Nimeona kuna wengi humu wenye akili butu. Hizi ndio voting patterns za last elections za Ukraine. Kama nchi yenu haina shida na ethnicity well and good. Lakini maeneo mengine ethnicity ndio kila kitu,especially the Balkans and former soviet countries. Kusema mambo ya ethnicity yamepitwa na wakati ni kuwa unrelistic na pia mjinga. Unakua kuwa Ukraine imekuwa ikiwapiga wakaazi wa Donetsk kwa miaka nane sasa? Huwezi wanyanyasa watu, upige marufuku lugha yao, uwanyeshee mabomu alafu utake wakupende. Hawa ethinic Russians wameteswa sana na ethnic Ukranians.
View attachment 2333152
Ni vyema ukajikita kujibu hoja yangu ya: Ni nani alikuwa nyuma ya matokeo ya kura iliyopigwa? Je, kulikuwa hakuna shinikizo kwenye Uchaguzi(referendum)
Hebu fuatilia :- 1. Vikundi vilivyokuwa vinaendesha hujuma dhidi ya Ukraine vilikuwa vinapata wapi Uungwaji mkono(support), Silaha na uwezeshwaji katika kampeni za kuhamasisha chuki dhidi ya Ukraine?
2. Ukabila ni sumu. Ukabila ni kifungo katika Akili na Nafsi za watu.
Inakuwaje hivo? Ni hivi...Anatokea mpuuzi mmoja (
Mtu binafsi au Serikali)na kuanzisha kampeni ya kuwaaminisha watu kwamba wanaonewa, wanadhulumiwa, Hawatendewi haki, wanafanyiwa ulaghai n.k.n.k.
Sio hivo tu, Mpuuzi huyo anaendelea kwa kuwarubuni baadhi ya watu(Kuwanunua) na kuwapa ufadhili-uchwara (i.e. anawageuza kuwa wasakatonge)na hao wasakatonge ndio wanaoendesha kampeni za kichini-chini na hamasa za kueneza chuki na wanaounda vikundi dhidi ya Serikali. Vikundi hivyo vinapewa mafunzo, silaha na ufadhili wa kifedha. Je, katika hali ya namna hiyo unategemea matokeo gani katika kura ya maoni?
Katika Ramani uliyoonesha hapo juu, hujiulizi ni kwa nini
blue iko pembezoni tu na iwe ni katika mpaka na Russia?
Katika hali ya kawaida ukitenda kosa na ikathibitika hivo unawajibishwa. Sasa uwajibishwaji kwa makosa ya kisiasa upo kwa wingi eneo lenye rangi ya blue. Wao wanadai kunyanyaswa. (Mengine kasome mwenyewe huko......)