaya ya Madini sasa hivi tumeanza kunufaika nayo na majuzi tu tumepokea Gawio la billion 100 kupitia win win situation

Miundombinu kama barabara sasa hivi Tanzania kunafikika kila eneo

Maji watu wengi wanapata maji safi na salama ingawa kuna changamoto ambazo ziaenda kuisha muda si mrefu

Serikali iko mbioni kupeleka muswada Bungeni ila sasa kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya

Elimu bure inaendelea kutolewa na zaidi sasa ni maboresho kama vifaa na stahiki za Walimu ndodondogo ambazo Serikali inazifanyia kazi na zingine tayari zimepatiwa ufumbuzi

Vituo vya afya vinajengwa kwa kasi kubwa kila kijiji na kata ili kumuondolea Mtanzania adha ya kusafiri mbali kutafuta huduma hasa mama zetu

Yako mengine mengi sana ya kumuelezea Dr John Pombe Magufuli kuwa anastahili kuchaguliwa tena na zaidi kupata kura za kishindo tarehe 28 October 2020


Alex Fredrick
FB_IMG_1602824048384.jpeg
 
Bajeti za Madawa kutoka Billion 34 mpaka sasa Billion 270

80% vijiji vyote vimepata Umeme

Tatizo la Umeme linakwenda kuwa historia kupitia mradi kubwa wa Stigles pale Rufiji ambao utatoa Megewati 2015

SGR itakwenda kuwa mkombozi kwa Nchi zaidi ya nane ambao baadhi yao miaka ya nyuma walitukimbia kwasababu ya ubabaishaji mkubwa Bandarini

Wafanyakazi hewa sasa ni Historia na Serikali kupitia Dr John Pombe Magufuli imekoa billion za kutosha ambazo sasa zinaingia sehemu nyingine.

Ubasharifu wa pesa za umma na matumizi mabovu kwa watendaji sasa hakuna tena

Sector ambayo tuliumizwa vibaya ya Madini sasa hivi tumeanza kunufaika nayo na majuzi tu tumepokea Gawio la billion 100 kupitia win win situation.

Miundombinu kama barabara sasa hivi Tanzania kunafikika kila eneo

Maji watu wengi wanapata maji safi na salama ingawa kuna changamoto ambazo ziaenda kuisha muda si mrefu

Serikali iko mbioni kupeleka muswada Bungeni ila sasa kila Mtanzania aweze kuwa na Bima ya afya

Elimu bure inaendelea kutolewa na zaidi sasa ni maboresho kama vifaa na stahiki za Walimu ndodondogo ambazo Serikali inazifanyia kazi na zingine tayari zimepatiwa ufumbuzi.

Vituo vya afya vinajengwa kwa kasi kubwa kila kijiji na kata ili kumuondolea Mtanzania adha ya kusafiri mbali kutafuta huduma hasa mama zetu.

Yako mengine mengi sana ya kumuelezea Dr John Pombe Magufuli kuwa anastahili kuchaguliwa tena na zaidi kupata kura za kishindo tarehe 28 October 2020




Alex Fredrick
FB_IMG_1602824048384.jpeg
FB_IMG_1602824048384.jpeg
 
Mwalimu alisema “Watanzania wamechoka na rushwa”. Tunayo kila sababu ya kuangalia jinsi Rais Magufuli alivyopambana na kero hii ambayo ni adui mkubwa wa haki za Watanzania, hasa wanyonge. Je, Rais Magufuli ameitikiaje rai hii ya Mwalimu Nyerere katika juhudi za kupambana na rushwa nchini kwa miaka mitano ya uongozi wake?

Ndani ya serikali Rais Magufuli ameelekeza juhudi kubwa kupambana na adui rushwa, uhujumu uchumi na ufisadi. Kwa mfano, mwaka mmoja tu baada ya kuingia madarakani Rais Magufuli alianzisha Mahakama ya Uhujumu Uchumi ambayo mpaka sasa imepokea mashauri 407, ambapo mashauri 385 tayari yamesikilizwa. Vilevile kupitia TAKUKURU serikali ya Rais Magufuli imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 273.38, zikiwemo fedha walizokuwa wamedhulumiwa wakulima. Kama hiyo haitoshi, tumeshuhudia viongozi na watanzania wala rushwa, wahujumu uchumi na wabadhirifu wakichukuliwa hatua za kisheria bila kujali uwezo wao wa kifedha.

Licha ya rushwa, Mwalimu Nyerere vilevile alisisitiza kwamba Tanzania inahitaji kiongozi ambaye anatambua kwamba Tanzania ni nchi ya maskini, hivyo nguvu na juhudi zinatakiwa zielekezwe katika ustawi wa afya, elimu, kilimo, biashara kwa Watanzania hawa wanyonge. Serikali ya Rais Magufuli imeelekeza juhudi zake katika kuboresha maisha ya Mtanzania hasa mnyonge kwa asilimia kubwa. Tukianza na elimu, Rais Magufuli amemuona Mtanzania maskini na kuamua kumpa elimu ya sekondari bila malipo. Kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, serikali ya Rais Magufuli imewapa kipaumbele cha kupewa mkopo watoto wa maskini na yatima, hivyo kuleta usawa na haki ya kupata elimu kati ya masikini na tajiri.

Katika Serikali ya Awamu ya Tano, Viashiria kadhaa vinaonesha umasikini umepungua na ustawi wa watu umeimarika. Baadhi ya viashiria hivyo ni: Usambazaji wa umeme vijijini umeongezeka kutoka asilimia 16.4 mwaka 2015 hadi asilimia 67.1 mwaka 2019, na umasikini wa mahitaji ya msingi umepungua kutoka asilimia 28.2 mwaka 2011/12 hadi asilimia 26.4 mwaka 2017/18. Aidha, kiwango cha umasikini wa chakula kimepungua kutoka asilimia 9.7 mwaka 2011/12 hadi asilimia 8.0 mwaka 2017/18.

Mwalimu alisisitiza sana kujitegemea, alitaka taifa lijenge uchumi wa kujitegemea, kila mwananchi kwa nafasi yake afanye kazi kwa juhudi na maarifa ili tuweze kujitegemea kiuchumi, kwa muktadha huo, Rais Magufuli ameedelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi, na amekwishaonyesha kwa vitendo namna kaulimbiu yake ya “Hapa Kazi Tu” ilivyowapa hamasa kubwa Watanzania kufanya kazi na hivyo juhudi hizi kuzaa matunda ya kuipaisha Tanzania katika uchumi wa kati.

Niseme tu kuwa ifikapo Oktoba 28, 2020 ni zamu yako Mtanzania mzalendo na mpenda maendeleo kumpitisha Rais Magufuli ili aendeleze juhudi hizi na maisha yako yazidi kuboreshwa kwa manufaa yako, familia yako, jamii inayokuzunguka, na taifa kwa ujumla.
 
TUMCHAGUE TENA DKT. JOHN P. MAGUFULI

Mwaka 2015 kilo moja ya meno ya tembo ilikuwa na thamani ya sh. 200,000/= kutokana na kutokuwa na udhibiti madhubuti, Bei hii ilipelekea kuongezeka kwa ujangili na mauaji makubwa ya Tembo Jambo lililopelekea Tanzania kuitwa "Eneo la kuondoa uhai" au kwa lugha rahisi "eneo la maangamizi"

Kwa Maana ya kwamba , Kwa Tanzania ilionesha Tembo wamepungua kutoka 109,051 mwaka *2009* Hadi kufikia 43,330 mwaka *2014*, ikiwa wameuawa zaidi ya Tembo 85,181 kwa *Miaka mitano* peke yake

Ambapo kila mwaka zaidi ya Tembo *Elfu kumi na Saba* waliuawa na pembe kusafirishwa kuuzwa Nje ya NCHI Jambo lilosababishwa kudorora kwa sekta ya utalii na maliasili na kutishia kutoweka/kufutika kabisa kwa Tembo katika mbuga zetu

Katika kipindi Cha miaka mitano ya Dkt. John P. Magufuli amedhibiti ujangili kwa kiasi kikubwa kupelekea idadi ya Tembo kuongezeka kutoka 43,330 mwaka 2014 mpaka kufikia zaidi ya Tembo 60,000 mwaka 2019.

#NITAMCHAGUATENAJPM
 
TUMCHAGUE TENA DKT. JOHN P. MAGUFULI

Mwaka 2015 kilo moja ya meno ya tembo ilikuwa na thamani ya sh. 200,000/= kutokana na kutokuwa na udhibiti madhubuti, Bei hii ilipelekea kuongezeka kwa ujangili na mauaji makubwa ya Tembo Jambo lililopelekea Tanzania kuitwa "Eneo la kuondoa uhai" au kwa lugha rahisi "eneo la maangamizi"

Kwa Maana ya kwamba , Kwa Tanzania ilionesha Tembo wamepungua kutoka 109,051 mwaka *2009* Hadi kufikia 43,330 mwaka *2014*, ikiwa wameuawa zaidi ya Tembo 85,181 kwa *Miaka mitano* peke yake

Ambapo kila mwaka zaidi ya Tembo *Elfu kumi na Saba* waliuawa na pembe kusafirishwa kuuzwa Nje ya NCHI Jambo lilosababishwa kudorora kwa sekta ya utalii na maliasili na kutishia kutoweka/kufutika kabisa kwa Tembo katika mbuga zetu

Katika kipindi Cha miaka mitano ya Dkt. John P. Magufuli amedhibiti ujangili kwa kiasi kikubwa kupelekea idadi ya Tembo kuongezeka kutoka 43,330 mwaka 2014 mpaka kufikia zaidi ya Tembo 60,000 mwaka 2019.

#NITAMCHAGUATENAJPM
 
Halo JF siasa.

Kulikuwa na tetesi zimezagaa mitandaoni kuwa Magufuli kaishiwa pumnzi na amewaomba January na Kinana waingilie Kati kuokoa Jahazi vinginevyo atashindwa uchaguzi huu.

Mbona swaoni miamba hii ya siasa zikiambatana na Magufuli?
Je yalikuwa ni majungu au wanasiasa hawa wa kuheshimika wamegoma?
 
Nianze na mgombea wa urais

1. Jiwe ni mtu wenye kisasi sana, ni mtu ambae ukimkwaza lazima alipize kisasi.

Zilizozo chini ya kapeti, huenda pia si jambo la chini ya kapeti likawa ni jambo linalojulikana na wengi... kuwa wazazi wa jiwe si watanzania inasemekana kwamba mama yake aliingia nchini akiwa na mimba ya Jiwe, na kupata pedeshee wa kisukuma na kumuowa mama yake na Jiwe akiwa ni mjamzito.

Jiwe ni mtanzania kwani ni mzaliwa wa Tanzania lakini asili ya wazazi wake sio Tanzania. Jiwe anaroho ya chuki na uwongo na wala hana huruma kama watanzania wengi tulivyo wapole na wenye huruma.

2. Jiwe ni mtu wa kulipiza kisasi, anakaa na chuki moyoni, watanzania tusisahau mashambulio yaliyotokea nchini na polisi kufucha ukweli wa matukio hayo ya kushambuliwa kwa viongozi wa kisiasa na hata wasio wanasiasa.

3. Kwanini CCM wanataka kuchukua majimbo mengi?
Kwanini Mgombea urais wa sisiemu anataka awe na wabungue wa chama chake bunge zima? Je vyama vingine vinawagombea wapumbavu wasiotaka maendeleo? Kuna hatari kubwa ya kubadili katiba ya nchi yetu na kujiwekea uhuru wa kuendelea kugombea na kuongoza nchi.

4. Kwa majimbo ambayo yalionesha kuikubali chadema lazima wataisoma namba baada ya ccm kuendelea kushika madalaka.
Chato walio mzomea nao wasubiri kulipiziwa kisasi kwa kumzomea jiwe.

5. Tukimpa tena mitano jiwe amalizie, interest zake hazipi kabisa katika kuongeza ajira, wala mishara anachojua ni kupandisha tu kodi.
Kwa jinsi ambavyo tumeonyesha kuto kumtaka na kumkataa, akiweza kupita tena hata kwa bao la mkono, lazima atarudi kutukomesha, kama anavyowakomesha wapimzani. Kwanini aliwazuhia wapimzani kufanya kampeni zao?

6. Katika jimbo nililopo, mwaka 2010 tulijionea ccm wakitangazwa washindi na kuchomwa kwa offisi ili kupoteza ushahidi wa ushindi huo batili. Je mwaka huu wizi wa kula za wabunge utafanyika katika majimbo mangapi?

7. Katika uboleshaji wa daftari la mpiga kula sisiemu wametumia mbinu ya kuongeza majina hewa, ambayo watayatumia kuongeza idadi ya kula zao feki. Tumelishuhudia hilo kwa waandikishaji wa majini ya wapiga kura wa vituo mbalimbali.

8. Kwanini wananchi tunazuhiliwa kufanya maandamano ya amani je si haki yetu kisheria ? Kwanini tunakataliwa kulinda kura zetu? Kwani kuna mtanzania mwenye shida ya kumuuwa mtanzania mwenzake kisa utofauti wa chama?

9. Kauli ya mgombea wa sisiemu bado imeniumiza kichwa na kua tata masikioni mwangu, aliposema kua chaguzi zote zilizopita hatukumwaga damu, watanzania tunajijua hakuna ambae anawaza kumshambulia mwenzake kisa utofauti wa chama, Je, kukisiwa huko kwa kumwagika kwa damu kutatokana na mashambulio ya watu gani na wakiwashambulia watu gani na kwa makosa yapi?

Nawatakia uchaguzi mwema wa amani wenye hekima na maarifa ya kuchagua kiongozi anaye tufaha.
 
Back
Top Bottom