Spika Job Ndugai, amejiuzulu Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugai sijawahi kumfagilia hajawahi kuwa na msimamo thabiti amekuwa na lugha za kejeli kwa wabunge, wananchi na hatimaye rais wa nchi. Wapinzani wake wa kisiasa amewacharaza bakora. Amehusika katika kutunga sheria kandamizi ambazo leo hii zitatumika kumuhukumu yeye.

Ndugai alikeji maneno matakatifu. "Mitaa ya Galilaya anaifamu sana huko alishatembelea sana kumuona mke wa masihi". Kishekesho kweli! Tunawashukuru malaika wa Mungu hawalali masaa 24 wako macho. Muda wote wako kazini wote. Mchimba kaburi huingia yeye mwenyewe.

Kwa wapinzani wa CCM tulieni kama Daudi vitani, hawana wa kupigana nao ingekuwa ni nyie lakini wamewafanyia hila. Wakikosa wakusozana naye watafanyiana hila wao kwa wao. "Nyamazeni kumia" tunajenga uchumi. Uchumi umeanza kujengwa bungeni kwa kuondoa wasema hovyo!

Mtikisiko upo! mafuriko yapo! Joto lipo juu! Tena lipo juu sana! Msitu bado haujashika moto lakini umekauka, majani yamekauka, miti yote imeshadondosha majani. Kaaeni kimya hivi vita siyo vya kwenu! Hivi vita ni vya kwao! Nyamazeni kimya.

Kwa mara ya kwanza ndiyo nimeona Rais muwazi mkweli! Muwazi kwa kuwa ametueleza ukweli kuhusu fedha zote alizokopa. Pia na matumizi yake amekuwa muwazi. Uwazi ni nguzo ya utawala bora. Nimeona madarasa mengi na bora yamejengwa kuliko wakati wowote katika historia ya nchi hii. Januari ya 2022 hakuna kushikana mashati kwa kuhusu kujenga madarasa bali unahitajika kufanya ukaguzi maalum kubaini waliocheza na fedha zetu. Kazi iendelee.

Mama yetu asiependa makuu mkimya na anyetumia kalamu yake vyema tunakuomba safisha kila chafu! Wale wabunge 19 feki wa Ndugai waondolewe bungeni. Hii itakujengea wewe na serikali unayoingoza heshima kubwa. Hakika hii ndiyo dhana halisi ya "Kazi Iendelee". Kichafu chochote kile kisihusishwe na serikali yako. Waache wao wafanye vitu vya aibu. Kina mama siku zote ni smart. Kazi iendelee!

Safisha sehemu zote chafu. Kesi zote za kutungwa muelekeze DPP azifute.

Mama ukikosa wapinzani nje ya CCM watotokea ndani ya CCM. Hao ni wabaya kuliko Lema na Msigwa. Wakipata watu wakuwachachafya watakimbilia majimboni mwao kusimamia maendeleo ya watu. Si unajua tena mtu akikosa kazi ya kufanya anabweteka na kuanza matusi kama ya Ndugai ya nchi kupigwa mnada!

Ruhusu mikutano ya siasa wote watatulia tuli na kukimbilia majimboni mwao kupambana na upinzani na siyo serikali. Sasa hivi wameshiba wanapambana na CCM.

Tunyamaze kimya vita hivi siyo vya kwetu. Siyo vya CCM wala CHADEMA ni vya Bwana. Mshindi wa vita hivi ni yule atakaye simama upande wa haki!

Kazi iendelee!
 
Mimi binafsi Mzanzibar asingeweza kunishinikiza alafu nijiuzuru. Ukizinngatia kazi yenyewe nimeipata kwa shida, baada ya kumdunda mtu kwa li-fimbo. Kingine huko Zanzibar kwao haturuhusiwi kudaka kazi, alafu eti aje atie maji kwenye kazi yangu huku bara!!!!
 
Lakini mkuu usisahau group la G 55 ndilo lililomuondoa madarakani Katibu Mkuu wa CCM Horace Kolimba na Waziri Mkuu John Malecela.
Kolimba aliambiwa ameshindwa kutumia nguvu za chama alizokuwa nazo kuwadhibiti wabunge wale.
Na Malecela kama mkuu wa shughuli za serikali bungeni ameshindwa kutumia ushawishi kuvunja tishio lile la kuigawa nchi.
Nyerere alisema Muungano wa serikali mbili ni Sera ya CCM, asiyeutaka kwanza ajiondoe kwenye chama hicho.
Kwahiyo kwa mujibu wa Nyerere chama hakikutumika ipasavyo kuwadhibiti G55.

Hivyo basi, utaona namna chama kilivyo na uwezo mkubwa wa kuvuruga maguvu ya muhimili huu muhimu.
 
Ule mwingine kwani hamuoni unavyofanya madudu na matapu tapu kwa ile kesi maarufu
Hata huu unaonekana ni rahisi mno kutikiswa, tatizo ni katiba au viongozi wakuu wa hii mihimili wameshindwa kusimamia vyema katiba?

Ndugai alikuwa mlinzi wa katiba ya 1977 sasa ni mhanga kwasababu haikumlinda kama kiongozi wa mhimili. Aliishi kwa mazoea na ubabe, good riddance
Kaacha joho kaondoka mtupu ! bila heshima yoyote
Wakati wa awamu ya 5 huu muhimili ulilaumiwa sana kwa kujipendekeza kwa serikali.........huenda Job alitaka kuivunja hii ndoa haramu kati ya bunge na serikali (japo alishiriki kuiasisi) sema wana Ccm wenzake na baadhi ya wapinzani hawakumuelewa badala yake wameangalia rekodi yake ya nyuma bila kujua hata saa mbovu kuna muda inasema ukweli.

Kwa wadau wa demokrasia hili tukio ni hatari kwa ustawi wa nchi yetu.
 
Jamaa muoga sana. Angeendelea kupambana tu.

Lakini sio mbaya maana ana kinga tayar.
 
Uzuri wa Tanzania ni pamoja na maajabu ya Historia inayotengenezwa/kutokea kila iitwapo leo.
Ingawa kuna wakati Historia hizo uambatana na majonzi kwa watu na pengine misiba.
Ninawapa pole wale wote waliopoteza ndugu, jamaa na rafiki kwenye ajali ya Boti kisiwani Pemba na ile ajali ya watu kugongwa na Loli Newala Mtwara.
Mwenyezi Mungu azilaze Mahala pema roho zao
Amina.
 
Nampongeza Ndugai kwa kujiuzulu.Rais Mwinyi aliwahi kujiuzulu na baadae akawa Rais.
Hoja ni kuwa wale wahuni na Chawa kamwe wasipewe nafasi.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
 
Tunaendelea kufukiza kuni mbichi kwenye pango!!!
 
Nampongeza Ndugai kwa kujiuzulu.Rais Mwinyi aliwahi kujiuzulu na baadae akawa Rais.
Hoja ni kuwa wale wahuni na Chawa kamwe wasipewe nafasi.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Kwahiyo supika naye atakuwa rais blaza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…