Sema una kaushabiki... NaJF imeanza kuwa tainted..sio kisima cha fikra huru Tena. Ukienda kwa warumi ongea kirumi..
Vijana hampigi kura kutwa kwenye mitandao kupiga soga.. mwanasiasa yeyote Mwenye akili anajua umuhimu wa watu wa vijijini ambao wengi wao Kiswahili hawakijui Kama unavyotaka Kujiaminisha.
Na kiongozi Kama utashindwa kuongea yale yanayogusa moyo wao kura hupati.. labda kitu usichokijua Duniani kote sera haikupeleki ikulu.. Ni ushawishi..
Sasa wewe nenda bukoba/umasaini au Ihemi na Tungamalenga huko uwashawishi na maneno yako ya mchakato uone Kama utapata kura..
Na kinachosikitisha ..na haka kanakuwa katrend humu-jf watu aidha kuongezea chunvi Sana matukio ya kampeni au kuyabadilisha badilisha kusuit their narrative,. Ni aibu kwa msomi kupindisha data aonekane yuko Sahihi... Na hii iwafikie wote vyama vyote na moderators mnaua brand ya JF.
Btw. Kwanza kwa hilo la kisukuma unayo picha ya video au rekodi ya sauti ya kampeni iliyoendeshwa kwa Kisukuma mwanzo mpaka mwisho!? Na Kama ipo haina version ambayo aliielezea kwa Kiswahili!?
Pili wewe upo Mwanza!? Katika eneo analoahidi na kumwaga sera allegedly fully kwa kisukuma!? Kama hapana una ndugu, jamaa au rafiki maeneo hayo ambaye amesema hakuelewa!? Kama huna jamaa na wala huna ndugu huko..
Kwann unataka sana kujua wao wameahidiwa Nini!? Wivu!? Tamaa!? Au!? Kwann wewe mtu wa temeke uwe very interested kujua Mlele wameahidiwa Nini!?
Sent from my Infinix X650 using
JamiiForums mobile app