Spika Ndugai: Asiyetaka tozo ya kizalendo atupe njia mbadala ya kupata fedha

Spika Ndugai: Asiyetaka tozo ya kizalendo atupe njia mbadala ya kupata fedha

Spika Ndugai amesema wabunge wameshapitisha tozo ya kizalendo kwenye miamala ya simu na sasa ni sheria hivyo asiyeitaka atupe njia mbadala ya kutufikisha 2025

Roho wa Bwana akamshukia mtumishi wake Jerry Slaa mbunge wa Ukonga naye akajibu; Wabunge tuanze kulipa kodi.

Labda kama Spika ana swali lingine....lakini sidhani.

Ijumaa kareem?

---
Baada ya mijadala mingi kuhusiana na tozo ya miamala ya simu hususani kwenye mitandao ya kijamii ,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ameibuka na kudai kuwa tozo hizo ni halali na kwamba fedha hizo zitachagiza masuala ya maendeleo ikiwemo huduma za kijamii kama vile shule,hospitali na maji.

Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kwamba kumekuwa na tozo kubwa katika miamala ya simu huku akipigilia msumari kwenye tozo hizo kwa kudai kuwa Bunge ndio limepitisha na kwamba wanaopinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala nini kifanyike huku akisisitiza lengo ni ifikapo 2025 Tanzania iwe Taifa tofauti katika suala la Maendeleo.

Akizungumza mapema leo Julai 23,2021,katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,Spika Ndugai amesema "Sisi kama Bunge tulikaa kwa pamoja na kujadiliana kisha tukaamua kuwa na tozo katika miamala ya simu kwa sababu fedha zitakazopatikana zitaenda katika mfuko Maalum ambao utawasaidia wananchi,"amesema na kuongeza;

"Tumepitisha na tukatunga sheria , tunataka kuliona hilo,sasa wewe ambaye unapinga tupe njia mbadala tutapata wapi fedha, tunafikaje 2025, kwa hiyo maamuzi ni hayo tumeyafanya, kwa nia njema kabisa kwamba 2025 tuwe tumetoka, tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni tofaut,CCM hoyee,nimemaliza,"amesema Spika huyo.

Chanzo: Malunde


Huyo atakuwa hajitambui kidogo!!, sasa atuambie baada ya 2025, kodi hiyo itasitishwa??!!---- yaani Bunge litapelekewa Muswada wa kufuta hiyo kodi???
 
Tatizo nyie manawaza watu wafe tu hivi nyie mna mkataba na mungu?
Na nyie kwa roho zenu za kinyama na kigaidi kwa nini msife?
Kutofautiana kimawazo ni kutafuta njia mbadala na sio kuwazia watu wafe.
Nyie mna faida gani kwenye hili taifa?

Tuonyeshe ni mtu gani wa upinzani anaeongoza kuchangia kodi kubwa hapa tanzania?

Bosi wenu mbowe mwenyewe ni mkwepa kodi,
Kodi ta miamala hakuna anayeipenda na kila mtu ametoa maoni yake kwa ustarabu na jambo liatashughulukiwa na tuataka wafanye haraka na sio kuchelewa na ikiwezekana wazuie huu utaratibu kuanzia sasa.

Lakini sio kuombeana vifo,
Kuombeana vifo ni uzwazwa na ugaidi.
Huo mjadala unaosema haumhusu Ndugai na majibu yake ya shombo? Yaani watanzania wanaolalamika anawaona wajinga ila yeye na genge lake wanaolishwa bure kwa kodi zetu. Yeye analipa nini huyo Pimbi zaidi ya kula na kuvishwa majoho bure? Kodi inakatwa kwa anayetuma tuseme ana uwezo sawa, inakatwa kwa anayetumiwa maskini yuko kijijini Msoga halafu anajitokeza pimbi asiyejua fedha inapatikanaje anajibu watu utumbo?
 
Spika Ndugai amesema wabunge wameshapitisha tozo ya kizalendo kwenye miamala ya simu na sasa ni sheria hivyo asiyeitaka atupe njia mbadala ya kutufikisha 2025

Roho wa Bwana akamshukia mtumishi wake Jerry Slaa mbunge wa Ukonga naye akajibu; Wabunge tuanze kulipa kodi.

Labda kama Spika ana swali lingine....lakini sidhani.

Ijumaa kareem?

---
Baada ya mijadala mingi kuhusiana na tozo ya miamala ya simu hususani kwenye mitandao ya kijamii ,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ameibuka na kudai kuwa tozo hizo ni halali na kwamba fedha hizo zitachagiza masuala ya maendeleo ikiwemo huduma za kijamii kama vile shule,hospitali na maji.

Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kwamba kumekuwa na tozo kubwa katika miamala ya simu huku akipigilia msumari kwenye tozo hizo kwa kudai kuwa Bunge ndio limepitisha na kwamba wanaopinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala nini kifanyike huku akisisitiza lengo ni ifikapo 2025 Tanzania iwe Taifa tofauti katika suala la Maendeleo.

Akizungumza mapema leo Julai 23,2021,katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,Spika Ndugai amesema "Sisi kama Bunge tulikaa kwa pamoja na kujadiliana kisha tukaamua kuwa na tozo katika miamala ya simu kwa sababu fedha zitakazopatikana zitaenda katika mfuko Maalum ambao utawasaidia wananchi,"amesema na kuongeza;

"Tumepitisha na tukatunga sheria , tunataka kuliona hilo,sasa wewe ambaye unapinga tupe njia mbadala tutapata wapi fedha, tunafikaje 2025, kwa hiyo maamuzi ni hayo tumeyafanya, kwa nia njema kabisa kwamba 2025 tuwe tumetoka, tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni tofaut,CCM hoyee,nimemaliza,"amesema Spika huyo.

Chanzo: Malunde
Huyu wimbi hili litaondoka nae, kavimbiwa pesa zetu
 
Nchi imeshaharibika. Kitendo cha kuruhusu biashara ya mkononi na kwenye meza ndo kifo cha kodi Tz. Nchi zilizoendelea hata karanga zinafungwa kwenye mfuko na kuwekwa barcode. ushuru unakuwa mdogo kiasi kwamba mfanyabiashara haumii lakini kila mfanya biashara analipa kodi. Sasa uongozi wetu umeona fahari kuruhusu biashara ziendeshwe kwa mtindo wa kuagiza mzigo wa kichina na kuwakabidhi machinga, sahau mapato ya serikali. Vijana badala ya kutumika kufanya kazi za uzalishaji wanafanya kazi ya kusaidia kuchepusha kodi na serikali imebariki.
Hizo za mikononi, Magufuri aliwambia angalau walipe elfu 20 mkaanza kubeza kuwa Magufuri mwizi,kisa kawambia machinga kulipa elfu 20,acha watukomeshe maana Watanzania atujui tunaitaji kuongozwa na Mtu yupi
 
Tozo ya miamala ni sahihi
Ila ongezea
Parking fee ya Toyo na bajaji
Hawa jamaa wamejaza Parking mjini na ndio wanufaika wa awamu hizi za 5 na 6
Wamachinga vitambulisho vyao viwe 50000
Kila mtu aliyeko mjini anatafuta pesa achangie kitu kwenye kukuza uchumi
 
Huyu anaweza kuwa alichaguliwa kutimiza diversity quota ya watu 'wafupi' bungeni kama ilivokuwa kwa viti maalum...Huwezi kutoa kauli kama hii...


Mniwie radhi ndugu zangu wenye 'low center of gravity' kama nimewakwaza.
 
Huduma za fedha kwa njia ya mitandao ya simu badala ya kuboreshwa ili serikali izidi kupata mapata makubwa kwa kushawishi wananchi wengi zaidi kuitumia kwani kodi yake haina chenga, wana-discourage huduma hii kwa maksudi! Kwa kiwango cha tuzo anayotetea mbunge huyu, watu watarudi kwenye mifumo ya awali (cash itashika hatamu) watakosa hata kodi ilokuwa ikipatikana kabla ya tozo mpya.

Wakati umefika hawa watunga sheria, n.k. nao walipe kodi zote pasiwe na double standard. Ukitaka wananchi kuwa na uzalendo, viongozi wanapaswa kuonesha mfano wa kile wanachokihubiri.

Nchi hii inautajiri mkubwa sana, madini, ardhi, maji, n.k. Mfano kupitia kilimo; tumezungukwa na vyanzo vikubwa vya maji lakini tunalima kwa kutegemea mvua ya mwenyenzi badala ya umwagiliaji. Utawakuta viongozi (watu wazima, wasomi, n.k)wamekalia kuwazuia wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi kwa kisingizio eti watapata njaa badala ya kuitumia hii kama fursa ya wanachi walowengi kupata ajira na nchi kujipatia fedha za kigeni kwa kuwaboreshea miundo mbinu, n.k.
 
Wao huko serikalini wanaishi maisha mazuri ya kifahari wao na familia zao, kila kuzuri kuzuri wanalala wao, kutibiwa kuzuri wanatibiwa wao, kula kuzuri wanakula wao, shule nzuri kwa watoto wao Wana soma wao, hata maziko mazuri wanapata wao,!

Sisi ndio tumekua watwana wao, kutafuta tufute sisi wao ndio watumie, wao ndio watupangie.

Mimi nawatakia yote, ila mwenyezi Mungu siku zote humkumbuka Alie mnyonge na humwokoa katika Shari zote, iwapo Kuna maisha baada ya haya Basi ni watakie hao wanaotupangia yote yalio mema!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazo jemaa KABISA kuchangia nchi yangu na maendeleo yake
wakati muafaka Kama wananchi tusikomae tu iondoelewr

TUTOE ushauri nn kifanyike seerikali iendelee kupata pesa za KUFANYA maendeleo ya NCHI yetu

nimeona dini zilizoea Kupitisha.mizigo bila Kodi leohii zinalipa...

Hili la wabunge kulipa.kodi.nalo n wazo jemaa pia na ikiwezekana kuwe na punguzo ktk posho wanazopata KUSAIDIA kuendeleza maendeleo ya NCHI yetu

kingine serkl ingekaa wakubaliane kiasi KIDOGo kaama n 200 ama 500 kilamhamala si mbaya huku kampuni zikiendelea kulipa kodizao kama kawaida....mwananchi atajisikia amechangia nchi yake..

kuwe na costant amount ushauri 200-500 KIla.mhamala SI.mbaya isiangalie kiasi anachotuma mtu...

nawatakia mjadala mwema nikisubiri wabunge nao wapewe hiihoja kujadili MBADALA wa hii tozo

kulipa mtalipa nchi iendee tuombee majadiliano mema

Mungu ibariki Tanzania

#VAAABARAKOA
#NAWAMIKONO
#COVID
#INAUA
 
Spika Ndugai amesema wabunge wameshapitisha tozo ya kizalendo kwenye miamala ya simu na sasa ni sheria hivyo asiyeitaka atupe njia mbadala ya kutufikisha 2025

Roho wa Bwana akamshukia mtumishi wake Jerry Slaa mbunge wa Ukonga naye akajibu; Wabunge tuanze kulipa kodi.

Labda kama Spika ana swali lingine....lakini sidhani.

Ijumaa kareem?

---
Baada ya mijadala mingi kuhusiana na tozo ya miamala ya simu hususani kwenye mitandao ya kijamii ,Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ameibuka na kudai kuwa tozo hizo ni halali na kwamba fedha hizo zitachagiza masuala ya maendeleo ikiwemo huduma za kijamii kama vile shule,hospitali na maji.

Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya wananchi kulalamika kwamba kumekuwa na tozo kubwa katika miamala ya simu huku akipigilia msumari kwenye tozo hizo kwa kudai kuwa Bunge ndio limepitisha na kwamba wanaopinga wanatakiwa kutoa mawazo mbadala nini kifanyike huku akisisitiza lengo ni ifikapo 2025 Tanzania iwe Taifa tofauti katika suala la Maendeleo.

Akizungumza mapema leo Julai 23,2021,katika kikao kazi kilichoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Anthony Mtaka,Spika Ndugai amesema "Sisi kama Bunge tulikaa kwa pamoja na kujadiliana kisha tukaamua kuwa na tozo katika miamala ya simu kwa sababu fedha zitakazopatikana zitaenda katika mfuko Maalum ambao utawasaidia wananchi,"amesema na kuongeza;

"Tumepitisha na tukatunga sheria , tunataka kuliona hilo,sasa wewe ambaye unapinga tupe njia mbadala tutapata wapi fedha, tunafikaje 2025, kwa hiyo maamuzi ni hayo tumeyafanya, kwa nia njema kabisa kwamba 2025 tuwe tumetoka, tuwe ni taifa la Tanzania ambalo ni tofaut,CCM hoyee,nimemaliza,"amesema Spika huyo.

Chanzo: Malunde
Wab hamna mbadala na ndio mnapitisha sheria

wananchi wanatoa Wapi wanze wao kuonyesha uzalendo kwa waliowatuma
 
Magari ya serikali kuwe na ukomo wa bei,mwisho iwe 150 hili ndilo gari atumie kiongozi wa juu.

Wengine watumie hata hardtop na Prado.Tunaishi kwa anasa huku tunategemea tozo kwenye simu
 
Back
Top Bottom